Diamond Platnumz Apokea Tuzo ya Diamond Play Button Kutoka YouTube

Diamond Platnumz Apokea Tuzo ya Diamond Play Button Kutoka YouTube

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Flava, Diamond Platnumz, ameweka rekodi mpya baada ya kukabidhiwa tuzo ya kifahari ya Diamond Play Button kutoka YouTube, ikiwa ni kutambua mafanikio ya kufikisha zaidi ya wafuasi milioni 10 kwenye chaneli yake rasmi. Tukio hilo lilifanyika jijini New York, Marekani, na linamweka Diamond katika nafasi ya kipekee kama mmoja wa wasanii wachache kutoka Afrika kufikia kiwango hicho. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond alithibitisha kupokea tuzo hiyo huku akionyesha shukrani kwa mashabiki, timu yake, familia, na YouTube kwa mafanikio hayo makubwa. “Thank you YouTube, My Fans, Team & Family! 10+ Million YouTube Subscribers 🙏🏽🔥” Aliandika Instagram. Diamond anakuwa msanii wa nne kutoka Afrika kupokea Diamond Play Button, akiungana na wasanii kama Mohamed Ramadan, Saad Lamjarred, na Soolking. Tuzo hii hutolewa na YouTube kwa chaneli zilizofikisha au kupita subscribers milioni 10, na ni alama ya ushawishi mkubwa wa kidijitali duniani. Mafanikio haya yanaimarisha nafasi ya Diamond si tu kama msanii wa Tanzania au Afrika Mashariki, bali pia kama nembo ya muziki wa Afrika kwenye majukwaa ya kimataifa. Mashabiki wake wamekuwa nguzo muhimu katika safari yake ya muziki, wakichangia kwa namna ya kipekee kwa kuangalia, kushirikisha na kusambaza kazi zake mtandaoni kwa zaidi ya muongo mmoja.

Read More
 Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, hatimaye amethibitisha kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Zuchu, katika sherehe ya ndoa iliyofanyika kwa faragha mwishoni mwa wiki. Taarifa za ndoa hiyo zilithibitishwa kupitia picha na video zilizoshirikiwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo Diamond na Zuchu walionekana wakiwa kwenye vazi la Kiislamu, pamoja na familia na marafiki wa karibu. Video hizo zilionyesha Zuchu akimwita Diamond “mume wangu” huku wakiwa kwenye gari baada ya sherehe, jambo lililozua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki. Mama wa Diamond, Bi Sandra Dangote, alituma ujumbe wa pongezi kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiwatakia heri wanandoa hao wapya na kusisitiza kuwa ni hatua muhimu kwa mwanaye. Ndoa hii imekuja baada ya uvumi wa muda mrefu kuhusu uhusiano wao, huku Diamond akiwahi kutangaza hadharani kuwa ana mpango wa kumuoa Zuchu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadan mwaka huu. Hata hivyo, mipango hiyo ilicheleweshwa, na hatimaye wawili hao wamefanikisha lengo hilo kwa shangwe na furaha. Mashabiki na wadau wa muziki wameendelea kuwatumia salamu za heri na baraka kwa maisha yao mapya ya ndoa. Wengi wameeleza matumaini kuwa ndoa hiyo italeta utulivu na kuimarisha zaidi kazi zao za muziki. Kwa sasa, wawili hao hawajatoa taarifa ya kina kwa vyombo vya habari, lakini mashabiki wanatarajia tamko rasmi kutoka kwao hivi karibuni.

Read More
 Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Zuchu, amezua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu mustakabali wa uhusiano wake na staa wa muziki,Diamond Platnumz Akihojiwa katika kipindi cha Refresh Show kinachorushwa na Wasafi TV, wakati wa hafla ya JP Night 2025, Zuchu alionesha wazi kuwa ndoa haipo kwenye mipango yake na Diamond, licha ya uhusiano wao wa muda mrefu ambao umeendelea kuibua gumzo mitandaoni. Mkali huyo wa ngoma ya “Sukari” ameweka wazi kuwa hatima ya ndoa kati yake na mpenzi wake, Diamond Platnumz, haiko mikononi mwake bali yaachwe kwa Mwenyezi Mungu kuamua. “Tumuachie Mungu, Atajua Wakati Sahihi na Mtu Sahihi.”, alisema Zuchu kwa utulivu, Huku akionekana mwenye utulivu na kujiamini, Zuchu hakufafanua zaidi kuhusu hali halisi ya uhusiano wao, lakini maneno yake yameeleweka kama ishara ya kuwepo kwa mashaka au uwezekano wa mabadiliko katika safari yao ya kimapenzi. Kauli hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki na wafuasi wa wawili hao ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakifuatilia kwa karibu uhusiano wao wa kimapenzi. Wengi walitarajia kuwa mwaka huu huenda ungekuwa wa hatua kubwa kama uchumba au ndoa, lakini kauli ya Zuchu imeonyesha bado kuna sintofahamu. Diamond Platnumz na Zuchu wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu, ingawa mara kadhaa wamekana au kutoa majibu ya kujihami kuhusu uhusiano huo. Licha ya kuonekana pamoja mara kwa mara kwenye matamasha na hafla za kifamilia, bado hakuna uthibitisho rasmi wa ndoa au uchumba kutoka kwa wawili hao.

Read More
 Eddy Kenzo Akerwa na Malipo ya Diamond Platnumz Katika Mbio za Coffee Marathon

Eddy Kenzo Akerwa na Malipo ya Diamond Platnumz Katika Mbio za Coffee Marathon

Mwanamuziki nyota wa Uganda, Eddy Kenzo, ameeleza masikitiko makubwa dhidi ya waandaaji wa Coffee Marathon kwa kumpa kipaumbele msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz, badala ya kuwatambua na kuwaunga mkono wasanii wa ndani ya nchi. Katika mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha ndani mapema wiki hii, Kenzo alieleza kusikitishwa kwake na taarifa kuwa Diamond alilipwa shilingi milioni 750 za Uganda kwa kushiriki katika tamasha hilo, kiasi anachokiona kuwa ni kikubwa mno, hasa ikizingatiwa kuwa wasanii wa Uganda wamekuwa wakipuuzwa kwenye matukio ya kitaifa. Katika hatua nyingine, alikosoa maisha ya kifahari aliyotengewa msanii huyo kutoka Tanzania huku wasanii wa Uganda wakiachwa bila msaada au kutambuliwa.  Kenzo amesisitiza kuwa hawezi kuiga chochote kutoka kwa Diamond Platnumz licha ya shinikizo zinazotolewa na Waganda kuwa wasanii wao wanapaswa kuboresha chapa zao na muonekano wao wa kisanii ili kuendana na nyakati zilizopo. “Mimi siwezi kuiga chochote kutoka kwa Diamond Platnumz. Hayo mambo wanayosema kuhusu chapa na kila kitu, siwezi kuwa hivyo. Siwezi kuanza kuvaa minyororo ya dhahabu ishirini, malezi yangu hayakuniandaa kwa hilo. Siwezi kuishi maisha ya kifahari wakati watoto wa Ghetto wanateseka. Bora nitumie pesa hizo kuboresha maisha yao,” alisema Kenzo katika mahojiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Uganda. Diamond Platnumz na Eddy Kenzo wanachukuliwa kuwa miongoni mwa wasanii wakubwa zaidi wa Afrika Mashariki kimataifa. Hata hivyo, Kenzo anaonekana kuwa mbele katika upande wa tuzo za kimataifa alizoshinda, ikiwemo uteuzi wake wa kihistoria katika Tuzo za Grammy.

Read More
 Malipo ya Diamond Yatikisa Uganda, Wasanii Aibua Mjadala Moto

Malipo ya Diamond Yatikisa Uganda, Wasanii Aibua Mjadala Moto

Msanii mashuhuri wa Uganda, Allan Toniks, amezua gumzo mitandaoni baada ya kulalamikia hadharani kiwango kidogo cha malipo alichopewa kwa kushiriki tamasha moja nchini humo. Kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), Toniks alifunguka kwa hasira kwamba alipewa chini ya dola 1,000, huku akishangaa serikali ya Uganda kutumia shilingi milioni 750 kumlipa staa wa Tanzania, Diamond Platnumz, kwa kushiriki kampeni ya kuhamasisha kahawa. “Na wanakuja kunipa chini ya dola 1000, nikikataa wanasema najifanya. 750M UGX? Acheni ujinga.” Aliandika kwa hasira. Kauli ya Toniks ilisambaa kwa kasi, ikizua mjadala mkubwa. Baadhi ya watu walimtetea, wakisema ni wazi kuwa wasanii wa ndani wanadharauliwa na kutopewa thamani stahiki licha ya mchango wao katika kukuza utamaduni wa nchi. Wengine walidai kuwa fedha hizo zingeweza kusaidia miradi ya kijamii au kuimarisha sanaa ya ndani, wakikumbusha kuwa wakazi wa Kiteezi wanahitaji milioni 200 pekee kuboresha maisha yao. Hata hivyo, wapo waliotetea hatua ya kumleta Diamond, wakisema ni msanii mwenye ushawishi mkubwa barani Afrika na kwamba uwepo wake unaleta mvuto wa kimataifa kwa kampeni ya kahawa. Kwao, hii ni mbinu ya kibiashara na kimkakati ambayo inaweza kusaidia sekta ya kilimo kuvuka mipaka. Tukio hili limeibua maswali kuhusu vipaumbele vya serikali ya Uganda, thamani ya sanaa ya ndani, na nafasi ya wasanii katika miradi ya kitaifa. Pia limeibua changamoto kwa wasanii wa Uganda kuwekeza zaidi katika kuboresha nembo zao binafsi ili kujiongezea heshima na nafasi kwenye majukwaa ya kitaifa na kimataifa.

Read More
 Lava Lava Aondoka Rasmi WCB Wasafi, Aanza Safari Mpya ya Muziki

Lava Lava Aondoka Rasmi WCB Wasafi, Aanza Safari Mpya ya Muziki

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Lava Lava, ameashiria rasmi kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya muziki kwa kuondoa machapisho yote kwenye ukurasa wake wa Instagram, hatua ambayo imewasha moto wa mijadala mitandaoni kuhusu hatima yake ya kisanii. Hatua hii imejiri saa chache tu baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa WCB Wasafi, Diamond Platnumz, kuthibitisha mbele ya waandishi wa habari kuwa Lava Lava ameondoka kwenye lebo hiyo rasmi bila kulazimika kulipa ada yoyote ya kuvunja mkataba. Zaidi ya hapo, Diamond alieleza kuwa wamempa Lava Lava kiasi cha pesa kama msaada ili kumuwezesha kuanzisha maisha ya kujitegemea katika tasnia ya muziki. “Tumeachana kwa amani, hakuna malipo yoyote aliyotakiwa kutoa, na kama familia, tumempa sapoti ya kifedha kuanza safari yake mpya,” alisema Diamond. Lava Lava, ambaye amekuwa chini ya lebo ya WCB kwa miaka kadhaa, amejijengea jina kwa nyimbo kadhaa zilizotamba kama Tuachane, Gundu, na Saula. Hatua ya kuondoka Wasafi inatafsiriwa na wengi kama ishara ya kutafuta uhuru zaidi wa kisanii na kusukuma mbele ndoto zake kwa mtazamo mpya. Mashabiki wake wameonyesha hisia mseto, wengine wakimsifu kwa ujasiri wa kuanza upya, huku wengine wakisubiri kwa hamu kuona mwelekeo mpya wa kazi yake ya muziki. Wakati huo huo, sekta ya burudani inasubiri kuona ikiwa Lava Lava ataibuka na label yake binafsi au ataungana na mtandao mwingine wa kimuziki. Kwa sasa, yote macho kwa Lava Lava, msanii anayechukua hatua ya mabadiliko kwa matumaini, heshima, na dira mpya.

Read More
 Hanstone Aibua Madai Mazito Dhidi ya WCB Wasafi

Hanstone Aibua Madai Mazito Dhidi ya WCB Wasafi

Msanii wa Bongo Fleva, Hanstone, amevunja ukimya kuhusu maisha yake ndani ya lebo ya WCB Wasafi, akieleza hadharani changamoto alizokumbana nazo kipindi alichokuwa akihudumu humo. Akizungumza juzi kwenye mahojiano, Hanstone alidai kuwa alikaa ndani ya WCB kwa kipindi cha miaka mitatu bila kutambulishwa rasmi kama msanii wa lebo hiyo. Katika kipindi hicho, alieleza kuwa alihusika katika kuandika nyimbo kwa wasanii wengine, wakiwemo majina makubwa kama Diamond Platnumz, lakini hakuwahi kulipwa chochote kwa kazi hiyo.  “Nilitumika kuandika nyimbo kwa wasanii waliokuwa juu, lakini sikuwahi kupewa nafasi yangu wala stahiki zangu. Niliamini kwenye mchakato, lakini haikuwa kama nilivyotarajia,” alisema Hanstone kwa hisia. Kwa muda mrefu, mashabiki na wadau wa muziki wamekuwa wakimtaja Hanstone kama msanii asiye na subira, sifa ambayo imeonekana kuwa chanzo cha yeye kutopata nafasi ya kung’aa akiwa chini ya lebo hiyo ya WCB. Hata hivyo, msanii huyo amekana madai hayo, akisema alijitahidi kuwa mvumilivu, lakini hakupata fursa aliyostahili. Kauli ya Hanstone imezua mjadala mkubwa mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakionesha huruma na kumuunga mkono, wakati wengine wakihimiza wasanii chipukizi kuwa na uvumilivu zaidi wanapojiunga na lebo kubwa kama WCB. Kwa sasa, bado haijajulikana ikiwa Hanstone atachukua hatua za kisheria au ataendelea na muziki kama msanii huru nje ya lebo hiyo. Mashabiki wanasubiri kwa hamu kuona hatua yake inayofuata.

Read More
 DIAMOND PLATINUMZ MBIONI KUAACHIA KOLABO NA DAVIDO

DIAMOND PLATINUMZ MBIONI KUAACHIA KOLABO NA DAVIDO

Kolabo mpya ya nyota wa muziki barani Afrika yaani Davido na diamondplatnumz inanukia, hii ni baada ya mtayarishaji lizer classic wa lebo ya WCB ambaye ni mtayarishaji wa kazi nyingi za Diamond kuonyesha sehemu ya project hiyo. Lizer anathibisha kwamba kazi mpya kutoka kwa wawili hao ipo na itakuja. Ame-share kupitia insta story yake akionekana akiiandaa kazi hiyo. Diamond na davido ambao hawana dogo kwenye kazi zao, ni wakali wa hitsong “My Number One Remix” iliyotoka zaidi ya miaka 8 iliyopita ikiwa ndio kolabo yao ya kwanza.

Read More
 AKAUNTI YA DIAMOND PLATNUMZ YAFUTWA YOUTUBE

AKAUNTI YA DIAMOND PLATNUMZ YAFUTWA YOUTUBE

Akaunti ya YouTube ya mwanamuziki wa Bongofleva Diamond Platnumz imefutwa na wamiliki wa YouTube kwa kile kinachoelezwa kwamba imekiuka miongozo ya mtandao huo. Ukiingia kwenye Akaunti hiyo kwa sasa, kuna ujumbe unasema ‘akaunti hii imefutwa kwa kukiuka Miongozo ya Jumuiya ya YouTube’ YouTube ya Diamond imefutwa ikiwa na zaidi ya Subscribers milioni 6.5 na jumla ya watazamaji Bilioni 1.5. Ilikuwa na zaidi ya video 700. Mpaka sasa haijafahamika sababu za YouTube kufuta akaunti hiyo ya YouTube ya Diamond Platnumz. Wikiendi iliyopita akaunti ya Youtube ya Diamond Platnumz ilidukuliwa na kupandishwa maudhui ya kampuni ya magari TESLA inayomilikiwa na tajiri Elon Musk ambaye pia aliingia LIVE kwenye channel hiyo.

Read More
 DIAMOND AFUNGUKA CHANZO CHA KUTOSHIRIKI TUZO ZA TANZANIA MUSIC AWARDS

DIAMOND AFUNGUKA CHANZO CHA KUTOSHIRIKI TUZO ZA TANZANIA MUSIC AWARDS

Staa wa Muziki wa Bongofleva Diamond Platnumz amefunguka sababu zilizomfanya asishiriki Tuzo za Muziki Tanzania (TMA) zilizomalika majuzi. Akizungumza na BBC Swahili jijini London, Uingereza, anasema kuwa kikubwa kilichomfanya asishiriki Tuzo hizo ni imani maana mara ya kwanza alinyimwa Tuzo wakati alistahili kupata na yeye ndo sababu ya Tuzo Kusitishwa kwa zaidi ya Miaka 9. Mbali na hayo, amekunusha madai kuwa mama yake mzazi, Bi. Sandra maarufu kama Mama Dangote ndiye amekuwa akimpangia mwanamke wa kumuoa.  Diamond amesema kwa sasa yeye ni mtu mzima hawezi kupangiwa na wanaozusha hilo wanamkosea sana mama yake. “Hapana kwanza wanamkosea sana mama yangu, hawezi kunipangia kwa umri wangu niliofika kweli nitapangiwa na mzazi?, hayo maisha yameshaishia zamani sana kwa kupangiwa na mzazi umuoe nani, usimuoe nani, mama yangu hawezi kunipangia,” amesema Diamond. Hata hivyo  amefunguka matamanio yake ya kuukimbia ubachela na kuingia kwenye maisha ya ndoa kwa kusema, “Kila binadamu anataka kuoa, nitaoa, natamani kuoa, naelekea kuoa, hiyo ni kauli sahihi zaidi, Bibi harusi watu watamuona. Natamani nitulie. Ubaya wa Watanzania wanataka kumpangia mtu muda wake, pengine bado sijajitosheleza kimaisha,”

Read More
 DIAMOND PLATNUMZ ATILIA SHAKA VIONGOZI WA SANAA TANZANIA

DIAMOND PLATNUMZ ATILIA SHAKA VIONGOZI WA SANAA TANZANIA

Hitmaker wa ngoma ya “Gidi” msanii Diamond Platnumz ameonesha kutoridhika na viongozi wa serikali waliopewa mamlaka ya kusimamia sanaa nchini Tanzania. Kupitia Instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Diamond ameandika ujumbe unaosomeka ” Serikali ina nia njema sana ya kukuza sanaa ila inatakiwa kuwa makini sana na watu wanaowateua kusimamia nyanja mbalimbali katika tasnia zetu. Maana watu hao wanachokifanya ni kuidhalilisha Taifa na kufanya Taifa letu lionekane halina weledi” Pamoja na kuandika hayo Diamond Platnumz hajaweka wazi ni viongozi gani ambao amewalenga katika ujumbe wake huo ila walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda msanii huyo hajafurahishwa na uamuzi wa Shirikisho la Muziki nchini Tanzania kumteua mchekeshaji Steve Nyerere kuwa msemaji wa Shirikisho hilo.

Read More
 DIAMOND PLATINUMZ KUONEKANA NETFLIX IJUMAA HII KUPITIA YOUNG, FAMOUS & AFRICAN REALITY SHOW

DIAMOND PLATINUMZ KUONEKANA NETFLIX IJUMAA HII KUPITIA YOUNG, FAMOUS & AFRICAN REALITY SHOW

Wakati ambao EP mpya ya msanii Diamond Platnumz “First of All”  ikiendelea kufanya vizuri kwenye digital Platforms mbalimbali, Habari njema kwa mashabiki wa nyota huyo ni kwamba, Ijumaa hii anatarajia kuonekana ndani ya jukwaa la Netflix kupitia reality show ya “Young, Famous and African” ambayo inaanza rasmi Machi 18. Diamond alipata shavu la kuwa moja ya wahusika katika show hiyo yenye matukio halisi na anakuwa Mtanzania mwingine kuonekana Netflix baada ya Idris Sultan ambaye Machi 26, 2021 alionekana kwenye mtandao huo kupitia filamu ‘Slay’ iliyokutanisha Mastaa wa Afrika kama Ramsey Nouah, Fabian Adeoye Lojede, Simphiwe Ngema, na Amanda Du-Pont. Filamu nyingine ambazo zinatarajiwa kuanza kuonyeshwa wiki hii ni pamoja na Human Resources, Top boy season 2, Rescued by Ruby,Windfall pamoja na Heist:The great robbery of Brazil Central Bank.

Read More