Kocha Kamau Asema Mathare Wako Tayari Kwa Mechi Dhidi ya Tusker

Kocha Kamau Asema Mathare Wako Tayari Kwa Mechi Dhidi ya Tusker

Kocha wa klabu ya Mathare United, John Kamau, amesema kuwa timu yake imejiandaa kikamilifu kusaka ushindi dhidi ya Tusker FC katika mechi ya Ligi Kuu ya Kenya itakayochezwa Jumatano hii kwenye Uwanja wa Kasarani. Akizungumza baada ya kuongoza kikosi chake katika hafla ya upanzi wa miti kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Kamau alisisitiza kuwa morali ya wachezaji wake iko juu kufuatia ushindi wao wa kwanza msimu huu uliopatikana mwishoni mwa juma lililopita. Mathare United, ambao walipambana vikali kurejea katika kiwango kizuri, wanatumia nafasi hii kujijengea msimamo bora katika ligi. Kocha Kamau ameweka wazi kuwa wanahitaji kuendeleza mwenendo mzuri wa matokeo ili kufikia malengo yao ya msimu huu. Kwa upande wa wapinzani wao, Tusker FC wanajikuta katika hali ngumu baada ya kupoteza mechi zote mbili za ufunguzi dhidi ya KCB na Posta Rangers. Hii itakuwa fursa kwao kutafuta pointi zao za kwanza, jambo linaloongeza ushindani wa mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu.

Read More
 Samsung Yatoa Uhuru Mpya kwa Watumiaji Kupitia Quick Settings

Samsung Yatoa Uhuru Mpya kwa Watumiaji Kupitia Quick Settings

Kampuni ya teknolojia ya Samsung imeanza kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wake wa uendeshaji, ikilenga kutoa uhuru zaidi kwa watumiaji kupitia toleo jipya la One UI 8.5. Mabadiliko haya makuu yanahusu sehemu ya Quick Settings na Lock Screen, ambazo sasa zitakuwa completely customizable, hatua inayoashiria ushindani wa moja kwa moja na mfumo wa iOS wa Apple pamoja na ule wa Google Pixel. Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Samsung, watumiaji wataweza kupangilia kila sehemu ya Quick Settings, kuchagua ukubwa wa vitufe, kuweka mpangilio wa sections wanavyotaka, na hata kubadilisha namna muonekano wa Lock Screen unavyoonekana. Hii ni mara ya kwanza kwa Samsung kuruhusu kiwango hiki cha uhuru katika muundo wa mfumo wake, hatua inayoonesha dhamira ya kampuni hiyo kuimarisha uzoefu wa mtumiaji. Maboresho haya yanaifanya One UI 8.5 kuwa ya kipekee zaidi, huku ikitoa nafasi kwa watumiaji kuunda muonekano wa simu zao kwa mtindo wa kipekee kulingana na ladha na mahitaji yao. Samsung inalenga kuvutia zaidi wapenzi wa ubinafsishaji (customization) ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakivutiwa na uwezo wa Pixel n iPhone katika maeneo hayo. Kwa sasa, mabadiliko haya yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi katika simu mpya zitakazokuja na One UI 8.5, kabla ya kusambazwa kwa masasisho kwenye baadhi ya vifaa vya zamani vya Samsung.

Read More
 Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Bien Azindua Rasmi Shindano la Open Verse Duniani

Msanii nyota wa Kenya, Bien, ameanzisha rasmi shindano la Open Verse Challenge kupitia wimbo wake maarufu “All My Enemies Are Suffering.” Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bien ametoa mwaliko kwa wasanii na wabunifu kutoka kote duniani kushiriki kwa kurekodi remix ya wimbo huo na kuonyesha ubunifu wao. Mshindi ataondoka na zawadi ya dola 1,000 za Kimarekani (takribani Shilingi 130,000 za Kenya). Bien amesema kuwa shindano hili limefunguliwa kwa kila mtu duniani na litafungwa mnamo tarehe 7 Novemba 2025. Washiriki wanatakiwa kupakia remix zao kwenye mitandao ya kijamii, kumtag Bien, na kutumia alama ya reli #AllMyEnemiesChallenge. Bien pia amefichua kuwa wakali wa muziki Khaligraph Jones (kutoka Afrika Mashariki) na rapa wa Nigeria Phyno (kutoka Afrika Magharibi) wanalifuatilia kwa karibu shindano hili. “Phyno alileta ladha ya Naija, sasa ni zamu yenu,” alisema Bien akiwatia moyo vipaji vipya. Kwa ushiriki wa majina makubwa ya muziki kutoka Mashariki na Magharibi mwa Afrika, mashabiki na wasanii chipukizi wanasubiri kwa hamu kuona ni nani atakayeibuka kidedea katika shindano hili linalotarajiwa kuwa kali zaidi mwaka huu.

Read More
 Sakata la Hakimiliki Lavuruga Kazi Mpya ya Nandy na Jux

Sakata la Hakimiliki Lavuruga Kazi Mpya ya Nandy na Jux

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nandy, ameonyesha kuchukizwa na hatua ya msanii chipukizi anayefahamika kama Bride Vuitton, ambaye amewasilisha maombi YouTube kutaka wimbo wake mpya “Sweety” aliomshirikisha Jux kushushwa kwa madai ya hakimiliki {copyright} Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nandy ameeleza kuwa kufika hatua aliyo nayo sasa kumemgharimu jitihada na uwekezaji mkubwa, jambo ambalo anaona halithaminiwi na kitendo cha Bride Vuitton. Amesema kuwa msanii huyo mchanga ameona sakata hilo kama fursa ya kujitengenezea umaarufu, lakini hajafikiria hasara kubwa ambayo hatua hiyo inaweza kusababisha kwa kazi yake mpya. Nandy ameongeza kuwa Bride Vuitton angetafuta njia nyingine za kujiweka kwenye tasnia bila kuhusisha kazi ya wasanii wenzake. Kwa mujibu wake, kitendo cha kutaka kushusha video ya “Sweety” siyo tu kumrudisha nyuma bali pia kinahatarisha ndoto na uwekezaji wake mzima. Hata hivyo, licha ya kukasirishwa na kitendo hicho, Nandy amewataka mashabiki wake pia kumpa sapoti Bride Vuitton kwa kusikiliza wimbo wake “Joro”, akisisitiza kuwa njia bora ya kupata nafasi katika muziki ni kupitia jitihada na uvumilivu, si kwa kuua ndoto za wengine.

Read More
 Okello Max Akiri Kudanganya Kuhusu Kuwa na Watoto

Okello Max Akiri Kudanganya Kuhusu Kuwa na Watoto

Msanii wa R&B na Afrobeat kutoka Kenya, Okello Max, amekiri kudanganya kuhusu kuwa na watoto, jambo ambalo kwa muda mrefu limekuwa likiwachanganya mashabiki wake. Katika mahojiano na mtangazaji Shiksha, Okello Max amefafanua kuwa watoto waliowahi kuonekana naye mara kwa mara si wake, bali ni ndugu wa mchumba wake. Hitmaker huyo wa Taya, ameeleza kuwa shinikizo la mara kwa mara kutoka kwa mashabiki na jamii lilimfanya kuamua kudanganya na kudai watoto hao ni wake, jambo ambalo sasa amelikiri halikuwa sahihi. Hata hivyo, msanii huyo amebainisha kuwa sasa ameamua kufunguka ili kuondoa dhana potofu na kuweka mambo wazi kwa mashabiki wake. Amesisitiza kuwa uongo huo ulikuwa matokeo ya shinikizo na si sehemu ya maisha yake halisi.

Read More
 Msanii wa Uganda Alien Skin Adaiwa Kukamatwa kwa Tu­huma za Mauaji

Msanii wa Uganda Alien Skin Adaiwa Kukamatwa kwa Tu­huma za Mauaji

Msanii mwenye utata kutoka Uganda, Alien Skin, ameripotiwa kuwekwa kizuizini baada ya kukamatwa mwishoni mwa juma kwa tuhuma za mauaji. Taarifa zinaeleza kuwa msanii huyo, ambaye ni bosi wa Fangone Forest, alinaswa na kikosi cha pamoja cha jeshi na polisi kilichozingira nyumba yake Jumamosi jioni. Inadaiwa kuwa katika upekuzi huo, maafisa wa usalama walikuta mapanga, upinde na mishale pamoja na silaha nyingine hatari nyumbani kwake, jambo lililoibua maswali zaidi kuhusu shughuli zake. Hata hivyo, vyombo vya usalama Uganda ikiwemo polisi na jeshi bado havijathibitisha rasmi kukamatwa kwake. Pamoja na hali hiyo, mashabiki wake wameanzisha kampeni mitandaoni wakitaka aachiliwe mara moja. Kwa mujibu wa mashabiki wake mitandaoni, kukamatwa kwake imehusishwa zaidi na kifo cha dansa mmoja maarufu wa Kampala ambaye alizikwa wiki iliyopita katika wilaya ya Mbale. Mashabiki wake wanadai msanii huyo ametupiwa lawama bila ushahidi wa moja kwa moja. Wakati huohuo, watumiaji kadhaa wa mitandao wamedai kuwa taarifa za kukamatwa kwake si za kweli, wakisisitiza kuwa Alien Skin yupo mafichoni na hajawahi kutiwa mbaroni. Madai ya kukamatwa kwa Alien Skin yameibuka saa chache tu baada ya Naibu Waziri wa Vijana nchini humo kuonya kuwa wasanii wanaoshirikiana na magenge ya kihalifu wako chini ya uchunguzi kwa makosa mbalimbali ikiwemo mauaji.

Read More
 Akothee Amkingia Kifua Azziad Dhidi ya Wakosoaji wa Mitandaoni

Akothee Amkingia Kifua Azziad Dhidi ya Wakosoaji wa Mitandaoni

Mwanamuziki, Akothee, amejitokeza kumtetea TikTok queen na mtangazaji Azziad Nasenya baada ya kuvamiwa mitandaoni kwa madai ya kuishi maisha ya kuigiza. Kupitia waraka wake Instagram, Akothee ameeleza kuwa anampenda na kumheshimu Azziad kwa kuwa na ndoto kubwa na kuonesha ujasiri wa kukimbizana na maisha. Amesisitiza kuwa hatua ya mrembo huyo kupata mkopo wa millioni 25 za Kenya na kununua nyumba akiwa na umri wa miaka 25 ni jambo la kupongezwa na si kulaumiwa, kwani ni nadra vijana kufanikisha mambo makubwa wakiwa na umri mdogo. Amesema kuwa wakati vijana wa rika la Azziad leo wanajitahidi kujenga maisha yao, wengi wa kizazi kilichomtangulia walihangaika na changamoto kubwa kama ndoa zilizoshindikana, kulea watoto peke yao na hata kutokuwa na akaunti ya benki wala ajira. Kwa maoni yake, hatua ya Azziad kuwekeza katika nyumba ni mfano bora wa kuchukua jukumu la maisha yake mapema. Akothee pia amekosoa wanaume wanaoendelea kumsema vibaya Azziad mitandaoni ilhali wao bado wanashindwa hata kumudu mikopo midogo. Kwa mtazamo wake, badala ya kumkosoa, Wakenya kwa jumla wana nafasi ya kujifunza kutoka kwake. Hata hivyo amehitimisha ujumbe wake kwa kusema kuwa Azziad ni msichana mwenye ndoto kubwa, anayeendelea kujijenga na kuwa chanzo cha msukumo kwa vijana wengi, na kwamba jamii inapaswa kusherehekea ujasiri wake badala ya kumshusha

Read More
 Victoria Kimani Asema Ukimya wa Mashabiki Unakatisha Tamaa

Victoria Kimani Asema Ukimya wa Mashabiki Unakatisha Tamaa

Mwanamuziki wa Kenya, Victoria Kimani, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kulalamikia zaidi ya watazamaji 25,000 wa Insta Story zake wanaoangalia maudhui yake bila kuonyesha ushirikiano wowote. Kupitia Instastory yake Instagram, Kimani amesema hali hiyo inamfanya ajihisi kupuuzwa licha ya watu wengi kutazama maudhui yake. Ameongeza kuwa hali ya kuwa na watazamaji wengi kimya inamfanya aone kama juhudi zake hazithaminiwi ipasavyo. Kupitia ujumbe wake, ametoa pia wito kwa mashabiki wake kuwa na ushirikiano wa karibu zaidi kwa kuonyesha mapenzi yao kupitia likes, maoni na ku-share au kushiriki maudhui yake. Mrembo huyo amesisitiza kuwa ushirikiano huo ni muhimu kwa wasanii kwa sababu huwapa motisha ya kuendelea kutoa kazi bora na kuendeleza uhusiano wa karibu na wafuasi wao.

Read More
 Terence Creative Afunguka Kuhusu Mapambano Dhidi ya Uraibu

Terence Creative Afunguka Kuhusu Mapambano Dhidi ya Uraibu

Mchekeshaji wa Kenya, Terence Creative, ameweka wazi safari yake ya kupambana na uraibu wa vileo, akifichua jinsi alivyoingia katika wakati mgumu maishani mwake kabla ya kurejea katika mstari sahihi. Akiangazia kipindi hicho kigumu, Terence amesema changamoto za uraibu wa pombe na uvutaji sigara zilimpelekea kupoteza mwelekeo na matumaini, lakini hakubaki peke yake. Amemshukuru mkewe Milly Chebi ambaye kwa wakati huo alikuwa mpenzi wake kwa kusimama naye na kumsaidia kuvuka kipindi cha giza katika maisha yake. Terence ameeleza kuwa upendo na uvumilivu wa mkewe ndiyo uliokuwa nguzo muhimu ya safari yake ya kupona na kupata nafasi mpya ya kuanza upya. Aidha, ametumia hadithi yake kuhamasisha wengine wanaokabiliwa na changamoto za uraibu kutafuta msaada na kutokata tamaa. Hata hivyo ametoa ushauri kwa vijana, akiwahimiza kufanya maamuzi sahihi wanapochagua wapenzi. Amesisitiza kuwa si kila mtu anaweza kusimama na mpenzi wake katika nyakati ngumu, hivyo vijana wanapaswa kuchukua tahadhari na kuchagua wenza watakaowaunga mkono kwa dhati.

Read More
 Bifu Laibuka Kati ya Toxic Lyrikali na Tipsy Gee Mtandaoni

Bifu Laibuka Kati ya Toxic Lyrikali na Tipsy Gee Mtandaoni

Rapa kutoka Kenya, Toxic Lyrikali, ameonyesha kutoridhishwa na skit iliyosambaa mtandaoni ikimuonesha mwenzake Tipsy Gee akijifananisha kuwa na mafanikio makubwa zaidi. Katika skit hiyo, Tipsy anaonekana akiendesha gari huku waigizaji waliobandikwa majina ya Toxic na Fathermoh wakiendesha bodaboda, jambo lililotafsiriwa kama kejeli kwao. Kupitia Instagram Toxic amechukizwa na kejeli hiyo na kumtaka Tipsy kuacha mbwembwe na kurudi studio kutoa muziki. Amesema wazi kuwa Tipsy amekuwa akiendesha maigizo mtandaoni badala ya kufanya kazi ya muziki, akimtupia lawama kuwa amegeuka kuwa TikToker anayejali kiki kuliko kutoa ngoma mpya. Kauli ya Toxic imekuja mara baada ya Tipsy Gee, kumtolea uvivu, akidai kwamba licha ya Toxic kumpuuza, yeye ndiye msanii aliye na mafanikio zaidi japo amekaa kwenye tasnia kwa mwaka mmoja pekee.

Read More
 Lutaaya Akanusha Kutelekeza Binti, Atoa Ushahidi wa Malipo ya Ada

Lutaaya Akanusha Kutelekeza Binti, Atoa Ushahidi wa Malipo ya Ada

Mbunge na mwanamuziki wa Uganda, Geoffrey Lutaaya, ameibuka na kujitetea vikali baada ya video ya msichana mwenye umri wa miaka 17, anayejulikana kama Nambatya, kusambaa mtandaoni ikimshutumu kwa kutelekeza majukumu ya kifamilia. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Lutaaya amekanusha madai hayo akionyesha stakabadhi anazodai ni ushahidi wa malipo ya ada kamili kwa ajili ya masomo ya Nambatya katika shule ya bweni ya Stella Maris Nsuube. Amefafanua kuwa mama wa msichana huyo ndiye aliyemtoa shuleni hapo na kumhamishia katika shule nyingine ya hadhi ya chini, Boston High School. Lutaaya pia amefichua kuwa wakati wa janga la COVID-19, alilazimika kulipa mama ya Nambatya kiasi cha Shilingi Milioni 6 za Uganda (UGX) ili kuepuka fedheha ya umma, hasa baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge. Ameongeza kuwa kwa sasa yuko tayari kumchukua binti huyo kuishi naye na familia yake na kumgharamia masomo nje ya nchi, akiamini kuwa hilo litampa mustakabali bora. Hata hivyo, video ya Nambatya ikieleza kuwa amekosa msaada wa kifedha na kutelekezwa na baba yake ilizua hasira kubwa mitandaoni. Wakosoaji walitilia shaka uadilifu wa Lutaaya kama kiongozi wa kisiasa, huku baadhi wakielekeza lawama kwa mke wake, Irene Namatovu, wakimtuhumu kwa kutokuwa na huruma kwa msichana huyo.

Read More
 Dayoo Aachwa na Meneja Wake Baada ya Kuuza Haki za Muziki Wake

Dayoo Aachwa na Meneja Wake Baada ya Kuuza Haki za Muziki Wake

Meneja wa muziki kutoka Tanzania, Mnene, ameweka wazi sababu kuu iliyomfanya kusitisha kazi yake ya usimamizi wa msanii Dayoo. Akipiga stori na Rick Media, Mnene amesema moja ya mambo yaliyomvunja moyo ni hatua ya Dayoo kuuza umiliki wa kazi zake za muziki (catalogue) bila kushirikisha timu yake ya usimamizi. Kwa mujibu wa meneja huyo, uamuzi wa Dayoo kuachia haki za umiliki wa nyimbo zake ulikuwa na athari kubwa kwa mustakabali wa kazi zao za pamoja, jambo lililosababisha migongano ya kimaslahi. Hata hivyo, Mnene amesisitiza kuwa anaendelea kumtakia Dayoo mafanikio katika safari yake ya muziki, licha ya kutengana kikazi. Kwa sasa, Meneja Mnene amesema ataendelea na mipango yake ya kusimamia vipaji vingine huku akisisitiza kuwa anaamini katika uwekezaji wa muda mrefu kwenye kazi za muziki.

Read More