Vera Sidika Amchana Eddie Butita Kuhusu Kauli za Boo Party

Vera Sidika Amchana Eddie Butita Kuhusu Kauli za Boo Party

Socialite wa Kenya Vera Sidika ameonekana kuchukizwa na matamshi ya mchekeshaji Eddie Butita aliyewakosoa wanaume waliohudhuria hafla yake ya hivi karibuni maarufu kama Boo Party. Kupitia video aliyoipakia mitandaoni, Vera amemshutumu Butita kwa kuwa na machungu kwa sababu hakupata mualiko wa kushiriki sherehe hiyo. Amesema hakuna mwanaume timamu ambaye angekataa mwaliko wa hafla kama hiyo, akidai ni wachache tu wenye majungu na wivu wanaoweza kutoa maneno ya kubeza. Aidha, amemshauri Butita kuacha kufuatilia maisha yake na kuacha majungu, akibainisha kuwa siku zijazo huenda akampatia mualiko rasmi ili ahudhurie moja ya sherehe zake. Mapema wiki hii, Vera alifanya Boo Party maalum kwa ajili ya kusherehekea hatua yake ya upasuaji wa urembo, baada ya kufanikisha kuongeza uthabiti wa matiti yake. Hafla hiyo ilivutia hisia tofauti mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza na wengine wakibeza. Kulingana na Butita, hakuelewa sababu ya wanaume kushiriki hafla ya aina hiyo.Alisema kwamba ilikuwa sawa kwa marafiki wa kike wa Vera kumuunga mkono, lakini aliona haikuwa na mantiki kwa wanaume kuhudhuria tukio lililolenga kusherehekea upasuaji wa mwili.

Read More
 Kauli ya Vera Sidika Yazima Uvumi wa Kurudiana na Brown Mauzo

Kauli ya Vera Sidika Yazima Uvumi wa Kurudiana na Brown Mauzo

Socialite maarufu wa Kenya, Vera Sidika, amezima madai yanayoenezwa mitandaoni kuwa anapanga kurudiana na mzazi mwenzake, mwanamuziki Brown Mauzo licha ya kuendelea kushirikiana naye katika malezi ya watoto wao. Kupitia ujumbe aliouweka kwenye Instagram, Vera amekanusha vikali uvumi huo na kueleza kuwa maamuzi yake yamelenga tu kuhakikisha watoto wao wanapata malezi bora. Amesisitiza kwamba hatua ya kuruhusu Brown kuwa karibu na watoto wao haimaanishi kuwa anataka kurejesha mahusiano, bali ni kutambua wajibu wake kama baba. Mwanamama huyo pia amewakumbusha mashabiki wake kuwa alishawahi kuandaa “divorce party” kama alama ya kufunga ukurasa wa ndoa yake na Mauzo, jambo analosema linatosha kuonyesha kuwa hawezi kurudiana naye. Hii inakuja baada ya mijadala kuzuka mitandaoni, mashabiki wakidai kitendo chake cha kumruhusu Brown Mauzo kuja nyumbani kwake na kukaa na watoto wao ni ishara ya wawili hao kutaka kufufua uhusiano wao wa kimapenzi.

Read More
 Vera Sidika Ajibu Ukosoaji Kuhusu Kumruhusu Brown Mauzo Kuwaona Watoto Wao

Vera Sidika Ajibu Ukosoaji Kuhusu Kumruhusu Brown Mauzo Kuwaona Watoto Wao

Mrembo maarufu kutoka Kenya, Vera Sidika, ameweka wazi msimamo wake baada ya kukosolewa kwa uamuzi wake wa kumruhusu aliyekuwa mpenzi wake, mwanamuziki Brown Mauzo, kutumia muda na watoto wao nyumbani kwake. Kupitia Inst story yake, Vera amesema hajawahi kumtegemea Mauzo kwa msaada wa kifedha na kwamba jambo analolipa kipaumbele ni uwepo wake kama baba katika maisha ya watoto wao. Amebainisha kuwa yeye mwenyewe alikulia kwenye familia yenye wazazi wote wawili, jambo lililomfanya atamani watoto wake wapate malezi yenye upendo na uwepo wa baba, bila kujali changamoto za kifedha. Akizungumzia dhamira ya Mauzo kama mzazi, Vera amesema amewahi kushuhudia jinsi alivyovunjika moyo baada ya kuzuiwa kumuona mtoto wake na mama wa mtoto wake kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kwa mujibu wake, hali hiyo ilionyesha wazi jinsi anavyothamini nafasi yake kama baba na hamu yake ya kuwa karibu na watoto wake. Aidha, Vera amekosoa vikali tabia ya baadhi ya akina mama kuwazuia baba kuona watoto wao kwa sababu ya changamoto za kifedha. Alisema kufanya hivyo ni kitendo cha ubinafsi kwa kuwa kinawanyima watoto nafasi ya kupokea upendo na malezi ya baba zao. Kauli ya Vera imezua mjadala mitandaoni, baadhi ya watu wakimsifu kwa ukomavu na mtazamo wake chanya kuhusu malezi ya pamoja, huku wengine wakisisitiza kuwa majukumu ya kifedha nayo ni sehemu muhimu ya malezi ya mzazi.

Read More
 Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Socialite maarufu nchini Kenya, Vera Sidika, amejibu tetesi kutoka kwa mashabiki waliodai kwamba amewatelekeza watoto wake kwa sababu ya kuwa safarini mara kwa mara. Kupitia ujumbe alioweka mtandaoni, Vera amesisitiza kuwa watoto wake daima wako chini ya uangalizi wa mzazi kila wakati. Amefafanua kuwa anapohitajika kuwa kwenye shughuli zake binafsi au kuendesha mikusanyiko katika nyumba yake ya kifahari, huomba baba ya watoto wake Brown Mauzo kukaa nao muda wote. Aidha,Mwanamama huyo amesema anaposafiri kwenda maeneo mbalimbali duniani, baba ya watoto hubaki nao nyumbani akisaidiana na wafanyikazi wa ndani (nannies) hadi atakaporudi. Kauli hiyo imekuja baada ya walimwengu kwenye mitandao ya kijamii kuibua maswali kuhusu malezi ya watoto wake, baadhi ya watu wakimlaumu kwa kutokuwa karibu nao kutokana na ratiba zake za mara kwa mara za safari na shughuli za kijamii.

Read More
 Vera Sidika Ashtua Wafuasi kwa Kauli Kali Dhidi ya Mammito

Vera Sidika Ashtua Wafuasi kwa Kauli Kali Dhidi ya Mammito

Sosholaiti maarufu wa Kenya, Vera Sidika, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kumtolea uvivu mchekeshaji Mammito Eunice kufuatia kauli yake kuhusu upasuaji wa kuongeza makalio (BBL). Mammito alikuwa ametupa dongo akidai wanawake wengi kutoka jamii ya Luhya wanapendelea sana urembo wa upasuaji, jambo ambalo halikumpendeza Vera. Kupitia Instastory yake, Vera alimjibu kwa kejeli, akimshambulia binafsi na kumshauri akubaliane na hali yake. “The fact hauna pesa ya BBL inashangaza. Please embrace your bones in peace.”, Aliandika Inststory Majibizano hayo yamezua mjadala mkubwa mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakimpongeza Vera kwa kujiamini, huku wengine wakimkosoa kwa kutumia maneno ya kudhalilisha. Tukio hili lilitokea wakati Vera akijaribu kukanusha madai ya wakosoaji waliokuwa wakipotosha kuhusu uhalali wa gari lake la kifahari aina ya Range Rover, ambalo alilishiriki kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Read More
 Asili ya Vera Sidika Yazua Mvutano Mitandaoni

Asili ya Vera Sidika Yazua Mvutano Mitandaoni

Mrembo maarufu mtandaoni Vera Sidika amejipata pabaya mbele ya walimwengu baada ya kudai kuwa watu wengi hudhani anatokea Jamaica au Afrika Kusini kutokana na muonekano wake. Kauli hiyo imeonekana kuwakera baadhi ya mashabiki waliomtaka akubali asili yake kama Mluya kutoka Kakamega badala ya kujipendekeza kwa umma. Mashabiki wengi walimshauri aache drama zisizo na msingi na kujikita zaidi katika malezi ya watoto wake. Wengine walimkosoa vikali wakidai kwamba anampigia mzazi mwenzie, Brown Mauzo, simu nyakati za usiku licha ya wawili hao kuachana rasmi. Baadhi ya wafuasi walionya kwamba kitendo hicho cha kumsumbua Mauzo huenda kikaathiri ndoa ya sasa ya msanii huyo. Hata hivyo, bado kuna kundi dogo la mashabiki wanaomtetea, wakisema kuwa umaarufu wa Vera umevuka mipaka ya Kenya na kwamba si jambo la kushangaza mashabiki wa kimataifa kumhusisha na tamaduni za mataifa mengine kutokana na taswira yake ya kimataifa.

Read More
 Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Mrembo maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa yeye ndiye msanii pekee nchini Kenya anayeendesha Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, ambayo haijabadilishwa sura (facelift), haijakodishwa wala kukopeshwa. Kupitia mitandao ya kijamii, Vera amejigamba kuwa gari hilo la kifahari ni la kwake binafsi, likiwa katika umbo jipya kabisa ambalo halijawahi kuonekana sana mitaani. Ameongeza kuwa wasanii wengi nchini hupendelea kuonyesha magari ya kukodi au ya mkopo kwa ajili ya kuonyesha maisha ya kifahari, lakini kwake, anamiliki gari hilo kihalali na kwa mapato yake halali. “Ni Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, wala si facelift kama zile watu huwa wanaweka za kukodi kwa picha tu,” Vera alisema Katika kuonyesha kiwango cha kifahari alicho nacho, Vera amefichua kuwa gharama ya kufanya photoshoot ya gari hilo pekee ilikuwa kubwa kiasi kwamba ingeweza kununua gari dogo. Kauli hiyo imeibua mijadala mikali miongoni mwa mashabiki, baadhi wakimsifia kwa ufanisi wake wa kifedha, huku wengine wakimtuhumu kwa majigambo na kueneza maisha ya anasa yasiyo na umuhimu mkubwa kwa jamii.

Read More
 Mrembo wa Kenya Vera Sidika Atwaa Tuzo ya Africa Golden Awards 2025

Mrembo wa Kenya Vera Sidika Atwaa Tuzo ya Africa Golden Awards 2025

Mrembo maarufu kutoka Kenya, Vera Sidika, ametangazwa mshindi wa tuzo ya Top Female Reality TV Star of the Year katika tuzo za Africa Golden Awards kwa mwaka 2025. Tuzo hiyo ilitangazwa rasmi kupitia ukurasa wa Instagram wa Africa Golden Awards, ambapo Vera alipongezwa kwa mchango wake mkubwa katika vipindi vya uhalisia (reality TV) na ushawishi wake mkubwa kwenye mitandao ya kijamii. Tuzo hiyo imemtambua kama mmoja wa wanawake walioleta ushawishi mkubwa katika burudani ya Afrika kwa mtindo wake wa maisha, maudhui yake ya kuvutia, na uwezo wake wa kuunganisha hadhira kubwa. Africa Golden Awards ni tuzo zinazolenga kutambua vipaji bora barani Afrika katika sekta mbalimbali ikiwemo filamu, muziki, uanahabari, mitindo na burudani kwa ujumla.

Read More
 Kauli ya Vera Sidika Yazua Hisia Tofauti Mitandaoni Kuhusu Wivu wa Wanaume

Kauli ya Vera Sidika Yazua Hisia Tofauti Mitandaoni Kuhusu Wivu wa Wanaume

Sosholaiti maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu baadhi ya wanaume wa Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera alidai kuwa wapo wanaume wanaowaonea wivu wanawake, hasa wale waliofanikiwa, na hata baadhi yao kuwa na wivu kwa wake au wapenzi wao. Kulingana na Vera, hali hiyo ya wivu inachangia matatizo mengi katika mahusiano ya kimapenzi. Aliongeza kuwa baadhi ya wanaume hushindwa kuvumilia mafanikio ya wake au wapenzi wao, jambo ambalo hupelekea migogoro na hata kuvunjika kwa mahusiano “Some Kenyan men are jealous of women, especially successful women. Some men are even jealous of their own girlfriends, wives. Yes, it happens. There’s jealousy in relationships btw.” Aliandika Kauli hiyo imeibua maoni tofauti kutoka kwa wafuasi wake na wanamitandao kwa ujumla. Baadhi wameunga mkono hoja hiyo wakisema kuwa wivu wa wanaume kwa wake zao ni jambo linalotokea hasa pale mwanamke anapoonekana kujiendeleza zaidi kimaisha. Wengine, hata hivyo, wamekosoa kauli hiyo wakidai kuwa ni ya kuwakandamiza wanaume na kwamba wivu unaweza kuwapo kwa pande zote mbili katika uhusiano. Vera Sidika, ambaye amekuwa kwenye uhusiano wa hadharani na kuzungumziwa sana kutokana na mtindo wake wa maisha wa kifahari, amekuwa pia akijitokeza mara kwa mara kuzungumzia masuala ya mahusiano, wanawake na mafanikio. Vera Sidika amekuwa mstari wa mbele katika kujieleza waziwazi kuhusu masuala ya kijamii na ya kifamilia, huku akitumia jukwaa lake la mitandao ya kijamii kuzungumzia mada mbalimbali zinazohusu maisha, mahusiano, na mafanikio ya wanawake.

Read More
 Vera Sidika Awajibu Wanaomkejeli kwa Kufanya Club Appearance Busia

Vera Sidika Awajibu Wanaomkejeli kwa Kufanya Club Appearance Busia

Sosholaiti na mfanyabiashara maarufu Vera Sidika amevunja kimya kufuatia kejeli za mitandaoni kutoka kwa baadhi ya Wakenya waliomkejeli kwa kufanya club appearance mjini Busia, hatua ambayo baadhi waliiita “recession indicator” ya maisha yake. Kupitia InstaStory yake, Vera alionekana kutoyumbishwa na maoni hayo, akisisitiza kuwa anajivunia kuwa na uwezo wa kuungana na mashabiki wake kote nchini, siyo tu katika miji mikubwa.  “Seems like Kenyans have just discovered a new vocabulary  ‘Recession indicator’. Kwani what’s wrong with me making a club appearance in Busia?” aliandika Vera. Katika ujumbe wake, Vera alifafanua kuwa hana aibu kufanya maonyesho au kujitokeza katika maeneo yote ya Kenya, kwani kila mahali kuna mashabiki wanaomheshimu na kumpenda.  “I love connecting with my fans in all parts of the country. Kama Busia wananitaka, basi nitaenda si kila mtu anaishi Nairobi!,” alisema. Baadhi ya mashabiki kwenye mitandao ya kijamii waliiunga mkono kauli ya Vera, wakisema ni jambo la heshima kuonyesha usawa kwa mashabiki wote, bila ubaguzi wa kijiografia. Lakini kwa upande mwingine, baadhi walionekana kudharau tukio hilo, wakilitafsiri kama ishara ya kuporomoka kwa hadhi ya Vera kama staa wa muda mrefu.

Read More
 Vera Sidika athibitisha kuwa mjamzito

Vera Sidika athibitisha kuwa mjamzito

Mrembo maarufu nchini Kenya, Vera Sidika ni mjamzito kwa mara nyingine ikiwa ni siku chache zimepata tangu tetesi  zilipoibuka mtandaoni kuwa amekuwa akificha tumbo lake mbele ya camera. Kupitia ukurasa wake wa instagram Vera amethibitisha kuwa anatarajia mtoto wake wa pili na mumewe Brown Mauzo huku akieleza ni furaha kwake kupata mtoto mwingine Mwanamama huyo wa mtoto mmoja amefichua kwamba amekuwa mjamzito kwa takriban miezi saba sasa kwani aligundua ana uja uzito alipokuwa amepanga kuenda nje ya nchi kufanyiwa upasuaji wa kuongeza matiti. Brown Mauzo kwa upande wake amemshukuru Vera Sidika kwa kuwa mke bora kwake na mama mzuri kwa mtoto wao, Asia Brown. Hata msanii huyo amemhakikishia kuwa ataendelea kumuonyesha upendo mkubwa huku akikiri kuwa anafurahia hatua nyingine katika ndoa yao. Utakumbuka wawili hao wamekuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka miwili na walibarikiwa na mtoto wao wa kwanza Oktoba mwaka jana.

Read More
 Vera Sidika afunguka kubeba ujauzito mwingine

Vera Sidika afunguka kubeba ujauzito mwingine

Mrembo maarufu nchini Kenya, Vera Sidika amevunja kimya kuhusu madai kuwa ni mjamzito kwa mara ya pili. Wanamitandao wamekuwa wakidai kuwa mama huyo ni mjamzito kwani amekuwa akificha tumbo lake kila anapoenda. “Mbona muamini hayo? hii ilikuwa mwaka jana nilipokuwa na mimba ya Asia na nilificha nikiwa nimevalia nguo hii, dah! watu wanaweza kueneza uvumi,” aliandika Vera Sidika Instagram. Uvumi huo unachukua nafasi baada ya Vera kuweka wazi kuwa amepanga kumpeleka mtoto wake, Asia Brown shuleni ifikapo Januari 2023.

Read More