Ogier Aandika Historia Ueno Rally del Paraguay

Ogier Aandika Historia Ueno Rally del Paraguay

Bingwa mara nane wa dunia katika mbio za magari za WRC, Sebastien Ogier, aliibuka mshindi wa mkondo wa Ueno Rally del Paraguay uliomalizika Jumapili usiku, na kuiweka kampuni ya Toyota kwenye ramani kwa mara nyingine tena. Ushindi huo ulimfanya Ogier kuifikisha Toyota jumla ya ushindi 102 kwenye historia ya mashindano ya WRC rekodi inayolingana na ile ya kampuni ya Citroen. Licha ya kukumbwa na changamoto kadhaa, hasa Ijumaa alipoteza takribani sekunde 40 baada ya gari lake kukosa pumzi kwenye gurudumu, Ogier aliweza kurejea kwa kishindo na kumaliza mbio akiwa kileleni. Huu ni ushindi wake wa 18 akiwa na Toyota, na kwa mafanikio haya, anakuwa dereva aliyeiletea kampuni hiyo ushindi mwingi zaidi akivunja rekodi aliyokuwa akiishikilia kwa pamoja na Kalle Rovanperä. Katika ushindani mkali wa mkondo huo, tatizo la gari kwenye awamu ya mwisho ya Wolf Power lilimwangusha Adrien Fourmaux, ambaye alishuka hadi nafasi ya nne. Nafasi ya pili ilichukuliwa na Elfyn Evans huku Thierry Neuville akifunga tatu bora kwa kumaliza katika nafasi ya tatu.

Read More