Vera Sidika Afichua Kununua iPhone zake Kutoka Maduka Rasmi Marekani

Vera Sidika Afichua Kununua iPhone zake Kutoka Maduka Rasmi Marekani

Socialite kutoka Kenya, Vera Sidika, amefichua kuwa hununua simu zake za iPhone moja kwa moja kutoka maduka rasmi ya Apple nchini Marekani na siyo Kenya kama namna baadhi ya watu wanavyodai. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Vera amesema kuwa hana imani na maduka mengi yanayouza vifaa vya teknolojia nchini humo, akieleza kuwa baadhi ya simu hizo huwa hazitoki moja kwa moja kwa Apple na huwa zimefanyiwa marekebisho kabla ya kuuzwa. Mama huyo wa watoto wawili, amesema hatua hiyo ni njia yake ya kujihakikishia ubora na usalama wa kifaa anachonunua, ikizingatiwa kwamba bidhaa ghushi zimekuwa changamoto kubwa sokoni. Kauli yake imezua mjadala mtandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimuunga mkono kwa kusema kuwa bidhaa bandia zimekuwa changamoto kubwa sokoni, huku wengine wakidai kuwa anajaribu kuonesha maisha ya kifahari.

Read More
 Vera Sidika Amuomboleza Raila Odinga Katika Siku ya Mashujaa

Vera Sidika Amuomboleza Raila Odinga Katika Siku ya Mashujaa

Socialite wa Kenya, Vera Sidika, ameonyesha huzuni yake kubwa kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Amolo Odinga, akimkumbuka kama shujaa wa kweli wa taifa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera amechapisha ujumbe wenye hisia kali akieleza kuwa maadhimisho ya Mashujaa Day mwaka huu yamekuwa tofauti kwani yanakuja siku tano tu baada ya taifa kumpoteza kiongozi huyo mashuhuri. Mama huyo wa watoto wawili, amesema kuwa bado haamini kwamba Raila hayupo tena duniani na kueleza kuwa mwaka huu kumbukumbu ya kuzaliwa kwa binti yake Asia imegubikwa na huzuni kubwa. Kwa mujibu wake, Raila atabaki kuwa shujaa wa kweli ambaye aligusa maisha ya Wakenya wengi. Vera ameongeza kuwa mchango wa Raila katika historia ya Kenya na mapambano ya demokrasia hautasahaulika kamwe. Kifo cha kiongozi huyo kimeendelea kugusa watu kutoka nyanja mbalimbali, huku mashabiki, viongozi, na wasanii wakiendelea kumuenzi kama shujaa wa kizazi chake aliyejitolea kwa haki, umoja, na maendeleo ya taifa.

Read More
 Vera Sidika: Nimechoka Kuwa Single, Nataka Mchumba Gen Z

Vera Sidika: Nimechoka Kuwa Single, Nataka Mchumba Gen Z

Socialite maarufu wa Kenya, Vera Sidika, amefichua kuwa sasa yuko tayari kurudi tena kwenye ulimwengu wa mapenzi na safari hii, anavutiwa na mwanaume wa kizazi cha Gen Z. Vera, ambaye ni mama wa watoto wawili, amekiri kuwa amekuwa single kwa muda mrefu sana na amekuwa akipitia kipindi kigumu cha upweke, akisema hata siku yake ya kuzaliwa mwaka huu haikuwa na msisimko kama ilivyokuwa zamani. Amesema hali hiyo imemfanya atambue umuhimu wa kuwa na mtu wa karibu, na sasa anaona yuko tayari kufungua moyo wake tena kwa mapenzi. Vera ameeleza kuwa anavutiwa na wanaume wa Gen Z kwa sababu wanajua kuonyesha mapenzi kwa vitendo, na hawana hofu ya kuzungumza hisia zao. Pia amesema vijana hao wana nguvu na hulka ya furaha, jambo analoamini litampa msisimko mpya maishani. Kauli yake imezua maoni mseto mtandaoni, baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa ujasiri wa kusema ukweli wake, huku wengine wakimtania kwa kutaka mwanaume kijana zaidi.

Read More
 Vera Sidika Azua Mjadala Mpya Baada ya Upasuaji wa Mdomo

Vera Sidika Azua Mjadala Mpya Baada ya Upasuaji wa Mdomo

Socialite wa Kenya, Vera Sidika, amethibitisha kwamba amefanyiwa upasuaji wa mdomo (lip procedure) wiki chache tu baada ya kupitia upasuaji wa kuinua maziwa (breast lift). Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Vera amesema kuwa upasuaji huo ni sehemu ya safari yake ya kujiboresha na kurejesha muonekano anaoupenda. Ameongeza kuwa yuko kwenye hatua ya kupona, na matokeo ya mwisho yatakuwa bora zaidi katika siku chache zijazo. Vera pia amewaonya mashabiki wake wasishangae wakimuona na mdomo uliofura wakati wa club appearances atakazozifanya wiki hii, akisema ni hali ya kawaida baada ya upasuaji huo. Tangazo hilo limezua gumzo mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa uaminifu wake wa kushiriki safari ya urembo hadharani, na wengine wakijadili jinsi mitindo ya vipodozi na upasuaji wa kuboresha miili inavyozidi kupata umaarufu miongoni mwa watu mashuhuri nchini.

Read More
 Vera Sidika Azima Uvumi wa Mpenzi Kupiga Picha Zake

Vera Sidika Azima Uvumi wa Mpenzi Kupiga Picha Zake

Socialite maarufu Vera Sidika amewaacha mashabiki wake wakiwa na mshangao baada ya kufichua kuwa yeye husafiri peke yake na hupiga picha zake zote mwenyewe akitumia remote ndogo na standi ya simu. Kupitia Instastory zake, Vera ameonyesha kifaa kidogo cha remote anachotumia kupiga picha, akieleza kuwa kama msafiri wa pekee yake, hupendelea njia hiyo badala ya kuwaomba watu wasiofahamika kumpiga picha. Mwanamama huyo amesema kuwa mara nyingi unapomuomba mgeni akupige picha, matokeo huwa si mazuri, hivyo amejizoesha kutumia teknolojia hiyo ndogo kumsaidia kupata picha anazotaka kwa urahisi. Kauli yake imekuja baada ya mashabiki wengi kuuliza mara kwa mara ni nani anayempiga picha anapokuwa safarini, kwani picha zake zimekuwa zikionekana za kitaalamu na zenye ubora wa juu. Baadhi ya mashabiki walidhani picha hizo zilikuwa zikichukuliwa na mpenzi wake, lakini Vera aamepuzilia mbali uvumi huo kwa kueleza wazi kuwa hana mpenzi kwa sasa na anaishi maisha ya ujasiri kama mwanamke anayejitegemea.

Read More
 Vera Sidika Amchana Eddie Butita Kuhusu Kauli za Boo Party

Vera Sidika Amchana Eddie Butita Kuhusu Kauli za Boo Party

Socialite wa Kenya Vera Sidika ameonekana kuchukizwa na matamshi ya mchekeshaji Eddie Butita aliyewakosoa wanaume waliohudhuria hafla yake ya hivi karibuni maarufu kama Boo Party. Kupitia video aliyoipakia mitandaoni, Vera amemshutumu Butita kwa kuwa na machungu kwa sababu hakupata mualiko wa kushiriki sherehe hiyo. Amesema hakuna mwanaume timamu ambaye angekataa mwaliko wa hafla kama hiyo, akidai ni wachache tu wenye majungu na wivu wanaoweza kutoa maneno ya kubeza. Aidha, amemshauri Butita kuacha kufuatilia maisha yake na kuacha majungu, akibainisha kuwa siku zijazo huenda akampatia mualiko rasmi ili ahudhurie moja ya sherehe zake. Mapema wiki hii, Vera alifanya Boo Party maalum kwa ajili ya kusherehekea hatua yake ya upasuaji wa urembo, baada ya kufanikisha kuongeza uthabiti wa matiti yake. Hafla hiyo ilivutia hisia tofauti mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza na wengine wakibeza. Kulingana na Butita, hakuelewa sababu ya wanaume kushiriki hafla ya aina hiyo.Alisema kwamba ilikuwa sawa kwa marafiki wa kike wa Vera kumuunga mkono, lakini aliona haikuwa na mantiki kwa wanaume kuhudhuria tukio lililolenga kusherehekea upasuaji wa mwili.

Read More
 Kauli ya Vera Sidika Yazima Uvumi wa Kurudiana na Brown Mauzo

Kauli ya Vera Sidika Yazima Uvumi wa Kurudiana na Brown Mauzo

Socialite maarufu wa Kenya, Vera Sidika, amezima madai yanayoenezwa mitandaoni kuwa anapanga kurudiana na mzazi mwenzake, mwanamuziki Brown Mauzo licha ya kuendelea kushirikiana naye katika malezi ya watoto wao. Kupitia ujumbe aliouweka kwenye Instagram, Vera amekanusha vikali uvumi huo na kueleza kuwa maamuzi yake yamelenga tu kuhakikisha watoto wao wanapata malezi bora. Amesisitiza kwamba hatua ya kuruhusu Brown kuwa karibu na watoto wao haimaanishi kuwa anataka kurejesha mahusiano, bali ni kutambua wajibu wake kama baba. Mwanamama huyo pia amewakumbusha mashabiki wake kuwa alishawahi kuandaa “divorce party” kama alama ya kufunga ukurasa wa ndoa yake na Mauzo, jambo analosema linatosha kuonyesha kuwa hawezi kurudiana naye. Hii inakuja baada ya mijadala kuzuka mitandaoni, mashabiki wakidai kitendo chake cha kumruhusu Brown Mauzo kuja nyumbani kwake na kukaa na watoto wao ni ishara ya wawili hao kutaka kufufua uhusiano wao wa kimapenzi.

Read More
 Vera Sidika Ajibu Ukosoaji Kuhusu Kumruhusu Brown Mauzo Kuwaona Watoto Wao

Vera Sidika Ajibu Ukosoaji Kuhusu Kumruhusu Brown Mauzo Kuwaona Watoto Wao

Mrembo maarufu kutoka Kenya, Vera Sidika, ameweka wazi msimamo wake baada ya kukosolewa kwa uamuzi wake wa kumruhusu aliyekuwa mpenzi wake, mwanamuziki Brown Mauzo, kutumia muda na watoto wao nyumbani kwake. Kupitia Inst story yake, Vera amesema hajawahi kumtegemea Mauzo kwa msaada wa kifedha na kwamba jambo analolipa kipaumbele ni uwepo wake kama baba katika maisha ya watoto wao. Amebainisha kuwa yeye mwenyewe alikulia kwenye familia yenye wazazi wote wawili, jambo lililomfanya atamani watoto wake wapate malezi yenye upendo na uwepo wa baba, bila kujali changamoto za kifedha. Akizungumzia dhamira ya Mauzo kama mzazi, Vera amesema amewahi kushuhudia jinsi alivyovunjika moyo baada ya kuzuiwa kumuona mtoto wake na mama wa mtoto wake kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kwa mujibu wake, hali hiyo ilionyesha wazi jinsi anavyothamini nafasi yake kama baba na hamu yake ya kuwa karibu na watoto wake. Aidha, Vera amekosoa vikali tabia ya baadhi ya akina mama kuwazuia baba kuona watoto wao kwa sababu ya changamoto za kifedha. Alisema kufanya hivyo ni kitendo cha ubinafsi kwa kuwa kinawanyima watoto nafasi ya kupokea upendo na malezi ya baba zao. Kauli ya Vera imezua mjadala mitandaoni, baadhi ya watu wakimsifu kwa ukomavu na mtazamo wake chanya kuhusu malezi ya pamoja, huku wengine wakisisitiza kuwa majukumu ya kifedha nayo ni sehemu muhimu ya malezi ya mzazi.

Read More
 Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Vera Sidika Ajibu Madai ya Kuwatelekeza Watoto Wake

Socialite maarufu nchini Kenya, Vera Sidika, amejibu tetesi kutoka kwa mashabiki waliodai kwamba amewatelekeza watoto wake kwa sababu ya kuwa safarini mara kwa mara. Kupitia ujumbe alioweka mtandaoni, Vera amesisitiza kuwa watoto wake daima wako chini ya uangalizi wa mzazi kila wakati. Amefafanua kuwa anapohitajika kuwa kwenye shughuli zake binafsi au kuendesha mikusanyiko katika nyumba yake ya kifahari, huomba baba ya watoto wake Brown Mauzo kukaa nao muda wote. Aidha,Mwanamama huyo amesema anaposafiri kwenda maeneo mbalimbali duniani, baba ya watoto hubaki nao nyumbani akisaidiana na wafanyikazi wa ndani (nannies) hadi atakaporudi. Kauli hiyo imekuja baada ya walimwengu kwenye mitandao ya kijamii kuibua maswali kuhusu malezi ya watoto wake, baadhi ya watu wakimlaumu kwa kutokuwa karibu nao kutokana na ratiba zake za mara kwa mara za safari na shughuli za kijamii.

Read More
 Vera Sidika Ashtua Wafuasi kwa Kauli Kali Dhidi ya Mammito

Vera Sidika Ashtua Wafuasi kwa Kauli Kali Dhidi ya Mammito

Sosholaiti maarufu wa Kenya, Vera Sidika, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kumtolea uvivu mchekeshaji Mammito Eunice kufuatia kauli yake kuhusu upasuaji wa kuongeza makalio (BBL). Mammito alikuwa ametupa dongo akidai wanawake wengi kutoka jamii ya Luhya wanapendelea sana urembo wa upasuaji, jambo ambalo halikumpendeza Vera. Kupitia Instastory yake, Vera alimjibu kwa kejeli, akimshambulia binafsi na kumshauri akubaliane na hali yake. “The fact hauna pesa ya BBL inashangaza. Please embrace your bones in peace.”, Aliandika Inststory Majibizano hayo yamezua mjadala mkubwa mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakimpongeza Vera kwa kujiamini, huku wengine wakimkosoa kwa kutumia maneno ya kudhalilisha. Tukio hili lilitokea wakati Vera akijaribu kukanusha madai ya wakosoaji waliokuwa wakipotosha kuhusu uhalali wa gari lake la kifahari aina ya Range Rover, ambalo alilishiriki kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Read More
 Asili ya Vera Sidika Yazua Mvutano Mitandaoni

Asili ya Vera Sidika Yazua Mvutano Mitandaoni

Mrembo maarufu mtandaoni Vera Sidika amejipata pabaya mbele ya walimwengu baada ya kudai kuwa watu wengi hudhani anatokea Jamaica au Afrika Kusini kutokana na muonekano wake. Kauli hiyo imeonekana kuwakera baadhi ya mashabiki waliomtaka akubali asili yake kama Mluya kutoka Kakamega badala ya kujipendekeza kwa umma. Mashabiki wengi walimshauri aache drama zisizo na msingi na kujikita zaidi katika malezi ya watoto wake. Wengine walimkosoa vikali wakidai kwamba anampigia mzazi mwenzie, Brown Mauzo, simu nyakati za usiku licha ya wawili hao kuachana rasmi. Baadhi ya wafuasi walionya kwamba kitendo hicho cha kumsumbua Mauzo huenda kikaathiri ndoa ya sasa ya msanii huyo. Hata hivyo, bado kuna kundi dogo la mashabiki wanaomtetea, wakisema kuwa umaarufu wa Vera umevuka mipaka ya Kenya na kwamba si jambo la kushangaza mashabiki wa kimataifa kumhusisha na tamaduni za mataifa mengine kutokana na taswira yake ya kimataifa.

Read More
 Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Vera Sidika Ajigamba: Mimi Ndiye Msanii Pekee Niliye na Range Rover Mpya Kenya

Mrembo maarufu na mfanyabiashara Vera Sidika amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa yeye ndiye msanii pekee nchini Kenya anayeendesha Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, ambayo haijabadilishwa sura (facelift), haijakodishwa wala kukopeshwa. Kupitia mitandao ya kijamii, Vera amejigamba kuwa gari hilo la kifahari ni la kwake binafsi, likiwa katika umbo jipya kabisa ambalo halijawahi kuonekana sana mitaani. Ameongeza kuwa wasanii wengi nchini hupendelea kuonyesha magari ya kukodi au ya mkopo kwa ajili ya kuonyesha maisha ya kifahari, lakini kwake, anamiliki gari hilo kihalali na kwa mapato yake halali. “Ni Range Rover mpya ya muundo wa kisasa, wala si facelift kama zile watu huwa wanaweka za kukodi kwa picha tu,” Vera alisema Katika kuonyesha kiwango cha kifahari alicho nacho, Vera amefichua kuwa gharama ya kufanya photoshoot ya gari hilo pekee ilikuwa kubwa kiasi kwamba ingeweza kununua gari dogo. Kauli hiyo imeibua mijadala mikali miongoni mwa mashabiki, baadhi wakimsifia kwa ufanisi wake wa kifedha, huku wengine wakimtuhumu kwa majigambo na kueneza maisha ya anasa yasiyo na umuhimu mkubwa kwa jamii.

Read More