Bien Afunguka Kufuatia Shinikizo za Wasanii Kuandaa Wimbo wa Kumuenzi Raila Odinga

Bien Afunguka Kufuatia Shinikizo za Wasanii Kuandaa Wimbo wa Kumuenzi Raila Odinga

Msanii wa Sauti Sol, Bien-Aimé Baraza, amefunguka baada ya shinikizo kutoka kwa baadhi ya wadau wa muziki waliohoji kwa nini wasanii wa Kenya hawakuandaa wimbo wa pamoja wa kumuomboleza hayati Raila Amolo Odinga. Kupitia sehemu ya maoni kwenye video ya YY Comedian iliyoenea mitandaoni, Bien ameacha ujumbe uliovutia hisia mseto mtandaoni kwa kuandika, “Watu wengine labda Baba afufuke ndio niwork nao.” Kauli hiyo imefafanuliwa na wengi kama ishara ya kuwepo kwa mgongano wa chini kwa chini kati yake na baadhi ya wasanii wa muziki nchini Kenya, ingawa wengine wameichukulia kama utani wa kawaida. Mashabiki mitandaoni wamegawanyika, baadhi wakisema Bien alikuwa anatania tu, huku wengine wakihisi kwamba maneno yake yanaakisi hali halisi ya ukosefu wa umoja miongoni mwa wasanii wa Kenya.

Read More
 Bien Asema Kifo cha Raila Ni Pigo kwa Demokrasia ya Kenya

Bien Asema Kifo cha Raila Ni Pigo kwa Demokrasia ya Kenya

Mwanamuziki Bien-Aimé Baraza wa kundi la Sauti Sol amefunguka kwa uchungu mkubwa kufuatia kifo cha kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga. Kupitia ujumbe alioweka kwenye mitandao yake ya kijamii, Bien amesema kuwa kifo cha Raila ni sawa na kupotea kwa hazina kubwa ya hekima na historia ya taifa. Ameongeza kuwa Odinga alikuwa kiongozi aliyebeba maono makubwa ya maendeleo ya Kenya na mchango wake katika siasa na jamii hauwezi kupuuzwa. Bien amewahimiza Wakenya kuendelea kudumisha maadili ya amani na ukweli ambao Raila aliwahi kuyapigania, huku akiwataka kuendeleza mapambano ya kujenga Kenya bora kama alivyokuwa akitaka mwanasiasa huyo mkongwe. Hata hivyo msanii huyo wa “All My Enemies Are Suffering”, amemalizia ujumbe wake kwa kumkumbuka Raila kama mtu ambaye atabaki hai mioyoni mwa Wakenya wote.

Read More