Willy Paul Afunguka Kujihusisha na Kiki Kabla ya Kuachia Nyimbo

Willy Paul Afunguka Kujihusisha na Kiki Kabla ya Kuachia Nyimbo

Msanii wa muziki wa Kenya, Willy Paul, amefunguka hadharani baada ya kukosolewa na baadhi ya mashabiki kwa kujihusisha na kiki au kuvutia umaarufu kabla ya kuachia kazi zake mpya. Kupitia Insta Story, Willy Paul ameeleza kuwa tabia hiyo ya kudhaniwa kuwa anafuata umaarufu ni sehemu ya mitazamo potofu ya baadhi ya mashabiki, na kwamba lengo lake ni kushirikiana na mashabiki wake na kuhakikisha nyimbo zake zinawafikia watu wengi. Mkali huyo wa Toto, ameongeza kuwa kutumia mitandao ya kijamii kuendesha mijadala au kuunganisha mashabiki siyo kutafuta kiki au clout bali ni mbinu ya kisasa ya kukuza muziki. Aidha, msanii huyo amesema kuwa kwa muda mrefu amekuwa akijitahidi kuunda uhusiano wa karibu na wapenzi wa muziki wake, huku akisisitiza kuwa kila hatua ya matangazo ya nyimbo yake ni kwa lengo la kushirikisha mashabiki na si kwa kujihusisha na umaarufu bandia. Kauli yake imekuja mara baada ya kushtumiwa na VJ Patelo kwa kukaidi makubaliano ya malipo baada ya video shoot, madai yaliyowafanya mashabiki kuhisi alitengeneza mazingira ya kuzungumziwa mtandaoni kabla ya kuachia wimbo wake mpya Ijumaa wiki hii.

Read More
 Willy Paul Akosoa Waandaaji wa CHAN kwa Kupuuza Wasanii wa Kenya

Willy Paul Akosoa Waandaaji wa CHAN kwa Kupuuza Wasanii wa Kenya

Msanii wa Kenya, Willy Paul, ameibua maswali kuhusu uteuzi wa wasanii waliopangwa kutumbuiza katika fainali ya Mashindano ya CHAN 2024 yatakayofanyika leo Jumamosi katika uwanja wa Kasarani ambapo Morocco itachuana na Madagascar. Kupitia Instastory,Willy Paul ameonekana kutoridhishwa na uteuzi huo, akidokeza kuwa waandaaji huenda walipuuzia nafasi ya kuhusisha wasanii wengine wa Kenya ambao wangeweza kupeperusha bendera ya taifa ipasavyo kwenye tukio hilo kubwa. Kauli ya Willy Paul sasa imechochea mjadala mitandaoni kuhusu nafasi ya wasanii wa Kenya katika matukio ya kimataifa, huku baadhi ya mashabiki wakihisi kuwa nchi inapaswa kupewa nafasi kubwa zaidi kupitia muziki wake kwenye majukwaa ya aina hii. Hayo yote yaliibuka muda mfupi baada ya waandaaji wa mashindano hayo kutangaza kuwa Savara wa Sauti Sol, nyota wa Tanzania Zuchu, na mshindi wa tuzo za kimataifa kutoka Uganda Eddy Kenzo, sio tu watatumbuiza siku ya fainali, bali pia wameandaa na kuimba anthem rasmi ya CHAN 2024.

Read More
 Willy Paul Aonya Wanaume Wanaopoteza Muda Kwa Wanawake

Willy Paul Aonya Wanaume Wanaopoteza Muda Kwa Wanawake

Msanii wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kujitokeza kama mshauri nasaha kwa wanaume, akiwataka kuweka kipaumbele maendeleo yao binafsi badala ya kutumia muda mwingi kuwafuata wanawake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul aliwahimiza wanaume kuelekeza nguvu na muda wao katika kutafuta fedha na kujijenga kimaisha. Alisisitiza kuwa tabia ya kuwabembeleza wanawake kupita kiasi inaweza kuwapotezea muda muhimu na kuwazuia kufanikisha malengo yao ya maisha. Kauli hiyo imezua maoni mseto miongoni mwa mashabiki, hasa ikizingatiwa kuwa inakuja siku moja tu baada ya kumshauri msanii mwenzake, Okello Max, ajikite zaidi katika kazi yake ya muziki. Alionya kuwa mienendo hiyo inaweza kuhatarisha mustakabali wa taaluma yake. Willy Paul, anayejulikana kwa mitazamo yake yenye utata, ameendelea kutumia mitandao ya kijamii kama jukwaa la kutoa ushauri na maoni kuhusu masuala ya kijamii na maisha ya vijana.

Read More
 Willy Paul Ampa Okello Max Ushauri Kuhusu Wanawake

Willy Paul Ampa Okello Max Ushauri Kuhusu Wanawake

Msanii nyota wa muziki wa Kenya, Willy Paul, ametoa ushauri kwa msanii Okello Max, akimtaka kuzingatia nidhamu ya maisha ili kuimarisha safari yake ya muziki. Katika ujumbe wake, Willy Paul alimpongeza Okello Max kwa kipaji chake cha kipekee, akisema ana uwezo mkubwa wa kisanaa na nafasi kubwa ya kufanikisha ndoto zake. Hata hivyo, alieleza kuwa kikwazo kikuu kwa msanii huyo ni masuala ya wanawake, akiongeza kwamba kuyashughulikia kwa umakini kutamwezesha kufika mbali zaidi katika taaluma yake. Ushauri huo umeibua maoni mchanganyiko mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakionyesha kukubaliana na hoja ya Willy Paul kwa kueleza kuwa maisha ya usanii yanahitaji nidhamu na umakini. Wengine, hata hivyo, walichukulia kauli hiyo kama utani wa kirafiki unaodhihirisha urafiki wa karibu kati ya wasanii hao wawili. Okello Max, ambaye amejizolea umaarufu kupitia sauti yake laini na mchanganyiko wa mitindo ya R&B na afrobeat, amekuwa akipanda chati za muziki nchini kwa wimbo na kolabo mbalimbali. Mashabiki wake sasa wanasubiri kuona kama atachukua hatua kufuatia ushauri huo wa wazi kutoka kwa Willy Paul, ambaye pia amepitia changamoto nyingi katika safari yake ya muziki na mara kwa mara hujitokeza kutoa maoni kwa wanamuziki chipukizi na wenzake.

Read More
 Willy Paul Amkosoa Jalang’o kwa Kumtema Luo Festival

Willy Paul Amkosoa Jalang’o kwa Kumtema Luo Festival

Mwanamuziki Willy Paul ameonyesha kukerwa na hatua ya mbunge wa Lang’ata, Phelix Odiwuor maarufu Jalang’o, ya kutomualika kutumbuiza kwenye tamasha la Luo Festival iliyofanyika wikiendi hii iliyopita. Kupitia ujumbe wake mtandaoni, Willy Paul ameonekana kushangaa na kuhoji sababu ya kuachwa nje ya orodha ya wasanii waliopangwa kutumbuiza, akisisitiza kuwa ana uhusiano wa karibu na jamii ya Wajaluo na alipaswa kupewa nafasi kwenye hafla hiyo. Tukio hilo limezua mjadala mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakimtaka Jalang’o kuzingatia vipaji mbalimbali bila kujali kabila au historia ya msanii, huku wengine wakieleza kuwa huenda kulikuwa na sababu za kiutendaji zilizosababisha msanii huyo kutoalikwa. Luo Festival ni moja ya matukio makubwa ya burudani yanayoandaliwa kila mwaka, yakileta pamoja maelfu ya mashabiki wa muziki na burudani kutoka pembe mbalimbali za nchi.

Read More
 Wimbo wa Willy Paul “Yes I Do” Wavuka Mipaka, Wapata Umaarufu Asia Pacific

Wimbo wa Willy Paul “Yes I Do” Wavuka Mipaka, Wapata Umaarufu Asia Pacific

Msanii maarufu wa muziki kutoka Kenya, Willy Paul, ameandika historia mpya katika safari yake ya muziki baada ya wimbo wake wa mapenzi “Yes I Do” kuanza kuvuma kwa kasi katika mataifa mawili ya visiwani Timor Leste na Fiji, yaliyoko kwenye ukanda wa Asia Pacific. Wimbo huo, aliouachia rasmi tarehe 28 Februari 2017 kwa kushirikiana na msanii mashuhuri kutoka Jamaica, Alaine, umeendelea kuwa na mvuto wa kipekee kwa mashabiki wapya, licha ya miaka kadhaa kupita tangu uzinduliwe. Kwa sasa, video ya “Yes I Do” kwenye YouTube ina zaidi ya watazamaji milioni 32, jambo linaloashiria mafanikio yake ya kudumu na ushawishi mkubwa wa muziki huo wa mapenzi. Kwa mujibu wa takwimu kutoka mitandao ya kijamii na majukwaa ya kidijitali ya kusikiliza muziki, “Yes I Do” imekuwa maarufu miongoni mwa vijana wa Timor Leste na Fiji, wengi wao wakiutumia kwenye video za TikTok, Instagram Reels, pamoja na maonyesho ya densi ya mtandaoni. Wimbo huo kuvuma, unadhihirisha uwezo wa muziki wa Afrika kufika mbali zaidi ya mipaka ya lugha, bara au tamaduni. Kufanikiwa kwa wimbo huo katika ukanda wa Asia Pacific ni hatua kubwa kwa Willy Paul, ambaye amekuwa akifanya juhudi kwa miaka kadhaa kupanua wigo wa muziki wake hadi kimataifa. Ingawa anajivunia umaarufu mkubwa ndani ya Afrika Mashariki, kupenya kwa kazi yake katika nchi za mbali ni ushahidi kuwa muziki wake unagusa mioyo ya watu duniani kote. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Willy Paul amewashukuru mashabiki wake kutoka Timor Leste na Fiji kwa mapokezi ya dhati na kuashiria kuwa anapanga kufanya ziara ya kimataifa au kushirikiana na wasanii wa eneo hilo katika siku zijazo. Kwa sasa, “Yes I Do” si tu wimbo maarufu kutoka Kenya, bali pia ni alama ya ushindi kwa muziki wa Kiafrika, ukithibitisha kuwa sauti ya Afrika inaweza kusikika na kupendwa kila pembe ya dunia.

Read More
 Willy Paul Awataka Mashabiki Wamsaidie Kuchagua Location ya Video Mpya

Willy Paul Awataka Mashabiki Wamsaidie Kuchagua Location ya Video Mpya

Msanii maarufu wa muziki wa Kenya, Willy Paul, ametangaza kuwa kwa sasa yuko katika harakati za kutafuta eneo bora la kupigia video ya wimbo wake mpya. Kupitia mitandao ya kijamii, mwanamuziki huyo alisema kuwa ana mipango mikubwa ya kuhakikisha video hiyo inakuwa ya kiwango cha juu, na hivyo anahitaji mandhari ya kuvutia itakayoendana na ubora wa kazi yake. “Natafuta location kali ya kushoot music video. Mnaweza nisaidia na ideas?” aliandika Willy Paul. Mashabiki wake wamejitokeza kwa wingi na kutoa mapendekezo tofauti, baadhi wakimtajia maeneo kama: Ngong Hills, The Alchemist, Westlands, Karura Forest, Watamu au Diani Beach na Nairobi Railway Museum. Willy Paul, ambaye hivi majuzi amekuwa akizua gumzo kutokana na mabadiliko ya kimuziki na mitindo, anaonekana kutaka kupeleka ubunifu wake kwenye kiwango kingine. Wimbo huu mpya unatarajiwa kuwa sehemu ya mradi mkubwa anaotarajia kuuzindua kabla ya mwisho wa mwaka. Mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona ni eneo gani atakalochagua na iwapo video hiyo itavunja rekodi kama kazi zake za awali

Read More
 Willy Paul Aitaka KPLC Kufidia Uharibifu wa Studio Yake Baada ya Hitilafu ya Umeme

Willy Paul Aitaka KPLC Kufidia Uharibifu wa Studio Yake Baada ya Hitilafu ya Umeme

Mwanamuziki wa Kenya, Willy Paul, ameibua hasira mitandaoni dhidi ya Shirika la Umeme nchini (KPLC) baada ya kudai kuwa vifaa vyake vyote vya studio vimeungua kutokana na hitilafu ya umeme. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Willy Paul alitoa ujumbe mkali kwa KPLC, akisisitiza kuwa wanapaswa kumlipa fidia kwa hasara aliyopata. “KPLC YOU MUST PAY!! ALL MY STUDIO EQUIPMENTS ARE NO MORE!! MMENICHOMEA KILA KITU KWA STUDIO, NOT JUST ME, THE WHOLE ESTATE HAS LOST VALUABLES!!! KPLC YOU MUST PAY ME!!!!” aliandika kwa ukali. Msanii huyo, ambaye pia ni mmiliki wa lebo ya muziki, amesema tukio hilo halikumdhuru yeye pekee, bali wakaazi wote wa mtaa anaoshi wamepoteza mali zao kutokana na hitilafu hiyo ya umeme. Ingawa hajatangaza thamani halisi ya vifaa vilivyoharibika, Willy Paul alisisitiza kuwa alikuwa amewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye studio hiyo. Mashabiki wake wengi wametuma jumbe za kumuunga mkono, huku wengine wakitaka KPLC kuwajibika na kueleza chanzo cha tatizo hilo. Hadi sasa, KPLC haijatoa tamko rasmi kuhusu madai ya msanii huyo. Wito wake wa kulipwa fidia kutoka KPLC umeibua mjadala mkubwa kuhusu uwajibikaji wa kampuni hiyo katika kusababisha uharibifu wa mali kutokana na hitilafu za umeme, suala ambalo limekuwa likijirudia kwa miaka mingi.

Read More
 Willy Paul Afungua Rasmi Duka la Pombe “Pozze Liquor” Jijini Nairobi

Willy Paul Afungua Rasmi Duka la Pombe “Pozze Liquor” Jijini Nairobi

Msanii maarufu wa muziki nchini Kenya, Willy Paul, amejiunga rasmi na biashara ya vinywaji baada ya kuzindua duka lake jipya la pombe linaloitwa Pozze Liquor. Duka hili limefunguliwa katika jengo la Safari Business Arcade, barabara ya USIU, jijini Nairobi. Kupitia mitandao ya kijamii, Willy Paul alithibitisha ufunguzi huo rasmi na kuwakaribisha mashabiki pamoja na wateja wote kutembelea duka hilo. Mwanamuziki huyo amesema lengo lake ni kutoa vinywaji vya ubora wa juu huku akichangia katika kukuza ajira kwa vijana. Willy Paul, anayejulikana kwa hits kali kama “Sitolia” na “Tamu Walahi”, anaendelea kupanua wigo wake wa biashara huku akitumia umaarufu wake kuvutia wateja kwenye sekta mbalimbali. Mashabiki wake wameonyesha furaha na kumpongeza kwa hatua hiyo mpya ya kibiashara, wakimtakia mafanikio mema katika safari yake ya ujasiriamali.

Read More
 Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Willy Paul akosolewa kwa kutumia Kshs millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake

Staa wa muziki nchini Kenya Willy Paul anazidi kupata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki mbali mbali wa muziki baada ya msanii huyo kuweka wazi kuwa alitumia kiasi cha shillingi millioni 3.5 kuandaa video ya wimbo wake mpya ‘Keki’ aliyomshirikisha Bahati. Kupitia post aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram akijinadi kutumia kiasi hicho cha fedha kwenye uandaaji wa video ya ngoma hiyo, baadhi ya mashabiki walioachia maoni yao kwenye chapisho hilo wameonekana kutofurahia viwango alivyoonesha kwenye nyimbo alizoziachia rasmi Januari 31 ambazo ni Keki pamoja na Paah. Kulingana na kauli za mashabiki, licha ya Willy Paul kutumia nguvu nyingi kutangaza ujio wa kazi hizo, alifeli kwenye suala la uandishi wa nyimbo wakihoji kuwa msanii ameishiwa na ubunifu wa kutoa nyimbo za kuvutia. Aidha wamempa changamoto kuwatafuta waandishi wazuri wa nyimbo na kuwalipa ili waweze kumuandikia nyimbo ambazo zina maudhui ya kuburudisha jamii sambamba na kuelimisha. Katika hatua nyingine wamemshauri kubadilisha prodyuza anayetayarisha kazi zake za muziki kutokana na kukosa ubunifu wa kuandaa nyimbo zinazoendana na nyakati zilizopo. Willy Paul ambaye yupo mbioni kuandaa tamasha lake muziki mnamo Februari 14 mwaka huu amepokea ukosoaji mkubwa sio tu kutoka kwa mashabiki bali pia kutoka kwa maprodyuza wa muziki nchini, wa hivi punde akiwa ni prodyuza Vinc on The Beat ambaye ameonekana kutoridhishwa na kiwango cha msanii huyo baada ya kuachia nyimbo mbili kwa pamoja alizomshirikisha msanii Bahati ambaye ni hasimu wake wa muda mrefu kwenye muziki.

Read More
 Willy Paul afunguka gharama aliyotumia kutayarisha wimbo wake mpya

Willy Paul afunguka gharama aliyotumia kutayarisha wimbo wake mpya

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo Willy Paul ameweka wazi gharama aliyotumia kutayarisha wimbo wake mpya uitwao “Umeme”. Kupitia ukurasa wake wa Instagram bosi huyo wa Saldido amejinasibu kuwa alitumia kiasi cha shillingi laki 5 kurekodi audio ya wimbo huo huku kutayarisha video ikimgharimu takriban shilling million 2 za Kenya. Haikushia hapo ameenda mbali zaidi na kujinadi kuwa yeye ndiye msanii wa kwanza kutumia kiasi hicho cha fedha katika tasnia ya muziki nchini Kenya. Hata hivyo amemalizia kwa kusema kuwa mwaka 2023 ataangazia ubora kwenye kutayarisha kazi zake za muziki na sio idadi ya nyimbo ambazo hazina ubora wowote. Kauli ya Willy Paul inakuja wakati anajiandaa kuachia video ya wimbo wake mpya “Umeme”, ambayo audio yake imefikisha Zaidi ya views laki 3 kwenye mtandao wa Youtube tangu iachiwe rasmi mapema mwaka huu.

Read More
 Willy Paul awajia juu wanablogu wa Kenya kwa kutangaza wasanii wa kigeni

Willy Paul awajia juu wanablogu wa Kenya kwa kutangaza wasanii wa kigeni

Msanii asiyeishwa na matukio kila leo, Willy Paul ameamua kuwachana mablogger wa Kenya kwa kile anachodai kuwa wamekosa uzalendo kwenye mchakato mzima wa kuwaunga mkono wasanii wa ndani (local artistes). Kupitia instastory yake ametoa ya moyoni kwa kusema kuwa njaa ya pesa imewaponza wanablogu wa humu nchini kiasi cha kuanza kutangaza sana muziki wa kigeni kwenye mitandao yao ya kijamii ilhali Kenya kuna wasanii wengi wenye vipaji. Bosi huyo wa “Saldido” amesema tatizo hilo lisipopata mwarubaini huenda tasnia ya muziki nchini ikapoteza mwelekeo kwani ma-blogger wa Kenya wamerubuniwa na mapromota wa nje ambao wamekuwa wakiwahonga mkwanja mrefu ili wawape wasanii wao kipau mbele kwenye majukwaa tofauti mtandaoni. Hata hivyo ametoa changamoto kwa wasanii kuamka na kupambania kazi zao ziwafikie watu wengi duniani kutokana na usaliti ambao wameoneshwa na wakenya wenzao.

Read More