Diana Marua Akanusha Madai ya Kufanyiwa Surgery Baada ya Kuonekana Kupungua Uzito
Staa wa mitandao ya kijamii nchini Kenya, Diana Bahati, amekanusha vikali madai yanayoenea mtandaoni kuwa amefanyiwa upasuaji baada ya kuonekana kupungua uzito. Kupitia InstaStory, Diana ameweka wazi kuwa hajafanya upasuaji wowote wa kubadili muonekano wake, akiisitiza kuwa madai hayo hayana ukweli wowote na ni uvumi tu wa mitandaoni. Mbali na hilo, Diana B pia amepuzilia mbali tetesi za kuwa mjamzito, akionekana kukata mzizi wa fitina mapema kabla uvumi huo haujashika kasi zaidi. Kauli yake imejiri siku moja tu baada ya kurejea mitandaoni kufuatia ukimya wa takriban mwezi mmoja, hali iliyochochea mashabiki kuanza kubuni nadharia mbalimbali kuhusu mabadiliko ya mwili wake. Baadhi walidai huenda alipitia upasuaji wa kupunguza uzito huku wengine wakihusisha kupungua kwake na ujauzito.
Read More