Tanasha Donna Atoa Tahadhari kwa Wanaomsema Vibaya Naseeb Junior
Msanii Tanasha Donna ameonyesha msimamo mkali na upendo wake kwa mwanawe, Naseeb Junior, baada ya kutuma ujumbe mzito unaoashiria kuwa yuko tayari kumlinda kwa gharama yoyote. Kupitia Instastory yake, Tanasha ameeleza kuwa hawezi kuvumilia mtu yeyote atakayemtaja vibaya au kumdhuru mtoto wake, akisisitiza kuwa yeyote atakayemgusa kwa njia yoyote atakuwa amejipatia adui wa maisha. Mrembo huyo, amesema upendo wake kwa Naseeb Junior ni wa dhati na wa kudumu, na kwamba atahakikisha anakuwa salama dhidi ya mashambulizi ya maneno au vitendo vinavyoweza kumuathiri. Tanasha amekuwa miongoni mwa wasanii wanaoweka wazi mapenzi yao kwa watoto wao, na mara nyingi huzungumzia jinsi uhusiano na mwanawe umembadilisha na kumpa nguvu mpya maishani.
Read More