Mchekeshaji Terence Creative Aomba Radhi Jamii ya Kisii kwa Matamshi ya Chuki 

Mchekeshaji Terence Creative Aomba Radhi Jamii ya Kisii kwa Matamshi ya Chuki 

Mchekeshaji kutoka Kenya Terence Creative amelazimika kuomba radhi jamii ya Kisii baada ya kutoa matamshi yaliyotafsiriwa kuwa ya chuki na kikabila kupitia ukurasa wake wa Facebook. Terence alizua mjadala mkali mtandaoni baada ya kuchapisha ujumbe unaodaiwa kumlenga aliyekuwa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i, akionekana kufanya utani kuhusu uwezekano wa kiongozi huyo kushinda urais mwaka 2027. Chapisho hilo liliwakasirisha baadhi ya wananchi, hususan kutoka jamii ya Kisii, waliolitafsiri kama kejeli na isiyoonyesha heshima kwa jamii nzima pamoja na viongozi wake. Baada ya wimbi la ukosoaji kuongezeka, mchekeshaji huyo alilazimika kufuta chapisho hilo na kuomba msamaha hadharani kwa jamii ya Kisii, akieleza hakuwa na nia mbaya wala dhamira ya kuudhi jamii ya Kisii. Terrence amesema kuwa ujumbe huo ulikuwa sehemu ya utani wa kawaida, lakini ukachukuliwa vibaya, akisisitiza kwamba anaipenda na kuithamini jamii hiyo pamoja na viongozi wake.

Read More
 Terence Creative Afunguka Kuhusu Mapambano Dhidi ya Uraibu

Terence Creative Afunguka Kuhusu Mapambano Dhidi ya Uraibu

Mchekeshaji wa Kenya, Terence Creative, ameweka wazi safari yake ya kupambana na uraibu wa vileo, akifichua jinsi alivyoingia katika wakati mgumu maishani mwake kabla ya kurejea katika mstari sahihi. Akiangazia kipindi hicho kigumu, Terence amesema changamoto za uraibu wa pombe na uvutaji sigara zilimpelekea kupoteza mwelekeo na matumaini, lakini hakubaki peke yake. Amemshukuru mkewe Milly Chebi ambaye kwa wakati huo alikuwa mpenzi wake kwa kusimama naye na kumsaidia kuvuka kipindi cha giza katika maisha yake. Terence ameeleza kuwa upendo na uvumilivu wa mkewe ndiyo uliokuwa nguzo muhimu ya safari yake ya kupona na kupata nafasi mpya ya kuanza upya. Aidha, ametumia hadithi yake kuhamasisha wengine wanaokabiliwa na changamoto za uraibu kutafuta msaada na kutokata tamaa. Hata hivyo ametoa ushauri kwa vijana, akiwahimiza kufanya maamuzi sahihi wanapochagua wapenzi. Amesisitiza kuwa si kila mtu anaweza kusimama na mpenzi wake katika nyakati ngumu, hivyo vijana wanapaswa kuchukua tahadhari na kuchagua wenza watakaowaunga mkono kwa dhati.

Read More
 Terence Creative Atoa Ushauri kwa Wasanii Kuhusu Maisha ya Baada ya Muziki

Terence Creative Atoa Ushauri kwa Wasanii Kuhusu Maisha ya Baada ya Muziki

Mchekeshaji maarufu nchini Kenya, Terence Creative, amewashauri wasanii wenzake kujiandaa kwa maisha ya baadaye akionya kwamba taaluma ya sanaa, hususan muziki, haiwezi kudumu milele. Kupitia ujumbe wake, Terence amesema ni muhimu kwa wasanii kufikiria zaidi ya umaarufu wa sasa na kutengeneza misingi imara ya maisha. Amewashauri kujiwekea akiba, kuwekeza kwenye mali kama ardhi na nyumba, na pia kufungua biashara za pembeni zitakazowawezesha kuwa na kipato cha kudumu hata wakati ambapo muziki au kazi ya sanaa haitawaletea mapato makubwa tena. Aidha, Terence amewahimiza wasanii kujali afya zao kwa kupata bima ya afya, na pia kupanga mustakabali wa familia zao kwa kuhakikisha watoto wao wana usalama wa kifedha na elimu bora. Ujumbe wake umewagusa mashabiki na wasanii wengi, huku ukionekana kama wito wa uwajibikaji na kutafakari juu ya maisha ya baadaye. Terence Creative amekuwa mstari wa mbele si tu katika kuleta burudani, bali pia katika kutoa mafunzo ya kijamii kupitia ucheshi na ushauri wake.

Read More
 Simulizi ya Maumivu: Terence Afunguka Kuhusu Mateso Baada ya Mahojiano

Simulizi ya Maumivu: Terence Afunguka Kuhusu Mateso Baada ya Mahojiano

Mchekeshaji na mtayarishaji maarufu wa maudhui, Terence Creative, amesimulia kwa uchungu jinsi alivyojikuta akiingia kwenye kipindi kigumu cha matatizo ya kiafya na ya kiuchumi, ambayo anahusisha moja kwa moja na mtu aliyempa nafasi ya kumhoji kama sehemu ya maudhui ya mtandaoni. Kulingana na Terence, muda mfupi baada ya mahojiano hayo, mambo yalianza kwenda kombo. Alieleza kuwa mipango yake ya kazi ilivurugika kabisa, mke wake Milly Chebby akaanza kuumwa bila sababu ya kueleweka, na hata mtoto wao naye alianza kupata matatizo ya kiafya. Katika harakati za kutafuta majibu, Terence alisema alijitosa kwenye maombi ya kina, na ndipo alipofunuliwa kiroho kwamba yule aliyemhoji alikuwa na nia mbaya na kwamba mtu huyo alitaka kuona maisha yake yakivurugika kabisa. Kwa mujibu wake, baada ya kujua chanzo cha matatizo hayo, aliingia katika kipindi cha maombi ya kina kwa msaada wa familia na watu wa karibu, na hatimaye hali yao ilianza kubadilika. Alitoa tahadhari kwa wasanii na watayarishaji wa maudhui kuwa makini na watu wanaowapa nafasi za mahojiano, kwani si kila mtu anayekuja kwa jina la kazi ana nia njema. Simulizi hiyo imewagusa mashabiki wengi, baadhi wakimpongeza kwa ujasiri wa kushiriki hadithi hiyo ya kiroho, huku wengine wakionya kuhusu hatari ya kutoa nafasi kwa watu wasiowajua vizuri, hata kama ni kwa sababu ya kazi au mahojiano ya kawaida. Hadi sasa, Terence hajataja jina wala maelezo ya moja kwa moja kuhusu content creator anayehisiwa, lakini ujumbe wake umetafsiriwa na wengi kama onyo kwa wasanii na watayarishaji wa maudhui kuwa makini na watu wanaoshirikiana nao katika kazi.

Read More