Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Mrembo maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa yeye ndiye msanii pekee nchini Kenya anayeendesha Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, ambayo haijabadilishwa sura (facelift), haijakodishwa wala kukopeshwa. Kupitia mitandao ya kijamii, Vera amejigamba kuwa gari hilo la kifahari ni la kwake binafsi, likiwa katika umbo jipya kabisa ambalo halijawahi kuonekana sana mitaani. Ameongeza kuwa wasanii wengi nchini hupendelea kuonyesha magari ya kukodi au ya mkopo kwa ajili ya kuonyesha maisha ya kifahari, lakini kwake, anamiliki gari hilo kihalali na kwa mapato yake halali. “Ni Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, wala si facelift kama zile watu huwa wanaweka za kukodi kwa picha tu,” Vera alisema Katika kuonyesha kiwango cha kifahari alicho nacho, Vera amefichua kuwa gharama ya kufanya photoshoot ya gari hilo pekee ilikuwa kubwa kiasi kwamba ingeweza kununua gari dogo. Kauli hiyo imeibua mijadala mikali miongoni mwa mashabiki, baadhi wakimsifia kwa ufanisi wake wa kifedha, huku wengine wakimtuhumu kwa majigambo na kueneza maisha ya anasa yasiyo na umuhimu mkubwa kwa jamii.

Read More
 Mrembo wa Kenya Vera Sidika Atwaa Tuzo ya Africa Golden Awards 2025

Mrembo wa Kenya Vera Sidika Atwaa Tuzo ya Africa Golden Awards 2025

Mrembo maarufu kutoka Kenya, Vera Sidika, ametangazwa mshindi wa tuzo ya Top Female Reality TV Star of the Year katika tuzo za Africa Golden Awards kwa mwaka 2025. Tuzo hiyo ilitangazwa rasmi kupitia ukurasa wa Instagram wa Africa Golden Awards, ambapo Vera alipongezwa kwa mchango wake mkubwa katika vipindi vya uhalisia (reality TV) na ushawishi wake mkubwa kwenye mitandao ya kijamii. Tuzo hiyo imemtambua kama mmoja wa wanawake walioleta ushawishi mkubwa katika burudani ya Afrika kwa mtindo wake wa maisha, maudhui yake ya kuvutia, na uwezo wake wa kuunganisha hadhira kubwa. Africa Golden Awards ni tuzo zinazolenga kutambua vipaji bora barani Afrika katika sekta mbalimbali ikiwemo filamu, muziki, uanahabari, mitindo na burudani kwa ujumla.

Read More
 Kauli ya Vera Sidika Yazua Hisia Tofauti Mitandaoni Kuhusu Wivu wa Wanaume

Kauli ya Vera Sidika Yazua Hisia Tofauti Mitandaoni Kuhusu Wivu wa Wanaume

Sosholaiti maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu baadhi ya wanaume wa Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera alidai kuwa wapo wanaume wanaowaonea wivu wanawake, hasa wale waliofanikiwa, na hata baadhi yao kuwa na wivu kwa wake au wapenzi wao. Kulingana na Vera, hali hiyo ya wivu inachangia matatizo mengi katika mahusiano ya kimapenzi. Aliongeza kuwa baadhi ya wanaume hushindwa kuvumilia mafanikio ya wake au wapenzi wao, jambo ambalo hupelekea migogoro na hata kuvunjika kwa mahusiano “Some Kenyan men are jealous of women, especially successful women. Some men are even jealous of their own girlfriends, wives. Yes, it happens. There’s jealousy in relationships btw.” Aliandika Kauli hiyo imeibua maoni tofauti kutoka kwa wafuasi wake na wanamitandao kwa ujumla. Baadhi wameunga mkono hoja hiyo wakisema kuwa wivu wa wanaume kwa wake zao ni jambo linalotokea hasa pale mwanamke anapoonekana kujiendeleza zaidi kimaisha. Wengine, hata hivyo, wamekosoa kauli hiyo wakidai kuwa ni ya kuwakandamiza wanaume na kwamba wivu unaweza kuwapo kwa pande zote mbili katika uhusiano. Vera Sidika, ambaye amekuwa kwenye uhusiano wa hadharani na kuzungumziwa sana kutokana na mtindo wake wa maisha wa kifahari, amekuwa pia akijitokeza mara kwa mara kuzungumzia masuala ya mahusiano, wanawake na mafanikio. Vera Sidika amekuwa mstari wa mbele katika kujieleza waziwazi kuhusu masuala ya kijamii na ya kifamilia, huku akitumia jukwaa lake la mitandao ya kijamii kuzungumzia mada mbalimbali zinazohusu maisha, mahusiano, na mafanikio ya wanawake.

Read More
 Vera Sidika Awajibu Wanaomkejeli kwa Kufanya Club Appearance Busia

Vera Sidika Awajibu Wanaomkejeli kwa Kufanya Club Appearance Busia

Sosholaiti na mfanyabiashara maarufu Vera Sidika amevunja kimya kufuatia kejeli za mitandaoni kutoka kwa baadhi ya Wakenya waliomkejeli kwa kufanya club appearance mjini Busia, hatua ambayo baadhi waliiita “recession indicator” ya maisha yake. Kupitia InstaStory yake, Vera alionekana kutoyumbishwa na maoni hayo, akisisitiza kuwa anajivunia kuwa na uwezo wa kuungana na mashabiki wake kote nchini, siyo tu katika miji mikubwa.  “Seems like Kenyans have just discovered a new vocabulary  ‘Recession indicator’. Kwani what’s wrong with me making a club appearance in Busia?” aliandika Vera. Katika ujumbe wake, Vera alifafanua kuwa hana aibu kufanya maonyesho au kujitokeza katika maeneo yote ya Kenya, kwani kila mahali kuna mashabiki wanaomheshimu na kumpenda.  “I love connecting with my fans in all parts of the country. Kama Busia wananitaka, basi nitaenda si kila mtu anaishi Nairobi!,” alisema. Baadhi ya mashabiki kwenye mitandao ya kijamii waliiunga mkono kauli ya Vera, wakisema ni jambo la heshima kuonyesha usawa kwa mashabiki wote, bila ubaguzi wa kijiografia. Lakini kwa upande mwingine, baadhi walionekana kudharau tukio hilo, wakilitafsiri kama ishara ya kuporomoka kwa hadhi ya Vera kama staa wa muda mrefu.

Read More
 Vera Sidika athibitisha kuwa mjamzito

Vera Sidika athibitisha kuwa mjamzito

Mrembo maarufu nchini Kenya, Vera Sidika ni mjamzito kwa mara nyingine ikiwa ni siku chache zimepata tangu tetesi  zilipoibuka mtandaoni kuwa amekuwa akificha tumbo lake mbele ya camera. Kupitia ukurasa wake wa instagram Vera amethibitisha kuwa anatarajia mtoto wake wa pili na mumewe Brown Mauzo huku akieleza ni furaha kwake kupata mtoto mwingine Mwanamama huyo wa mtoto mmoja amefichua kwamba amekuwa mjamzito kwa takriban miezi saba sasa kwani aligundua ana uja uzito alipokuwa amepanga kuenda nje ya nchi kufanyiwa upasuaji wa kuongeza matiti. Brown Mauzo kwa upande wake amemshukuru Vera Sidika kwa kuwa mke bora kwake na mama mzuri kwa mtoto wao, Asia Brown. Hata msanii huyo amemhakikishia kuwa ataendelea kumuonyesha upendo mkubwa huku akikiri kuwa anafurahia hatua nyingine katika ndoa yao. Utakumbuka wawili hao wamekuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka miwili na walibarikiwa na mtoto wao wa kwanza Oktoba mwaka jana.

Read More
 Vera Sidika afunguka kubeba ujauzito mwingine

Vera Sidika afunguka kubeba ujauzito mwingine

Mrembo maarufu nchini Kenya, Vera Sidika amevunja kimya kuhusu madai kuwa ni mjamzito kwa mara ya pili. Wanamitandao wamekuwa wakidai kuwa mama huyo ni mjamzito kwani amekuwa akificha tumbo lake kila anapoenda. “Mbona muamini hayo? hii ilikuwa mwaka jana nilipokuwa na mimba ya Asia na nilificha nikiwa nimevalia nguo hii, dah! watu wanaweza kueneza uvumi,” aliandika Vera Sidika Instagram. Uvumi huo unachukua nafasi baada ya Vera kuweka wazi kuwa amepanga kumpeleka mtoto wake, Asia Brown shuleni ifikapo Januari 2023.

Read More
 Vera Sidika adaiwa kuwa mjamzito

Vera Sidika adaiwa kuwa mjamzito

Soshalaiti maarufu mtandaoni Vera Sidika amedaiwa kuwa mjamzito. Tetesi hizo zimeibuka mara baada ya wengi kumuona kwenye mitandao ya kijamii akiwa ameficha tumbo lake mbele ya camera jambo ambalo si kawaida yake. Lakini pia nguo kubwa (Oversize) ambayo amekuwa akivalia katika siku za hivi karibuni limefanya walimwengu kupigia mstari kuwa mrembo huyo ni mjamzito. Ikiwa ni kweli Vera Sidika ana ujauzito kwa sasa, basi huyo atakuwa mtoto wa pili kwa staa huyo mwenye umri wa miaka 33 na mchumba wake msanii Brown Mauzo.

Read More
 Wimbo wa Vera Sidika waweka rekodi ya kutopendwa kwenye mtandao wa Youtube nchini Kenya

Wimbo wa Vera Sidika waweka rekodi ya kutopendwa kwenye mtandao wa Youtube nchini Kenya

Video ya Wimbo wa Vera Sidika ‘Popstar’ unatajwa kuwa video ya muziki isiyopendwa zaidi nchini Kenya kwenye mtandao wa YouTube. Kulingana na program ya Dislike Viewer plugin, Video ya wimbo huo ,imepata zaidi ya dislikes 39,000, ikiipiku video ya Willy Paul ‘Lamba Nyonyo’ iliyotoka miaka 3 iliyopita ambayo ina zaidi ya dislikes 38,000, Vera Sidika aliachia video wimbo wa ‘Popstar’   Oktoba 7 2022  baada ya kudai  kufanya upasuaji wa kupunguza makalio yake akiwa na lwngo ya kutangaza  wimbo wake mpya.

Read More
 Vera Sidika atamani kupata mtoto wa kiume

Vera Sidika atamani kupata mtoto wa kiume

Mwanasosholaiti Vera Sidika amesema kuwa anatamani kuwa na mtoto wa kiume siku za mbeleni ili wawe na ukaribu kama wa bintiye Asia Brown na baba yake Brown Mauzo. Vera amesema kuwa sababu yake ya kutamani kuwa na mtoto wa kiume ni kuwa anauonea wivu urafiki wa karibu ambao Asia na Brown Mauzo wako nao. “Mwenyenzi Mungu, naombea miujiza katika maisha yangu, natumai huko mbeleni utanipa mtoto wa kiume, nitamringia mume wangu, awacha tu,” alisema Vera anayetamba na ngoma, Popstar. Vera ambaye hivi karibuni kaachia wimbo wake mpya ‘Popstar’ amejaliwa mtoto mmoja na Msanii wa muziki Kenya, Brown Mauzo baada kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, Otile Brown ambaye ni msanii pia.

Read More
 Vera Sidika awatolea uvivu wanaokosoa nywele za binti yake Asia Brown

Vera Sidika awatolea uvivu wanaokosoa nywele za binti yake Asia Brown

Soshalaiti maarufu mtandaoni kutoka nchini Kenya Vera Sidika ameshindwa kuwavumilia wanaokashifu mtindo wa nywele ya binti yake mchanga Asia Brown ambayo alikuwa amesukwa  kwenye kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Vera amesema watu wanaomunyoshea kidole cha lawama kuwa anamtesa binti yake kwa kumwekea nywele nzito kichwani ni malimbukeni kwani nywele zilizotumika kumsuka sio nzito kama inavyodaiwa mtandaoni. Aidha mrembo huyo ambaye amegeukia muziki amesema hawezi kumudhuru mwanae na kitu asichokijua, hivyo watu waache kumsema vibaya kama mama asiyejali maslahi ya binti yake. Kauli ya Vera Sidika imekuja baada ya walimwengu mtandaoni kumkashifu kwa hatua ya kutumia nywele aina braids kumsuka binti yake kitendo ambacho wengi walihoji kuwa mrembo analimdhulumu mtoto huyo mchanga kwa kumbebesha nywele nzito kichwani.

Read More
 Vera Sidika atumia millioni 2 kuongeza maziwa

Vera Sidika atumia millioni 2 kuongeza maziwa

Mrembo kutoka nchini Kenya, Vera Sidika amefichua kiasi cha fedha alichotumia kufanyiwa upasuaji wa kuongeza matiti yake. Akijibu maswali kwenye ukurasa wake wa Instagram, mke huyo wa Brown Mauzo alisema kuwa alitumia zaidi ya shillingi millioni 2 na upasuaji huo ulifanyiwa nje ya nchi ya Kenya. “Ilinigharimu dola elfu 20,” alisema Vera ambaye ni Mama wa mtoto mmoja. Lakini pia ameweka wazi kuwa baada ya kujifungua bintiye mwaka jana, aliweza kumnyonyesha bila matatizo yoyote kwani alichagua upasuaji ambao ungemwezesha kunyonyesha bila tashwishi yoyote. Sidika alipoulizwa kama matiti yake bado yako imara hata baada ya kujifungua alisema kuwa hayajawahi kulegea licha ya kumnyoyesha mtoto wa

Read More
 Vera Sidika awafunguka mdomo waliodhani makalio yake ni batili

Vera Sidika awafunguka mdomo waliodhani makalio yake ni batili

Mrembo Vera Sidika amekanusha madai ya kufanya upasuaji kuongeza makalio yake kwa kusema kuwa makalio yake ni ya asili. Katika kikao cha maswali na majibu kwenye mtandao wa Instagram na Mashabiki zake Vera amekiri kuwa athari za dawa za kupangaza uzazi ndio ilichangia ukubwa wa makalio yake. Mama huyo wa mtoto mmoja amesema alipata unyanyapa mkubwa akiwa shule ya upili mashinani kutokana na watu kumbandika majina ya kukejeli muonekano wa makalio yake lakini alipohamia Nairobi watu walimfanya ajihisi mwenye thamani baada ya kushirikishwa kwenye video ya wimbo  wa ‘You Guy’  wa kundi la P-Unit. Katika hatua nyingine Vera Sidika amesisitiza kuwa matiti yake sio ya asili ambapo ameweka wazi kuwa alifanyiwa upasuaji uliogharimu shillingi millioni 2 za Kenya ili kuongeza ukubwa wake. Wiki iliyopita Vera Sidika aliteka mitandao ya kijamii baada ya kuposti picha iliyofanyiwa ukarabati wa kupunguza makalio yake ambapo alijitokeza na kudai kuwa alilazimika kufanyiwa upasuaji wa kupunguza makalio kutokana na matatizo ya kiafya lakini ilikuja ikabainika kuwa ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya kuzungumziwa mitandaoni kabla ya ujio wa wimbo wake mpya uitwao Popstar.

Read More