Wasanii na wanahabari waomboleza kifo cha Raila Odinga

Wasanii na wanahabari waomboleza kifo cha Raila Odinga

Sekta ya burudani na vyombo vya habari nchini Kenya zimeingia katika majonzi makubwa kufuatia taarifa za kifo cha kiongozi wa upinzani na mwanasiasa mkongwe, Raila Amolo Odinga, ambaye amefariki dunia nchini India kutokana na mshtuko wa moyo. Kifo chake kimezua simanzi kote nchini humo, huku wadau wa sekta ya burudani na habari wakijitokeza kutoa rambirambi zao kupitia mitandao ya kijamii. Wasanii na wanahabari wameelezea Raila kama kiongozi wa kipekee aliyekuwa na uhusiano wa karibu na vijana, wakiwemo wabunifu na waandishi wa habari. Wengi wamesema Raila alikuwa na uelewa mpana wa umuhimu wa sanaa na vyombo vya habari katika kukuza taifa, na mara nyingi alionekana kuhudhuria hafla za burudani, mikutano ya kijamii na matamasha ya vijana. Baadhi ya watangazaji na wanahabari wamesema Raila alikuwa nguzo muhimu katika kuhimiza uhuru wa kujieleza na uhuru wa vyombo vya habari, akiamini kwamba taifa lenye demokrasia thabiti lazima liruhusu sauti tofauti kusikika. Wameeleza kuwa kifo chake kimeacha pengo lisilo na mfano katika historia ya kisiasa na kijamii nchini Kenya. Mitandao ya kijamii imefurika jumbe za huzuni na kumbukumbu za maisha ya Raila, huku maelfu ya wananchi, wasanii, waandishi wa habari na viongozi wakitumia alama za reli kama #RIPRailaOdinga, #RestInPeaceBaba, na #ThankYouBaba kueleza hisia zao. Wengine wamechapisha picha na video za matukio ya zamani zikionyesha Raila akishirikiana na vijana na kushiriki matukio ya kijamii.

Read More
 Raila Odinga afariki dunia nchini India

Raila Odinga afariki dunia nchini India

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Amolo Odinga, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80 nchini India, vyombo vya habari vya kimataifa vimeripoti. Kwa mujibu wa taarifa, Raila aliaga dunia kutokana na mshtuko wa moyo (cardiac arrest) alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Kochi, nchini India. Vyanzo vya karibu na familia vinaeleza kuwa Odinga alikuwa amesafiri India wiki moja iliyopita kwa uchunguzi wa kiafya na matibabu ya ufuatiliaji. Madaktari walijaribu kumhudumia kwa muda mrefu, lakini jitihada zao hazikuzaa matunda. Odinga, ambaye amekuwa mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi mkubwa katika historia ya Kenya, alihudumu kama Waziri Mkuu kuanzia mwaka 2008 hadi 2013 katika serikali ya mseto iliyoongozwa na Rais mstaafu Mwai Kibaki. Aidha, aliwahi kuwa Mbunge wa Lang’ata, Waziri wa Nishati, na baadaye Waziri wa Barabara kabla ya kuunda chama cha ODM kilichompa umaarufu mkubwa. Raila pia alikuwa kiongozi wa upinzani kwa miongo kadhaa, akigombea urais mara kadhaa bila kufanikiwa, huku akiendelea kuwa sauti kuu ya mageuzi ya kisiasa na utetezi wa demokrasia nchini Kenya. Kifo chake kimetokea wakati ambapo alikuwa akijihusisha na shughuli mbalimbali za kisiasa na maandalizi ya mageuzi ya Afrika kupitia Umoja wa Afrika (AU). Wakenya wengi wameelezea huzuni na mshtuko mkubwa kufuatia taarifa hizo, huku mitandao ya kijamii ikifurika jumbe za rambirambi, baadhi wakimtaja kama “Baba wa taifa la pili” kwa mchango wake mkubwa katika harakati za kidemokrasia na kupinga ukandamizaji wa haki za wananchi.

Read More
 Ben Githae akerwa na wanaomkejeli baada ya mrengo wa Azimio la Umoja kupoteza uchaguzi

Ben Githae akerwa na wanaomkejeli baada ya mrengo wa Azimio la Umoja kupoteza uchaguzi

Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Ben Githae ameonekana kuchukizwa na kitendo cha mashabiki kuendelea kumkejeli hata baada ya mrengo wa azimio la umoja kupoteza uchaguzi mkuu uliokamilika. Akizungumza kwenye hafla ya kuchangisha pesa huko Mlima Kenya, Githae amekiri kuumizwa sana na kauli ya watu wanaokumbusha kila mara namna mrengo aliokuwa anaunga mkono wa Azimio la umoja ulivyopoteza uchaguzi wa Agosti 9 huku akiwataka marafiki zake kumkubali kama mmoja wao badala ya kumsema vibaya kwa misingi ya kisiasa. Hitmaker huyo wa “Mabataro” amesema kwa sasa ameshakubali matukio kuwa muungano wa Azimio la umoja ulipoteza uchaguzi huku akisisitiza kuwa hana budi kukumbatia serikali ya Kenya Kwanza inayoongozwa na Rais William Ruto. Miezi mitano iliyopita Ben Githae alikuwa gumzo nchini baada ya kuachia wimbo wa kisiasa uitwao “Kenya Is Safe”, wimbo ambao alikuwa anamsifia Raila Odinga kwa hatua ya kumchagua Martha Karua kama mgombea mwenza wa Azimio kwenye uchaguzi wa Agosti 9 ambapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa Kenya ipo salama mikononi mwa Odinga na Karua.

Read More
 MAWAKILI WA RAILA ODINGA NA SAUTI SOL WAKUTANA.

MAWAKILI WA RAILA ODINGA NA SAUTI SOL WAKUTANA.

Mawakili wa Kinara wa ODM Raila Odinga na wale wa kundi la muziki la Sauti Sol wamekutana kwa ajili ya mazungumzo ili kutatua mgogoro wa hakimiliki ulioibuka mapema wiki hii baada ya wimbo wa Sauti Sol “Extravaganza” kupigwa kwenye mkutano wa Azimio. Wakili wa kundi la Sauti Sol, Moriasi Omambia ndiye amethibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter. “Ningependa kuthibitisha kwamba kundi linaloongoza kampeni za Raila Odinga na mawakili wao wanashirikiana nasi katika juhudi za kutatua mzozo uliopo kuhusu hakimiliki. Tunatambua kujitolea kwao katika kutafuta kusuluhisha jambo hili haraka iwezekanavyo.”  imesomeka tweet hiyo ya Omambia. Utakumbuka Chama cha ODM cha Raila Odinga kilitoa taarifa hapo awali kikisema kwamba walitumia muziki wa Sauti Sol kwa sababu wanapenda kazi za kundi hilo.

Read More