Willy Paul atangaza hali ya hatari mwaka 2023

Willy Paul atangaza hali ya hatari mwaka 2023

Ikiwa tunaelekea mwishoni mwa mwaka 2022, Msanii Willy Paul amefunguka kubadili aina maisha yake mwaka 2023. Kupitia instastory yake msanii huyo ametoa ya moyoni kwa kusema kwamba amechukua hatua hiyo kuwaepuka marafiki wanafiki waliokuwa wanamtafuta kipindi cha matatizo. Bosi huyo wa Saldido amesema mwaka huu umempa funzo kuwa mtu maarufu huwa na marafiki pale tu anapokuwa juu lakini akipata matatizo hutengwa na hata watu wake wa karibu. Hata hivyo amesema watu pekee ambao atawapa kipaumbele maishani mwake kama marafiki zake wa dhati mwaka 2023 ni mama yake mzazi pamoja na watoto wake.

Read More
 Willy Paul adai umaarufu umemnyima uhuru mtaani

Willy Paul adai umaarufu umemnyima uhuru mtaani

Hitmaker wa “Tamu Wallahi”, Msanii Willy Paul amedai kwamba stress ya umaarufu imemnyima uhuru wa kutembea mitaani na kufanya shughuli zake kwa amani. Hii ni baada ya watu wasiojulikana kumvamia na kumdhalilisha akiwa Casavara Lounge Jijini Nairobi ambako alienda kuwachukua marafiki zake waliokuwa wamekwama katika chimbo hilo la burudani. Kupitia instastory yake ameandika ujumbe wa masikitiko akieleza namna watu wamekuwa wakitumia jina lake kujitakia makuu huku akiwataka mashabiki kutomuona wa kitofauti kwani yeye ni binadamu wa kawaida kama watu wengine. Aidha ameenda mbali na kujinasibu kuwa anashukuru Mungu kumpa moyo wa kutolipiza kisasi kipindi ambacho watu wanamvunjia heshima kwa kumshushia matusi na taarifa za uongo mtandaoni.

Read More
 Willy Paul atamba kuwa msanii pekee Kenya kupenya Kimataifa

Willy Paul atamba kuwa msanii pekee Kenya kupenya Kimataifa

Nyota wa muziki nchini Willy Paul ameingia kwenye headlines kwa mara nyingine, mkali huyo kwa sasa amekuwa ni mtu wa kutupa Breaking News kila uchao hii ni baada ya kusema kuwa yeye ndiye msanii wa kwanza Kenya kushika namba moja kwenye mtandao maarufu duniani wa The Shaderoom kupitia single yake “I DO.” Kupitia instastory yake Willy Paul ameeleza kuwa wimbo huo pia ulishika nafasi ya pili kwenye mtandao wa Apple TV USA lakini hakuna blogu yeyote nchini iliandika kuhusu mafanikio yake hayo kwa sababu kipindi hicho hakuwa msanii wao pendwa. Hata hivyo, ameenda mbali zaidi na kutamba kuwa mwakani anaenda kuandika historia yake kipekee kwenye muziki wake huku akiwasihi mashabiki wamuunge mkono katika harakati za kuupeleka muziki wa Kenya kimataifa la sivyo atajipambania mwenyewe na mtu asije akafurahia juhudi zake. Kauli ya Willy Paul inakuja siku chache mara baada ya kujinasibu kuwa yeye ndio msanii pekee kutoka Afrika Mashariki ambaye ana ngoma ambayo imepenya Kimataifa huku akiutaja wimbo wake wa “I DO” kama wimbo ambao unapigwa duniani kote.

Read More
 Willy Paul amtukana matusi ya nguoni msanii chipukizi kwa kukosoa muziki wake

Willy Paul amtukana matusi ya nguoni msanii chipukizi kwa kukosoa muziki wake

Staa wa muziki nchini Willy Paul ameamua kumjibu msanii chipukizi aitwaye JR Music Kenya kwa kukosoa uimbaji wake kwenye muziki. Kupitia ukurasa wake wa Twitter amedai kuwa hajawahi kumlazimisha mtu kusikiliza muziki wake  na yeyote ambaye anahisi nyimbo zake hazifurahishi arekodi wimbo wake mwenyewe ambao utamfurahisha. Hitmaker huyo wa “Tamu Walahi” ametoa matusi ya nguoni kwa msanii huyo kwa kusema kwamba hana muda wa kupishana naye kwa sasa ikizingatiwa kuwa amejikita zaidi kwenye suala la kutoa muziki mzuri. Kauli ya Willy Paul imekuja mara baada ya msanii JR Music kudai anashangazwa namna Willy paul anashindana na Bahati wakati muziki wao duni huku akionekana kumuunga mkono Mchekeshaji Eric Omondi ambaye amekuwa akiwashinikiza wasanii wa Kenya waache kulaza damu kwenye muziki wao. Hakuishia hapo alienda mbali zaidi na kuuponda muziki wa msanii Otile Brown kwa kusema kwamba msanii huyo ameishiwa na mawazo kwa sababu katika siku za karibuni amekuwa akilazimisha mistari kwenye nyimbo zake. Hata hivyo baadhi watumiaji wa mitandao ya kijamii wamemkingia kifua Willy Paul kwa kumshambulia jamaa huyo kwa kusema kuwa atoe muziki mzuri kwanza badala ya kutumia majina ya wasanii hao kujitafutia umaarufu.

Read More
 Jovial akanusha uvumi wa kutoka kimapenzi na Willy Paul

Jovial akanusha uvumi wa kutoka kimapenzi na Willy Paul

Msanii wa kikw kutoka Kenya Jovial  kwa mara ya kwanza amevunja kimya chake kuhusu uvumi wa kutoka kimapenzi na msanii mwenzake Willy Paul. Akimjibu shabiki kupitia ukurasa wake wa Facebook, Jovial ameweka wazi kuwa Pozee sio mpenzi wake kama watu wanavyodai mitandaoni huku akisisitiza kuwa uhusiano wake na bosi huyo wa saldido ulikuwa wa kikazi tu na si vinginesvyo. “Je, Pozee ni mpenzi wako wa dhati?” Shabiki mmoja aliuliza. Jovial akamjibu “Itoshe! Pozee si mpenzi wangu! Ni rafiki tu, ilikuwa biashara ambapo sote tulipata faida! Kwa sasa tumerudi kwa maisha yetu ya kawaida,. Hitmaker huyo wa Mi Amor amesema ameamua kufichua hayo kwa kuwa ameshindwa kuvumilia maswali ya walimwengu wanaolazimisha uhusiano wake na Willy Paul wakati hakuna kitu inaendelea kati yao. “Nimekabwa na maswali yenu! Mungu anisaidie kwa yatakayofuata! Aiii! Mayooo!” ameandika Jovial. Utakumbuka wawili hao walihisiwa kutoka kimapenzi walipojiachia kimahaba Zaidi miezi kadhaa iliyopita wakati walikuwa watangaza wimbo wao wa pamoja uitwao “Lalala”

Read More
 Shabiki Achora Tattoo Yenye Jina la Willy Paul Kifuani Mwake

Shabiki Achora Tattoo Yenye Jina la Willy Paul Kifuani Mwake

Mwanamke mmoja raia wa Kenya ambaye ni shabiki mkubwa wa mwanamuziki Willy Paul ameshindwa kuficha upendo wake kwa msanii huyo kiasi cha kuchora tattoo jina lake kifuani . Shabiki huyo aliyetambuliwa kama Lizah Njeri awali alikuwa ameandika bango au poster akikiri mapenzi yake kwa mwanamuziki huyo ambapo alitembea katika mitaa ya Nairobi akiwa amebeba bango lililokuwa na jina na mawasiliano yake. “Willy Pozee mwanaume wa ndoto yangu. Wewe ni crush wangu wa maisha, mimi ni Lizah Njeri naahidi kukupenda milele. ” Kukiri mapenzi yake kwa willy paul kupitia maneno ya bango haikutosha, Alienda mbali Zaidi na  kuchora tattoo kifuani mwake kwa wino wa kudumu kwa maneno yaliyosomeka ‘Pozee’. Akizungumza katika mahojiano na Trudy Kitui, Lizah Njeri alisema anampenda sana Willy Paul na matamanio yake ni kwamba siku moja watakuwa marafiki wakubwa na kuishia kuwa wapenzi. Lakini Pia alikiri kutumia picha ya willy paul kama wallpaper kwenye simu yake.

Read More
 Msanii Willy Paul atumia Kshs 500,000 kununua runinga ya inch 86

Msanii Willy Paul atumia Kshs 500,000 kununua runinga ya inch 86

Mwanamuziki kutoka Kenya Willy Paul ameamua kutuonyesha jeuri za pesa anazozitolea jasho kupitia muziki wake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ametusanua kuwa amenunua runinga ya inch 86 aina ya LG iliyomgharimu kiasi cha shillingi laki 5 za Kenya. Bosi huyo wa Saldido amesema amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kusherekea mafanikio ya wimbo wake mpya You aliyomshirikisha Guchi kutoka Nigeria. Hata hivyo ametoa changamoto kwa wasanii wa Kenya kuacha wivu ya mafanikio kwa wasanii wenzao na badala yake watie bidii kwenye kazi zao ili waweze kukithi mahitaji yao ya kimsingi ikiwemo kuvalia vizuri. Willy Paul kwa sasa anafanya vizuri na single yake mpya You akiwa ameshirikisha Guchi kutoka Nigeria ambayo ina zaidi ya watazamaji laki 5 tangu iachiwe rasmi wiki kadhaa zilizopita.

Read More
 Willy Paul awasihi Wasanii wa Kenya kuacha kufanya Kiki katika muziki

Willy Paul awasihi Wasanii wa Kenya kuacha kufanya Kiki katika muziki

Mwanamuziki Willy Paul amewataka wasanii wa muziki nchini Kenya kufanya kazi kwa bidii na kuacha kutegemea kiki katika kukuza muziki wao. Kupitia Insta story yake, mwanzilishi huyo wa lebo ya Saldido amewashauri wanamuziki kupunguza kutengeneza kiki ambazo zitakuja kuwaaribia kazi zao siku za mbeleni na badala yake kuweka juhudi zaidi katika kuzalisha maudhui yenye ubora. “Ombi langu kwa tasnia ya muziki wa Kenya. Kazi Zaidi, Kiki kidogo! Hivi karibuni mtakumbuka maneno haya,” aliandika. Hali ya tasnia ya muziki nchini Kenya imeibua mjadala mkubwa mitandaoni katika siku za hivi karibuni huku wasanii mbalimbali wakishinikiza muziki wao upewe kipau mbele zaidi kwenye vyombo vya habari huku wengine wakilalamikia kutotendewa haki na mapromota pamoja na mashabiki.

Read More
 Willy Paul awajibu wanaomsema vibaya mtandaoni

Willy Paul awajibu wanaomsema vibaya mtandaoni

Staa wa muziki nchini Willy Paul amewajibu wanaomsema vibaya mtandaoni kuwa ana kiburi tangu aanze kupata mafanikio kwenye muziki wake. Kupitia Instastory yake amesikitishwa na madai hayo kwa kusema kuwa ana haki ya kuwa na majivuno kwa sababu anajikimu kimaisha bila usaidizi wa mtu yeyote huku akitamba kuwa yeye ni msanii mwenye kipaji zaidi nchini Kenya. “Ati nikona kiburi?? Waah sio poa, but si kila mmoja na maisha yake? Si hakuna mtu ananilisha? Alafu si nikona chapa na life fiti alafu mimi ni sexy luo?? Plu I’m the most talented musician hapa Kenya.” Ameandika. Ujumbe wake huo umeibua hisia mseto miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ambapo wamemtaka aache masuala ya kulalamika kila mara anapokosolewa mtandaoni kwani anajidhalalisha kwa mashabiki zake kwa kuonyesha mapungufu yake. Ukumbukwe tangu Willy Paul ajiondoe kwenye muziki wa injili na kugeukia muziki wa kidunia amekuwa akipokea ukosoaji mkubwa kutoka kwa baadhi ya mashabiki kutokana na matukio ambayo msanii huyo amekuwa akijihusisha kwenye muziki wake.

Read More
 Willy Paul awapa somo wasanii wa Kenya kwa kuiga muziki wake

Willy Paul awapa somo wasanii wa Kenya kwa kuiga muziki wake

Bosi wa Saldido International, Msanii Willy Paul ameibuka na kutema nyongo kwa wasanii wa Kenya kwa kile anachokitaja kuwa wamekosa ubunifu kwenye muziki wao. Kupitia instastory yake Hitmaker huyo wa “Tamu Walahi” ametoa ya moyoni kwa kusema kuwa wasanii wengi katika siku za karibuni wamekuwa wakimuiga kwenye suala la utoaji wa nyimbo, kitendo ambacho amehoji kuwa imemfanya kusitisha mchakato mzima wa kuachia ngoma zake kwa ajili ya kuwapisha wasanii hao kuachia kazi zao. Hata hivyo walimwengu wamehoji kuwa huenda ujumbe huo unamlenga Mr. Seed ambaye juzi kati aliachia wimbo wake “Dawa ya Baridi Remix” akiwa amemshirikisha msanii wa Nigeria, Guchi ambaye kipindi cha nyuma Willy Paul alidokeza kuwa ana wimbo wa pamoja naye.

Read More
 Willy Paul afunguka ubaguzi unaoendelea kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya

Willy Paul afunguka ubaguzi unaoendelea kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya

Msanii Willy Paul a ameamua kutoa ya moyoni kuhusu namna madalali wamekuwa kizingiti kwa wasanii kupenya kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya. Kupitia instastory amesema amesikitishwa na namna wasanii wasiokuwa na vipaji wanapewa kipaumbele kwenye matamasha ya muziki huku wasanii wanaotoa muziki mzuri wakiambulia patupu. Amesema kenya ina wasanii wengi ambao wanafanya vizuri kimuziki lakini wamenyimwa nafasi ya kuonyesha dunia kazi zao kutokana na madalali ambao wamevamia tasnia ya muziki kuwazingatia wasanii wasiokuwa na vipaji. Hata hivyo ametaka tasnia ya muziki nchini kufanyiwa maboresho kwa kuwaondoa  wasanii wanaolemaza juhudi za wasanii walio na vipaji  kutanua wigo wa muziki ili uweze kuwafikia watu wengi duniani. Hata hivyo hajajulikana ni kitu gani hasa kilimpelekea msanii huyo kuzungumza jambo hilo ila baadhi ya watu wanahisi huenda amenyimwa nafasi ya kutumbuiza kwenye moja ya matamasha ya muziki nchini.

Read More
 Willy Paul asherekea mafanikio yake ya muziki kwa kujizawadi gari aina ya Mercedes-Benz

Willy Paul asherekea mafanikio yake ya muziki kwa kujizawadi gari aina ya Mercedes-Benz

Staa wa muziki nchini Willy Paul amejizawadi gari aina ya Mercedes-Benz C-Class ambapo inatajwa kuwa ametoa kiasi cha takriban shilling millioni 6 kuinunua. Kupitia ukurasa wake instagram mkali huyo wa tamu wallahi ameshare video fupi ikionyesha muonekano wa gari hilo huku akisema amechukua hatua ya kujizawadi kutokana na mafanikio makubwa ambayo anazidi kupata kwenye kazi zake za sana. Lakini pia amewashukuru mashabiki kwa kumuunga mkono na kumuonyesha upendo kwenye muziki wake huku akiahidi kuachia nyimbo kali zenye maudhui safi mfululizo bila kupoa. “God did it again!!! Glory be to the most high God.. thank you my father for yet another beautiful gift… Decided to gift myself for the good job I’ve been doing.. for the CLEAN CONTENT I’ve been releasing… I intend to keep it that way… and to you my fans that gave me a second chance Asanteni. It is because of your generosity that I am where I am today… Another mercedesbenz double sunroof hehe” Ameandika Instagram. Kauli yake inakuja baada ya kutokea kwenye orodha ya wasanii kumi waliotizwa Zaidi katika mtandao wa youtube nchini ambapo kwenye orodha hiyo iliyotawalia na wanamuziki kutoka Nigeria na Tanzania alikamata nafasi ya saba na kuwa msanii pekee kutoka Kenya aliyepata mafanikio hayo.

Read More