Bien Awataka Wasanii wa Kenya Kuepuka Shows Wanakodhulumiwa
Msanii wa muziki kutoka Kenya na mwanachama wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, ametoa wito mzito kwa wasanii nchini humo kutokubali kufanya maonyesho katika maeneo au matukio ambayo wanadharauliwa au kudhulumiwa. Kupitia ujumbe wake aliouweka kwenye mitandao ya kijamii, Bien amewapongeza wasanii wa Kodong Clan kwa uamuzi wao wa kujiondoa kwenye show ya Asake, akisema hatua hiyo ni ishara ya kujithamini na kulinda heshima yao kama wasanii. Bien amesisitiza kuwa wasanii hawapaswi kulazimika kuvumilia dharau au manyanyaso kwa kisingizio cha kupata nafasi ya kupiga show. Kauli hiyo ya Bien imekuja siku moja baada ya kundi la Kodong Clan kutangaza kujiondoa kwenye tamasha la Tukutane GA13y x Asake, wakidai kukiukwa kwa mkataba pamoja na kudharauliwa na waandaaji wa tamasha hilo.
Read More