WILLY PAUL AWAJIA JUU WALIOTAKA KIMSHUSHA KIMUZIKI

WILLY PAUL AWAJIA JUU WALIOTAKA KIMSHUSHA KIMUZIKI

Staa wa muziki nchini Willy Paul amerusha jiwe gizani kwa madalali waliotaka kumshusha kimuziki miaka ya hapo nyuma. Kupitia instagram yake Pozze amejitapa kuwa huu ndio muda wake wa kuwaaminisha wote waliomdharau kipindi hicho kuwa ana uwezo wa kuupeleka muziki wake kimataifa bila usaidizi wa mtu yeyote. Haikuishia hapo Hitmaker huyo wa “Toto” ameenda mbali zaidi na kutusanua kuwa kuna kipindi walimkatisha tamaa kuwa hatoweza kufanya project yeyote na ikafanikiwa kwa sababu hakuwa na mawazo ya kugeuza muziki wake kuwa biashara. “Walisema hatujiwezi, walisema hatuna akili ya bizz…lakini tables just turned.. watalilia kwa choo gui!!”, Aliandika kwa machungu. Utakumbuka kabla ya Willy Paul kugeukia muziki wa kidunia miaka kadhaa iliyopita, alikumbwa na kashfa nyingi kwenye kiwanda cha muziki wa injili nchini Kenya, kashfa alizozitaja kuwa zilitengenezwa na baadhi ya wadau wa muziki waliotaka kumshusha kimuziki.

Read More
 WILLY PAUL ACHUKIZWA NA WASANII WA KENYA KUMKIMBIA KWENYE BIRTHDAY

WILLY PAUL ACHUKIZWA NA WASANII WA KENYA KUMKIMBIA KWENYE BIRTHDAY

Hitmaker wa “Tamu Walahi”, Msanii Willy Paul amesikitishwa na hatua ya wasanii wenzake kutomuonyesha upendo wakati wa kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwake juzi kati. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Willy Paul ameposti video akiwa na mashabiki zake ambapo amesema alitarajia wasanii wenzake wamtakia heri ya siku ya kuzaliwa lakini cha kushangaza hakuna hata mmoja ambaye alisimama naye kwenye siku yake hiyo muhimu. Hata hivyo amewashukuru mashabiki pamoja na baby mama wake kwa upendo ambao walimuonyesha kwenye birthday yake huku akisema amefarajika sana na salamu zao za heri. “This are my fans!! They surprised me today, I must say I’m very humbled by this action…. I expected some people that i share alot with to atleast wish me a happy birthday… but non of them did… I’m glad my daughters mother wished me a happy one!! Love you all and thank you for making my sad birthday a happy one… bless you!.” Ameandika kwa uchungu. Willy Paul ambaye alitimiza umri wa miaka 29 Septemba 2 mwaka huu, kwa sasa yupo mbioni kuwabariki mashabiki zake na album yake ya tatu iitwayo Not Thing But Love ambayo kwa mujibu wake huenda ikaingia sokoni mwakani.

Read More
 WILLY PAUL AWATAKA WASANII KUCHUKULIA HATUA KAMPUNI ZINAZOSUSIA KULIPA PESA ZAO

WILLY PAUL AWATAKA WASANII KUCHUKULIA HATUA KAMPUNI ZINAZOSUSIA KULIPA PESA ZAO

Msanii nyota nchini Willy Paul ametoa changamoto kwa wasanii wenzake kuzichukulia hatua kali za kisheria kampuni au mapromota wanaokataa au kuchelesha malipo yao wanapotumbuiza kwenye shoo zao. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa Instagram Willy Paul amesema wasanii waache suala la kuwahurumia wateja wao wanapochelesha pesa zao kwani ndiyo njia pekee watapewa heshima kwenye shughuli zao za kimuziki. Hitmaker huyo wa “Toto” amesema wasanii wanapodai haki yao mara nyingi makampuni au mapromota huwa wanaingiwa na jeuri kiasi cha kutochukua simu zao kitendo ambacho amedai sio cha kingwana. Hata hivyo hajabainika ni kitu gani kilichopelekea Willy Paul kutoa madai hayo ingawa walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji huenda kuna mtu amekataa kumlipa msanii huyo pesa zake na ndio maana ameamua kutumia mitandao ya kijamii kutoa ya moyoni kuhusu mapromota au makampuni kuchelesha malipo ya wasanii.

Read More
 WALIMWENGU MTANDAONI WAMSHAMBULIA WILLY PAUL KISA KIKI

WALIMWENGU MTANDAONI WAMSHAMBULIA WILLY PAUL KISA KIKI

Walimwengu mtandaoni wamewatolea uvivu staa wa muziki nchini Willy Paul baada msanii huyo kudai kuna binti wa mwigizaji wa kipindi cha Vioja Mahakama amemuibia simu aina iPhone nyumbani kwake. Kupitia comments walizoziachia katika post ya Willy Paul kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram wamemtaka msanii huyo aache suala la kuendekeza kiki kwenye muziki wake na badala yake atoe muziki mzuri ambao utajiuza wenyewe. Aidha wameenda mbali zaidi na kusema kwamba hitmaker huyo wa ngoma ya “Toto” amekosa ubunifu kwenye masuala ya kutengeneza matukio yatakayomfanya azungumziwe mtandaoni kwani kiki aliyoitengeneza haina mashiko ya kuteka hisia za watu. Kauli hiyo ya walimwengu imekuja mara baada ya Willy Paul kumpa binti anayedai kuwa ni wa mwigizaji wa Vioja Mahakama makataa ya siku moja kurejesha simu yake la sivyo atamuaibisha vibaya baba yake mzazi.

Read More
 WILLY PAUL AMTAKA BAHATI AACHE SIASA

WILLY PAUL AMTAKA BAHATI AACHE SIASA

Msanii nyota nchini Willy Paul inaonekana hajafurahishwa namna ambavyo msanii mwenzake Bahati anavyohangaishwa kwenye azma yake ya kuwa mbunge Mathare. Hii ni baada ya Bahati kurushiana maneno makali na Katibu Mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna kwenye mtandao wa Twitter baada ya muungano wa Azimio la Umoja kumtangaza Anthony Olouch kuwa mgombea wao kwenye kinyanganyiro cha ubunge Mathare. Kupitia mtandao wa twitter Willy Paul amenshauri Bahati  aachane kabisa na masuala ya siasa na badala yake arudi kwenye uimbaji waendelezee harakati zao za kuupeleka muziki wa kenya kimataifa. Kauli hiyo ya Willy Paul imeshabikiwa na watumiaji wa mitandao ya kijamii wengi wakionekana kumtaka Bahati ajiondoe kwenye siasa kwa sababu hatawezana nayo kwa kuwa ni jambo linalohitaji ujasiri mkubwa. Haya yanajiri wakati huu Bahati ameingia kwenye ugomvi na muungano wa Azimio la Umoja baada ya muungano kumtaka ajiuzulu kwenye azma yake ya kuwa Mbunge mathare kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 na badala yake aungu mkono azma ya mbunge wa sasa Mathare Anthony Oluoch ambaye anatetea kiti chake kwa mara ya pili.

Read More
 WILLY PAUL AISUTA VIKALI SAFARICOM KISA MAPATO YA SKIZA TUNE

WILLY PAUL AISUTA VIKALI SAFARICOM KISA MAPATO YA SKIZA TUNE

Staa wa muziki nchini Willy Paul ameonesha kusikitishwa na kampuni ya safaricom kutoongeza mapato ya wasanii kupitia Skiza tune. Kupitia instastory yake kwenye mtandao wa instagram willy paul ameisuta vikali kampuni ya safaricom akitaka maelezo kamili kuhusu kupunguzwa kwa mapato ya wasanii kupitia skiza tune. Himaker huyo wa ngoma ya toto amesema alitarajia mapato ya skiza tune ya wasanii itaongezeka baada ya rais Kenyatta kutia saini msaada wa hakimiliki kuwa sheria, mswaada ambao ungetoa fursa kwa wasanii kufaidi na mapato ya kazi zao. Utakumbukwa sheria mpya ya hakimiliki ilipendekeza wasanii kupata asilimia 52 ya mapato yao kupitia kazi zao huku huku mtoa huduma wa mawasiliano akiambulia asilimia 43  ya mapato.

Read More
 WILLY PAUL APEWA SOMO NA MASHABIKI KISA KIKI

WILLY PAUL APEWA SOMO NA MASHABIKI KISA KIKI

Baadhi ya wadau wa muziki nchini wamewatolea uvivu msanii Willy Paul baada ya mkali huyo kuonekana kutengeneza matukio kwa ajili ya kutangaza kazi yake mpya ambayo itaingia sokoni hivi karibuni. Kupitia mitandao yao ya kijamii wamwataka Willy Paul waache suala la kuendekeza kiki kwenye muziki wao na badala yake atoe muziki mzuri ambao utajiuza wenyewe. Aidha wametoa changamoto kwa Bosi huyo Saldido kuwa mbunifu kwenye ishu ya kutengeneza matukio yatakayomfanya azungumziwe mtandaoni kwani kiki anazozitengeneza hazijafikia viwango vya kuteka hisia za watu. Kauli hiyo ya wadau hao wa muziki imekuja mara baada ya Willy Paul kurekodi video akidai kuwa kuna baadhi ya wasanii wanahujumu juhudi zake za kuupeleka muziki wake kimataifa kwa kumfanyia vitendo vya kishirikina.

Read More
 WILLY PAUL ATAMANI KUINGIA KWENYE NDOA

WILLY PAUL ATAMANI KUINGIA KWENYE NDOA

Staa wa muziki nchini Willy Paul ameweka wazi matamanio yake ya kuingia kwenye ndoa. Kupitia instagram yake Willy Paul ameposti picha akiwa amevalia vizuri na kusindikiza na caption inayoelezea hisia yake ya kutamani kuoa hivi karibuni na mwanamke wa ndoto yake. “Kijana ya salome anapanga kuoa.. shida yake ni, anependa kuvaa vizuri sana… atawezana na ndoa kweli??”, Ameandika Instagram. Hitmaker huyo wa ngoma ya Toto hajaweka bayana kama kweli analifanyia kazi jambo hilo ila mashabiki wamempongeza kwa hatua hiyo ya kutaka kuingia kwenye ndoa huku wengi wakimshinikiza afanye hivyo kwani ametosha kabisa kuwa mume wa mtu. Hata hivyo wajuzi wa mambo wanahoji kuwa huenda msanii huyo anatumia suala hilo kutangaza wimbo wake mpya ambao utatoka hivi karibuni. Ngoma ya mwisho Willy paul kuachia ilikuwa “Chocolate” ambayo kwa sasa inafanya vizuri youtube kwani ndani ya miezi 2 imeweza kutazamwa mara millioni 1.2.

Read More
 WILLY PAUL AFUNGUKA SABABU ZA KUJA NA MUONEKANO MPYA

WILLY PAUL AFUNGUKA SABABU ZA KUJA NA MUONEKANO MPYA

Mionekano kwa wasanii si jambo la kuchukulia poa, bali ni kazi. Ni moja ya njia za branding na kujiweka machoni mwa mashabiki muda wote. Msanii nyota nchini Willy Paul amefunguka sababu za kunyoa nywele zake aina ya dreadlocks wiki iliyopita. Katika mahojiano yake hivi karibuni Willy Paul amesema kuwa ameamua kuja na muonekano mpya kwa sababu ameacha kabisa miendo yake ya zamani ambayo amedai kuwa yalimletea matatizo kwenye safari yake ya muziki. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Chocolate” ameweka wazi sababu ya ukimya wake kwenye mitandao ya kijamii akisema kwamba kuna project ambayo anaifanyia kazi kwa sasa hivyo mashabiki wakae mkao wa kula.

Read More
 WILLY PAUL ADATA NA SHEPU YA SOCIALITE MAARUFU MTANDAONI AMBER RAY

WILLY PAUL ADATA NA SHEPU YA SOCIALITE MAARUFU MTANDAONI AMBER RAY

Mwanamuziki Nyota nchini, Willy Paul ameweka wazi kuzimia umbo la Mwanasosholaiti maarufu nchini, Amber Ray. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Hitmaker huyo wa ngoma ya “Toto” amepost picha ya pamoja akiwa na Amber Ray na kusema kwamba mrembo huyo hajafanya upasuaji wowote kuongeza sehemu yoyote ya mwili wake kama wanavyofanya akina dada wengi kwa sasa. “Hiyo nguo imepiga kona, chochote unachoona kwake ni real,” amendika Willy Paul Insta. Ujumbe huo umetafsiriwa kuwa ni vijembe kwa msanii Niccah The Queen ambaye juzi kati amerushiana maneno makali na Amber Ray kwenye mitandao ya kijamii mara baada ya Nicah kudai kuwa Amber Ray amekuwa na mazoea ya kutoka kimapenzi na waume wa watu. Utakumbuka Willy Paul amekuwa akimsifia Amber Ray katika siku za hivi karibuni kupitia mitandao yake kijamii ikiashiria kuwa huenda mrembo huyo ameshirikishwa kwenye wimbo mpya wa Willy Paul kama Video Queen.

Read More
 KLONS MELODY AJIONDOA KWENYE LEBO YA SALDIDO INTERNATIONAL

KLONS MELODY AJIONDOA KWENYE LEBO YA SALDIDO INTERNATIONAL

Uongozi wa Lebo ya muziki ya Saldido International ukiongozwa na Willy Paul umetangaza kumalizika kwa mkataba baina yao na msanii Klons Melody. Kupitia ukurasa wake Instagram, Willy Paul amemshukuru Klons Melody kwa uwepo ndani ya Saldido International katika kipindi cha miezi kumi, lakini pia amemtakia Kila la kheri na kuahidi kuendelea kumpa ushirikiano kwenye kazi zake. Klons Melody alisainiwa na lebo ya Saldido International Mei 11, mwaka 2021 na kuachia kazi kadha ikiwemo Odi Love na Atoti Jaber. Utakumbuka mwezi Novemba 21 Willy Paul alimsaini msanii wake iitwaye Queen P, miezi kadhaa baada ya msanii wake wa kwanza Miss P kujiondoa kwenye lebo hiyo.

Read More
 WILLY PAUL: MIMI NA DIAMOND NDIO WASANII PEKEE TUNAOWAKILISHA AFRIKA MASHARIKI KIMATAIFA

WILLY PAUL: MIMI NA DIAMOND NDIO WASANII PEKEE TUNAOWAKILISHA AFRIKA MASHARIKI KIMATAIFA

Staa wa muziki nchini Willy ameingia kwenye headlines mitandaoni mara baada ya kujigamba kuwa yeye na Diamond Platinumz ndio wasanii pekee wanaowakilisha Afrika mashariki kimataifa kupitia muziki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Mkali huyo wa ngoma ya Toto ameeleza kwamba yeye na Diamond Platnumz ndio wanamuziki ambao wana uwezo wa kupeleka mbali zaidi muziki wa Afrika Mashariki huku akiwataja Davido na Wizkid kuwa tayari wameshafanya hivyo kwa Nigeria na ukanda wao wa Afrika Magharibi. Hata hivyo amehapa kujitolea kwa hali na mali kuhakikisha kwamba anaupigania muziki wa Afrika mashariki ufike mbali zaidi huku akiwatolea uvivu wasanii wenzake waache kulaza damu na badala yake watie bidii kwenye kazi zao za ili muziki wa ukandu huu uweze kufika mbali zaidi. Kauli hiyo ya Willy Paul imeibua mjadala mzito miongoni mwa walimwengu kwenye mitandao ya kijamii ambapo wengi wameonekana kupuzilia mbali kauli hiyo kwa kusema kwamba msanii huyo anatafuta kiki kwa ajili ya kuachia wimbo wake mpya.

Read More