Msanii Sanaipei Tande Apinga Shinikizo la Kijamii Kuhusu Ndoa
Mwanamuziki na muigizaji wa Kenya Sanaipei Tande ameibua mjadala mtandaoni baada ya kueleza kuwa kuolewa sio lazima katika maisha. Akizungumza kwenye mahojiano ya hivi karibuni, mwimbaji huyo wa wimbo “Amina” amesema kuwa ingawa anaheshimu taasisi ya ndoa, anaamini si kila mtu amekusudiwa kufunga ndoa. Amefafanua kuwa ndoa ni kitu kizuri, lakini si kwa kila mtu, kwani baadhi ya watu hupata amani na utimilifu wao kupitia njia tofauti za maisha. Sanaipei ameongeza kuwa mara nyingi jamii huweka shinikizo kwa wanawake kuingia kwenye ndoa hata pale ambapo hawajajiandaa, jambo ambalo mara nyingine husababisha ndoa zisizo na furaha. Amesisitiza kuwa maamuzi kama hayo yanapaswa kufanywa kwa hiari na utayari wa mtu binafsi badala ya presha za kijamii. Kauli yake imepongezwa na mashabiki wengi ambao wamemsifu kwa ujasiri na mtazamo wa kweli kuhusu maisha ya wanawake. Wengi wameeleza kuwa Sanaipei amekuwa sauti ya busara katika jamii inayopima mafanikio kupitia ndoa.
Read More