Diamond Awasihi Vijana Kutokata Tamaa Maishani

Diamond Awasihi Vijana Kutokata Tamaa Maishani

Mwanamuziki nyota wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amewahimiza vijana kutokata tamaa katika maisha na badala yake waendelee kuweka juhudi ili kufikia malengo yao. Akizungumza baada ya Mama Asha Baraka kuteuliwa kuwa Mbunge Maalum, Diamond amesema uteuzi huo ni ushahidi kuwa juhudi na uvumilivu huzaa matunda, kwani Mama Asha amesimama mara 20 bila mafanikio katika chaguzi zilizopita. Mkali huyo wa ngoma ya Msumari, amesema vijana wanapaswa kujifunza kutokana na mfano wa Mama Asha Baraka, ambaye licha ya kushindwa mara nyingi, hakuwahi kukata tamaa hadi akatambuliwa na kuteuliwa kushika nafasi hiyo ya heshima. Diamond amesisitiza kuwa mafanikio hayaji kwa urahisi na kwamba kila changamoto ni sehemu ya safari ya mafanikio.

Read More
 Diamond Platnumz: Kuwa Msanii Nchini Tanzania Ni Kazi Ngumu Sana

Diamond Platnumz: Kuwa Msanii Nchini Tanzania Ni Kazi Ngumu Sana

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake baada ya kukosolewa vikali mitandaoni kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kutosimama na wananchi katika kipindi ambacho taifa linakumbwa na machungu ya kisiasa na kijamii. Kupitia Instastory yake, Diamond ameonekana kujibu wakosoaji wake kwa njia ya mafumbo, akisema kuwa msanii nchini Tanzania ni kazi ngumu sana hasa unapojaribu kudumisha amani na heshima katikati ya misukosuko ya kisiasa. Kauli yake inakuja wakati mashabiki wake wakionyesha hasira na majonzi, wakimtuhumu kwa kukaa kimya wakati baadhi ya Watanzania wanaomboleza wapendwa wao waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya kupinga uchaguzi wa Oktoba 29 uliokumbwa na utata. Wapo wanaoamini kuwa Diamond, akiwa msanii mwenye ushawishi mkubwa Afrika Mashariki, anapaswa kutumia sauti yake kutetea wananchi, ilhali wengine wanamtetea wakisema kuwa amechagua ukimya ili kulinda taaluma yake na kuepuka migongano ya kisiasa

Read More
 Watanzania Waanza Ku-unfollow Wasanii Waliomuunga Mkono Rais Samia Suluhu

Watanzania Waanza Ku-unfollow Wasanii Waliomuunga Mkono Rais Samia Suluhu

Baadhi ya Watanzania wameanzisha kampeni kubwa ya mitandaoni ya kuwa-unfollow wasanii maarufu waliomuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika harakati zake za kurejea madarakani. Miongoni mwa waliokumbwa na wimbi hilo ni staa wa Bongo Fleva Diamond Platnumz, ambaye inaripotiwa amepoteza zaidi ya wafuasi 100,000 ndani ya saa 12 pekee. Msanii mwingine anayelengwa ni Harmonize, ambaye naye amekuwa mhanga wa hasira za mashabiki mitandaoni. Watanzania wengi wanawalaumu wasanii hao kwa kutumia ushawishi wao na majukwaa yao ya kijamii kuiunga mkono serikali wanayoitaja kuwa kandamizi inayoongozwa na Rais Suluhu Hassan. Hata hivyo, mjadala mkali umeibuka mitandaoni baadhi wakisema wasanii wana haki ya kuwa na misimamo yao ya kisiasa, huku wengine wakisisitiza kwamba mastaa wanapaswa kusimama na wananchi nyakati za migogoro ya kisiasa. Kampeni hiyo ya kufuta ufuasi au Ku-unfollow imekuja wakati ambapo hali ya kisiasa nchini Tanzania imezidi kuwa tete, kufuatia maandamano na mvutano unaoendelea baada ya matokeo ya uchaguzi yaliyokumbwa na utata mkubwa.

Read More
 Diamond Atoa Ujumbe wa Faraja na Amani Kwa Watanzania

Diamond Atoa Ujumbe wa Faraja na Amani Kwa Watanzania

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ameungana na Watanzania katika kipindi hiki cha huzuni na maombolezo kufuatia ghasia zilizoripotiwa baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, akisisitiza umuhimu wa imani, umoja na upendo miongoni mwa wananchi. Kupitia ujumbe wake mtandaoni, Diamond alisema kuwa hakuna jambo hutokea bila mapenzi ya Mungu, akiongeza kuwa kila tukio lina sababu ya kimungu inayoweza kuleta baraka na mafanikio kwa taifa endapo watu watadumisha amani na mshikamano. Msanii huyo amewataka Watanzania kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu ili awajaalie amani zaidi ya waliyoipata hapo awali, upendo, umoja, na maendeleo kwa wote. Amemaliza ujumbe wake kwa kuwaombea waliopoteza maisha wapumzike kwa amani na kwamba taifa lipate faraja na nguvu ya kusonga mbele kwa matumaini mapya. Kauli ya Diamond inakuja baada ya tetesi kusambaa mtandaoni zikidai kuwa Diamond na familia yake waliondoka nchini Tanzania kwa hofu ya kushambuliwa, baada ya baadhi ya biashara za wasanii waliomuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan kuripotiwa kushambuliwa na waandamanaji waliopinga uchaguzi huo.

Read More
 Diamond Platnumz Aondoa Video na Machapisho ya Kuunga Mkono Rais Samia

Diamond Platnumz Aondoa Video na Machapisho ya Kuunga Mkono Rais Samia

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ameondoa video na machapisho yote ya hivi karibuni kwenye mitandao yake ya kijamii yaliyomuonyesha akimuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan na chama tawala cha CCM. Video hizo, ambazo zilikuwa zimeenea sana mtandaoni, zilionyesha Diamond akitumbuiza katika kampeni na ziara za kisiasa za Rais Samia na chama cha CCM, akionesha wazi uungwaji mkono wake kwa serikali na juhudi za rais huyo kutafuta muhula mwingine wa uongozi. Hatua hii imekuja wakati ambapo Tanzania inakabiliwa na mzozo wa kisiasa na maandamano ya kumpinga Rais Samia, yaliyosambaa katika miji kadhaa ikiwemo Dar es Salaam, Arusha, na Mwanza. Maandamano hayo yamechochewa na madai ya kukandamizwa kwa viongozi wa upinzani na kukamatwa kwa wanaharakati. Hadi sasa, Diamond hajatoa kauli rasmi kuhusu hatua yake, lakini wachambuzi wanasema anaweza kuwa anajitenga na lawama kutokana na mvutano wa kisiasa unaoendelea nchini humo.

Read More
 Diamond Platnumz Atangaza Msimu wa Pili wa Tamasha la “Diamonds Are Forever”

Diamond Platnumz Atangaza Msimu wa Pili wa Tamasha la “Diamonds Are Forever”

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, ametangaza kurejea na msimu wa pili wa tamasha lake kubwa la “Diamonds Are Forever”, kama ishara ya shukrani kwa mashabiki wake kutokana na upendo na sapoti kubwa wanayoendelea kumpa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond amesema ameguswa na mapenzi na uaminifu wa mashabiki wake, akieleza kuwa wamekuwa sehemu muhimu ya mafanikio yake katika muziki. Msanii huyo anayefanya poa na ngoma yake ya Sasampa, ameongeza kuwa tamasha hilo litakuwa ni njia ya kusherehekea safari yake ya kimuziki na kuwashukuru wote waliomuunga mkono tangu mwanzo. Tamasha la kwanza la “Diamonds Are Forever” lilifanyika mwaka 2012 katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, na liliweka historia kubwa katika muziki wa Tanzania kwa kujumuisha maonyesho makubwa na maelfu ya mashabiki.

Read More
 Diamond Platnumz Atuma Salamu za Pole kwa Wakenya Kufuatia Kifo cha Raila Odinga

Diamond Platnumz Atuma Salamu za Pole kwa Wakenya Kufuatia Kifo cha Raila Odinga

Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ametuma salamu za rambirambi kwa wananchi wa Kenya kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Odinga. Kupitia Insta Story Instagram, Diamond ameposti picha yake akiwa anaongea na marehemu Raila wakati wa hafla ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2022 katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi, akielezea masikitiko yake na kumtakia kiongozi huyo pumziko la amani. Hitmaker huyo wa Nani, ameambatanisha ujumbe wake huo na wimbo wa Zabron Singers uitwao Inaniuma, ishara ya huzuni na uchungu aliouhisi kufuatia kifo cha kiongozi huyo ambaye alimfahamu binafsi. Diamond alikuwa miongoni mwa wasanii waliotoa burudani wakati wa kampeni za mwisho za Raila mwaka 2022, hafla iliyohudhuriwa na maelfu ya watu. Inadaiwa kwamba msanii huyo alinufaika pakubwa na ushiriki wake katika kampeni hizo, akipokea takribani shilingi milioni 10 za Kenya kwa kutumbuiza kwenye tamasha hilo kubwa.

Read More
 Mama Dangote Asema Akifariki, Diamond Atapata Tabu Sana

Mama Dangote Asema Akifariki, Diamond Atapata Tabu Sana

Mama mzazi wa staa wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, maarufu kama Mama Dangote, amesema wazi kuwa akifariki dunia, mwanawe atapata tabu sana kutokana na jinsi anavyomtegemea kihisia. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Mama Dangote ameeleza kwa hisia jinsi Diamond alivyorudi kutoka safarini na kuanza kudeka kama mtoto mdogo, hali inayomgusa sana kama mzazi. Amesema kuwa tabia hiyo inaonyesha namna mwanawe anavyompenda na kumthamini kama mama, licha ya kuwa mtu mzima mwenye umaarufu na mafanikio makubwa. Mama Dangote, amesema Diamond anayejulikana kwa jina la utani Tom Kaka, amekuwa na uhusiano wa karibu sana naye kiasi kwamba kuondoka kwake kungemuumiza sana mwanawe huyo. Mwanamama huyo ameongeza kwa utani kuwa “mtoto kwa mama hakui,” akimaanisha kuwa kwa mama, mtoto atasalia kuwa mtoto milele bila kujali umri au hadhi yake. Ujumbe huo umevuta hisia za mashabiki wengi mtandaoni, wengi wakimpongeza Mama Dangote kwa maneno yake ya upendo na wengine wakigusia uhusiano wa kipekee uliopo kati yake na mwanamuziki huyo nyota wa Afrika Mashariki.

Read More
 Diamond Platnumz Aweka Rekodi Mpya kwenye Audiomack

Diamond Platnumz Aweka Rekodi Mpya kwenye Audiomack

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva na hitmaker wa ngoma Msumari, Diamond Platnumz, ameweka historia mpya baada ya kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kufikisha wafuasi milioni 1 kwenye mtandao wa Audiomack. Takwimu hizo zinaonesha ukuaji mkubwa wa ushawishi wake kwenye majukwaa ya kidijitali, ikithibitisha nafasi yake kama mmoja wa wasanii wakubwa barani Afrika. Audiomack, ambayo ni moja ya majukwaa makubwa ya kusikiliza muziki duniani, imekuwa chachu muhimu kwa wasanii wa Kiafrika kufikia mashabiki kimataifa. Kupitia mafanikio haya, Diamond Platnumz ameendeleza rekodi yake ya kuwa kinara wa mitandao mbalimbali ya muziki kama YouTube, Boomplay, Spotify na Apple Music, ambapo nyimbo zake zimeendelea kufanya vizuri ndani na nje ya Tanzania. Mashabiki wake wamempongeza kwa mafanikio hayo, wakimtaja kama mfano wa kuigwa katika kukuza muziki wa Afrika Mashariki kimataifa

Read More
 Diamond Awapa Vijana Somo Zito Kuhusu Mapenzi na Maisha

Diamond Awapa Vijana Somo Zito Kuhusu Mapenzi na Maisha

Staa wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ametoa ushauri mzito kwa vijana ambao bado hawajaoa, akiwataka kuacha kudharau miili yao na kupoteza fedha kwa kuwa na wanawake wengi. Kupitia ujumbe aliouandika SnapChat, Diamond amewaonya vijana kwamba tabia ya kubadilisha wapenzi mara kwa mara haiwezi kuwasaidia kufanikisha ndoto zao wala kuwapeleka popote kimaisha. Mwanamuziki huyo amesema kuwa hekima ya kweli ni kujitambua na kuamua kutulia na mpenzi mmoja, au wawili, huku akieleza kuwa kiwango cha juu kabisa kisipite watatu. Aidha, ameongeza kuwa katika hali ya changamoto kubwa, vijana wanaweza kuwa na wanne pekee. Ushauri huo umewavutia mashabiki wengi mitandaoni, huku baadhi wakipongeza msimamo wa Diamond kama njia ya kuhamasisha vijana kuheshimu maisha yao na kutumia rasilimali zao kwa uangalifu.

Read More
 Diamond Platnumz Apokea Tuzo ya Diamond Play Button Kutoka YouTube

Diamond Platnumz Apokea Tuzo ya Diamond Play Button Kutoka YouTube

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Flava, Diamond Platnumz, ameweka rekodi mpya baada ya kukabidhiwa tuzo ya kifahari ya Diamond Play Button kutoka YouTube, ikiwa ni kutambua mafanikio ya kufikisha zaidi ya wafuasi milioni 10 kwenye chaneli yake rasmi. Tukio hilo lilifanyika jijini New York, Marekani, na linamweka Diamond katika nafasi ya kipekee kama mmoja wa wasanii wachache kutoka Afrika kufikia kiwango hicho. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond alithibitisha kupokea tuzo hiyo huku akionyesha shukrani kwa mashabiki, timu yake, familia, na YouTube kwa mafanikio hayo makubwa. “Thank you YouTube, My Fans, Team & Family! 10+ Million YouTube Subscribers 🙏🏽🔥” Aliandika Instagram. Diamond anakuwa msanii wa nne kutoka Afrika kupokea Diamond Play Button, akiungana na wasanii kama Mohamed Ramadan, Saad Lamjarred, na Soolking. Tuzo hii hutolewa na YouTube kwa chaneli zilizofikisha au kupita subscribers milioni 10, na ni alama ya ushawishi mkubwa wa kidijitali duniani. Mafanikio haya yanaimarisha nafasi ya Diamond si tu kama msanii wa Tanzania au Afrika Mashariki, bali pia kama nembo ya muziki wa Afrika kwenye majukwaa ya kimataifa. Mashabiki wake wamekuwa nguzo muhimu katika safari yake ya muziki, wakichangia kwa namna ya kipekee kwa kuangalia, kushirikisha na kusambaza kazi zake mtandaoni kwa zaidi ya muongo mmoja.

Read More
 Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, hatimaye amethibitisha kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Zuchu, katika sherehe ya ndoa iliyofanyika kwa faragha mwishoni mwa wiki. Taarifa za ndoa hiyo zilithibitishwa kupitia picha na video zilizoshirikiwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo Diamond na Zuchu walionekana wakiwa kwenye vazi la Kiislamu, pamoja na familia na marafiki wa karibu. Video hizo zilionyesha Zuchu akimwita Diamond “mume wangu” huku wakiwa kwenye gari baada ya sherehe, jambo lililozua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki. Mama wa Diamond, Bi Sandra Dangote, alituma ujumbe wa pongezi kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiwatakia heri wanandoa hao wapya na kusisitiza kuwa ni hatua muhimu kwa mwanaye. Ndoa hii imekuja baada ya uvumi wa muda mrefu kuhusu uhusiano wao, huku Diamond akiwahi kutangaza hadharani kuwa ana mpango wa kumuoa Zuchu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadan mwaka huu. Hata hivyo, mipango hiyo ilicheleweshwa, na hatimaye wawili hao wamefanikisha lengo hilo kwa shangwe na furaha. Mashabiki na wadau wa muziki wameendelea kuwatumia salamu za heri na baraka kwa maisha yao mapya ya ndoa. Wengi wameeleza matumaini kuwa ndoa hiyo italeta utulivu na kuimarisha zaidi kazi zao za muziki. Kwa sasa, wawili hao hawajatoa taarifa ya kina kwa vyombo vya habari, lakini mashabiki wanatarajia tamko rasmi kutoka kwao hivi karibuni.

Read More