Tusker FC yashinda 2-0 dhidi ya Bidco United kombe la Mozzart
Mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker FC, wameendeleza wimbi lao la ushindi baada ya kuibwaga Bidco United mabao 2-0 katika mchuano mkali wa awamu ya 32 ya Kombe la Mozzart Bet uliopigwa leo katika uwanja wa Police Sacco. Tusker FC ilianza mchezo huo kwa kasi, ikitawala safu ya kiungo na kutengeneza nafasi nyingi za hatari. Jitihada hizo zilijibu mapema katika kipindi cha kwanza pale mshambuliaji Bless Bakai alipotikisa nyavu na kuwapatia Wana Tusker bao la uongozi. Licha ya Bidco United kujaribu kurudi mchezoni, Tusker ilipigilia msumari wa mwisho kupitia kwa Stephen Etyang, aliyefunga bao la pili na kuhakikisha timu yake inasonga mbele kwa kishindo. Ushindi huu unaongeza matumaini ya Tusker kutwaa taji msimu huu, huku Bidco wakisalia katikati ya jedwali baada ya kushindwa kupata hata bao la kufuta machozi. Mechi za kombe hilo la Mozzartbet zitaendelea mwishoni mwa wikendi hii huku Shabana wakiwa nyumbani dhidi ya Muhoroni FC katika pambano ambalo linatarajiwa kuwa kali zaidi. KCB watakuwa Embu kuchuana na Zetech Titans ilihali Polisi FC itakuwa katika uwanja wa Zoonzi Kesuli kukutana na Police FC katika uwanja wa Zoonzi TBM Kemuri. Bandari itaikaribisha Bombani stars huko Kwale.
Read More