Bien Awataka Wasanii wa Kenya Kuepuka Shows Wanakodhulumiwa

Bien Awataka Wasanii wa Kenya Kuepuka Shows Wanakodhulumiwa

Msanii wa muziki kutoka Kenya na mwanachama wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, ametoa wito mzito kwa wasanii nchini humo kutokubali kufanya maonyesho katika maeneo au matukio ambayo wanadharauliwa au kudhulumiwa. Kupitia ujumbe wake aliouweka kwenye mitandao ya kijamii, Bien amewapongeza wasanii wa Kodong Clan kwa uamuzi wao wa kujiondoa kwenye show ya Asake, akisema hatua hiyo ni ishara ya kujithamini na kulinda heshima yao kama wasanii. Bien amesisitiza kuwa wasanii hawapaswi kulazimika kuvumilia dharau au manyanyaso kwa kisingizio cha kupata nafasi ya kupiga show. Kauli hiyo ya Bien imekuja siku moja baada ya kundi la Kodong Clan kutangaza kujiondoa kwenye tamasha la Tukutane GA13y x Asake, wakidai kukiukwa kwa mkataba pamoja na kudharauliwa na waandaaji wa tamasha hilo.

Read More
 Bien Aibua Gumzo Baada ya Kudai Ana Fahali Aitwaye Sauti Sol

Bien Aibua Gumzo Baada ya Kudai Ana Fahali Aitwaye Sauti Sol

Staa wa muziki kutoka Kenya, Bien Aime Baraza, amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa anamiliki fahali anayejulikana kwa jina la Sauti Sol. Kupitia maelezo yake, Bien amesema awali alikuwa na fahali wawili, lakini mmoja aliuziwa na mama yake mzazi, na hivyo kubaki na fahali mmoja ambaye alimpa jina hilo linalofanana na kundi lake la muziki. Bien ameeleza kuwa kwa sasa fahali huyo ameanza kupewa mafunzo maalum ya kupigana na fahali wengine, ikiwa ni maandalizi ya kushiriki mashindano ya kupiganisha fahali. Mashindano hayo yanajulikana kudhaminiwa na jamii ya Waluhya, hasa kutoka Kaunti ya Kakamega nchini Kenya, na ni sehemu ya tamaduni na burudani za kitamaduni katika eneo hilo. Hata hivyo, Bien amesema amesema anajivunia fahali wake na ana matumaini kuwa “Sauti Sol” itafanya vyema endapo itashiriki mashindano hayo, huku akisisitiza kuwa anathamini na kuheshimu tamaduni ya Waluhya ambayo ndio chimbuko lake

Read More
 Bien Aachia Remix Nane Mpya za Wimbo Wake “All My Enemies Are Suffering”

Bien Aachia Remix Nane Mpya za Wimbo Wake “All My Enemies Are Suffering”

Mwanamuziki nyota Bien ameendeleza kasi ya mafanikio ya kibao chake “All My Enemies Are Suffering” baada ya kuachia rasmi remix nane mpya za wimbo huo. Katika remixes hizo, Bien amewaleta pamoja mastaa wengi wakubwa kutoka maeneo mbalimbali ya Afrika, akiwemo Tobe Nwigwe, Breeder LW, Khaligraph Jones, Original Stinger, Yemi Alade na Jerau, miongoni mwa wengine. Ushirikiano huo umeupa mradi huo ladha tofauti tofauti, kuanzia rap kali, afro-fusion hadi mitindo ya Kisoul. Kwa mujibu wa wachambuzi wa burudani, hatua ya Bien ni mkakati wa kupanua wigo wa wimbo huo kimataifa na kuendeleza ushawishi wake katika muziki wa kizazi kipya barani Afrika. Kuachiwa kwa remixes hizo pia imekuja mara baada ya toleo la asili la wimbo huo kutajwa na Spotify kama moja ya nyimbo bora barani Afrika mwaka 2025 kupitia playlist ya Best of African Heat, ambapo ilikamata nafasi ya tisa.

Read More
 Bien Amaliza Ugomvi wake na Otile Brown

Bien Amaliza Ugomvi wake na Otile Brown

Msanii Bien Baraza kutoka Kenya, ametangaza kuwa tofauti zake na mwimbaji Otile Brown sasa zimefikia mwisho, na wawili hao wako katika uhusiano mzuri. Akizungumza kwenye mahhojiano kupitia Mic Cheque Podcast, Bien amesema kuwa wamezungumza na kusameheana baada ya kipindi cha kutokuelewana kilichodumu kwa muda. Bien amefichua kuwa wakati wa mzozo wao, Otile aliuchukulia suala hilo kwa uzito kiasi cha kumzuia (Block) kwenye mitandao ya kijamii, hatua iliyokuwa ishara ya sintofahamu iliyotanda kati yao Bien amempongeza Otile kwa juhudi na kazi yake kwenye muziki, akieleza kuwa licha ya tofauti zao, amekuwa akimthamini kama msanii mwenye nidhamu na bidii ya kazi. Mashabiki wamepokea habari hii kwa furaha, wakitumai kuwa hatua hiyo inaweza kufungua milango ya ushirikiano wa kimuziki kati ya wasanii hao wawili maarufu nchini.

Read More
 Bien Atimiza Ahadi ya Kshs 130,000 kwa Mshindi wa All My Enemies Are Suffering Challange

Bien Atimiza Ahadi ya Kshs 130,000 kwa Mshindi wa All My Enemies Are Suffering Challange

Msanii wa Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, amemkabidhi rasmi rapper Original Stinger KSh130,000 baada ya kumtangaza mshindi wa “All My Enemies Are Suffering” Challenge, shindano lililovutia mamia ya vijana wanaochipukia katika muziki. Akizungumza alipokabidhi fedha hizo, Bien amemsifu Stinger kwa kufanya kazi yake kwa bidii na kumpongeza kwa kutumia muziki kama nguzo ya kujikwamua na kujiendeleza. Ameongeza kuwa shindano hilo lililenga kuwapa nafasi wasanii chipukizi kuonyesha uwezo wao na kupata kutambulika katika tasnia ya muziki. Original Stinger, kwa upande wake, ameonyesha shukrani kwa Bien na mashabiki wote waliomuunga mkono, akisema kuwa ushindi huo umempa nguvu mpya ya kuendelea kutengeneza muziki wenye ubora na kusukuma brand yake mbele zaidi. Tuzo hiyo ilitolewa mbele ya mashabiki katika hafla maalum iliyoandaliwa kwa heshima ya DJ AG kutoka Uingereza ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya kwa ziara ya kikazi.

Read More
 Bien wa Sauti Sol Ataka Mwili wake Uchomwe Moto Akiaga Dunia

Bien wa Sauti Sol Ataka Mwili wake Uchomwe Moto Akiaga Dunia

Mwanamuziki Bien kutoka kundi la Sauti Sol ameibua mjadala mtandaoni baada ya kueleza mtazamo wake binafsi kuhusu namna angetaka kuzikwa endapo siku yake ya kuaga dunia itawadia. Katika maelezo yake, Bien amesisitiza kuwa hataki kabisa kufukiwa kaburini, akiamini kuwa kaburi ni upotevu wa ardhi na sio njia anayopendelea. Mkali huyo wa All My Enemies Are Suffering, amesema kuwa iwapo ataondoka duniani, angetaka mwili wake uchomwe na majivu yake yatupwe baharini au yahifadhiwe kwenye kifaa kama hourglass ili familia iweze kutumia kwa shughuli za kawaida au michezo. Hata hivyo, Bien amesisitiza kuwa huu ni msimamo wake binafsi na angependa uheshimiwe kama ilivyo, jambo linaloibua mjadala mpana kuhusu namna watu wanavyotaka kukumbukwa baada ya maisha yao duniani.

Read More
 Bien Amtangaza Original Stinger Mshindi wa “A11 My Enemies Are Suffering” Challenge

Bien Amtangaza Original Stinger Mshindi wa “A11 My Enemies Are Suffering” Challenge

Mwanamuziki Bien Baraza ametangaza msanii chipukizi Original Stinger kuwa mshindi wa shindano lake la mtandaoni “All My Enemies Are Suffering Challenge” Katika tangazo hilo, Bien ameeleza kuwa Original Stinger alishinda kutokana na ubunifu, utofauti na kiwango cha juu cha utendaji katika kazi yake, ambacho kilimtofautisha na washiriki wengine wengi waliokuwa wamejitokeza. Bien amemzawadia mshindi huyo kiasi cha KSh130,000, kama motisha kwa kazi yake na kama sehemu ya juhudi za kuunga mkono vipaji vipya katika muziki wa Kenya. Ametoa pia shukrani zake kwa washiriki wote waliojitokeza, akisema kuwa ubunifu ulioonekana katika shindano hilo unaonyesha ukuaji mkubwa wa tasnia ya muziki Afrika Mashariki. Kupitia shindano hilo, wasanii walihimizwa kuonyesha ubunifu wao kwa kutumia wimbo wa Bien, na mamia ya vijana walituma kazi zao kwa matumaini ya kushinda. Original Stinger alitajwa kuwa miongoni mwa walioleta delivery kali zaidi, sauti thabiti na ujumbe ulioendana na mahitaji ya shindano.

Read More
 Bien Akana Utambulisho Wake Asema Yeye ni Gen Z

Bien Akana Utambulisho Wake Asema Yeye ni Gen Z

Mwanamuziki wa Sauti Sol, Bien, ameibua mazungumzo mtandaoni baada ya kueleza kuwa anajitambulisha kama Gen Z na si millennial kama umri wake unavyopendekeza. Akiwa kwenye mahojiano ya That Zed Podcast, Bien ameelezea mtazamo wake kwamba kizazi hakipaswi kuamuliwa na mwaka wa kuzaliwa pekee, bali pia namna mtu anavyohisi na kujiweka katika ulimwengu wa sasa. Katika mazungumzo hayo, Bien ameonyesha kuamini kuwa mienendo, fikra za kisasa na mtazamo wa kubadilika kwa haraka ndivyo vinavyomfanya ajione karibu zaidi na kizazi cha Gen Z. Amefafanua kuwa anahusiana zaidi na namna vijana wa kizazi hicho wanavyotumia teknolojia, mtandao na mabadiliko ya kijamii. Kauli hiyo imezua mjadala mkali mitandaoni, mashabiki wengine wakicheka mtazamo wake huku wengine wakiona hatua hiyo kama njia ya kuonyesha ukaribu wake na kizazi kipya ambacho kimekuwa na ushawishi mkubwa katika muziki na utamaduni wa mtandaoni.Bien Asema Anajitambulisha Kama Gen Z, Siyo Millennial

Read More
 Bien Afunga Rasmi Shindano la “All My Enemies Are Suffering”

Bien Afunga Rasmi Shindano la “All My Enemies Are Suffering”

Msanii nyota kutoka kundi la Sauti Sol, Bien Aime Baraza, amefunga rasmi shindano lake la muziki “All My Enemies Are Suffering Open Verse Challenge”, lililovutia mamia ya washiriki kutoka Kenya na mataifa jirani. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Bien ametangaza kuwa hatua ya kupokea video mpya imekamilika, na sasa timu yake iko katika mchakato wa kuchagua mshindi atakayejinyakulia zawadi ya shilingi 130,000 za Kenya. Mshindi wa shindano hilo anatarajiwa kutangazwa tarehe 21 Novemba 2025, siku ambayo Bien amesema itakuwa maalum kwa kusherehekea vipaji vipya vya muziki vinavyochipukia nchini Kenya. Challange hiyo ilizinduliwa mapema mwezi Oktoba kama njia ya kuhamasisha ubunifu miongoni mwa wanamuziki wachanga, ambapo washiriki waliombwa kuongeza mistari yao kwenye kipande cha wimbo maarufu “All My Enemies Are Suffering”..

Read More
 Bien Apongeza Kodong Klan kwa Onyesho la Lililouza Tiketi Zote Nairobi

Bien Apongeza Kodong Klan kwa Onyesho la Lililouza Tiketi Zote Nairobi

Msanii kutoka kundi la Sauti Sol, Bien Aime Baraza, amewapongeza wanamuziki wa Kodong Klan kwa mafanikio makubwa ya onyesho lao lililofanyika katika ukumbi wa Masshouse Jijini Nairobi, ambapo tiketi zote ziliuzwa. Katika ujumbe wake wa pongezi, Bien ameeleza kuwa onyesho hilo lilikuwa miongoni mwa maonyesho bora zaidi aliyowahi kushuhudia katika tasnia ya muziki, akisisitiza kuwa wasanii wa Kenya wameendelea kuthibitisha ubora wao katika sanaa ya muziki. Mkali huyo wa ngoma ya My Enemies Are Suffering, amesema kwamba mashabiki walipata thamani ya pesa zao na hata kudokeza kuwa kiwango cha ubora kilichoonyeshwa kingestahili malipo ya juu zaidi. Bien pia ameonyesha fahari yake kwa mafanikio ya Kodong Klan, akisema kundi hilo limejenga msingi imara katika tasnia ya muziki wa Kenya.

Read More
 Bien Atajwa Kutumbuiza Afro Nation Portugal 2026

Bien Atajwa Kutumbuiza Afro Nation Portugal 2026

Mwanamuziki wa Kenya, Bien-Aimé Baraza, amepata mafanikio makubwa baada ya kutangazwa rasmi kuwa miongoni mwa mastaa watakaotumbuiza kwenye tamasha kubwa la kimataifa la Afro Nation Portugal 2026. Tamasha hilo, linalotajwa kuwa moja ya makubwa zaidi duniani kwa muziki wa Afrobeats na muziki wa Kiafrika, litafanyika kuanzia Julai 3 hadi 5 katika jiji la Portimão, Algarve nchini Ureno. Bien atapanda jukwaa moja na majina makubwa duniani akiwemo Wizkid, Asake, Tyla, Gunna, Mariah the Scientist, na Olamide, miongoni mwa wengine. Uwepo wake katika orodha hii unatajwa kama ushindi mkubwa kwa muziki wa Kenya na uthibitisho wa nafasi ya wasanii wa Afrika Mashariki katika ramani ya muziki wa kimataifa. Afro Nation Portugal, tangu kuanzishwa kwake, limekuwa kivutio kikubwa kwa mashabiki wa muziki kutoka kote ulimwenguni, likijulikana kwa kukutanisha wakali wa Afrobeat, Amapiano, Dancehall na Hip Hop kwenye jukwaa moja.

Read More
 Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Msanii nyota wa Kenya, Bien, ameanzisha rasmi shindano la Open Verse Challenge kupitia wimbo wake maarufu “All My Enemies Are Suffering.” Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bien ametoa mwaliko kwa wasanii na wabunifu kutoka kote duniani kushiriki kwa kurekodi remix ya wimbo huo na kuonyesha ubunifu wao. Mshindi ataondoka na zawadi ya dola 1,000 za Kimarekani (takribani Shilingi 130,000 za Kenya). Bien amesema kuwa shindano hili limefunguliwa kwa kila mtu duniani na litafungwa mnamo tarehe 7 Novemba 2025. Washiriki wanatakiwa kupakia remix zao kwenye mitandao ya kijamii, kumtag Bien, na kutumia alama ya reli #AllMyEnemiesChallenge. Bien pia amefichua kuwa wakali wa muziki Khaligraph Jones (kutoka Afrika Mashariki) na rapa wa Nigeria Phyno (kutoka Afrika Magharibi) wanalifuatilia kwa karibu shindano hili. “Phyno alileta ladha ya Naija, sasa ni zamu yenu,” alisema Bien akiwatia moyo vipaji vipya. Kwa ushiriki wa majina makubwa ya muziki kutoka Mashariki na Magharibi mwa Afrika, mashabiki na wasanii chipukizi wanasubiri kwa hamu kuona ni nani atakayeibuka kidedea katika shindano hili linalotarajiwa kuwa kali zaidi mwaka huu.

Read More