Vera Sidika Amchana Eddie Butita Kuhusu Kauli za Boo Party
Socialite wa Kenya Vera Sidika ameonekana kuchukizwa na matamshi ya mchekeshaji Eddie Butita aliyewakosoa wanaume waliohudhuria hafla yake ya hivi karibuni maarufu kama Boo Party. Kupitia video aliyoipakia mitandaoni, Vera amemshutumu Butita kwa kuwa na machungu kwa sababu hakupata mualiko wa kushiriki sherehe hiyo. Amesema hakuna mwanaume timamu ambaye angekataa mwaliko wa hafla kama hiyo, akidai ni wachache tu wenye majungu na wivu wanaoweza kutoa maneno ya kubeza. Aidha, amemshauri Butita kuacha kufuatilia maisha yake na kuacha majungu, akibainisha kuwa siku zijazo huenda akampatia mualiko rasmi ili ahudhurie moja ya sherehe zake. Mapema wiki hii, Vera alifanya Boo Party maalum kwa ajili ya kusherehekea hatua yake ya upasuaji wa urembo, baada ya kufanikisha kuongeza uthabiti wa matiti yake. Hafla hiyo ilivutia hisia tofauti mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza na wengine wakibeza. Kulingana na Butita, hakuelewa sababu ya wanaume kushiriki hafla ya aina hiyo.Alisema kwamba ilikuwa sawa kwa marafiki wa kike wa Vera kumuunga mkono, lakini aliona haikuwa na mantiki kwa wanaume kuhudhuria tukio lililolenga kusherehekea upasuaji wa mwili.
Read More