Harmonize amkingia Diamond kwa kukosa show nchini Rwanda

Harmonize amkingia Diamond kwa kukosa show nchini Rwanda

Msanii Harmonize ameonyesha uzalendo kwa kumuombea msamaha msanii mwenzake Diamond Platnumz huko nchini Rwanda kutokana na Diamond kushindwa kufika kwenye show aliyotakiwa aifanye December 23 mwaka jana jijini Kigali, pale BK Arena. Kwenye mahojiano aliyoyafanya na RwandaTV Harmonize mwishoni alikuwa akipewa shukurani ya kufika kwenye kipindi na akatumia nafasi hiyo kuomba msamaha kwa wanyarwanda kwa niaba ya Diamond Platnumz kwa kutokufika kwenye show. Kwenye maelezo yake alisema kuwa hajui tatizo lilikuwa nini lakini kwenye maisha huwezi kujua nini kinatokea hivyo aliwaomba wamsamehe ili tuupeleke muziki wetu wa Afrika Mashariki kwenye hatua inayofuata, japo hakulitaja jina la diamondplatnumz moja kwa moja hali iliyomfanya mtangaazaji kumuuliza ‘Unamaanisha Diamond?” na Harmonize alijibu “yeah yeah”.

Read More
 Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Harmonize na Rayvanny watupiana maneno makali mtandaoni

Msanii wa Bongofleva, Rayvanny ametapika nyongo kumuhusu Harmonize, ni vita ya maneno ambayo ilianzia kwenye insta story kufuatia Harmonize kuwataka wasanii kuacha kuimba nyimbo za kutukuza pombe kwani zinaharibu Jamii. Tamko hili lilimgusa Rayvanny ambaye aliibuka na kumjibu Harmonize kwamba, asiongee chochote kuhusu nyimbo za pombe kwani hajawahi kufanya nyimbo za aina hiyo na zikafanya vizuri. Rayvanny hakuishia hapo, ni kama alikuwa amekaa na kitu rohoni kwa muda mrefu sana kuhusu Harmonize. Kupitia insta story yake usiku wa kuamkia leo ameongea mengi ikiwemo kumchana Harmonize kuwa ana roho mbaya, mbinafsi kwa kutaka kumfunga Jela kufuatia lile sakata la mtoto wa Kajala, Paula. Mmiliki huyo wa Next Level Music, aliendelea kutema nyongo kwa kusema amemsaidia Harmonize kimuziki ikiwemo kumuandikia verse nzima kwenye wimbo wa “Paranawe” na “Happy Birthday” lakini pia alifunguka kwamba, ameilipa lebo ya WCB shillingi milioni 53 za Kenya lakini hakuwahi kufungua mdomo wake kuongea.

Read More
 Harmonize awaasa wasanii kupunguza nyimbo za pombe

Harmonize awaasa wasanii kupunguza nyimbo za pombe

Msanii wa Bongo Fleva Harmonize amewashauri wasanii wenzake wapunguze kuimba nyimbo za pombe hasa mwezi huu wa januari. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema sio watu wote wanakunywa pombe ila nyimbo za kuhamasisha pombe zimekuwa nyingi sana. “Wasanii punguzeni nyimbo za pombe..msidhanii hii nchi kila mtu ni mlevi..Hata tunaokunywa juma 3 hatunywi tukizisikia nyimbo za pombe kama unatonesha kidonda!!! Hasa hasa JANUARRY hii”, Aliandika Instastory. Kauli hiyo ya mtu mzima Harmonize imeonekana kuzua hisia kinzani miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ambapo msanii mwenzake Rayvanny amelazimika kuingilia kati mjadala huo kwa kumtaka bosi huyo wa Konde Gang kukoma kuzungumzia masuala ambayo hayamhusu. “Huna Ngoma ya pombe uliowahi ku hit sasa utaongea nini kuhusu pombe shut the f****ck up #NITONGOZE VIDEO COMING SOON”, Aliandika instastory.

Read More
 Kajala sio meneja tena Konde Music Worldwide

Kajala sio meneja tena Konde Music Worldwide

Meneja wa Harmonize, Dk. Sebastian Ndege maarufu Jembe ni Jembe amefichua kuwa Kajala Msanja sio Meneja tena katika Lebo ya Konde Music Worldwide yake Harmonize. Hata hivyo, amesema Kajala ameendelea kuwa mwanafamilia na anaamini mahusiano yake na Harmonize hayajawahi kuharibu kazi. “Yeye ni mpenzi wa zamani wa msanii wangu ila sio sehemu ya Lebo, alikuwa Meneja lakini si Meneja tena kwa sababu mambo yalikuwa yanagongana, uhusiano, kazi, familia.” alisema. “Tunamheshimu na tunathamini mchango wake kwa Konde Gang na uhusiano aliojenga alipokuwa nasi. Tulifurahi.” alisisitiza Jembe.

Read More
 Harmonize amshukuru Sallam SK kumtaja namba 10 kwa wasanii waliofanya vizuri 2022

Harmonize amshukuru Sallam SK kumtaja namba 10 kwa wasanii waliofanya vizuri 2022

Hitmaker wa “Outside”, Msanii Harmonize ameshukuru meneja wa Diamond Platnumz, Sallam SK kwa kumuweka kwenye orodha ya wasanii waliofanya vizuri mwaka 2022. Kupitia insta story yake amemshukuru Sallam SK kwa kumtaja namba 10 katika list yake ambapo ameenda mbali zaidi na kujifananisha na mchezaji nyota Duniani, Lionel Messi ambaye huvaa jezi namba kumi mgongoni. “Thank You Kipara no Mara Waa!!!!. 10. MESSI+”, Ameandika. Siku ya jana Sallam SK alitoa list yake ya wasanii 10 wa Bongo Fleva waliofanya vizuri mwaka 2022, akiwapanga kuanzia nafasi ya 1 mpaka ya 10.

Read More
 Harmonize kutambulisha meneja na wasanii wapya Konde Gang

Harmonize kutambulisha meneja na wasanii wapya Konde Gang

Baada ya kuachana na aliyekuwa Meneja wake lakini pia mpenzi wake Kajala Frida , Msanii wa Bongofleva Harmonize ametangaza rasmi kutambulisha meneja wake mpya kama Suprise kwenye usiku wa Harmo-Night , show yake ya kufungia mwaka anayotarajia kuifanya siku ya tarehe 25 mwezi huu. Kupitia insta story, Harmonize amefunguka kuutumia usiku huo pia kutambulisha wasanii wengine wapya kwenye lebo ya Konde Gang. Lakini pia amedai kuwa ataitumia show yake ya Harmo Night 2022, kupima upendo na unafiki wa wasanii wenzie haswa aliofanya nao kazi ya pamoja na kuzalisha Hit songs. Harmonize amesema kuwa endapo wasanii hao watashindwa kununua meza kuelekea show yake hiyo basi ndio utakuwa mwisho wa yeye kuongea nao huku akisisitiza kuwa hata kama msanii ana show nje ya Dar es salaam basi anunue meza na kualika watu wake.

Read More
 Ngoma ya  Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya Harmonize ‘Weed Language’ yarejeshwa Youtube

Ngoma ya ‘Weed language’ ya staa wa muziki wa Bongo Fleva , Harmonize imerejeshwa tena katika mtandao wa Youtube wa msanii Konshens masaa kadhaa yaliyopita. Harmonize jana kupitia ukurasa wake wa kijamii wa instagram aliahidi atauondoa wimbo huo kwenye mitandao yote ya kijamii baada ya kukiri kuwa maudhui ya wimbo huo yanakiuka maadili, mila na desturi pamoja na miongozo ya mamlaka za serikali nchini Tanzania. Hata hivyo Harmonize alioundoa katika mtandao wake wa Youtube ila kwa sasa unapatikana katika chaneli ya Konshens aliyemshirikisha katika ngoma hiyo.

Read More
 Harmonize atangaza kuanza kutoza KSh. Millioni 5.2 kwa kolabo

Harmonize atangaza kuanza kutoza KSh. Millioni 5.2 kwa kolabo

Msanii wa Bongofleva Harmonize ameweka wazi rasmi kwa sasa anaanza kutoza kiasi cha KSh. Milioni 5.2 kwa ajili ya kufanya naye Kolabo, lakini sharti la kwanza wimbo uwe mkali. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram amekazia kwamba kuna mtu fulani atamtoza kiasi cha KSh. Milioni 26 atakapo hitaji kolabo naye. Lakini pia Harmonize amebainisha kwamba kama mwanamuziki hajatengeza hits zaidi ya 10 kwa mwaka 2022 asimuongeleshe, na hii ndio mood yake ya mwezi Disemba.

Read More
 Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa Diamond, Sallam SK ajibu disstrack ya Harmonize

Meneja wa mwanamuziki Diamond Platnumz, Sallam SK amemjibu Harmonize kufuatia mashairi yake kwenye wimbo “Champion” alioshirikishwa na rapa Kontawa. Harmonize kwenye sehemu fupi ya wimbo huo aliimba kwamba, kwa sasa Konde Gang ni Jeshi la watu wawili akiwa na maana kwamba ni yeye na Ibraah pekee yaani baada Killy, Cheed na Anjella kujiondoa. Sallam ama Mendez leo Jumanne kupitia ukurasa wake wa Instagram amehoji kwamba, “Kwa hiyo kaua lebo kafungua kundi, wanajiita.. “Wagambo mtu mbili” au nimeelewa vibaya ” ameandika kupitia ukurasa wake. Utakumbuka tangu ameondoka WCB Wasafi, Harmonize hajawa na wakati mzuri na Lebo hiyo hasa Sallam SK ambaye mara kadhaa wameonekana kupisha kauli mtandaoni na hata walipokutana.

Read More
 Mwanamuziki wa Bongofleva H. Baba amtolea uvivu Harmonize kwa kumuiga Wizkid

Mwanamuziki wa Bongofleva H. Baba amtolea uvivu Harmonize kwa kumuiga Wizkid

Msanii wa Bongofleva H. Baba amedai kitendo cha Harmonize kumchagua Kajala kuwa Meneja wake ni matokeo ya kumuiga Wizkid ambaye mke wake, Jada P ndiye Meneja wake. H. Baba amesema Meneja na mahusiano ni vitu viwili tofauti, huwezi kuvichanganya na kupata matokeo mazuri na pengine ndio sababu ya baadhi ya wasanii kuondoka Konde Music. “Wanataka kuiga kwa Wizkid, hawawezi. Meneja au mke wa Wizkid alikuwa anamsimamia Chris Brown, kwa hiyo kuja kumsimamia Wizkid ni jambo jepesi kwa sababu ana uzoefu, sasa huyu dada yetu hana uzoefu wa hicho” amesema H. Baba. Utakumbuka tangu Kajala Masanja amekuwa Meneja wa Konde Music, wasanii watatu, Cheed, Killy na Anjella wameachana na lebo hiyo.

Read More
 Mchumba wa Harmonize, Kajala Masanja athibitisha kuwa mjamzito

Mchumba wa Harmonize, Kajala Masanja athibitisha kuwa mjamzito

Mchumba wa msanii Harmonize, Kajala Masanja amewafunga midomo walimwengu mara baada ya kuthibitisha kuwa ana ujauzito wa Bosi wa Konde Gang. Kupitia instastory yake ameposti kipande cha video akilishika tumbo lake linaloonekana ni mjamzito na kuandika; “I can’t wait…” ujumbe ambao umewaaminisha mashabiki kuwa kweli ni mjamzito. Hata hivyo wajuzi wa mambo kwenye mitandao ya kijamii wamepinga taarifa hiyo huku wakihoji kuwa sio tumbo la Kajala ambalo linaonekana kwenye video hiyo bali inaweza ikawa ni Ujauzito wa mtu wao wa Karibu.

Read More
 Harmonize afunguka juu ya maendeleo ya album yake mpya “Boss Lady”

Harmonize afunguka juu ya maendeleo ya album yake mpya “Boss Lady”

Msanii kutokea Konde Music, Harmonize amesema ni nyimbo nne tu ndio zimesalia ili aweze kutoa albamu kwa ajili ya mchumba wake, Kajala. Hata hivyo, Harmonize amesema tayari kuna nyimbo kama nane zimetoka ambazo ni Deka, Nitaubeba, Mtaje, You, Utanikumbuka, Wote, Vibaya na Miss Bantu. Albamu hiyo Harmonize ameiipa jina la ‘The Bosslady’ na anafanya hivyo kuonyesha ni kiasi gani anampenda Kajala ambaye amemteua kuwa Meneja wake na Konde Music Worldwide kwa ujumla. Albamu hiyo itakuwa na nyimbo 12 na inatarajiwa kutoka Desemba mwaka huu ikiwa ni albamu ya nne kwa Harmonize baada ya Afro East, High School na Made For Us.

Read More