Willy Paul Awatahadharisha Mashabiki Dhidi ya Mtu Anayejifanya Ndugu Yake

Willy Paul Awatahadharisha Mashabiki Dhidi ya Mtu Anayejifanya Ndugu Yake

Msanii nyota wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, ametoa onyo kali kwa mashabiki wake na umma kwa ujumla kuchukua tahadhari kuhusu mtu anayejifanya kuwa ndugu yake. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Willy Paul amesema kuna mtu anayefanana naye kwa sura ambaye amekuwa akiwahadaa watu kwa kujifanya ni ndugu yake wa karibu, hatua ambayo imemsaidia mhusika huyo kupata misaada na hata kuwahadaa baadhi ya watu kwa maslahi binafsi. Msanii huyo ameweka wazi kuwa hana uhusiano wowote na mtu huyo na kwamba hakumpa ruhusa kutumia jina lake kwa namna yoyote. Ameeleza kusikitishwa na tabia hiyo akisema inaharibu jina lake na inaweza kuwaweka watu hatarini kudhulumiwa au kudanganywa. Willy Paul amewataka mashabiki wake kuwa waangalifu na kuthibitisha taarifa zozote wanazopata kabla ya kuchukua hatua, huku akisisitiza kuwa mawasiliano yake rasmi hupatikana kupitia kurasa zake zilizothibitishwa pekee. Hitmaker huyo wa Party This Year, amedokeza kuwa yuko tayari kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mhusika huyo endapo ataendelea kutumia jina lake vibaya na kuwadanganya watu.

Read More
 Willy Paul Atangaza Hali ya Hatari kwa Wapinzani Kwenye Muziki

Willy Paul Atangaza Hali ya Hatari kwa Wapinzani Kwenye Muziki

Staa wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ametoa onyo kali kwa wakosoaji wake akiwataka wajiandae kwa kipindi kigumu katika mwaka mpya wa 2026, akisema kuwa atakuwa kila mahali kama hewa ya oksijeni. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Willy Paul amesisitiza kuwa hakuna kitu kitakachomzuia kutimiza malengo yake licha ya chuki, maneno ya kukatisha tamaa na ukosoaji unaomkabili mara kwa mara. Msanii huyo amesema kuwa ukimya wake katika kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka 2025 haukuwa dalili ya kupotea, bali ulikuwa ni maandalizi ya kurejea kwa nguvu zaidi. Hata hivyo ameongeza kuwa mwaka 2026 utakuwa wa kihistoria kwake, akiahidi kutoa kazi nyingi zitakazomuweka kwenye kila kona ya tasnia ya burudani, kuanzia redio, mitandao ya kijamii hadi majukwaa ya muziki.

Read More
 Willy Paul Aweka Rekodi Mpya Boomplay Kama Msanii wa Kiume Anayesikilizwa Zaidi

Willy Paul Aweka Rekodi Mpya Boomplay Kama Msanii wa Kiume Anayesikilizwa Zaidi

Msanii nyota wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, ameweka rekodi mpya kwenye jukwaa la muziki la Boomplay baada ya kutajwa kuwa msanii wa kiume anayesikilizwa zaidi kwenye mtandao huo. Willy Paul amefikisha jumla ya wasikilizaji milioni 107 huku wimbo wake “Keki” aliomshirikisha Bahati ukitajwa kuwa wimbo uliosikilizwa zaidi mwaka 2025. Kupitia mitandao ya kijamii, msanii huyo amewashukuru mashabiki wake akisema wameendelea kumuunga mkono kwa dhati, jambo lililomfikisha kileleni katika safari yake ya muziki. Rekodi hii mpya inaongeza orodha ya mafanikio ya Willy Paul na inaonyesha wazi kuwa bado ni mmoja wa wasanii wenye nguvu kubwa katika soko la muziki wa kidijitali nchini Kenya na kanda ya Afrika Mashariki.

Read More
 Willy Paul Akiri Kuogopa Kufanya Kazi na Bien Baada ya Tukio la Matusi Studio

Willy Paul Akiri Kuogopa Kufanya Kazi na Bien Baada ya Tukio la Matusi Studio

Msanii nyota wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ametangaza hadharani kuwa hatofanya kazi ya pamoja tena na msanii wa Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza baada ya tukio la matusi studioni. Akifafanua uamuzi wake, Willy Paul ameeleza kuwa wakati wa ushirikiano wao wa awali alikumbana na mazingira magumu yenye matusi na maneno ya kudhalilisha. Amedai kuwa wakati wa kurekodi wimbo wao wa pamoja, alikumbana na matusi ya mara kwa mara bila sababu za msingi wakiwa studioni, hali iliyomfanya ajihisi kudhalilishwa na kuumizwa kisaikolojia. Miaka mitano iliyopita, wawili hao walitoa wimbo uitwao “Kamati ya Roho Chafu”, uliopata mafanikio makubwa sokoni. Hata hivyo, Willy Paul sasa amefichua kuwa nyuma ya mafanikio hayo kulikuwa na kumbukumbu chungu isiyofurahisha. Kwa sasa, msanii huyo ameweka msimamo thabiti kuwa hataki kurudia makosa ya zamani, akisisitiza kuwa hakuna uwezekano wa ushirikiano mwingine kati yake na Bien katika siku zijazo.

Read More
 Willy Paul Akanusha Madai kuwa VJ Patelo Ndio Amefanya Wimbo Wake Kuwa Hit

Willy Paul Akanusha Madai kuwa VJ Patelo Ndio Amefanya Wimbo Wake Kuwa Hit

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, amekanusha vikali madai yanayosambaa mtandaoni kwamba umaarufu wa wimbo wake mpya “Hii Design” umetokana zaidi na dance challenge ya VJ Patelo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul amepinga vikali madai hayo, akisema kuwa mafanikio ya wimbo huo yanatokana na ubora wake, sio juhudi za mtu mmoja kama inavyodaiwa. Amesema kuwa watu wanapaswa kuacha kudharau kazi yake na kuhusisha mafanikio ya “Hii Design” na challenge hiyo pekee, akisisitiza kuwa wimbo tayari ulikuwa na nguvu kubwa wenyewe. Msanii huyo ameongeza kuwa track hiyo ni kali na imepokelewa vyema na mashabiki hata kabla ya challenge kuanza kusambaa. Tangu kuachiwa kwa wimbo huo, baadhi ya mashabiki wamekuwa wakidai kuwa challenge ya VJ Patelo imechangia pakubwa kupandisha watazamaji na kuifanya ngoma hiyo kuwa maarufu kwenye mitandao ya kijamii.

Read More
 Willy Paul: Siwezi Kuwa Kwenye Mahusiano na Mwanamke Mlevi

Willy Paul: Siwezi Kuwa Kwenye Mahusiano na Mwanamke Mlevi

Staa wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ameweka wazi msimamo wake kuhusu mahusiano ya kimapenzi, akisema hawezi kamwe kuwa na uhusiano na mwanamke mlevi. Kupitia ujumbe aliouweka mtandaoni, , Willy Paul amesema kuwa anapendelea kubaki single kuliko kujihusisha kimapenzi na mwanamke anayependa pombe kupita kiasi. Mkali huyo wa ngoma ya Ngunga, amesema wanawake wa aina hiyo mara nyingi hawana nidhamu wala mwelekeo wa maisha, jambo analoliona halifai kwa mtu anayemtafuta mwenza wa kweli. Hata hivyo ameongeza kuwa anaomba Mungu amuepushe na wanawake wenye tabia za ulevi, akisisitiza kuwa heri abaki bila mpenzi kuliko kuwa na mwanamke mlevi.

Read More
 Willy Paul Alalamikia Mashabiki Kutompa Heshima Anazostahili

Willy Paul Alalamikia Mashabiki Kutompa Heshima Anazostahili

Staa wa muziki kutoka nchini Kenya, Willy Paul, ameelezea masikitiko yake kuhusu jinsi mashabiki wa muziki wa Kenya wanavyomchukulia poa, akidai kuwa licha ya mafanikio yake makubwa kimataifa, bado hatambuliwi ipasavyo nyumbani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, msanii huyo amesema kuwa yeye ndiye msanii pekee wa Kenya ambaye nyimbo zake zinachezwa zaidi kimataifa kuliko za wasanii wengine wengi, lakini mashabiki wa ndani wanapuuzia juhudi zake. Willy Paul amesisitiza kuwa ukweli unabaki kuwa yeye ndiye msanii anayejulikana zaidi nje ya nchi na anaamini kuwa muda utakuja ambapo mashabiki wa nyumbani watatambua thamani ya kazi zake. Kauli yake imekuja baada ya content creator wa mitandaoni Ruth K kumtaja kama msanii wa kimataifa anayepaswa kupewa heshima zaidi kutokana na ushawishi wake nje ya mipaka ya Kenya.

Read More
 Willy Paul Asema Ameoa Rasmi, Apuuza Video ya Zamani

Willy Paul Asema Ameoa Rasmi, Apuuza Video ya Zamani

Msanii wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, amejitokeza kufafanua kuhusu video ya zamani iliyosambaa mtandaoni ikimuonyesha akisema kwamba hatawahi kuoa. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Willy Paul amefafanua kuwa video hiyo ni ya kitambo, kabla hajaoa, na kwamba kwa sasa yuko kwenye ndoa halali na mke wake anayemuita my Ngunga. Ameonyesha kuchukizwa na jinsi mashabiki wanavyotumia video za zamani kuvuruga maisha yake ya sasa ya ndoa. Msanii huyo amesisitiza kuwa anataka watu waheshimu ndoa yake na waache kutumia taarifa za zamani kumharibia jina. Aidha, ametumia fursa hiyo kueleza kuwa kwa sasa yuko katika kipindi kipya cha maisha kinachozingatia familia na kazi yake ya muziki. Kauli yake imekuja mara baada ya video yake kusambaa mitandaoni akisema hana mpango wa kuoa, akisisitiza kuwa kiwango cha usaliti katika mahusiano ya sasa kimekuwa kikubwa mno, jambo linalomfanya asione sababu ya kuingia kwenye ndoa.

Read More
 Willy Paul Asema Hataki Ndoa Maishani Mwake

Willy Paul Asema Hataki Ndoa Maishani Mwake

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, amewashangaza mashabiki wake baada ya kufichua kwamba hana mpango wa kuoa, licha ya kuwa na moja ya nyimbo kubwa zaidi katika taaluma yake inayotumika sana kwenye harusi. Kupitia mahojiano aliyofanya hivi karibuni, Willy Paul amesema kuwa kiwango cha usaliti katika mahusiano ya siku hizi kimemfanya apoteze imani katika ndoa. Kwa mujibu wake, watu wengi wamekuwa wakisaliti wenza wao, jambo ambalo limeharibu maana halisi ya upendo wa kweli. Msanii huyo ambaye amewahi kutoa nyimbo kadhaa za mapenzi, ikiwemo wimbo wa “Yes I Do” unaotumika sana kama wedding anthem, amesema kuwa licha ya mafanikio yake katika muziki wa mapenzi, hana mpango wa kuingia kwenye ndoa kwa sasa. Willy Paul amesema anachagua kuzingatia kazi yake ya muziki badala ya kuhusisha maisha yake binafsi na ndoa ambayo, kwa mtazamo wake, si imara tena katika kizazi cha leo.

Read More
 Willy Paul Atoa Wito wa Kuanzishwa kwa Siku Maalum ya “Raila Odinga Day”

Willy Paul Atoa Wito wa Kuanzishwa kwa Siku Maalum ya “Raila Odinga Day”

Staa wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ametoa wito kwa serikali kuanzisha siku maalum ya kitaifa iitwayo “Raila Odinga Day” na kusimika sanamu ya kiongozi huyo Jijini Nairobi kama ishara ya heshima kwa mchango wake mkubwa kwa taifa. Kupitia ujumbe alioutoa kwenye mitandao ya kijamii, Willy Paul amesema hatua hiyo itakuwa njia bora ya kudumisha urithi wa kisiasa na kijamii wa aliyekuwa Waziri Mkuu, hayati Raila Amolo Odinga, ambaye amekuwa nembo ya mapambano ya demokrasia nchini Kenya kwa zaidi ya miongo mitatu. Wito wa Willy Paul unakuja wakati taifa linaendelea kuomboleza kifo cha kiongozi huyo mashuhuri, ambaye alizikwa jana katika nyumba yake ya milele huko Bondo, kaunti ya Siaya. Endapo pendekezo hilo litatekelezwa, “Raila Odinga Day” itakuwa miongoni mwa siku za kitaifa zinazoheshimu viongozi waliotoa mchango mkubwa kwa taifa, huku sanamu yake katikati ya jiji la Nairobi ikitarajiwa kuwa alama ya kumbukumbu na heshima ya kizazi kijacho.

Read More
 Willy Paul Akarabati Duka la Pozze Liquor Baada ya Kuvamiwa

Willy Paul Akarabati Duka la Pozze Liquor Baada ya Kuvamiwa

Staa wa muziki Willy Paul ametangaza kurejea kwa huduma katika duka lake la vileo, Pozze Liquor, siku chache baada ya wahuni kuvamia na kuharibu mali ya thamani ya mamilioni ya fedha. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul ameeleza kuwa duka hilo limekarabatiwa kikamilifu, limejazwa upya bidhaa, na sasa limeboreshwa mara kumi zaidi. Hitmaker huyo wa Ngunga, ameshukuru mashabiki wake kwa maombi na usaidizi waliompa wakati wa kipindi kigumu, akisisitiza kuwa uharibifu uliotokea haukuwa mkubwa kuliko imani yake kwa Mungu. Duka la Pozze Liquor lililoko jijini Nairobi linajulikana kwa kuuza vileo vya kiwango cha juu na limekuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki wa msanii huyo. Mashabiki wengi wamempongeza kwa kurejea kwa nguvu upya, wakimtaja kama mfano wa uvumilivu na bidii katika biashara.

Read More
 Willy Paul Atoa Wito kwa Umma Kuwasaidia Kuwatambua Wezi Walioiba Duka Lake

Willy Paul Atoa Wito kwa Umma Kuwasaidia Kuwatambua Wezi Walioiba Duka Lake

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, ametoa wito kwa umma kumsaidia kuwatambua wahalifu waliovamia na kupora duka lake la pombe. Tukio hilo lilinaswa kwenye kamera za CCTV ambazo sasa msanii huyo ameziweka wazi hadharani kupitia ukurasa wake wa Instagram. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul amesema kuwa tayari amepata video kamili ya tukio hilo, ikionyesha wazi sura za wahusika waliohusika. Kwenye video hiyo, anaeleza kuwa mtu mmoja aliyekuwa amevaa koti jeupe na mwanamke aliyeonekana akiwa amevalia mavazi meusi yote ndio wanaoonekana kuongoza uvamizi huo. Msanii huyo amehimiza umma kutoa taarifa yoyote itakayosaidia katika kuwatambua wahusika hao, akisisitiza kuwa polisi wameanza uchunguzi na wamechukua hatua za haraka kuhakikisha waliohusika wanakamatwa. Tukio hilo limezua hisia kali mitandaoni baada ya CCTV kuonyesha namna uvamizi huo ulivyotekelezwa, ambapo kundi la watu liliingia kwa nguvu na kupora bidhaa mbalimbali kwenye duka hilo la pombe, lililodaiwa kushambuliwa na wahuni waliopangwa.

Read More