Msanii Justina Syokau Alalamika Kuhusu Baba wa Mtoto Wake Kukimbia Majukumu
Msanii wa Injili kutoka Kenya, Justina Syokau amedai kuwa baba wa mtoto wake, ambaye ni ndugu wa damu wa kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka, ameshindwa kabisa kutimiza wajibu wake wa kifamilia. Akipiga stori na Podcast ya Mwakideu Live, Justina amesema mwanaume huyo hajawahi kujitokeza kusaidia malezi ya mtoto wao, akisema hata mahitaji ya msingi kama sare za shule na vitabu vya masomo hayajawahi kutolewa. Hitmaker huyo wa 2020, ameeleza kuwa mzigo wote wa kumlea mtoto umebaki mabegani mwake licha ya familia hiyo kujulikana kuwa na ushawishi mkubwa kisiasa. Justina pia amefichua kuwa Kalonzo Musyoka mwenyewe aliwahi kukutana na mtoto huyo mara moja na kutoa mchango wa shilingi elfu mbili pekee, hatua aliyodai haikutosha ukizingatia mahitaji ya mtoto kwa ujumla.
Read More