Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Msanii nyota wa Kenya, Bien, ameanzisha rasmi shindano la Open Verse Challenge kupitia wimbo wake maarufu “All My Enemies Are Suffering.” Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bien ametoa mwaliko kwa wasanii na wabunifu kutoka kote duniani kushiriki kwa kurekodi remix ya wimbo huo na kuonyesha ubunifu wao. Mshindi ataondoka na zawadi ya dola 1,000 za Kimarekani (takribani Shilingi 130,000 za Kenya). Bien amesema kuwa shindano hili limefunguliwa kwa kila mtu duniani na litafungwa mnamo tarehe 7 Novemba 2025. Washiriki wanatakiwa kupakia remix zao kwenye mitandao ya kijamii, kumtag Bien, na kutumia alama ya reli #AllMyEnemiesChallenge. Bien pia amefichua kuwa wakali wa muziki Khaligraph Jones (kutoka Afrika Mashariki) na rapa wa Nigeria Phyno (kutoka Afrika Magharibi) wanalifuatilia kwa karibu shindano hili. “Phyno alileta ladha ya Naija, sasa ni zamu yenu,” alisema Bien akiwatia moyo vipaji vipya. Kwa ushiriki wa majina makubwa ya muziki kutoka Mashariki na Magharibi mwa Afrika, mashabiki na wasanii chipukizi wanasubiri kwa hamu kuona ni nani atakayeibuka kidedea katika shindano hili linalotarajiwa kuwa kali zaidi mwaka huu.

Read More
 Bien Aongoza Kama Msanii Anayetazamwa Zaidi YouTube Kenya 2025

Bien Aongoza Kama Msanii Anayetazamwa Zaidi YouTube Kenya 2025

Mwanamuziki Bien, ambaye zamani alikuwa mwanachama wa kundi la Sauti Sol, ameibuka kinara katika orodha ya wasanii wa Kenya wanaotazamwa zaidi kwenye YouTube kwa mwaka 2025. Kwa mujibu wa YouTube Charts Kenya, Bien amefikisha jumla ya watazamaji milioni 78.7, akithibitisha nafasi yake kama mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa kwenye tasnia ya muziki nchini Kenya. Akimfuata kwa karibu ni msanii wa ohangla Prince Indah aliyepata watazamaji milioni 64.7, huku Willy Paul akishika nafasi ya tatu kwa jumla ya watazamaji milioni 61.9. Otile Brown naye aliorodheshwa katika nafasi ya nne baada ya kupata watazamaji milioni 55.3, akionyesha kuwa bado ni miongoni mwa wanamuziki maarufu zaidi nchini humo. Wachambuzi wa burudani wanasema ukuaji wa takwimu hizi unaonyesha jinsi mashabiki wa muziki nchini Kenya wanavyotumia YouTube kama jukwaa kuu la kusikiliza na kutazama kazi za wasanii wao wa nyumbani, jambo linaloongeza ushindani na kuimarisha tasnia ya muziki wa Kenya.

Read More
 Bien Awaonya Wanaoidharau Maisha ya Ndoa

Bien Awaonya Wanaoidharau Maisha ya Ndoa

Mwanamuziki Bien, kutoka kundi la Sauti Sol, ameweka wazi mtazamo wake kuhusu ndoa akisema kwamba ni jambo zuri na lenye manufaa kwa mtu binafsi na hata kwa jamii. Akipiga stori na SPM Buzz, Bien amesema kuwa licha ya kuwepo kwa mitazamo tofauti kutoka kwa watu wengine, yeye anaamini ndoa inaleta ukuaji wa kweli katika maisha ya mtu. Ameeleza kuwa watu wanaoona ndoa kama mzigo au kizuizi wanakosea, kwani yeye mwenyewe ni mfano hai wa mafanikio na mabadiliko chanya yanayotokana na ndoa yake. Kwa mujibu wa msanii huyo, ndoa siyo kikwazo cha maendeleo kama inavyodhaniwa na baadhi ya watu, bali ni chanzo cha baraka na chachu ya ukuaji wa mtu binafsi na kifamilia. Kauli ya Bien imekuja baada ya socialite wa Kenya, aitwaye Chebet Rono, kuzua mjadala mitandaoni akidai kuwa ndoa hubamba mafala. Kauli ambayo iliibua hisia mseto, huku watumiaji wa mitandao ya kijamii wakijadiliana kwa mapana kuhusu mustakabali na maana ya ndoa kwa vijana wa kizazi cha sasa.

Read More
 Director Trevor Ampongeza Bien kwa Kumlipa Vizuri GenZ Goliath Katika Video Mpya ya Muziki

Director Trevor Ampongeza Bien kwa Kumlipa Vizuri GenZ Goliath Katika Video Mpya ya Muziki

Mkurugenzi Mkuu wa Watayarishaji wa Maudhui ya Kidijitali nchini Kenya, Director Trevor, amemsifu msanii Bien kwa kumuonesha heshima ya hali ya juu Gen Z Goliath kwa kumlipa vizuri na kumhudumia ipasavyo kwa ajili ya kuonekana kwa muda mfupi kwenye video ya muziki. Kupitia mitandao ya kijamii, Director Trevor ameweka wazi kuwa Bien alifuata taratibu zote za kazi kwa kulipa kiwango kamili cha malipo, kugharamia usafiri wa Goliath kwa kutumia gari la kifahari aina ya Toyota LX570, pamoja na malazi ya kiwango cha juu wakati wa kutayarisha video ya wimbo wake mpya “All My Enemies Are Suffering” Hii ni tofauti na matukio ya awali ambapo wasanii na waigizaji chipukizi walilalamika kutolipwa au kupuuzwa baada ya kuchangia mafanikio ya kazi mbalimbali za burudani. Mashabiki wengi wamelipongeza tukio hilo wakisema kuwa ni mfano wa kuigwa kwa wasanii wakubwa kuonyesha heshima na kuthamini mchango wa vipaji vinavyochipuka. Aidha, hatua hiyo imeibua matumaini kwa vijana wengi kuwa na imani na kazi yao huku wakijua kuwa juhudi zao zinaweza kutambuliwa na kuthaminiwa kikamilifu. Video ya wimbo mpya wa Bien,“All My Enemies Are Suffering” umewavutia wengi si tu kwa ubora wa maudhui bali pia kwa jinsi ulivyowajumuisha majina maarufu kama DJ Shiti na Gen Z Goliath, ambao wameongeza ucheshi na mvuto katika video hiyo.

Read More
 NACADA Yajibu Bien: “Sio Unafiki Bali Ni Hatua ya Kulinda Afya ya Umma”

NACADA Yajibu Bien: “Sio Unafiki Bali Ni Hatua ya Kulinda Afya ya Umma”

Mamlaka ya Kitaifa ya Kudhibiti Matumizi ya Dawa za Kulevya (NACADA) imejibu vikali matamshi ya msanii Bien wa kundi la Sauti Sol, aliyekosoa pendekezo la kuwapiga marufuku wasanii na watu mashuhuri kutangaza bidhaa za vileo. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, NACADA imesisitiza kuwa hatua hiyo haifungamani na unafiki wa maadili wala juhudi za kukandamiza uhuru wa wasanii, bali inalenga kulinda afya ya umma hasa vijana, ambao ndio walio katika hatari zaidi ya kushawishika na ulevi kupitia ushawishi wa watu maarufu. Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Bien kusema kuwa hatua hiyo ni unafiki na kwamba wasanii wana haki ya kujipatia kipato kupitia matangazo ya kibiashara. Hata hivyo, NACADA imetoa wito kwa wasanii kutumia ushawishi wao kuhamasisha maisha yenye afya na kutoa matumaini kwa jamii badala ya kushabikia bidhaa zinazoweza kuwa hatari kwa maisha ya wengi.

Read More
 Bien na Matata Wauza Tiketi Zote Paris, Waweka Historia Mpya ya Muziki wa Kenya

Bien na Matata Wauza Tiketi Zote Paris, Waweka Historia Mpya ya Muziki wa Kenya

Wasanii nyota wa Kenya Bien-Aimé Baraza (maarufu kama Bien) na kundi la Matata wameweka historia kwa kuuza tiketi zote katika onyesho lao la muziki lililofanyika mjini Paris, Ufaransa, Ijumaa usiku hatua inayotajwa kama ushindi mkubwa kwa muziki wa Kenya kimataifa. Tamasha hilo lililoandaliwa katika ukumbi maarufu wa La Bellevilloise, ulioko katikati ya jiji la Paris, liliwaleta pamoja mamia ya mashabiki kutoka mataifa mbalimbali waliokuwa na hamu ya kushuhudia utambulisho wa muziki wa Kenya  kuanzia Afro-pop ya Bien hadi dansi na miondoko ya Matata. Bien, ambaye ni mwanachama wa zamani wa kundi la Sauti Sol, alitumbuiza kwa nyimbo maarufu kama Inauma, Dimension na Too Easy, huku kundi la Matata likiwasha jukwaa kwa mitindo yao ya kipekee inayochanganya Gengetone, Afrobeat na Hip-hop ya kisasa. Kwa mujibu wa waratibu wa tamasha hilo, tiketi zote ziliisha siku chache kabla ya onyesho hilo, ishara ya kupanda kwa umaarufu wa muziki wa Kenya katika soko la kimataifa. Wakenya wanaoishi ughaibuni walijitokeza kwa wingi, wengi wao wakijivunia kuona wasanii kutoka nyumbani wakipeperusha bendera ya Kenya kwa ufanisi mkubwa. Mitandao ya kijamii ilifurika na video za mashabiki wakicheza kwa furaha, huku wakisifia ubora wa muziki na utumbuizaji wa hali ya juu. Matukio kama haya yanatajwa kuwa hatua muhimu katika kutangaza muziki wa Afrika Mashariki duniani, hasa wakati ambapo wasanii wa Nigeria na Afrika Kusini wamekuwa wakitawala majukwaa ya kimataifa.

Read More
 Bien Ajitetea Baada ya Kauli Tatanishi Kuhusu Wanawake wa Kenya

Bien Ajitetea Baada ya Kauli Tatanishi Kuhusu Wanawake wa Kenya

Mwanamuziki maarufu kutoka Kenya na mshiriki wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, amevunja ukimya kufuatia mjadala ulioibuka mitandaoni kuhusu mstari wa wimbo wake mpya unaozungumzia wanawake wa Kenya kuwa na foreheads kubwa (paji kubwa za uso). Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram, Bien alisisitiza kuwa wimbo wake ni kazi ya sanaa inayopaswa kuchukuliwa kwa upana na si kwa hisia binafsi Bien aliongeza kuwa kauli yake haikuwa ya matusi bali ya mapenzi na shukrani kwa wanawake wa Kiafrika, hasa mke wake, Chiki Kuruka, ambaye ni mhamasishaji wa mazoezi ya mwili na mpenda sanaa.  “I love our women with foreheads. I could never be with a woman who doesn’t have a forehead. Have you seen my wife?” Aliandika akimjibu shabiki aliyemkosoa vikali kuhusu wimbo wake mpya unaotajwa kuwa na mistari ya kuudhi, hasa kwa wanawake wa Kenya.. Kauli yake imeibua maoni mbalimbali mitandaoni. Wapo waliomsifu kwa kuwa na ujasiri wa kusimama na kazi yake, huku wakiona mstari huo kama ucheshi wa kawaida, lakini pia wapo waliodai kuwa wasanii wanapaswa kuwa makini zaidi na lugha wanayotumia kwa kuwa wana ushawishi mkubwa kwa jamii. Bien wa Sauti Sol na Diamond Platnumz wameachia wimbo mpya unaoitwa “Katam”. Wimbo huu umetoka hivi karibuni na umepokelewa vizuri sana na mashabiki wao. “Katam” ni wimbo wa mapenzi unaosherehekea uzuri na umoja barani Afrika, na unawaunganisha wasanii hawa wawili wakubwa wa Afrika Mashariki.

Read More
 Msanii Bien Atikisa Marekani, Aipa Heshima Kenya Katika The Breakfast Club

Msanii Bien Atikisa Marekani, Aipa Heshima Kenya Katika The Breakfast Club

Msanii mashuhuri wa Kenya, Bien Aime Baraza, ameweka historia kwa kuwa msanii wa kwanza kutoka Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla kuhojiwa katika kipindi maarufu cha The Breakfast Club nchini Marekani. Hatua hii imepokelewa kwa shangwe kubwa na mashabiki wa muziki barani Afrika, ikionekana kama mafanikio makubwa kwa muziki wa ukanda huu. Katika mahojiano hayo ya kipekee, Bien alifunguka kuhusu maisha yake ya kifamilia, akisisitiza umuhimu wa uwazi katika ndoa yake. Mkali huyo wa bendi ya Sauti Sol, alionyesha kuwa uaminifu na ushirikiano ndio msingi wa mafanikio yao ya kindoa. “Kwenye nyumba yangu, pesa ni za familia. Mke wangu ana ufikiaji wa pesa zangu zote nami pia nina ufikiaji wa pesa zake zote,” alisema Bien kwa uwazi, Mbali na maisha ya nyumbani, Bien pia aligusia muziki wa Kenya na alitoa heshima kwa vipaji vya hapa nyumbani kwa kueleza wasanii anaowakubali zaidi. “Wasanii ninaowapenda sana Kenya ni Nyashinski, Ywaya kutoka kundi la Watendawili, Kodong Klan na Njerae,” alieleza Bien, Hatua yake ya kuonekana kwenye The Breakfast Club inachukuliwa kama ushindi mkubwa kwa muziki wa Afrika Mashariki na imezidi kuonyesha kuwa wasanii kutoka ukanda huu wana nafasi kubwa kwenye jukwaa la kimataifa. Mashabiki mitandaoni wameonyesha fahari na pongezi, wakimpongeza Bien kwa kulipeperusha vyema bendera ya Kenya kimataifa.

Read More
 Shabiki Aweka Historia Kwenye Tamasha la Bien New York kwa Pendekezo la Ndoa la Kushtukiza

Shabiki Aweka Historia Kwenye Tamasha la Bien New York kwa Pendekezo la Ndoa la Kushtukiza

Tamasha la Bien jijini New York liligeuka kuwa jukwaa la mapenzi na mshangao, pale ambapo shabiki mmoja aliwashangaza wote kwa kutoa pendekezo la ndoa mbele ya umati mkubwa wa mashabiki waliofurika kwenye ukumbi huo uliojaa hadi pomoni. Bien, mwanamuziki mahiri kutoka Kenya na mwanachama wa kundi maarufu la Sauti Sol, alikuwa akitumbuiza kwa hisia moja ya nyimbo zake za mahaba, alipokatizwa kwa heshima na shabiki huyo aliyepanda jukwaani akiwa ameambatana na mchumba wake. Kwa msaada wa timu ya Bien, alipanda jukwaani na kutangaza upendo wake hadharani kwa kutoa pendekezo la ndoa mbele ya mashabiki wote. Mashabiki walilipuka kwa shangwe na vigelegele wakati mwanamke huyo alikubali pendekezo hilo huku machozi ya furaha yakitiririka. Bien, alionekana kuguswa na tukio hilo la kipekee. “Hii ndiyo maana ya muziki – kuunganisha watu, kuleta mapenzi na kumbukumbu zisizosahaulika. Hongera kwa wapenzi wetu wapya!” alisema Bien Pendekezo hilo limekuwa gumzo mitandaoni, likipokelewa kwa furaha na msisimko na mashabiki kutoka kila kona ya dunia. Wengi wameelezea tukio hilo kama moja ya matukio ya kipekee kuwahi kutokea katika tamasha la muziki, na ushahidi kuwa muziki wa Bien si tu wa kusikiliza bali pia wa kuishi. Tamasha hilo lilikuwa sehemu ya ziara ya kimataifa ya Bien kama msanii wa kujitegemea, na sasa linaacha kumbukumbu si tu kwa sababu ya muziki mzuri, bali pia kwa kuwa sehemu ya safari ya mapenzi ya watu wawili.

Read More
 Bien Aandika Historia The Radar Radio, Awasilisha Utambulisho wa Mkenya kwa Ubunifu

Bien Aandika Historia The Radar Radio, Awasilisha Utambulisho wa Mkenya kwa Ubunifu

Msanii maarufu kutoka Kenya na mmoja wa wanamuziki wa kundi la Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, ameweka historia mpya kwa kuwakilisha Kenya na Afrika Mashariki kwenye kipindi maarufu cha The Radar Radio nchini Uingereza. Hii ni baada ya kuonekana kwenye kipindi hicho kwa freestyle ya kipekee, akifuatia nyayo za msanii Kaycyy, ambaye alikuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kushiriki. Kilichoifanya freestyle ya Bien kuwa ya kipekee si tu uwezo wake wa kutunga na kuwasilisha kwa ustadi, bali pia hatua yake ya kuleta kuku hai studio kama ishara ya utamaduni wake wa Kiluhya na mzizi wake wa Kiafrika. Hatua hiyo imetafsiriwa kama tamko la fahari ya utambulisho wake wa asili, na imepokelewa kwa hisia tofauti mitandaoni. The Radar Radio ni jukwaa maarufu duniani ambalo limewahi kuwakaribisha wasanii wakubwa kama Drake, Central Cee, Ice Spice na wengine wengi, likiwa ni sehemu ya kuonesha vipaji halisi kupitia maonyesho ya freestyle. Kwa Bien, huu ulikuwa wakati wa kuonesha kuwa muziki wa Afrika Mashariki unaweza kusimama bega kwa bega na muziki wa kimataifa, huku ukidumisha mizizi ya kitamaduni. Hatua yake imepongezwa sana na mashabiki barani Afrika na diaspora, wengi wakisema kuwa ni mfano bora wa jinsi wasanii wa Kiafrika wanavyoweza kutumia jukwaa la kimataifa kueneza utamaduni wao kwa njia ya ubunifu. Bien kwa sasa anaendelea na kazi yake ya muziki kama msanii wa kujitegemea baada ya mafanikio makubwa akiwa na Sauti Sol. Uwepo wake kwenye The Radar ni hatua nyingine kubwa katika safari yake ya kimataifa.

Read More
 Bien-Aime Ajitangaza Kuwa Balozi wa Gitaa la Jawaya la Fancy Fingers

Bien-Aime Ajitangaza Kuwa Balozi wa Gitaa la Jawaya la Fancy Fingers

Katika tukio lililowashangaza na kuwaburudisha mashabiki wa muziki wa Afrika Mashariki, msanii mashuhuri Bien-Aime Baraza ametangaza kuwa yeye ndiye balozi rasmi wa chapa ya gitaa ya Jawaya, inayomilikiwa na mwanamuziki mwenzake wa Sauti Sol, Fancy Fingers. Kupitia ujumbe wake uliojaa mzaha aliouweka kwenye mitandao ya kijamii, Bien alisema kwamba amejichagulia nafasi ya kuwa “brand ambassador” wa Jawaya, akisisitiza kuwa mapenzi yake kwa muziki na ubora wa gitaa hilo hayawezi kupuuzwa. Tangazo hilo limezua gumzo mitandaoni, huku mashabiki wakielezea furaha na msisimko wao juu ya ushirikiano huo wa kipekee. Jawaya ni chapa ya gitaa iliyotengenezwa kwa ubunifu wa hali ya juu, ikichanganya usanii wa Kiafrika na teknolojia ya kisasa. Ikiwa ni zao la ubunifu wa Fancy Fingers, gitaa hilo linalenga kuwatia moyo wanamuziki wa Kiafrika kutumia vifaa vya kiwango cha kimataifa vilivyotengenezwa barani mwao. Ingawa Bien hajatangaza kama kuna mkataba rasmi wa ubalozi, hatua yake inaonyesha mshikamano wa dhati baina ya wasanii, na kuhimiza kuunga mkono bidhaa zinazotoka kwa vipaji vya nyumbani. Kwa kutumia umaarufu wake, Bien anaongeza mvuto na mwanga kwa chapa ya Jawaya, na huenda akasaidia kuifikisha kwa hadhira kubwa zaidi, ndani na nje ya bara la Afrika. Kwa sasa, mashabiki na wachambuzi wa muziki wanasubiri kwa hamu kuona kama uhusiano huu wa kirafiki utafanyika rasmi—au ikiwa Bien ataendelea kujiita balozi kwa jina tu, huku akipiga gitaa la Jawaya kwa ustadi na fahari.

Read More
 Bien wa Sauti Sol ahirisha ziara yake ya muziki nchini Marekani

Bien wa Sauti Sol ahirisha ziara yake ya muziki nchini Marekani

Mwimbaji maarufu nchini Kenya anayeunda kundi la Sauti Sol, Bien Aime Baraza ametangaza kuahirisha ziara yake ya muziki nchini Marekani Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Duke Concept Entertainment kupitia ukurasa wao rasmi wa Instagram, maamuzi hayo yametokana na kukosekana kwa baadhi ya wanachama muhimu wa bendi ambao kwa mujibu wao ingeathiri mchakato mzima wa kutoa burudani kwa mashabiki. Pamoja na kuahirisha ziara hiyo Bien amewaomba radhi mashabiki zake kwa usumbufu uliojitokeza huku akiwajuza walionunua tiketi kuwa wasiwe na hofu kwani tiketi hizo zitatumika pale watakapotangaza tena kufanyika kwa shows hizo hivi karibuni. Bien alipaswa kuanza ziara yake hiyo ya “Alusa Why Are You Topless” mnamo tarehe 5 mwezi Februari mwaka huu ambapo angeanzia huko Atalanta na kuihitimisha Februari 16 Jijini New York.

Read More