Sauti Sol mbioni kuachia Album mpya

Sauti Sol mbioni kuachia Album mpya

Kundi la Sauti Sol limetangaza ujio wa Album hiyo ambayo kwa mujibu wao itaingiaa sokoni mwaka huu. Kundi hilo ambalo lilichukua mapumziko kwenye muziki kwa muda wa miaka 2 wamethibitisha taarifa hiyo kupitia ukurasa wao wa. “New year, New Album”, Waliandika Hata hivyo hawajaweka wazi ni lini hasa Album hiyo itaingia sokoni wala wasanii ambao watasikika kwenye album hiyo. Hii itakuwa ni album yao ya sita tangu waanze safari yao ya muziki miaka 17 iliyopita baada ya Midnight Train ya mwaka wa 2020. Album zingine ni kama Sol Filosofia (2011), Mwanzo (2009), Afrikan Sauce (2019), na Live and Die in Afrika (2015).

Read More
 Kundi la Sauti Sol lakashfiwa mtandaoni kwa kutetea watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja

Kundi la Sauti Sol lakashfiwa mtandaoni kwa kutetea watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja

Kundi la muziki nchini Sauti Sol limepata ukosoaji mkubwa kutoka kwa walimwengu kwenye mitandao ya kijamii baada ya kukemea vikali mauji ya mwanaharakati wa mapenzi ya jinsia moja Edwin Chiloba ambaye anadaiwa kuuwawa na mchumba wake Jackson Odhiambo. Kwenye posti ya Sauti Sol kwenye mtandao wa Twitter iliyokuwa ikikashifu jamii kwa mauji ya jamaa huyo, Wakenya wameomekana kukerwa na kitendo cha kundi hilo kuwalaumu wanajamii kwa masuala yasiokuwa na msingi. “It’s not the “Society” that did the heinous act. It’s her LGBT partner. Just a point of information.”, Aliandika mtumiaji mmoja wa Twitter Baadhi ya wakenya wameitaka Sauti Sol kukoma kuihusisha jamii na mauji ya mwendazake Chiloba na badala yake waelekeze lawama zao kwa mtuhumiwa aliyetekeza ukatili huo kwani chanzo cha mauji hayo yanakwenda kinyume na maadili ya kiafrika. “Why do gay people feel special. Let’s adhere to our traditions, norms and cultures. Before muanze kufundisha wengine tabia, jifundisheni”, Aliandika mtumiaji mmoja wa Twitter Hata hivyo wamewatolea uvivu wasanii wa Sauti Sol kwa kutetea maslahi ya watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsi moja huku wakisalia kimya kwa mauji ya kiholela ambayo yamekuwa yakifanyika nchini kila kuchao. “Bwana sauti sol stop advocating for LGBTQ nonsense. Watu wanakufa kule Kisii daily, kule Baringo watu wanakufa daily . Why point out only this!,” Aliandika mtumiaji mmoja wa Twitter.

Read More
 Sauti Sol watoa tamko baada ya tamasha la Sol Fest kupata ukosoaji mkubwa mtandaoni

Sauti Sol watoa tamko baada ya tamasha la Sol Fest kupata ukosoaji mkubwa mtandaoni

Kundi  la Sauti Sol limetoa tamko baada ya mashabiki kujitokeza kwenye mitandao ya kijamii na Kuwatupia lawama juu ya kuchelewa kupanda jukwaani kwenye Tamasha la Sol Festival lililofanyika wikiendi hii iliyopita nchini Kenya. Mashabiki walidai kuwa walikaa muda mwingi kuwasubiria mastaa hao licha ya kuwa tamasha lilikuwa ni lao lakini walifika Alfajiri na kutumbuiza kwa muda mchache kisha kuondoka jukwaani. Kupitia ukurasa wao wa Instagram sautisol, waliwashukuru mashabiki kwa kufanikisha tamasha hilo huku wakiahidi kufanya makubwa kwenye hafla ijayo ya Sol Fest. “Tunapenda kuwashukuru na kuwahakikishia mashabiki wetu wote kwamba tutajipanga vyema wakati mwingine na tuwaalika kutoa maoni ya kuboresha tamasha letu lijalo,” sehemu ya ujumbe wao umesomeka. Hata hivyo, baadhi ya mashabiki hawakuridhika na taarifa hiyo huku wakihoji ni kwa nini hawajaomba radhi kwa kitendo chao cha kufika jukwaani kwa kuchelewa. “Msamaha uko wapi?” aliuliza mtumiaji mmoja wa Instagram.

Read More
 Eric Omondi apigwa marufuku kuhudhuria tamasha la Sol Fest 2022

Eric Omondi apigwa marufuku kuhudhuria tamasha la Sol Fest 2022

Ikiwa imesalia siku chache kabla ya tamasha la Sol Fest , Msanii Bien ameweka mkazo juu ya msimamo wa Sauti Sol kutomruhusu mchekeshaji Eric Omondi kuhudhuria tamasha lao linalotarajiwa kufanyika Desemba 17 mwaka huu jijini Nairobi. Kupitia post yake aliyoiweka Instagram, Bien amewahakikishia mashabiki watakao hudhuria tamasha la Sol Fest kwamba Eric Omondi hatoruhusiwa kamwe kuingia kwenye tamasha hilo. Bien pia amedai kuna uwezekano mkubwa Eric Omondi akatumia janja janja za kila aina kuzamia kwenye tamasha hilo, lakini hatofanikiwa kutokana na ulinzi madhubuti utakao wekwa. Video Clip ya hivi karibuni ikimuonyesha Eric Omondi akiongea na waandishi wa habari kuhusu kuchukiwa na wasanii wengi nchini, inasadikika ndio chanzo cha zuio hilo kutoka kwa wana Sauti Sol. Omondi kwenye mahojiano hayo alidai ana maadui wengi sana hasa wasanii, hivyo kila tamasha atakalo kuwa akihudhuria basi atakuwa na ulinzi mkubwa wa watu na mbwa, akilitolea mfano tamasha la Sol Fest kuwa atahudhuria tamasha hilo akiwa na idadi ya mbwa 20.

Read More
 Sauti Sol waweka wazi pesa wanazotoza makampuni kutumia nyimbo zao kwa matangazo

Sauti Sol waweka wazi pesa wanazotoza makampuni kutumia nyimbo zao kwa matangazo

Wasanii wa kundi la Sauti sol wameweka wazi kiasi cha pesa wanacholipishwa kwa makampuni ambayo yanalenga kutumia nyimbo zao kwenye shughuli za kibiashara. Kwenye mahojiano na Ayo TV wasanii hao wakiongozwa na Bien Aime Baraza amesema wanatoza shillingi millioni 12 kwa matangazo huku akibainisha kuwa hawalipishi mashabiki wanaotumia nyimbo zao kwa ajili ya kujiburudisha. Lakini pia wamezungumzia umuhimu wa wasanii wa Afrika Mashariki kuwa na umoja kwenye suala kuupeleka muziki wa ukanda huu kimataifa kwa kuwataka washirikiana kwenye nyimbo zao kama njia moja ya kubadilisha mashabiki. Hata hivyo wamedokeza ujio wao mpya kama kundi kwa kuwataka mashabiki wakae mkao wa kupokea kazi zao mpya ikizingatiwa kuwa wana mpango wa kuachia album mpya mwakani (2023). Utakumbuka mara ya mwisho wasanii wa sauti sol kufanya kazi pamoja ilikuwa mwaka 2020 kupitia Album yao ya Midnight Train.

Read More
 Bien wa Sauti Sol ajibu madai ya Crystal Asige kufungua kesi mahakamani dhidi ya Sol Generation

Bien wa Sauti Sol ajibu madai ya Crystal Asige kufungua kesi mahakamani dhidi ya Sol Generation

Mwimbaji wa Sauti Sol amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya aliyekuwa msanii wa Sol Generation Crystal Asige kuwasilisha kesi mahakamani dhidi ya bendi hiyo maarufu kwa kukiuka mkataba wake. Akizungumza na Mpasho, Bien amesema bendi ya Sauti Sol iko tayari kukutana na seneta huyo mteule ambaye anawakilisha watu wanaoishi na ulemavu, mahakamani kupata mwanga kuhusu mgogoro unaozingira mkataba wake na lebo ya Sol Generation. “Tukutane kortini na kuweka hati zetu zote mezani. Tunaweza tu kufuata njia aliyochagua. Masuala hayo yanaweza kushughulikiwa vyema mahakamani kama alivyofanya,” Bien alisema. Kwa mujibu wa nyaraka za mahakama, Asige anaitaka mahakama kuwashurutisha wasanii wa Sauti Sol kuweka wazi kiasi cha pesa ambacho walipata kutoka kwa nyimbo alizoshirikisha tangu mwaka 2019. Nyimbo hizo ni pamoja na Lenga, Extravaganza, Ukiwa Mbali, Intro na Favourite Song. Lakini pia anaitaka mahakama kuagiza kundi la Sauti Sol kumlipa fidia huku akisisitiza wawasilishe taarifa zote za leseni kuhusu nyimbo alizoshirikishwa. Crystal Asige ameishtaki Sol Generation Records Limited, Bien-Aime Baraza, Polycarp Otieno, Willis Chimano, Delvin Mudigi na KLM Royal Dutch Airlines Kenya.

Read More
 Savara wa Sauti Sol atangazwa balozi mpya wa kinywaji cha Kenya Cane

Savara wa Sauti Sol atangazwa balozi mpya wa kinywaji cha Kenya Cane

Msanii wa Sauti Sol, Savara ametangazwa kuwa balozi mpya wa knywaji cha Kenya Cane Kupitia ukurasa wake wa Instagram Savara amesema ni jambo la faraja kufanya kazi na Kenya Cane kwani huo ni mwanzo wa ushirikiano mzuri kati yake na kampuni hiyo. Lakini pia ameishukuru uongozi wake pamoja na wadau wote waliofanikisha dili hilo huku akiahidi kuiongezea kampuni hiyo mauzo kutokana na ushawishi kwenye jamii. “I have worked hard to bring out my genius through art. I am on my journey to more greatness and I am proud to partner with Kenya Cane as the Official Brand Ambassador. I appreciate all parties that made this possible. I love my team. Now to more amazing art. Twende kazi #TheGreatsToastTwice”, Ameandika Instagram Hata hivyo Kampuni ya Kenya Cane imesema imeingia mkataba na Savara kwa kuwa wanaamini atasaidia kuzinyanyua bidhaa za kampuni hiyo kuwafikia wateja wengi.

Read More
 Bien awapa somo wasanii wa Kenya jinsi ya kukuza muziki wao

Bien awapa somo wasanii wa Kenya jinsi ya kukuza muziki wao

Mwanakikundi wa Sauti Sol, Bien amekanusha madai yaliyoibuliwa na mchekeshaji Eric Omondi kuwa siri yake ya kuingia kwenye chati za Apple Music imetokana na kiki kwenye muziki wake. Bien amesema hajawahi tengeneza matukio kwa ajili ya kutangaza muziki wake huku akisema mafanikio yake yamechangiwa na kujituma kwenye suala la kutoa muziki mzuri. Msanii huyo ametoa changamoto kwa wasanii kuacha kutengeneza matukio yakuchafuana mtandaoni kwa lengo la kujitafuatia umaarufu na badala yake wawekeze muda wao kutoa muziki mzuri. Bien ni msanii pekee kutoka Kenya aliyefanikiwa kuingiza nyimbo mbili kwenye chati za Apple Music Top 100. Nyimbo hizo ni pamoja na; Inauma ambayo ilikamata nafasi ya 40 huku “Dimension” aliyomshirikisha Fully Focus ikikamata nafasi ya 87.

Read More
 SAUTI SOL WATAJWA WASANII VINARA KWENYE TAMASHA LA AFROPALOOZA NCHINI UGANDA

SAUTI SOL WATAJWA WASANII VINARA KWENYE TAMASHA LA AFROPALOOZA NCHINI UGANDA

Baada ya kutumbuiza kwenye michuano ya Kikapu maarufu kama Basketball Africa nchini Rwanda wiki moja iliyopita, kundi la sauti sol limetajwa kama wasanii vinara kwenye uzinduzi wa tamasha la Afropalooza oktoba 9 mwaka huu nchini uganda. Wasanii wengine watakaowasha moto wa burudani siku hiyo ni pamoja na, Cindy, Lilian Mbabazi, Spice Diana, Maurice Kirya, Ykee Benda, Winnie Nwagi, Vinka, Navio. Tamasha la Afropalooza ambalo litafanyika kati ya tarehe 7 na 9 Oktoba katika ukumbi wa Lugogo Cricket Oval, jijini Kampala litawaleta pamoja zaidi ya wasanii 60.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AWATOLEA UVIVU WANAOKOSOA SERIKALI

BIEN WA SAUTI SOL AWATOLEA UVIVU WANAOKOSOA SERIKALI

Msanii wa Sauti Sol, Bien Aime Baraza ameonekana kuchukizwa na kitendo cha baadhi ya watu kuiombea serikali iweze kufeli kwenye utendaji kazi wake ili wapate maneno ya kuwachamba waliochagua uongozi wa sasa. Kupitia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram hitmaker huyo wa “Inauma” amewashangaa wanaoendeleza tabia hiyo mitandaoni kwa kusema kuwa huo ni ushamba uliopitiliza ikizingatiwa kuwa msimu wa siasa ulikamilika. Bien ameenda mbali zaidi na kuwataka wanaoeneza propaganda mtandaoni kuacha kadhia hiyo na badala yake wazipambanie familia zao, kwani zama za kuwazia serikali mabaya zimepitwa na wakati. Bien amekuwa moja kati ya wasanii ambao wamekuwa mstari wa mbele kuzungumzia masuala ya siasa bila uwoga wowote, utakumbuka juzi kati alishinikiza serikali kupunguza bei ya unga wa sima kwa kuwa wakenya wengi wanapitia wakati mgumu kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha.

Read More
 BIEN AFUNGUKA KUHUSU WASANII WA KIGENI KUTUMBUIZA KENYA

BIEN AFUNGUKA KUHUSU WASANII WA KIGENI KUTUMBUIZA KENYA

Msanii wa Sauti Sol Bien Aime Baraza amefunguka kuhusu suala la wasanii wa mataifa mengine kupewa kipau mbele kwenye hafla za kisiasa hapa nchini Kenya. Akipiga stori na Mpasho, Bien amesema wasanii wa kigeni wanapotumbuiza nchini ni faida kwa wasanii wa ndani kwa kuwa wasanii wa Kenya pia hupokea upendo wanaposafiri nje ya nchi. Mkali huyo wa ngoma ya “Inauma” ametaka wasanii wa kigeni kuruhusiwa kutumbuiza nchini bila kubaguliwa huku akiwataka wanaoshinikiza wasanii hao kupigwa marufuku kwenye majukwaa ya muziki nchini kuacha ubinafsi. Katika hatua nyingine amempongeza aliyekuwa msanii wa Sol Generation Crystal Asige kwa kuteuliwa kama Seneta anayewakilisha watu wanaoishi na changamoto ya ulemavu nchini. Bien amemtaja Crystal kama mwanamke mwenye akili sana huku akisema kwamba ana uhakika atawatumikia watu hao kwa uadilifu kwani ni jambo ambalo amekuwa akiliota kwa kipindi kirefu.

Read More
 BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

BIEN WA SAUTI SOL AWATAKA WASANII WA KENYA KUIMBA NYIMBO ZA KIINGEREZA

Mwanamuziki wa Sauti Sol, Bien ametoa changamoto kwa wasanii nchini kuanza kutumia lugha ya kiingereza kwenye nyimbo zao ili muziki wa Kenya uweze kufika mbali zaidi. Bien amesema licha ya wasanii wa Kenya kutoa muziki mzuri wengi wao wamekuwa wakitumia lugha ya Sheng kwenye nyimbo zao jambo analosema limewafanya wasanii kushindwa kutanua wigo wa muziki wao kimataifa. Katika hatua nyingine Bien amekiri kuwa hakuwa anajitambua kimuziki kabla ya wasanii wa kundi la Sauti Sol kuanza kufanya kazi zao kama wanamuziki wa kujitegemea. Hitmaker wa “Inauma” amesema amejifunza mambo mengi kama msanii huru ikiwemo kutayarisha na kuandilka nyimbo zake mwenyewe.

Read More