Luciano Ataka Rais William Ruto Kuhalalisha Bangi Kenya

Luciano Ataka Rais William Ruto Kuhalalisha Bangi Kenya

Msanii nyota wa reggae kutoka Jamaica, Luciano, ameibua mjadala mzito mtandaoni baada ya kumtaka Rais William Ruto kuzingatia hatua ya kuifanya Kenya kuwa miongoni mwa nchi za kwanza barani Afrika kuhalalisha bangi. Akizungumza na Radio Citizen, Luciano amesifu ushawishi mkubwa wa kitamaduni wa Kenya barani Afrika na duniani, akisema kuwa uhalalishaji wa bangi unaweza kufungua milango mipya ya kiuchumi na kitabibu. Kwa mujibu wa msanii huyo, nchi zilizoidhinisha matumizi ya bangi kwa udhibiti maalum zimefaidika kupitia ongezeko la mapato ya serikali, kupanuka kwa sekta ya kilimo, na maendeleo katika tafiti za tiba mbadala. Hata hivyo, msanii huyo ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya kwa ziara yake ya muziki, amesisitiza kuwa uamuzi kuhalalisha bangi unaweza kuibadilisha Kenya kiuchumi na kuiweka katika ramani ya kimataifa kama taifa linaloongoza katika mageuzi ya kisera.

Read More
 Luciano Aomboleza Kifo cha Raila Odinga

Luciano Aomboleza Kifo cha Raila Odinga

Msanii nguli wa muziki wa reggae kutoka Jamaica, Luciano, amejiunga na mamilioni ya watu duniani wanaoomboleza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Amolo Odinga. Kupitia ujumbe wake Instagram, Luciano ameeleza masikitiko yake kwa kumpoteza Raila aliyekuwa na nafasi kubwa katika historia ya Kenya na bara la Afrika. Ametoa pole zake kwa familia ya Odinga na wananchi wote wa Kenya, akiwataka wabaki imara na kuendelea kuwa na imani katika kipindi hiki kigumu. Luciano, anayefahamika kwa nyimbo zenye ujumbe wa amani na matumaini kama It’s Me Again Jah na Sweep Over My Soul, ameahidi kuzuru Kenya hivi karibuni kwa onyesho maalum la faraja, ili kuwatia moyo Wakenya kupitia muziki wake. Hata hivyo msanii huyo amehitimisha salamu zake kwa kuimba wimbo wa kumuomboleza Raila Odinga, akimtaja kama kiongozi shujaa, mwenye maono na aliyejitoa kwa ajili ya watu wake. Taarifa yake imepokelewa kwa hisia miongoni mwa mashabiki wa reggae na wafuasi wa Raila Odinga, wengi wakimsifu Luciano kwa kuonyesha upendo na mshikamano na wananchi wa Kenya katika kipindi hiki cha majonzi.

Read More