Geofrey Lutaaya Ataka Ambulance Aliyotoa Kwa Wananchi Irejeshwe Baada ya Kushindwa Ubunge

Geofrey Lutaaya Ataka Ambulance Aliyotoa Kwa Wananchi Irejeshwe Baada ya Kushindwa Ubunge

Mwanamuziki aliyegeukia siasa nchini Uganda Geofrey Lutaaya ameripotiwa kutaka ambulance aliyoinunua kwa wananchi wakati wa kampeni irejeshwe, kufuatia kushindwa kwake kwenye uchaguzi wa ubunge uliomalizika hivi karibuni. Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu, Lutaaya ametoa makataa ya mwezi mmoja akitaka ambulance hiyo irudishwe kwake. Inadaiwa kuwa msanii huyo amechukizwa na matokeo ya uchaguzi baada ya kupoteza kiti cha ubunge, hali iliyomfanya abadili msimamo wake kuhusu msaada huo alioutoa kwa wananchi. Wakati wa kampeni, Lutaaya alinunua ambulance ambayo aliikabidhi kwa jamii kama sehemu ya mchango wake katika kuboresha huduma za afya, hatua iliyopokelewa kwa furaha kubwa na wakazi wa eneo la Kakuuto. Hata hivyo, hatua ya sasa ya kutaka irejeshwe imeibua maswali na hasira miongoni mwa wananchi, wengi wakisema msaada huo ulikuwa kwa manufaa ya umma na haukupaswa kuwa wa masharti ya kisiasa.

Read More
 Geoffrey Lutaaya Ashindwa Kiti cha Ubunge Kakuuto Kupitia NUP

Geoffrey Lutaaya Ashindwa Kiti cha Ubunge Kakuuto Kupitia NUP

Mgombea wa chama cha National Unity Platform (NUP), Geoffrey Lutaaya, ameshindwa katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Kaunti ya Kakuuto wilayani Kyotera, baada ya kupoteza dhidi ya mgombea wa chama tawala cha NRM, Ismail Lubega. Lutaaya, ambaye alikuwa anawania kutetea kiti hicho, aliingia bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2021 baada ya kuchaguliwa kuiwakilisha NUP katika Bunge la 11 la Uganda. Hata hivyo, safari yake ya kisiasa imepata pigo kufuatia matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika juzi, ambapo Lubega wa NRM ameibuka mshindi. Geoffrey Lutaaya anafahamika sana katika tasnia ya muziki nchini Uganda. Alipata umaarufu mkubwa mwishoni mwa miaka ya 1990 akiwa mmoja wa wanachama waanzilishi wa bendi maarufu Eagles Production, iliyotoa wasanii wakubwa na nyimbo zilizotikisa Afrika Mashariki.

Read More
 Lutaaya Akanusha Kutelekeza Binti, Atoa Ushahidi wa Malipo ya Ada

Lutaaya Akanusha Kutelekeza Binti, Atoa Ushahidi wa Malipo ya Ada

Mbunge na mwanamuziki wa Uganda, Geoffrey Lutaaya, ameibuka na kujitetea vikali baada ya video ya msichana mwenye umri wa miaka 17, anayejulikana kama Nambatya, kusambaa mtandaoni ikimshutumu kwa kutelekeza majukumu ya kifamilia. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Lutaaya amekanusha madai hayo akionyesha stakabadhi anazodai ni ushahidi wa malipo ya ada kamili kwa ajili ya masomo ya Nambatya katika shule ya bweni ya Stella Maris Nsuube. Amefafanua kuwa mama wa msichana huyo ndiye aliyemtoa shuleni hapo na kumhamishia katika shule nyingine ya hadhi ya chini, Boston High School. Lutaaya pia amefichua kuwa wakati wa janga la COVID-19, alilazimika kulipa mama ya Nambatya kiasi cha Shilingi Milioni 6 za Uganda (UGX) ili kuepuka fedheha ya umma, hasa baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge. Ameongeza kuwa kwa sasa yuko tayari kumchukua binti huyo kuishi naye na familia yake na kumgharamia masomo nje ya nchi, akiamini kuwa hilo litampa mustakabali bora. Hata hivyo, video ya Nambatya ikieleza kuwa amekosa msaada wa kifedha na kutelekezwa na baba yake ilizua hasira kubwa mitandaoni. Wakosoaji walitilia shaka uadilifu wa Lutaaya kama kiongozi wa kisiasa, huku baadhi wakielekeza lawama kwa mke wake, Irene Namatovu, wakimtuhumu kwa kutokuwa na huruma kwa msichana huyo.

Read More