Facebook Yatangaza Kufunga Messenger Kuanzia Desemba 15
Kampuni ya Meta, inayomiliki Facebook, imetangaza rasmi kuwa itafunga app ya Messenger kuanzia tarehe 15 Desemba mwaka huu. Hatua hii inalenga kubadilisha jinsi watumiaji wanavyowasiliana ndani ya mtandao huo wa kijamii, hasa kwa wale wanaotumia vifaa vya kompyuta kama vile Macs na Windows. Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya kampuni hiyo, mabadiliko haya yataanza kwa watumiaji wa kompyuta mwaka huu, kisha kuenea kwenye majukwaa mengine mwaka ujao, huku lengo likiwa kuunganisha huduma za mawasiliano ndani ya Facebook yenyewe. Hii ina maana kwamba app ya Messenger itaondolewa kabisa, na badala yake huduma za ujumbe zitapatikana moja kwa moja ndani ya Facebook. Messenger ilianza kama Facebook Chat mwaka 2008, kabla ya kubadilishwa rasmi kuwa app huru ya kuchati mwaka 2011. Ilizinduliwa ili kushindana na majukwaa mengine ya ujumbe kama vile WhatsApp, iMessage, WeChat, na Skype. Kwa miaka mingi, Messenger imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano miongoni mwa watumiaji wa Facebook, ikiruhusu uchapishaji wa maandishi, picha, video, na hata simu za sauti na video. Hata hivyo, kuondolewa kwa app hiyo huru ni ishara kuwa Meta inalenga kurahisisha huduma zake kwa kuziunganisha ndani ya jukwaa moja. Katika mfumo mpya, Facebook itaendelea kuwa mtandao wa kijamii wenye huduma za ujumbe (messaging), machapisho (posts), Reels, Groups, na communities, lakini yote yakifikiwa kupitia app moja tu — Facebook. Hatua hii inatarajiwa kuathiri mamilioni ya watumiaji wa Messenger duniani kote, hasa wale waliokuwa wakiitumia kama njia kuu ya mawasiliano nje ya app ya Facebook yenyewe.
Read More