Msanii mkongwe nchini Sanaipei Tande amefungukwa kwa mara ya kwanza sababu za kutofanya collabo na msanii Willy Paul.
Hitmaker huyo wa “Najuta” amesema alidinda kufanya collabo na Willy Paul kwa sababu msanii huyo ana skendo nyingi lakini pia anapenda sana kujihusisha na masuala ya kiki kuutangaza kazi za muziki kitu ambacho anadai kwamba hakipendi kabisa.
Sanapei Tande amemtaka Willy Paul aheshimu maamuzi yake na badala yake aendelee kutia bidii kwenye kazi zake za muziki.
Hata hivyo Willy Paul ameonekana kusikitishwa na matamshi ya Sanaipei Tande kwa kusema kwamba hakutarajia msanii huyo anaweza toa kauli kama hiyo ikizingatiwa kuwa alitaka kufanya nae collabo kwa sababu ni moja kati ya watu ambao walimu-inspire kimuziki.