20 Percent Ataka Wasanii Wanaoimba Matusi Kufungwa Jela

20 Percent Ataka Wasanii Wanaoimba Matusi Kufungwa Jela

Msanii mkongwe kwenye gemu ya Bongo Fleva, 20 Percent, ametoa kauli nzito kuhusu wimbi la wasanii kutoa nyimbo zenye matusi, akisema suluhisho si kufungia kazi hizo bali kuwaadhibu moja kwa moja wasanii wanaohusika. Akizungumza kupitia kipindi cha Funky Friday, 20 Percent amesema kuwa hatua ya mamlaka husika kufungia au kuzuia nyimbo haitoshi kudhibiti maudhui machafu, akisisitiza kuwa adhabu kali dhidi ya wasanii ndio itakayowazuia kurudia makosa. Amesema wazi kuwa, ili kulinda maadili ya jamii na kizazi kinachokua, ni muhimu kuangalia chanzo hasa wasanii wanaotunga na kurekodi matusi badala ya kupambana na matokeo pekee. Kwa mujibu wa 20 Percent, kufungwa jela kwa wasanii wanaoimba matusi kutakuwa fundisho na onyo kwa wengine wanaofikiria kuchafua taswira ya muziki wa Bongo Fleva kwa maudhui yasiyofaa.

Read More
 20 PERCENT AMJIBU HARMONIZE

20 PERCENT AMJIBU HARMONIZE

Hatimaye ahadi ya Harmonize ya kuingia studio na kufanya kolabo na 20 percent pindi tu akitua Tanzania kutoka nchini Marekani imepokelewa kwa mikono miwili na mkali huyo wa zamani. 20 Percent ametumia insta story yake kwenye mtandao wa Instagram kumjibu Harmonize kuwa “Promise is like a debt”  kwa maana yupo tayari hivyo Harmonize atimize alichokiahidi. 20 percent ambaye ni mshindi wa tuzo tano za Kili Music Awards mwaka wa 2010, aliwahi kutamba na ngoma kama Maisha ya Bongo, Mama Neema, Money Money, Tamaa Mbaya na nyingine kibao. Haya yanajiri baada ya usiku wa kuamkia Oktoba 25 kuwa mrefu sana kwa harmonize ambaye alionekana akiburudika na midundo ya 20 Percent na kupelekea kutoa ahadi ya kufanya nae kolabo, sambamba na kueleza kuwa ni ndoto yake ya muda mrefu.

Read More