BAHATI AFUNGUKA CHANZO CHA UKIMYA WAKE

BAHATI AFUNGUKA CHANZO CHA UKIMYA WAKE

Hatimaye staa wa muziki nchini Bahati ameamua kuvunja kimya chake kwa mara ya kwanza baada ya kupoteza ubunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu. Kwenye mahojiano na Nairobi News mkali huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amefichua kuwa hali sio shwari katika familia yake hasa upande mke wake Diana. Bahati hata hivyo amepata kigugumzi kueleza kwa kina kinachoendelea ndani ya familia yake licha mtandao huo kumsisitizia kuweka wazi kinachomsibu. Siku chache zilizopita Diana aliposti picha ya njiwa mweupe kwenye background nyeusi na kusindikiza na ujumbe unaosomeka ” Only in the Darkness, Can you see the Stars .” Ujumbe huo uliowaacha mashabiki njia panda ikizingatiwa kuwa alikuwa amezima uwanja wa kutoa maoni kwenye posti yake instagram. Mashabiki hata hivyo walienda mbali na kuhoji kuwa huenda kuna habari mbaya imemtokea mwanamama huyo ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi nane. Mara ya mwisho Diana kuonekana hadharini ilikuwa kwenye hafla ya baby shower yake ambapo alifunguka kupitia changamoto nyingi kwenye safari yake ya uja uzito.

Read More
 MASAUTI AKIRI KUPATA UGUMU KUFIKIA BAHATI

MASAUTI AKIRI KUPATA UGUMU KUFIKIA BAHATI

Hitmaker wa “Sing’oki”, msanii Masauti amekiri kupata ugumu kumfikia msanii mwenzake Bahati tangu kukamilika kwa uchaguzi mkuu Agosti 9 mwaka huu nchini Kenya. Masauti amedai Bahati hapokei simu wala hajibu jumbe zake kwenye mtandao wa Instagram, kitendo ambacho kinampa wasi wasi kuhusu hali ya mkali huyo wa ngoma ya “Adhiambo.” Kauli ya Masauti imekuja mara baada ya moja ya shabiki yake kwenye mtandao wa Instagram kumuuliza kama ana mpango wa kufanya kazi ya pamoja na Bahati. Utakumbuka Bahati amekuwa kimya tangu apoteze kiti cha ubunge eneo la Mathare kwenye uchaguzi ambao alidai kwamba ulikumbwa na udanganyifu mwingi.

Read More
 BAHATI AKIRI BADO NI MWANAMUZIKI WA NYIMBO ZA INJILI

BAHATI AKIRI BADO NI MWANAMUZIKI WA NYIMBO ZA INJILI

Hitmaker wa ngoma ya “Adhiambo”, Msanii Bahati amedai kwamba bado yeye ni msanii wa injili kwani alimuahidi Mungu kwamba hatawahi kumuacha. Akizungumza kwenye mahojiano na Mzazi Willy M. Tuva, msanii huyo amesema kwamba mafanikio yake katika maisha yameletwa na neema ya Mungu, hivyo basi hawezi kuziacha njia zake. Katika hatua nyingine Bahati ametusanua kuhusu ndoto yake ya kuwa rais wa Kenya mwaka wa 2037 kwa kusema kwamba amekuwa akiota ndoto hiyo kwa kipindi kirefu tangu alipokalia kiti cha rais kwenye mkutano wa kisiasa huko Kasarani. Utakumbuka Bahati alikuwa mgombea wa kiti cha ubunge eneo la Mathare kwenye uchaguzi mkuu uliokamilika juzi kati lakini kwa bahati mbaya alishindwa baada ya mpinzani wake Anthony Oluoch kuibuka kidedea kwenye kinyang’anyiro cha ubunge eneo hilo.

Read More
 BAHATI AWAJIBU WANAOMKOSOA MTANDAONI KWA KUSHINDWA UBUNGE MATHARE

BAHATI AWAJIBU WANAOMKOSOA MTANDAONI KWA KUSHINDWA UBUNGE MATHARE

Mwanamuziki aliyegeukia siasa, Bahati amewajibu kitaalamu wanaomubeza kwenye mitandao ya kijamii baada ya kupoteza kiti cha ubunge Mathare kwenye uchaguzi mkuu uliokamilika majuzi nchini Kenya. Katika mahojiano yake hivi karibuni Bahati amesema hatojutia maamuzi yake ya kuwania ubunge Mathare kwa kuwa amejifunza mambo mengi kwenye ulingo wa siasa licha ya kwamba zoezi zima la kuhesabu kura lilikumbwa na dosari. Hitmaker huyo wa “Adhiambo” amesema wanaomkosoa kwenye mitandao ya kijamii wanamuonea kijicho kutokana na hatua kubwa aliyopiga maishani. Utakumbuka baadhi ya mastaa akiwemo Willy Paul walimkejeli Bahati kwa kumpongeza mpinzani wake Anthony Oluoch ambaye ndiye mbunge mteule wa Mathare, kaunti ya Nairobi.

Read More
 BAHATI AWEKA WAZI GHARAMA YA KAMPEINI YAKE YA KISIASA

BAHATI AWEKA WAZI GHARAMA YA KAMPEINI YAKE YA KISIASA

Mwanamuziki Kevin Bahati Kioko maarufu kama Bahati ambaye pia ni mgombea Ubunge katika Jimbo la Mathare kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu nchini, amefunguka kiasi cha pesa ambacho ametumia hadi sasa kwenye kampeni zake. Kwenye mahojiano yake na Millard Ayo, Bahati ambaye anagombea nafasi hiyo kwa tiketi ya chama cha Jubilee amesema ametumia kiasi cha shillingi millioni 33 za Kenya kuendesha kampeni zake. Mbali na hilo Hitmaker huyo wa Adhiambo amesema ametenga zaidi ya KSh. 10 millioni kwa ajili ya siku ya Uchaguzi tu ambao utafanyika Kesho Jumanne huku akisisitiza kuwa pesa za kampeini zake za kisiasa zilitoka kwa wasamaria wema  wakiwemo marafiki pamoja na chama chake cha Jubilee. Hata hivyo Bahati ambaye anawania kiti cha ubunge eneo la Mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9 mwaka huu amedokeza kwamba ana mpango wa kuwania wadhfa wa juu kwenye uchaguzi wa mwaka wa 2037, akisema ni ndoto yake kuwa rais wa taifa la Kenya.

Read More
 BAHATI AFUNGUKA KUVAMIWA NA MAJANGILI KUMSHINIKIZA AJIONDOE UBUNGE MATHARE

BAHATI AFUNGUKA KUVAMIWA NA MAJANGILI KUMSHINIKIZA AJIONDOE UBUNGE MATHARE

Msanii aliyegeukia siasa Bahati amedai kuwa mpenzi wake Antony Oluoch alimtumia majangili kumtishia maisha ili ajiondoe kwenye azma yake ya ubunge Mathare Kupitia mitandao yake ya kijamii Bahati amesema vijana hao ambao sio wakaazi wakaazi alimvamia na kumpiga kiasi cha kurarua shati lake la chama chake cha Jubilee huku wakimtishia kuwa wataangamazia kama atajiuzulu kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amesema mpinzani wake huyo amejaribu kila njia kuzima ndoto yake lakini amesema kidete kwa ajili ya watu wa Mathare ambao wamehangaika kwa muda mrefu. Hata hivyo amepuzilia mbali shinikizo za kutaka kujiondoa kwenye ubunge Mathare huku akidai kuwa atakuwa kwenye debe Agosti 9 ambapo akiwarai wakaazi wa mpe kura kwa wingi licha ya vitisho anavyozidi kupokea kila kuchao. Kauli ya Bahati imekuja mara baada ya Raila Odinga kuahidi kumpa kazi kwenye serikali yake na kumtaka ampe nafasi Mbunge wa sasa wa Mathare Athony Oluoch kutetea kiti chake kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Read More
 BAHATI NA DIANA B MBIONI KUPATA MTOTO WATATU

BAHATI NA DIANA B MBIONI KUPATA MTOTO WATATU

Wanandoa mashuhuri nchini Diana Marua na Bahati wamefichua kuwa wanatarajia kupata mtoto wa tatu hivi karibuni. Wakitoa taarifa hiyo njema kwenye chaneli yao ya You Tube, wanandoa hao wamesema kwamba tayari ‘wanampenda’ mtoto wao huyo ambaye hajazaliwa. “kila siku nakutafutia , kwa vile nakulombotov … nakutamkia baraka, nakutakia fanaka, kutoa sadaka nyota yako itawaka, tamka isiyokua na mipaka … malaika wakulinde … na si twakusiburi kama mwisho …” wamesikika wakiimba kwenye video waliyoichapisha chaneli zao za Youtube. Wawili hao wana watoto wawili pamoja, Heaven na Majesty na mashabiki wamewapongeza kwa mafanikio hayo huku wakiwatakia heri wakati huu wanatarajia kumpata mtoto wao wa tatu.

Read More
 BAHATII AIDHINISHA NA TUME YA IEBC KUWANIA UBUNGE MATHARE AGOSTI 9

BAHATII AIDHINISHA NA TUME YA IEBC KUWANIA UBUNGE MATHARE AGOSTI 9

Msanii aliyegeukia siasa Kevin Kioko Bahati  amethibitisha rasmi na tume ya IEBC kuwa miongoni mwa wagombea watakaowania ubunge Mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Hii ni baada ya tume hiyo kuorodhesha jina lake kwenye gazeti lake rasmi licha ya Muungano wa Azimio la Umoja kumtaka ajiondoe kwenye kinyanganyiro cha ubunge mathare kwa ajili ya kumpa nafasi mbunge wa sasa Anthony Oluoch kutetea kiti chake. Kulingana na notisi hiyo Bahati atawania ubunge Mathare kupitia tiketi ya chama ya jubilee. Bahati amepokea taarifa hiyo kwa furaha huku akisema kuwa IEBC imeheshimu matakwa ya wakaazi wa eneo bunge la Mathare. “When Jesus says yes, nobody can say no! I have been the most fought MP candidate; my loosing opponent tried everything to threaten me & make sure I step down but look at what God has done! It’s official now,”  Ameandika kupitia  twitter. Bahati kwa sasa atachuana na wagombea wengine wa ubunge mathare kutoka vyama mbali mbali vya kisiasa.  

Read More
 EDWIN SIFUNA AMVUA NGUO BAHATI BILA HURUMA, ADAI THAMANI YAKE NI KSH. 200.

EDWIN SIFUNA AMVUA NGUO BAHATI BILA HURUMA, ADAI THAMANI YAKE NI KSH. 200.

Katibu wa chama cha ODM Edwin Sifuna amepuzilia mbali madai yaliyoibuliwa na staa wa muziki nchini Bahati kuwa alihongwa shillingi millioni 50 kujiondoa kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Mwanasiasa huyo amesema madai ya Bahati ambaye ni mchanga kisiasa hayana ukweli wowote, hivyo msanii huyo anatumia mgogoro uliopo kati yake na chama cha Jubilee kutafuta uhuruma kutoka kwa wakenya. “Yaani kama kuna mtu ako na KSh 50 million mahali eti anataka kuchukua apee Bahati, huyo mtu kichwa yake ni mbaya. Afanyie nini? Ya nini?” Amesema Sifuna. Sifuna alienda mbali na kumtolea uvivu Bahati kwa kusema kwamba pesa ambazo hitmaker huyo wa “Adhiambo” anapaswa kupewa ili ajiondoe kwenye azma yake kuwa mbunge Mathare ni shilingi mia 2. “Hapo naweza chukua mia mbili nimbuyie nayo handkerchief nibaki an hiyo pesa ingine kwa sababu ya machozi alafu nimlipie salon ya mwaka moja hiyo nywele yake. Hakuna kitu ingine ya kumpatia.” Amekazia Sifuna. Kauli ya Edwin Sifuna imekuja mara ya Bahati kumtuhumu kuwa amekuwa kizingiti kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 Mwaka huu. Bahati alienda mbali na kudai kuwa Sifuna ndio alichochea chama cha Jubilee kumuondoa kama mperusha bendera ya ubunge wa Mathare kupitia Muungano wa Azimio la Umoja ili kumpa nafasi mbunge wa sasa Anthony Oluoch.

Read More
 DIANA B AMKINGIA KIFUA BAHATI KUFUKUZWA EMBAKASI MASHARIKI

DIANA B AMKINGIA KIFUA BAHATI KUFUKUZWA EMBAKASI MASHARIKI

Mwanamitandao aliyegeukia muziki Diana B amevunja kimya chake mara baada ya mume wake ambaye ni mgombea wa kiti cha ubunge Mathare Kevin Bahati kufukuzwa kwenye mkutano wa kisiasa wa Azimio la umoja huko Embakasi Mashariki, jijini Nairobi. Kupitia Instagram yake Diana B amempa moyo mume wake kwa kusema kwamba aendelee kuipigania ndoto yake kuwa mbunge kwa kuwa wapinzani wameanza kuingiwa na uoga kiasi cha kuanza kumpiga vita kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa mathare baada ya uchaguzi wa Agosti 9 mwaka huu. “You are a force that cannot be ignored!!! The way to the top can never be reached without opposition. keep pushing… God got you, Mathare people already know who is best for them,” Amesema Diana B Kwa upande wake Bahati ameeleza kuwa wapinzani wake waliumizwa na uwepo wake kwenye mkutano huo wa Kisiasa ndiposa wakaamua kufukuza. Hitmaker huyo wa  ngoma ya Adhiambo amedai kuwa waliokuwa wanasimamia mkutano huo walilazimika kusitisha mkutano ghafla licha ya watu kumtaka awahutubie. Hata hivyo katibu wa ODM Edwin Sifuna amesisitiza kuwa mgombea wao wa kiti cha ubunge mathare kupitia azimio la umoja ni Anthony Oluoch, hivyo  bahati aache kutumia  jina lake kutafuta kiki kwani akuhusika kivyovyote kumshurutisha ajiondoe kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare.

Read More
 BAHATI AKIRI  KUHONGWA MILLIONI 50 KUJIONDOA KWENYE KINYANG’ANYIRO CHA UBUNGE MATHARE

BAHATI AKIRI KUHONGWA MILLIONI 50 KUJIONDOA KWENYE KINYANG’ANYIRO CHA UBUNGE MATHARE

Staa wa muziki nchini  Bahati amefunguka tusioyajua kuhusu azma yake ya  kuwa mwanasiasa Akizungumza na Radio Citizen, Bahati amesema alihongwa shilling millioni 50 kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Mathare ili kumpa nafasi mpinzani wake Anthony Oluoch nafasi ya kiti chake kwa mara ya pili kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Msanii huyo amesema kuwa wapinzani wake wote si wakazi wa Mathare na wamekuwa wakimshirikisha kwenye mazungumzo ili kumshawishi kulegeza msimamo wake wa kuwania ubunge wa eneo hilo. “Niliambiwa nitapewa kazi. Lakini sitafuti kazi, najitafutia riziki kutokana na muziki wangu,” alisema. Watu wamekuja na ofa wanataka kunilipa ili niondoke madarakani. Wamenipa mamilioni, hadi Ksh.50 milioni. Wanajua wakifika ofisini watapata pesa hizo,” Bahati alisema. Kulingana na hitmaker huyo wa ngoma ‘Sweet Love’, ambaye anagombea ubunge kupitia tiketi ya chama cha Jubilee, washindani wake wamegundua kuwa hawezi kuhujumiwa kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa Mathare na sasa wanatumia njia zingine kumshawishi. Bahati amemtaja mpinzani wake Anthony Oluoch, kuwa mmoja wa wale waliomwendea, wakiomba msaada wake. “Aliniambia nimfanyie wimbo wa kampeni na kumuunga mkono. Wanataka kumtumia mtu kutoka Mathare kufika kwa watu,” aliongeza. Hata hivyo ameapa kutojiondoa katika kinyang’anyiro cha ubunge Mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9 kwani hakuna marafiki wa kweli katika siasa. “Ninakosa marafiki wa kweli, kwenye siasa unakaa na rafiki ambaye anasema asichomaanisha. Wanasiasa wengi si wa kweli,” alisema. Matamshi ya Bahati yanajiri wakati ambapo yuko katika njia panda na Muungano wa Azimio la umoja, ambao hivi majuzi ulimtangaza Anthony Oluoch kama mgombeaji wao wanayempendelea kuwania kiti cha ubunge Mathare.

Read More
 BAHATI AMVUA NGUO EDWIN SIFUNA NA RACHAEL SHEBESH KISA SIASA ZA MATHARE

BAHATI AMVUA NGUO EDWIN SIFUNA NA RACHAEL SHEBESH KISA SIASA ZA MATHARE

Msanii aliyegeukia siasa nchini Bahati amemtolea uvivu katibu mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna na Rachael Shebesh baada ya wawili hao kumtaka ajiuzulu kwenye azma yake ya kuwania ubunge ili kumpisha mbunge wa sasa wa Mathare Anthony oluoch kutetea kiti chake. Msanii huyo amewasuta vikali wawili hao kwa kueneza propaganda kuwa amejiondoa kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare huku akiwataka wakome kuitaja jina lake kwenye siasa zao duni. Bahati amesema hakuna kitu kitamzuia kwenye azma yake ya kuwawakilisha wakaazi wa Mathare bungeni baada ya uchaguzi wa Agosti 9 licha ya kupewa vitisho na kuzushiwa taarifa za uongo. Kauli ya bahati imekuja mara baada ya mwenyekiti wa Jubilee kaunti ya Nairobi kudai kuwa Bahati atajiondioa kama mwaniaji wa ubunge mathare kumpisha mbunge wa sasa Athony Oluoch kutetea kiti chake kwani ni chaguo lao kama muungano wa Azimio. Hii sio mara ya kwanza kwa azma ya Bahati kuwa mbunge wa Mathare kukumbwa na matatizo, mapema mwezi Aprili mwaka huu chama cha Jubilee ilitupilia mbali cheti chake kwa ajili ya kumshinikiza ampishe mbunge wa sasa Athony Olouch awe mwaniaji wa ubunge Mathare kupitia chama cha ODM.

Read More