Harmonize Ajibu Kwa Hasira Tuhuma za Kumdai Ibraah

Harmonize Ajibu Kwa Hasira Tuhuma za Kumdai Ibraah

Staa wa muziki wa Bongo Fleva na mwanzilishi wa lebo ya Konde Gang, Rajab Abdul Kahali maarufu kama Harmonize, hatimaye ameweka wazi uhusiano wa sasa kati yake na aliyekuwa msanii wake, Ibraah. Hili ni baada ya tetesi nyingi kuzagaa kuhusu kuvunjika kwa ushirikiano wao uliodumu kwa miaka minne. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Harmonize alithibitisha rasmi kuwa Ibraah si sehemu ya Konde Gang tena, na sasa anafanya kazi kama msanii huru. Katika kueleza hali halisi ya kuondoka kwa Ibraah, Harmonize alikanusha vikali madai kwamba alimtoza msanii huyo kiasi cha Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya kuvunja mkataba wao. “Ni kweli mdogo wangu Chinga alinipigia simu na kuniambia anataka kutoka Konde Gang. Nilimtakia kila la kheri, lakini nikamshauri azungumze na viongozi wa lebo iwapo anahitaji kununua catalogue ya nyimbo zake,” alisema Harmonize huku akisisitiza kuwa hakuna madai yoyote ya kifedha baina yao. Harmonize aliongeza kuwa madai yaliyosambaa mitandaoni kuhusu deni hilo hayana ukweli wowote na yamekuwa yakimchafua bila sababu. “Simdai Ibraah pesa hiyo, na siwezi kupenda pesa yangu ije kunichafua mimi mwenyewe,” alisema kwa msisitizo. Katika upande mwingine wa mazungumzo hayo, Harmonize alifunguka kuhusu mustakabali wa Konde Gang, akieleza kuwa lebo hiyo iko tayari kufungua milango kwa vipaji vipya. Alisema kuwa licha ya changamoto, Konde Gang bado inaendelea na jukumu lake la kuibua na kulea wasanii chipukizi wenye ndoto kubwa. Taarifa hiyo imeibua hisia mbalimbali kutoka kwa mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva, wengi wakimpongeza Harmonize kwa ukomavu wake wa kiuongozi na namna alivyosimamia suala hilo kwa hekima na utulivu. Kwa sasa, wadau wa muziki na mashabiki kwa ujumla wanasubiri kuona Ibraah atajielekeza wapi akiwa kama msanii huru, huku nafasi mpya zilizofunguliwa ndani ya Konde Gang zikisubiri kujazwa na vipaji vipya vinavyokuja na njaa ya mafanikio.

Read More
 Harmonize atangaza ujio wa wimbo mpya kuhusu wapenzi wa zamani

Harmonize atangaza ujio wa wimbo mpya kuhusu wapenzi wa zamani

Mwanamuziki wa Bongofleva Harmonize ametangaza kuachia wimbo mpya Ijumaa hii, kueleka siku ya kutoa wimbo huo, Kupitia Insta Story yake kwenye mtandao wa Instagram Harmonize ametoa ufafanuzi kuhusu wimbo wake mpya unaotarajiwa kutoka, akisisitiza kuwa hauhusiani na mpenzi wake wa zamani. “HAIHUSINI NA X WANGU YEYOTE!!! NINA HESHIMA KUBWA SANA KWAO WOTE.”, Amesema Harmonize. Kiongozi huyo wa konde gang ameeleza kuwa hawezi kuimba kuhusu mpenzi wake wa zamani, kwa sababu heshima na upendo wake kwao umebadilika na kuwa wa kifamilia. “KAMA NIKIMUIMBAJI X WANGU YEYOTE HAITOKUWA KAZI KUBWA KAMA MNAVYO DHANI! ILA NDO SIWEZI UPENDO WANGU UNAUPITILIZA NA KUWA KAMA KAKA MDOGO KWENYE FAMILIA. SO HATA TIKTOKA TUMESHINDWA HESHIMA NA ADABU YANGU KWENYE FAMILIA INABAKI PALE PALE, SO HATA AKINIUNIKA TUNAKUTANA KWENYE VIKAO VYA FAMILIA 😂.” Ameeleza. Pia, ameongeza kuwa wimbo huu ni kwa niaba ya watu wote walioachana na wapenzi wao, sio maisha yake binafsi pekee. “HIZI GOMA NI KWA NIABA YA XXX WOTE DUNIANI, MSINIPENDE KUAONA MNAYAWATA WAKWENU TUU KISA NIMEMBA MTE 😂 SEE YOU ON FRIDAY KUMEKUCHA!!!”, Ameongeza Harmonize.

Read More
 Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Wakati bado Bahati anaendelea kufanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Nowe Sweety,’ ameonyesha kuwa hataki kulaza damu kuhusu muziki,ameonekana ujio wa kazi yake mpya na msanii wa BongoFleva Harmonize. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bahati amepost picha akiwa na Harmonize na kuandika ‘2023 are You Ready for Us??? Brother  @Harmonize_tz ‘ na Harmonize akajibu kwa kuandika ‘SEND IT BRO I HAVE ONLY ONE WATSP NUMBER LOVE YOU NO MARA WAA !!! GETO BOYS ‘. Iwapo Bahati atafanikiwa kuachia wimbo wake na Harmonize atakuwa ameongeza orodha ya wasanii wa Bongoflava aliofanya nao kazi ikizingatiwa kuwa ana kazi ya pamoja na  Rayvanny, Mbosso na Aslay.

Read More
 Harmonize amkingia Diamond kwa kukosa show nchini Rwanda

Harmonize amkingia Diamond kwa kukosa show nchini Rwanda

Msanii Harmonize ameonyesha uzalendo kwa kumuombea msamaha msanii mwenzake Diamond Platnumz huko nchini Rwanda kutokana na Diamond kushindwa kufika kwenye show aliyotakiwa aifanye December 23 mwaka jana jijini Kigali, pale BK Arena. Kwenye mahojiano aliyoyafanya na RwandaTV Harmonize mwishoni alikuwa akipewa shukurani ya kufika kwenye kipindi na akatumia nafasi hiyo kuomba msamaha kwa wanyarwanda kwa niaba ya Diamond Platnumz kwa kutokufika kwenye show. Kwenye maelezo yake alisema kuwa hajui tatizo lilikuwa nini lakini kwenye maisha huwezi kujua nini kinatokea hivyo aliwaomba wamsamehe ili tuupeleke muziki wetu wa Afrika Mashariki kwenye hatua inayofuata, japo hakulitaja jina la diamondplatnumz moja kwa moja hali iliyomfanya mtangaazaji kumuuliza ‘Unamaanisha Diamond?” na Harmonize alijibu “yeah yeah”.

Read More
 Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Msanii wa Bongofleva, Rayvanny ametapika nyongo kumuhusu Harmonize, ni vita ya maneno ambayo ilianzia kwenye insta story kufuatia Harmonize kuwataka wasanii kuacha kuimba nyimbo za kutukuza pombe kwani zinaharibu Jamii. Tamko hili lilimgusa Rayvanny ambaye aliibuka na kumjibu Harmonize kwamba, asiongee chochote kuhusu nyimbo za pombe kwani hajawahi kufanya nyimbo za aina hiyo na zikafanya vizuri. Rayvanny hakuishia hapo, ni kama alikuwa amekaa na kitu rohoni kwa muda mrefu sana kuhusu Harmonize. Kupitia insta story yake usiku wa kuamkia leo ameongea mengi ikiwemo kumchana Harmonize kuwa ana roho mbaya, mbinafsi kwa kutaka kumfunga Jela kufuatia lile sakata la mtoto wa Kajala, Paula. Mmiliki huyo wa Next Level Music, aliendelea kutema nyongo kwa kusema amemsaidia Harmonize kimuziki ikiwemo kumuandikia verse nzima kwenye wimbo wa “Paranawe” na “Happy Birthday” lakini pia alifunguka kwamba, ameilipa lebo ya WCB shillingi milioni 53 za Kenya lakini hakuwahi kufungua mdomo wake kuongea.

Read More
 Harmonize awaasa wasanii kupunguza nyimbo za pombe

Harmonize awaasa wasanii kupunguza nyimbo za pombe

Msanii wa Bongo Fleva Harmonize amewashauri wasanii wenzake wapunguze kuimba nyimbo za pombe hasa mwezi huu wa januari. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema sio watu wote wanakunywa pombe ila nyimbo za kuhamasisha pombe zimekuwa nyingi sana. “Wasanii punguzeni nyimbo za pombe..msidhanii hii nchi kila mtu ni mlevi..Hata tunaokunywa juma 3 hatunywi tukizisikia nyimbo za pombe kama unatonesha kidonda!!! Hasa hasa JANUARRY hii”, Aliandika Instastory. Kauli hiyo ya mtu mzima Harmonize imeonekana kuzua hisia kinzani miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ambapo msanii mwenzake Rayvanny amelazimika kuingilia kati mjadala huo kwa kumtaka bosi huyo wa Konde Gang kukoma kuzungumzia masuala ambayo hayamhusu. “Huna Ngoma ya pombe uliowahi ku hit sasa utaongea nini kuhusu pombe shut the f****ck up #NITONGOZE VIDEO COMING SOON”, Aliandika instastory.

Read More
 Kajala sio meneja tena Konde Music Worldwide

Kajala sio meneja tena Konde Music Worldwide

Meneja wa Harmonize, Dk. Sebastian Ndege maarufu Jembe ni Jembe amefichua kuwa Kajala Msanja sio Meneja tena katika Lebo ya Konde Music Worldwide yake Harmonize. Hata hivyo, amesema Kajala ameendelea kuwa mwanafamilia na anaamini mahusiano yake na Harmonize hayajawahi kuharibu kazi. “Yeye ni mpenzi wa zamani wa msanii wangu ila sio sehemu ya Lebo, alikuwa Meneja lakini si Meneja tena kwa sababu mambo yalikuwa yanagongana, uhusiano, kazi, familia.” alisema. “Tunamheshimu na tunathamini mchango wake kwa Konde Gang na uhusiano aliojenga alipokuwa nasi. Tulifurahi.” alisisitiza Jembe.

Read More
 Harmonize amshukuru Sallam SK kumtaja namba 10 kwa wasanii waliofanya vizuri 2022

Harmonize amshukuru Sallam SK kumtaja namba 10 kwa wasanii waliofanya vizuri 2022

Hitmaker wa “Outside”, Msanii Harmonize ameshukuru meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK kwa kumuweka kwenye orodha ya wasanii waliofanya vizuri mwaka 2022. Kupitia insta story yake amemshukuru Sallam SK kwa kumtaja namba 10 katika list yake ambapo ameenda mbali zaidi na kujifananisha na mchezaji nyota Duniani, Lionel Messi ambaye huvaa jezi namba kumi mgongoni. “Thank You Kipara no Mara Waa!!!!. 10. MESSI+”, Ameandika. Siku ya jana Sallam SK alitoa list yake ya wasanii 10 wa Bongo Fleva waliofanya vizuri mwaka 2022, akiwapanga kuanzia nafasi ya 1 mpaka ya 10.

Read More
 Harmonize kutambulisha meneja na wasanii wapya Konde Gang

Harmonize kutambulisha meneja na wasanii wapya Konde Gang

Baada ya kuachana na aliyekuwa Meneja wake lakini pia mpenzi wake Kajala Frida , Msanii wa Bongofleva Harmonize ametangaza rasmi kutambulisha meneja wake mpya kama Suprise kwenye usiku wa Harmo-Night , show yake ya kufungia mwaka anayotarajia kuifanya siku ya tarehe 25 mwezi huu. Kupitia insta story, Harmonize amefunguka kuutumia usiku huo pia kutambulisha wasanii wengine wapya kwenye lebo ya Konde Gang. Lakini pia amedai kuwa ataitumia show yake ya Harmo Night 2022, kupima upendo na unafiki wa wasanii wenzie haswa aliofanya nao kazi ya pamoja na kuzalisha Hit songs. Harmonize amesema kuwa endapo wasanii hao watashindwa kununua meza kuelekea show yake hiyo basi ndio utakuwa mwisho wa yeye kuongea nao huku akisisitiza kuwa hata kama msanii ana show nje ya Dar es salaam basi anunue meza na kualika watu wake.

Read More
 Ngoma ya  Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya ‘Weed language’ ya staa wa muziki wa Bongo Fleva , Harmonize imerejeshwa tena katika mtandao wa Youtube wa msanii Konshens masaa kadhaa yaliyopita. Harmonize jana kupitia ukurasa wake wa kijamii wa instagram aliahidi atauondoa wimbo huo kwenye mitandao yote ya kijamii baada ya kukiri kuwa maudhui ya wimbo huo yanakiuka maadili, mila na desturi pamoja na miongozo ya mamlaka za serikali nchini Tanzania. Hata hivyo Harmonize alioundoa katika mtandao wake wa Youtube ila kwa sasa unapatikana katika chaneli ya Konshens aliyemshirikisha katika ngoma hiyo.

Read More
 Harmonize atangaza kuanza kutoza KSh. Millioni 5.2 kwa kolabo

Harmonize atangaza kuanza kutoza KSh. Millioni 5.2 kwa kolabo

Msanii wa Bongofleva Harmonize ameweka wazi rasmi kwa sasa anaanza kutoza kiasi cha KSh. Milioni 5.2 kwa ajili ya kufanya naye Kolabo, lakini sharti la kwanza wimbo uwe mkali. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram amekazia kwamba kuna mtu fulani atamtoza kiasi cha KSh. Milioni 26 atakapo hitaji kolabo naye. Lakini pia Harmonize amebainisha kwamba kama mwanamuziki hajatengeza hits zaidi ya 10 kwa mwaka 2022 asimuongeleshe, na hii ndio mood yake ya mwezi Disemba.

Read More
 Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Sallam SK amemjibu Harmonize kufuatia mashairi yake kwenye wimbo “Champion” alioshirikishwa na rapa Kontawa. Harmonize kwenye sehemu fupi ya wimbo huo aliimba kwamba, kwa sasa Konde Gang ni Jeshi la watu wawili akiwa na maana kwamba ni yeye na Ibraah pekee yaani baada Killy, Cheed na Anjella kujiondoa. Sallam ama Mendez leo Jumanne kupitia ukurasa wake wa Instagram amehoji kwamba, “Kwa hiyo kaua lebo kafungua kundi, wanajiita.. “Wagambo mtu mbili” au nimeelewa vibaya ” ameandika kupitia ukurasa wake. Utakumbuka tangu ameondoka WCB Wasafi, Harmonize hajawa na wakati mzuri na Lebo hiyo hasa Sallam SK ambaye mara kadhaa wameonekana kupisha kauli mtandaoni na hata walipokutana.

Read More