Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya
Mrembo maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa yeye ndiye msanii pekee nchini Kenya anayeendesha Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, ambayo haijabadilishwa sura (facelift), haijakodishwa wala kukopeshwa. Kupitia mitandao ya kijamii, Vera amejigamba kuwa gari hilo la kifahari ni la kwake binafsi, likiwa katika umbo jipya kabisa ambalo halijawahi kuonekana sana mitaani. Ameongeza kuwa wasanii wengi nchini hupendelea kuonyesha magari ya kukodi au ya mkopo kwa ajili ya kuonyesha maisha ya kifahari, lakini kwake, anamiliki gari hilo kihalali na kwa mapato yake halali. “Ni Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, wala si facelift kama zile watu huwa wanaweka za kukodi kwa picha tu,” Vera alisema Katika kuonyesha kiwango cha kifahari alicho nacho, Vera amefichua kuwa gharama ya kufanya photoshoot ya gari hilo pekee ilikuwa kubwa kiasi kwamba ingeweza kununua gari dogo. Kauli hiyo imeibua mijadala mikali miongoni mwa mashabiki, baadhi wakimsifia kwa ufanisi wake wa kifedha, huku wengine wakimtuhumu kwa majigambo na kueneza maisha ya anasa yasiyo na umuhimu mkubwa kwa jamii.
Read More