Khaligraph Ajibu kwa Utani Madai ya Kuigiza Maisha na Muziki

Khaligraph Ajibu kwa Utani Madai ya Kuigiza Maisha na Muziki

Msanii nyota wa hip hop nchini Kenya, Khaligraph Jones, ameonekana kuguswa na kauli za mtangazaji Rapcha the Sayantist, aliyemshutumu vikali kwa kudai kuwa muziki wake na maisha yake yote ni ya kuigiza. Katika kujibu lawama hizo, Khaligraph ametumia ukurasa wake wa Instagram kwa mtindo wa utani, akionekana kugeuza matusi hayo kuwa fursa ya kumsaidia Rapcha kupata umaarufu zaidi. Amesisitiza kuwa kutajwa kwake ni njia rahisi ya kupata kiki, na akaenda mbali kwa kuwahimiza mashabiki wake wamfuate Rapcha mitandaoni. Pia ametoa dondoo kwamba anajiandaa kuachia freestyle mpya, hatua ambayo mashabiki wameihusisha na majibu ya muziki kwa ukosoaji aliopewa. Mashabiki mitandaoni wamegawanyika, baadhi wakiona kuwa Khaligraph ameonyesha busara kwa kutochukua mambo kwa hasira, huku wengine wakimtuhumu Rapcha kwa kutumia lugha ya matusi na kushusha heshima ya moja ya wasanii wakubwa zaidi wa hip hop Afrika Mashariki. Hayo yote yameibuka mara baada ya Rapcha kwenye moja ya Podcast kudai kuwa kila kitu kuhusu Khaligraph ni cha kubuni kuanzia lafudhi yake, madai ya kutoka Kayole, mtindo wa mavazi hadi muziki anaoutoa.

Read More
 Jaketi la Khaligraph Lapigwa Mnada kwa Dola 100

Jaketi la Khaligraph Lapigwa Mnada kwa Dola 100

Jamaa mmoja nchini Kenya ameibua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa anauza jaketi alilopewa na Rapa Khaligraph Jones, wakati wa onyesho lililofanyika Machakos. Kwa mujibu wa jamaa huyo, jaketi hilo ni zawadi ya moja kwa moja kutoka kwa Papa Jones. Hata hivyo, amesema sasa amelazimika kuliuza kwa bei ya dola 100 (takribani KSh 13,000) akieleza kuwa ana mahitaji ya kifedha. Taarifa hiyo imezua maoni tofauti mitandaoni. Baadhi ya mashabiki wameshangazwa na uamuzi wa kuuza zawadi ya msanii mkubwa kama Khaligraph, huku wengine wakisisitiza kuwa mara tu zawadi inapotolewa, mwenye kupokea ana uhuru wa kuamua atalifanyia nini. Mpaka sasa, Khaligraph Jones hajaweka wazi msimamo wake kuhusu suala hilo, na kuacha mashabiki wakijiuliza kama kweli jaketi hilo ni la ukweli au ni mbinu ya kutafuta kiki.

Read More
 Khaligraph Ageuza Kejeli Kuwa Faida Kupitia OG Omollo Sweatpants

Khaligraph Ageuza Kejeli Kuwa Faida Kupitia OG Omollo Sweatpants

Msanii wa Hip Hop nchini Kenya, Khaligraph Jones, ameonyesha ubunifu na ujasiri kwa kugeuza kejeli alizopokea kutoka kwa rapa Octopizzo kuwa fursa ya biashara. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Khaligraph alizindua Limited Edition OG Omollo Custom Sweatpants, hatua iliyowaacha mashabiki wake wakimpongeza kwa uamuzi wa kipekee. Khaligraph ambaye anafanya vizuri na single yake mpya “Confuse” amehitimisha ujumbe wake kwa kutumia hashtag maarufu #respecttheogs, ishara ya kuendeleza msimamo wake wa kudumisha heshima na ushawishi katika anga ya muziki wa rap nchini humo. Uamuzi huo ulionekana kama jibu la moja kwa moja kwa kejeli kutoka kwa rapa mwenzake, Octopizzo, ambaye alinukuliwa akisema “Kuna rapper flani huvaa sweatpants from January to December na timber ya yellow.” Badala ya kuchukua maneno hayo kwa njia hasi, Khaligraph aliuchukua mtindo huo na kuubadilisha kuwa bidhaa ya kibiashara, hatua iliyotafsiriwa na mashabiki kama “clap back” ya kishujaa. Mashabiki wengi walimsifu kwa ubunifu huo, wakisema ni mfano bora wa jinsi msanii anaweza kutumia ukosoaji kujinufaisha.

Read More
 Khaligraph Jones Atamani Kununua Tena Subaru Yake ya Zamani

Khaligraph Jones Atamani Kununua Tena Subaru Yake ya Zamani

Rapa Khaligraph Jones, ametangaza kuwa anatamani kununua tena gari lake la zamani aina ya Subaru Forester ambalo liliwahi kuwa sehemu ya maisha yake kabla ya kupata umaarufu mkubwa. Khaligraph ameeleza kupitia mitandao ya kijamii kuwa anataka kulipata tena Subaru hilo, akiwataka mashabiki wanaofahamu lilipo kumjulisha. Hatua hiyo imezua hisia tofauti mitandaoni, wengi wakikumbuka jinsi gari hilo lilivyokuwa sehemu ya safari yake ya muziki kabla ya kupata mafanikio makubwa Tangazo hili linakuja wiki chache baada ya rapa wa Marekani, Rick Ross, kusema bado anamiliki BMW iliyotumika kwenye video ya wimbo wake maarufu Hustlin’ zaidi ya miaka 15 iliyopita. Wadadisi wa muziki wanasema hatua ya Khaligraph huenda ni jaribio la kuonyesha kuthamini safari yake ya muziki na mafanikio aliyopata tangu siku za mwanzo.

Read More
 Khaligraph Jones Athibitisha Kufungwa kwa Mradi wa Khali Cartel

Khaligraph Jones Athibitisha Kufungwa kwa Mradi wa Khali Cartel

Msanii maarufu wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Khaligraph Jones, ametangaza kwamba msururu wake wa rap cypher unaotambulika kama Khali Cartel ulimalizika rasmi mwaka jana. Kupitia Instagram Stories, Khaligraph alijibu shabiki aliyemuuliza kuhusu hatma ya mradi huo, akieleza kuwa Khali Cartel ilitimiza lengo lake kuu la kukuza na kutambulisha wasanii chipukizi kwenye tasnia ya muziki. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2018, Khali Cartel imekuwa jukwaa muhimu kwa wasanii wachanga kuonesha umahiri wao wa kurap, huku ikichangia kwa kiasi kikubwa kugundua na kukuza vipaji vipya katika tasnia ya muziki wa hip hop nchini Kenya. Hata hivyo, Khaligraph hakubainisha iwapo ataanzisha mradi mpya wa aina hiyo, bali alichukua fursa hiyo kuwashukuru mashabiki na wasanii wote waliokuwa sehemu ya safari ya Khali Cartel hadi mwisho wake.

Read More
 Khaligraph Jones Ashinda Tuzo ya Best Lyricist in Africa, Awaangusha Mastaa Wakubwa

Khaligraph Jones Ashinda Tuzo ya Best Lyricist in Africa, Awaangusha Mastaa Wakubwa

Rapa nguli wa Kenya, Khaligraph Jones, ameweka historia kwa kutwaa tuzo ya Best Lyricist in Africa katika tuzo za mwaka huu za 2025 Africa Golden Awards, akiibuka mshindi mbele ya majina makubwa ya muziki barani Afrika. Katika kipengele hicho kilichoandaliwa kwa ushindani mkali, Khaligraph aliwashinda wasanii wakubwa kama Burna Boy (Nigeria), Sarkodie (Ghana), Nasty C (Afrika Kusini), MI Abaga, Olamide, Asake, Emtee, Cassper Nyovest, Stonebwoy, na wengine wengi waliokuwa wakimezewa mate kwa uwezo wao wa kishairi na ubunifu wa maneno. Tuzo hiyo ni ushindi mkubwa si tu kwa Khaligraph mwenyewe bali pia kwa tasnia ya muziki wa hip hop nchini Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla, huku mashabiki wakimpongeza kwa kuonyesha kuwa muziki wa Kenya una nafasi kubwa kwenye jukwaa la kimataifa. Kupitia mitandao ya kijamii, mashabiki wake walimiminika kwa pongezi, wengi wakisema ushindi huo ni wa haki kutokana na ustadi wake wa kubeba ujumbe mzito kwenye mistari na kujituma kwake kwenye sanaa. Khaligraph, anayefahamika pia kama Papa Jones, ameendelea kuwa na ushawishi mkubwa kwenye muziki wa hip hop Afrika, akiwakilisha Kenya kwa nguvu katika majukwaa ya kimataifa. Ushindi huu unakuja kama uthibitisho kuwa kazi yake ya muda mrefu na bidii imelipa. Tuzo za Africa Golden Awards hutambua vipaji bora kutoka bara la Afrika katika nyanja mbalimbali za burudani, na mwaka huu ushindani ulikuwa mkali kuliko wakati wowote.

Read More
 Khaligraph Jones Afichua Changamoto za Wasanii Waliochini ya Lebo

Khaligraph Jones Afichua Changamoto za Wasanii Waliochini ya Lebo

Rapa maarufu kutoka Kenya, Khaligraph Jones, ameibua mjadala mkali mtandaoni baada ya kudai kuwa wasanii wengi walioko chini ya lebo kubwa za muziki wanapitia hali ngumu kifedha licha ya kuonekana wanaishi maisha ya kifahari. Kupitia mitandao ya kijamii, Khaligraph alifichua kuwa licha ya kupokea ofa nyingi za kusaini mikataba na lebo mbalimbali, aliamua kusalia huru na kusimamia kazi zake mwenyewe. Anaeleza kuwa wasanii wengi wakubwa wapo kwenye madeni makubwa na kwamba uhuru wa kifedha ndio umemwezesha kuendelea vizuri bila presha ya mikopo au masharti magumu ya mikataba. Rapa huyo anasema kuwa anathamini uhuru wa kifedha kuliko mvuto wa mikataba inayokuja na majina makubwa lakini haina manufaa ya moja kwa moja. Anaeleza kuwa maisha yake ni ya amani kwa sababu anamiliki kile anachonacho na hana mzigo wa madeni unaomkosesha amani. “Wengi wao mnaowaona ni wakubwa, lakini wako kwa madeni makubwa sana. Wengine wanateseka kimyakimya. Mimi nilikataa hizo deals zote, niko huru, sina deni, na naball kwa amani na mali yangu,” alisema Khaligraph. Katika ujumbe huo, Khaligraph alionyesha pia matumaini ya kupata mafanikio zaidi na kuboresha maisha yake, akitaja magari ya kifahari kama sehemu ya malengo yake ya baadaye. Kauli zake zimezua mjadala miongoni mwa mashabiki na wadau wa muziki, wengi wakiona kuwa ni onyo kwa wasanii chipukizi wawe makini na mikataba wanayosaini. Khaligraph ameendelea kujijengea jina kama msanii anayejitegemea kupitia lebo yake ya Blue Ink, huku akiendelea kung’ara ndani na nje ya Kenya. Wakati baadhi ya mashabiki walimpongeza kwa msimamo wake, wengine walihisi kuwa sio rahisi kwa kila msanii kujisimamia bila msaada wa lebo kubwa. Hata hivyo, ujumbe wake umeibua mjadala mpana kuhusu changamoto za kifedha zinazowakumba wasanii licha ya umaarufu wao.

Read More
 Khaligraph Awatolea Uvivu Mashabiki Wanaomkosoa mtandaoni

Khaligraph Awatolea Uvivu Mashabiki Wanaomkosoa mtandaoni

Msanii maarufu wa muziki wa rap nchini Kenya, Khaligraph Jones, ameonyesha wazi kutoridhishwa na baadhi ya mashabiki wake ambao wamekuwa wakimpa ushauri wa namna anavyopaswa kuendesha kazi zake, hasa kuhusu maeneo ya kurekodia video zake. Kupitia ujumbe alioutoa mtandaoni, Khaligraph alieleza kuchoshwa na mashabiki wanaomshauri asirekodi video zake nyumbani kwake. Akiwa na msimamo mkali, alisema kuwa uamuzi wa kutumia nyumba yake kama sehemu ya kurekodia ni wa kimakusudi na una umuhimu wa kisanaa kwake.  “Wengi wenu mnasema nisifanye video nyumbani. Lakini nyumba yangu siilijenga kwa sababu gani? Kama si kuitumia kwa kazi zangu, ni kwa nini iwepo?” alisema Khaligraph. Rapa huyo alisisitiza kuwa hajawahi kuwa na matatizo ya bajeti au kutokuwa na nafasi ya kusafiri kwa ajili ya kurekodia, kwani tayari amefanya kazi katika nchi mbalimbali kama Nigeria, Marekani, na Afrika Kusini. “Suala si hela au uwezo wa kusafiri, ni chaguo la msanii. Wengine mnadhani mnaweza kuniambia nifanye nini na wapi. Weka ushauri huo kwa familia yako. Hapa tuko sawa,” aliongeza kwa ukali. Khaligraph, ambaye anajulikana kwa mtindo wake wa kusema ukweli bila kupindisha maneno, alihitimisha kwa kusema kwamba yeye si msanii wa kufuata shinikizo la mitandao ya kijamii, na ataendelea kufanya kile anachokiamini ni bora kwa muziki wake. Kauli hiyo imeibua hisia tofauti mtandaoni, baadhi ya mashabiki wakimuunga mkono kwa msimamo wake thabiti, huku wengine wakihisi kuwa alipaswa kuchukulia maoni hayo kwa mtazamo wa kujenga. Hili si tukio la kwanza kwa Khaligraph Jones kujibu mashabiki kwa sauti ya ukali. Akiwa miongoni mwa wasanii wanaojulikana kwa kusema ukweli bila kuficha, anaendelea kudhihirisha kuwa hatishwi na presha ya mitandao ya kijamii na anaamini katika maono yake mwenyewe kama msanii huru.

Read More
 Wasanii Wapaza Sauti Kufuatia Kujeruhiwa kwa Arrow Bwoy na Polisi Wakati wa Maandamano ya Amani

Wasanii Wapaza Sauti Kufuatia Kujeruhiwa kwa Arrow Bwoy na Polisi Wakati wa Maandamano ya Amani

Tukio la kujeruhiwa kwa msanii mashuhuri wa muziki wa Kenya, Arrow Bwoy, na polisi wakati wa maandamano ya amani limezua taharuki kubwa mitandaoni na kusababisha wasanii wenzake kuibua hisia kali za hasira na kukemea ukatili wa polisi. Arrow Bwoy alikuwa ameungana na rapa maarufu Khaligraph Jones pamoja na raia wengine katika maandamano ya kupinga ukatili wa vyombo vya usalama. Hata hivyo, maandamano hayo yaliishia kwa vurugu baada ya polisi kuwatawanya waandamanaji kwa kutumia mabomu ya machozi na nguvu kupita kiasi, hali iliyomwacha Arrow Bwoy amejeruhiwa. Khaligraph Jones alilalamikia tukio hilo kupitia mitandao ya kijamii, akisema kwa uchungu kuwa waandamanaji walikuwa wakifanya maandamano kwa amani, lakini walishambuliwa na polisi waliokuwa wakifyatua mabomu ya machozi moja kwa moja kwao. Alisema kitendo hicho ni mfano tosha wa ukatili wa polisi unaopaswa kukomeshwa mara moja. “Unapofanya maandamano ya amani halafu wanaanza kukupiga risasi za mabomu ya machozi… Kukomesha ukatili wa polisi nchini Kenya ni muhimu sana. #RespectTheOGs,”  Alielezea kwa uchungu Khaligraph Jones, ambaye alikuwa sambamba na Arrow Bwoy wakati wa maandamano hayo. Naye mchumba wa Arrow Bwoy na mama wa mtoto wake, Nadia Mukami, alionekana kuguswa sana na tukio hilo. Kupitia ujumbe alioutuma mtandaoni, aliandika kwa hasira kuwa polisi hawapaswi kumshika baba wa mtoto wake na kutaka ukatili huo ukome mara moja. “Nyinyi mafala msimguse baba watoto wangu!!!! #EndPoliceBrutality Nimejam ata!!!!!,” Aliandika kwa hasira Instagram. Kauli za wasanii hao zimeungwa mkono na maelfu ya mashabiki na wakenya wa kawaida, huku wengi wakitumia mitandao ya kijamii kulaani hatua ya polisi kutumia nguvu dhidi ya waandamanaji wa amani. Hashtag kama #EndPoliceBrutality na #RespectTheOGs zimeendelea kutrendi huku wito ukitolewa kwa serikali kuwajibisha maafisa waliohusika. Tukio hili limezua mjadala mpana kuhusu haki ya kuandamana na uhuru wa kujieleza nchini Kenya, huku wasanii wakionyesha kuwa wako tayari kusimama na wananchi kupigania haki na mabadiliko katika jamii.

Read More
 Rapa Khaligraph Jones Akanusha Madai ya Sabato Kuhusu Simu

Rapa Khaligraph Jones Akanusha Madai ya Sabato Kuhusu Simu

Rapa maarufu wa Kenya Khaligraph Jones amekanusha vikali madai yaliyotolewa na mchekeshaji na mtoaji maudhui mtandaoni Sabato, maarufu kama “Sauti ya Ground”, kuwa alikaidi ombi la msaada wa simu. Akizungumza kupitia mahojiano na SPM Buzz, Khaligraph alieleza kuwa hajawahi kupokea ombi hilo kutoka kwa Sabato, wala hajawahi kuonana naye ana kwa ana kwa lengo hilo.  “Anajua Sabato, buda buda, hujakuja ofisi yangu kuniambia nikununulie simu bro. Najua mambo zako bro, lakini hata kwa field yako, watu kama wewe wanahitajika kukamilisha mzunguko,” Alisema kwa msisitizo. Khaligraph aliongeza kuwa amekuwa akimnyamazia Sabato kwa muda mrefu, licha ya kusikia na kuona kauli mbalimbali mitandaoni. Hata hivyo, alisema amefikia hatua ya kuweka mambo wazi kwa sababu ya kuenea kwa maelezo yanayoweza kupotosha mashabiki. “Nilikuwa nimekunyamazia for the longest time. Najua mambo zako bro, lakini hakuna kitu Sabato. Hakuna mtu anaweza kusema kitu juu ya OG saa hii,” Aliongeza. Khaligraph aliweka wazi kuwa hajawahi kukataa kumsaidia mtu yeyote mwenye shida halisi, lakini hakubaliani na wale wanaotumia jina lake mitandaoni kwa kiki au kutafuta huruma ya mashabiki. Mpaka sasa, Sabato hajatoa tamko lolote rasmi kujibu kauli ya Khaligraph. Hata hivyo, mashabiki na wanamitandao wameanza kujadili suala hilo kwa makini, huku wengi wakisubiri iwapo Sabato atajibu au kuomba radhi.

Read More
 Muonekano Mpya wa Khaligraph Jones Bila Nywele Wazua Gumzo Mitandaoni

Muonekano Mpya wa Khaligraph Jones Bila Nywele Wazua Gumzo Mitandaoni

Rapa maarufu wa Kenya, Khaligraph Jones, amewashangaza mashabiki wake baada ya kufichua muonekano mpya bila nywele (bald look), hatua ambayo imezua gumzo mitandaoni. Kupitia mitandao ya kijamii, Khaligraph anayejulikana pia kama The OG, alichapisha picha na video zikimuonesha akiwa na kichwa kipara, mbali na mtindo wake wa kawaida wa nywele fupi au zilizonyolewa kwa ustadi. Licha ya kutoeleza sababu rasmi ya kubadilisha mtindo wake wa nywele, muonekano huo mpya umechukuliwa kama ishara ya mabadiliko katika mtazamo wake wa kisanii au mtindo wa maisha. Mashabiki wake wengi waliitikia kwa mshangao na maoni ya ucheshi, huku wengine wakimsifu kwa ujasiri na kuonekana mwenye mvuto zaidi katika muonekano huo mpya. Wapo pia waliodokeza kuwa huenda ni maandalizi ya mradi mpya wa muziki au muonekano maalum kwa video ya wimbo unaokuja. Khaligraph, ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kukuza muziki wa rap nchini Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla, anajulikana kwa mabadiliko ya mara kwa mara katika muonekano na ubunifu wa kisanaa, jambo linalomfanya aendelee kuwa gumzo kwenye tasnia ya burudani. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona iwapo muonekano huo mpya unaashiria mwanzo wa awamu mpya katika maisha yake ya muziki.

Read More
 Khaligraph Jones Ampongeza DJ Sadic kwa Kuongeza Uzito na Kuweka Bidii Gym

Khaligraph Jones Ampongeza DJ Sadic kwa Kuongeza Uzito na Kuweka Bidii Gym

Msanii maarufu wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Khaligraph Jones, amempongeza DJ Sadic kwa mabadiliko yake ya kimwili baada ya kuongeza uzito kutokana na juhudi zake za mara kwa mara kwenye mazoezi ya viungo. Katika mahojiano ya hivi karibuni, Khaligraph alielezea jinsi alivyoshtushwa na mabadiliko ya DJ Sadic, ambaye zamani alikuwa mwembamba kupita kiasi. “Kama DJ Sadic anaweza shona, kila mtu anaweza shona. Alikuwa amekonda anatoshana na uzi,” alisema Khaligraph kwa ucheshi, akimaanisha jinsi DJ huyo alikuwa mwembamba kabla ya kuanza mazoezi. Mkali huyo wa Ngoma ya Ting Bad Malo” aliendelea kueleza jinsi video za DJ Sadic zikimpa motisha ya kuendelea na mazoezi. “Huwa naona video zake nasema, huyu jamaa alikuwa amekonda anishinde mimi? Nakimbia zoezi.” Kauli hiyo imepokelewa kwa vicheko mitandaoni huku mashabiki wakimpongeza DJ Sadic kwa bidii zake na kumpongeza Khaligraph kwa kutambua mafanikio ya wengine. DJ Sadic, ambaye kwa muda mrefu amejulikana kwa kujituma kwenye tasnia ya muziki, sasa anaonekana pia kuwa mfano bora wa kujali afya ya mwili. Khaligraph, ambaye pia ni mpenzi wa mazoezi, ameendelea kuwa mhamasishaji mkubwa wa maisha ya kiafya miongoni mwa wasanii na mashabiki wake. Uhusiano huu wa motisha kati ya wasanii hawa wawili unadhihirisha umuhimu wa kujali afya hata katika maisha ya kazi yenye shughuli nyingi.

Read More