BAHATI AFUNGUKA KUVAMIWA NA MAJANGILI KUMSHINIKIZA AJIONDOE UBUNGE MATHARE

BAHATI AFUNGUKA KUVAMIWA NA MAJANGILI KUMSHINIKIZA AJIONDOE UBUNGE MATHARE

Msanii aliyegeukia siasa Bahati amedai kuwa mpenzi wake Antony Oluoch alimtumia majangili kumtishia maisha ili ajiondoe kwenye azma yake ya ubunge Mathare Kupitia mitandao yake ya kijamii Bahati amesema vijana hao ambao sio wakaazi wakaazi alimvamia na kumpiga kiasi cha kurarua shati lake la chama chake cha Jubilee huku wakimtishia kuwa wataangamazia kama atajiuzulu kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amesema mpinzani wake huyo amejaribu kila njia kuzima ndoto yake lakini amesema kidete kwa ajili ya watu wa Mathare ambao wamehangaika kwa muda mrefu. Hata hivyo amepuzilia mbali shinikizo za kutaka kujiondoa kwenye ubunge Mathare huku akidai kuwa atakuwa kwenye debe Agosti 9 ambapo akiwarai wakaazi wa mpe kura kwa wingi licha ya vitisho anavyozidi kupokea kila kuchao. Kauli ya Bahati imekuja mara baada ya Raila Odinga kuahidi kumpa kazi kwenye serikali yake na kumtaka ampe nafasi Mbunge wa sasa wa Mathare Athony Oluoch kutetea kiti chake kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Read More
 BAHATI NA DIANA B MBIONI KUPATA MTOTO WATATU

BAHATI NA DIANA B MBIONI KUPATA MTOTO WATATU

Wanandoa mashuhuri nchini Diana Marua na Bahati wamefichua kuwa wanatarajia kupata mtoto wa tatu hivi karibuni. Wakitoa taarifa hiyo njema kwenye chaneli yao ya You Tube, wanandoa hao wamesema kwamba tayari ‘wanampenda’ mtoto wao huyo ambaye hajazaliwa. “kila siku nakutafutia , kwa vile nakulombotov … nakutamkia baraka, nakutakia fanaka, kutoa sadaka nyota yako itawaka, tamka isiyokua na mipaka … malaika wakulinde … na si twakusiburi kama mwisho …” wamesikika wakiimba kwenye video waliyoichapisha chaneli zao za Youtube. Wawili hao wana watoto wawili pamoja, Heaven na Majesty na mashabiki wamewapongeza kwa mafanikio hayo huku wakiwatakia heri wakati huu wanatarajia kumpata mtoto wao wa tatu.

Read More
 BAHATII AIDHINISHA NA TUME YA IEBC KUWANIA UBUNGE MATHARE AGOSTI 9

BAHATII AIDHINISHA NA TUME YA IEBC KUWANIA UBUNGE MATHARE AGOSTI 9

Msanii aliyegeukia siasa Kevin Kioko Bahati  amethibitisha rasmi na tume ya IEBC kuwa miongoni mwa wagombea watakaowania ubunge Mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Hii ni baada ya tume hiyo kuorodhesha jina lake kwenye gazeti lake rasmi licha ya Muungano wa Azimio la Umoja kumtaka ajiondoe kwenye kinyanganyiro cha ubunge mathare kwa ajili ya kumpa nafasi mbunge wa sasa Anthony Oluoch kutetea kiti chake. Kulingana na notisi hiyo Bahati atawania ubunge Mathare kupitia tiketi ya chama ya jubilee. Bahati amepokea taarifa hiyo kwa furaha huku akisema kuwa IEBC imeheshimu matakwa ya wakaazi wa eneo bunge la Mathare. “When Jesus says yes, nobody can say no! I have been the most fought MP candidate; my loosing opponent tried everything to threaten me & make sure I step down but look at what God has done! It’s official now,”  Ameandika kupitia  twitter. Bahati kwa sasa atachuana na wagombea wengine wa ubunge mathare kutoka vyama mbali mbali vya kisiasa.  

Read More
 EDWIN SIFUNA AMVUA NGUO BAHATI BILA HURUMA, ADAI THAMANI YAKE NI KSH. 200.

EDWIN SIFUNA AMVUA NGUO BAHATI BILA HURUMA, ADAI THAMANI YAKE NI KSH. 200.

Katibu wa chama cha ODM Edwin Sifuna amepuzilia mbali madai yaliyoibuliwa na staa wa muziki nchini Bahati kuwa alihongwa shillingi millioni 50 kujiondoa kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Mwanasiasa huyo amesema madai ya Bahati ambaye ni mchanga kisiasa hayana ukweli wowote, hivyo msanii huyo anatumia mgogoro uliopo kati yake na chama cha Jubilee kutafuta uhuruma kutoka kwa wakenya. “Yaani kama kuna mtu ako na KSh 50 million mahali eti anataka kuchukua apee Bahati, huyo mtu kichwa yake ni mbaya. Afanyie nini? Ya nini?” Amesema Sifuna. Sifuna alienda mbali na kumtolea uvivu Bahati kwa kusema kwamba pesa ambazo hitmaker huyo wa “Adhiambo” anapaswa kupewa ili ajiondoe kwenye azma yake kuwa mbunge Mathare ni shilingi mia 2. “Hapo naweza chukua mia mbili nimbuyie nayo handkerchief nibaki an hiyo pesa ingine kwa sababu ya machozi alafu nimlipie salon ya mwaka moja hiyo nywele yake. Hakuna kitu ingine ya kumpatia.” Amekazia Sifuna. Kauli ya Edwin Sifuna imekuja mara ya Bahati kumtuhumu kuwa amekuwa kizingiti kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 Mwaka huu. Bahati alienda mbali na kudai kuwa Sifuna ndio alichochea chama cha Jubilee kumuondoa kama mperusha bendera ya ubunge wa Mathare kupitia Muungano wa Azimio la Umoja ili kumpa nafasi mbunge wa sasa Anthony Oluoch.

Read More
 DIANA B AMKINGIA KIFUA BAHATI KUFUKUZWA EMBAKASI MASHARIKI

DIANA B AMKINGIA KIFUA BAHATI KUFUKUZWA EMBAKASI MASHARIKI

Mwanamitandao aliyegeukia muziki Diana B amevunja kimya chake mara baada ya mume wake ambaye ni mgombea wa kiti cha ubunge Mathare Kevin Bahati kufukuzwa kwenye mkutano wa kisiasa wa Azimio la umoja huko Embakasi Mashariki, jijini Nairobi. Kupitia Instagram yake Diana B amempa moyo mume wake kwa kusema kwamba aendelee kuipigania ndoto yake kuwa mbunge kwa kuwa wapinzani wameanza kuingiwa na uoga kiasi cha kuanza kumpiga vita kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa mathare baada ya uchaguzi wa Agosti 9 mwaka huu. “You are a force that cannot be ignored!!! The way to the top can never be reached without opposition. keep pushing… God got you, Mathare people already know who is best for them,” Amesema Diana B Kwa upande wake Bahati ameeleza kuwa wapinzani wake waliumizwa na uwepo wake kwenye mkutano huo wa Kisiasa ndiposa wakaamua kufukuza. Hitmaker huyo wa  ngoma ya Adhiambo amedai kuwa waliokuwa wanasimamia mkutano huo walilazimika kusitisha mkutano ghafla licha ya watu kumtaka awahutubie. Hata hivyo katibu wa ODM Edwin Sifuna amesisitiza kuwa mgombea wao wa kiti cha ubunge mathare kupitia azimio la umoja ni Anthony Oluoch, hivyo  bahati aache kutumia  jina lake kutafuta kiki kwani akuhusika kivyovyote kumshurutisha ajiondoe kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare.

Read More
 BAHATI AKIRI  KUHONGWA MILLIONI 50 KUJIONDOA KWENYE KINYANG’ANYIRO CHA UBUNGE MATHARE

BAHATI AKIRI KUHONGWA MILLIONI 50 KUJIONDOA KWENYE KINYANG’ANYIRO CHA UBUNGE MATHARE

Staa wa muziki nchini  Bahati amefunguka tusioyajua kuhusu azma yake ya  kuwa mwanasiasa Akizungumza na Radio Citizen, Bahati amesema alihongwa shilling millioni 50 kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Mathare ili kumpa nafasi mpinzani wake Anthony Oluoch nafasi ya kiti chake kwa mara ya pili kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Msanii huyo amesema kuwa wapinzani wake wote si wakazi wa Mathare na wamekuwa wakimshirikisha kwenye mazungumzo ili kumshawishi kulegeza msimamo wake wa kuwania ubunge wa eneo hilo. “Niliambiwa nitapewa kazi. Lakini sitafuti kazi, najitafutia riziki kutokana na muziki wangu,” alisema. Watu wamekuja na ofa wanataka kunilipa ili niondoke madarakani. Wamenipa mamilioni, hadi Ksh.50 milioni. Wanajua wakifika ofisini watapata pesa hizo,” Bahati alisema. Kulingana na hitmaker huyo wa ngoma ‘Sweet Love’, ambaye anagombea ubunge kupitia tiketi ya chama cha Jubilee, washindani wake wamegundua kuwa hawezi kuhujumiwa kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa Mathare na sasa wanatumia njia zingine kumshawishi. Bahati amemtaja mpinzani wake Anthony Oluoch, kuwa mmoja wa wale waliomwendea, wakiomba msaada wake. “Aliniambia nimfanyie wimbo wa kampeni na kumuunga mkono. Wanataka kumtumia mtu kutoka Mathare kufika kwa watu,” aliongeza. Hata hivyo ameapa kutojiondoa katika kinyang’anyiro cha ubunge Mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9 kwani hakuna marafiki wa kweli katika siasa. “Ninakosa marafiki wa kweli, kwenye siasa unakaa na rafiki ambaye anasema asichomaanisha. Wanasiasa wengi si wa kweli,” alisema. Matamshi ya Bahati yanajiri wakati ambapo yuko katika njia panda na Muungano wa Azimio la umoja, ambao hivi majuzi ulimtangaza Anthony Oluoch kama mgombeaji wao wanayempendelea kuwania kiti cha ubunge Mathare.

Read More
 BAHATI AMVUA NGUO EDWIN SIFUNA NA RACHAEL SHEBESH KISA SIASA ZA MATHARE

BAHATI AMVUA NGUO EDWIN SIFUNA NA RACHAEL SHEBESH KISA SIASA ZA MATHARE

Msanii aliyegeukia siasa nchini Bahati amemtolea uvivu katibu mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna na Rachael Shebesh baada ya wawili hao kumtaka ajiuzulu kwenye azma yake ya kuwania ubunge ili kumpisha mbunge wa sasa wa Mathare Anthony oluoch kutetea kiti chake. Msanii huyo amewasuta vikali wawili hao kwa kueneza propaganda kuwa amejiondoa kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare huku akiwataka wakome kuitaja jina lake kwenye siasa zao duni. Bahati amesema hakuna kitu kitamzuia kwenye azma yake ya kuwawakilisha wakaazi wa Mathare bungeni baada ya uchaguzi wa Agosti 9 licha ya kupewa vitisho na kuzushiwa taarifa za uongo. Kauli ya bahati imekuja mara baada ya mwenyekiti wa Jubilee kaunti ya Nairobi kudai kuwa Bahati atajiondioa kama mwaniaji wa ubunge mathare kumpisha mbunge wa sasa Athony Oluoch kutetea kiti chake kwani ni chaguo lao kama muungano wa Azimio. Hii sio mara ya kwanza kwa azma ya Bahati kuwa mbunge wa Mathare kukumbwa na matatizo, mapema mwezi Aprili mwaka huu chama cha Jubilee ilitupilia mbali cheti chake kwa ajili ya kumshinikiza ampishe mbunge wa sasa Athony Olouch awe mwaniaji wa ubunge Mathare kupitia chama cha ODM.

Read More
 BAHATI AIDHINISHWA NA TUME YA UCHAGUZI NCHINI KENYA KUWANIA UBUNGE MATHARE

BAHATI AIDHINISHWA NA TUME YA UCHAGUZI NCHINI KENYA KUWANIA UBUNGE MATHARE

Mwanamuziki aliyegeukia siasa Bahati ameshindwa kuficha furaha yake baada ya tume ya IEBC kumuidhinisha kuwa atawania ubunge wa Mathare kwenye uchaguzi mkuu ujao kupitia Tiketi ya chama cha Jubilee. Kupitia ukurasa wake wa instagram bahati ameandika waraka mrefu wa kuwashukuru kumshukuru mungu, chama cha jubilee na watu wa mathare kwa kumpa nafasi ya kuwawakilisha kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti huku akitoa wito kwa wafuasi wake wampe kura ili aweze kuleta mabadiliko. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amesema ndoto yake na watu wa mathare imetimia kwa kuwa wamekuwa wakiomba kwa muda kumpata mbunge ambaye ni mzaliwa wa eneo hilo. Wasanii wengine walioidhinishwa na IEBC ni mchekeshaji Jalang’o ambaye ni mgombea wa ubunge Lang’at kupitia cha cha ODM, na Mc Jessy ambaye ni mgombea wa ubunge Imenti Kusini.

Read More
 BAHATI AFIKISHA SUBSCRIBERS MILLIONI MOJA YOUTUBE

BAHATI AFIKISHA SUBSCRIBERS MILLIONI MOJA YOUTUBE

Nyota wa muziki nchini Bahati amefikisha idadi ya subscribers Milioni 1 kwenye mtandao wa Youtube. Bahati ambaye alijiunga na mtandao wa youtube Agosti 7, mwaka 2012  amepata subscribers wengi kutokana na kazi zake mbalimbali anazoziweka katika mtandao huo. Baadhi ya matukio anayoyaweka  katika channel yake ni shoo anazozifanya, video zake za muziki pamoja na utayarishaji wa video za nyimbo zake. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” hadi sasa Kupitia channel yake ya YouTube kazi zake zimetazamwa zaidi ya mara milioni  172 tangu ilipofunguliwa rasmi  channel yake ya youtube miaka 10 iliyopita. Bahati anakuwa msanii wa pili nchini mwenye wafuasi wengi katika mtandao wa youtube baada ya Oitle Brown ambaye ndiye alikuwa msanii wa kwanza nchini kufikisha subscribers milllioni moja youtube.

Read More
 BAHATI AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA RAILA ODINGA KUSHINDWA KUMTAMBUA JUKWAANI

BAHATI AZUA GUMZO MTANDAONI BAADA YA RAILA ODINGA KUSHINDWA KUMTAMBUA JUKWAANI

Staa wa muziki nchini Bahati amezua gumzo mtandaoni mara baada ya mgombea wa urais kupitia Muungano wa Azimio la Umoja Raila Odinga kushindwa kumtambua akiwa jukwaani. Raila ambaye alikuwa anawatambulisha wagombea wa viti mbali mbali vya kisiasa kupitia Azimio la Umoja huko Kamkunji, jijini Nairobi alijipata amemuita Bahati jina la Mathew baada ya wandani wake kujaribu kumtambulisha msanii huyo kwake. Sasa jambo hilo limezuia mjadala mzito miongoni mwa wakenya kwenye mitandao ya kijamii ambapo baadhi wameonekana kumkejeli Bahati wakihoji ni kwa nini Raila alishindwa kumtambua msanii huyo mbele ya umma ikizingatiwa Bahti mwenyewe amekuwa akijinadi kwamba ana ukaribu na mgombea huyo wa urais kupitia muungano wa Azimio laUmoja. Hata hivyo wafuasi wa Raila Odinga wameonekana kumkingia kifua mwanasiasa huyo kwa kusema kwamba ana mambo mengi ya kuwaza kutokana na shinikizo za uchaguzi mkuu wa Agosti 9. Utakumbuka miezi kadhaa iliyopita Bahati aliachia wimbo wa uitwao “Fire” aliyomshirikisha Raila Odinga ambapo alimwagia sifa kinara huyo wa chama cha ODM kwenye azma yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu.

Read More
 BAHATI AKABIDHIWA CHETI CHA KUWANIA UBUNGE MATHARE KUPITIA CHAMA CHA JUBILEE

BAHATI AKABIDHIWA CHETI CHA KUWANIA UBUNGE MATHARE KUPITIA CHAMA CHA JUBILEE

Staa wa muziki nchini Bahati ameshindwa kuficha furaha yake baada ya kukabidhiwa tena cheti chake cha kuwania ubunge mathare kupitia  chama cha Jubilee Katika mkao na wanahabari bahati amemshukuru Rais Uhuru Kenyatta kwa kumpa nafasi tena kuwania ubunge kwa tiketi ya chama cha Jubilee na kinara wa ODM Raila Odinga kwa kumuamini kugombea ubunge wa mathare kupitia mwavuli wa Azimio la Umoja. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Adhiambo” amesema ndoto yake na watu wa Mathare imetimia kwa kuwa wamekuwa wakiomba kwa muda kumpata mbunge ambaye ni mzaliwa wa eneo hilo. Hata hivyo amewashukuru wajumbe wa Jubilee na wakaazi wa Mathare kwa ujumla kwa kumkingia kifua alipony’ang’anywa cheti cha jubilee wiki kadhaa zilizopita huku akitoa rai waendelee kumuunga mkono kwenye azma yake ya kuwa mbunge wa Mathare. Kwa sasa Bahati anatarajiwa kumenyana  na wapinzani wake kutoka vyama mbali mbali kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9, 2022.

Read More

BAHATI AFUNGUKA SABABU ZA KUTOWANIA BUNGE MATHARE KAMA MGOMBEA HURU

Staa wa muziki nchini Bahati ameweka wazi kuwa hatagombea kama mgombea binafsi kwenye kinyanganyiro cha ubunge wa mathare, siku chache baada ya kuangua kilio aliposhurutishwa na chama cha jubilee kujiuzulu wadhfa wa ubunge kwa ajili ya kumpa nafasi mbunge wa sasa tom olouch. Bahati amesema atakuwa amekisaliti chama chake cha Jubilee akiwania kiti ubunge mathare kama mgombea huru, jambo ambalo amedai hayuko tayari kukifanya. Katika mahojiano na Radio Maisha, Bahati hata hivyo ameshikilia kuwa bado ana Cheti chake cha Uteuzi na ana matumaini kuwa jina lake litawasilishwa kwa tume ya uchaguzi  IEBC leo. ‘Naweza kukuambia kitu? Unajua kwangu, sina haja na kuwa mgombea huru, kwa sababu nahisi hiyo ni kama kukisaliti chama changu na ninaamini pia chama hakitasaliti watu wao… kwa sababu … kina nafasi kwa vijana …’’ Bahati alisema. Msanii huyo aliyelelewa Mathare hata hivyo amesema kuwa amefanya mazungumzo na chama hicho baada ya kutakiwa kurejesha Cheti chake na hivyo amewatolea hofu wafuasi wake kuwa mambo yatakuwa mazuri hivi karibuni. “Mgombea wangu…waliitisha mkutano … nilifikiri chama kilitaka kunifadhili, lakini waliniomba nijiuzulu kama mgombea wa ubunge mathare kwa ajili ya mbunge wa sasa… Wanajua mashinani mambo yamebadilika… nimefanya mazungumzo upya na chama …” alifichua.

Read More