Msanii Tory Lanez Afeli Kujaribu Kubatilisha Hukumu ya Jinai ya 2022

Msanii Tory Lanez Afeli Kujaribu Kubatilisha Hukumu ya Jinai ya 2022

Msanii wa muziki wa Marekani, Tory Lanez, ameshindwa katika jitihada zake za kuwasilisha ushahidi mpya ili kubatilisha hukumu yake ya jinai ya mwaka 2022. Lanez alifungua maombi mawili kuhusiana na shambulio la risasi lililotokea mwaka 2020 lililomkabili Megan Thee Stallion. Moja ya maombi hayo yalilenga kuanzisha hoja kwamba dereva wa mwendesha gari wa Peterson hakushuhudia kwenye kesi, huku lingine likitaka kuwasilisha tamko jipya kutoka kwa mlinzi wa Kelsey Harris, rafiki wa zamani wa karibu wa mwathiriwa. Hata hivyo, maombi yote mawili yamekataliwa Jumanne na Mahakama ya Rufaa ya California. Timu ya kisheria ya Lanez ilidai kwenye mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika Mei mwaka huu kwamba Bradley Jennings, aliyekuwa mlinzi na dereva wa Harris, alishuhudia mazungumzo ambapo Harris alidai kuwa ndiye aliyefatwa na bunduki na kuipiga mara kadhaa, na kwamba Peterson alishika mkono wake na hivyo bunduki ilipiga risasi zaidi. Lengo la ushahidi huo lilikuwa kuonesha kwamba bunduki ilipigwa risasi kwa bahati mbaya na si Lanez. Uamuzi wa mahakama kukataa ushahidi mpya unamaanisha kuwa Tory Lanez hatakuwa na nafasi ya kuutumia kama msingi wa kubatilisha hukumu yake. Kesi ya jinai ya mwaka 2022 hivyo inasalia thabiti, na msanii huyo sasa anakabiliana kikamilifu na athari za kisheria zinazotokana na makosa aliyopatikana nayo.

Read More
 Guardian Angel Awatolea Uvivu Wanaopinga Utajiri Wake

Guardian Angel Awatolea Uvivu Wanaopinga Utajiri Wake

Mwanamuziki wa injili nchini Kenya, Guardian Angel, amewajibu vikali wakosoaji wanaopinga au kutilia shaka hali yake kiuchumi, baada ya kufichua kwamba hutumia takribani KSh 1.5 milioni kila mwezi. Kupitia Instastory yake kwenye mtandao wa Instagram, Ameeleza kuwa anaishi katika mtaa wa kifahari wa Karen na pia anamiliki shamba lenye ukubwa wa ekari tano katika eneo la Lukenya. Kwa mujibu wa Guardian Angel, Wakristo wengi hawana imani ya kuona wenzao wakifanikiwa, jambo linaloonyesha changamoto katika kuelewa baraka na mafanikio yanayotoka kwa Mungu. Anasema ataendelea kushirikisha mashabiki wake kuhusu safari yake ya maisha bila kujali maoni ya wakosoaji. Kauli yake imeibua mjadala mitandaoni, huku baadhi wakimuunga mkono na wengine wakimshuku wakihoji kwamba msanii huyo anajinasibu na mali ya mke wake ambaye ana anagharamia Maisha yake ya muziki.

Read More
 Butita Amkingia Kifua Flaqo Kufuatia Skit Yenye Utata

Butita Amkingia Kifua Flaqo Kufuatia Skit Yenye Utata

Mchekeshaji na mtayarishaji wa maudhui nchini Kenya, Eddie Butita, amejiunga na mjadala ulioibuka kufuatia skiti ya hivi karibuni ya Flaqo inayodaiwa kuwalenga wafanyi biashara wa forex wanaodaiwa kuwa utajiri wao unatokana na biashara ya ushoga au mahusiano ya jinsia moja. Kupitia mitandao yake ya kijamii Butita alisisitiza kuwa katika skiti hiyo, Flaqo hakumtaja mtu yeyote moja kwa moja, jambo linalomfanya ashangae ni kwa nini baadhi ya watu wanajihisi kushambuliwa ikiwa kweli hawahusiki na masuala yaliyoigizwa. Aliongeza kuwa sanaa na ucheshi huwa na jukumu la kuibua mijadala na kutoa nafasi ya jamii kujitazama kwenye kioo. Skiti hiyo ya Flaqo imezua mjadala mkali mitandaoni, ambapo baadhi ya wafuasi wake wamejitokeza kumtetea wakisema ni kazi ya kisanii inayotumia kejeli na utani kufichua uhalisia wa maisha, huku wakosoaji wakidai kuwa kugusia masuala yenye utata kama biashara ya “Sim2” au Ushoga ni kukiuka maadili na heshima, na kwamba inaweza kuathiri heshima ya sekta nyingine kama forex trading. Mjadala huu unaonekana kugawanya maoni ya umma, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa uhuru wa ubunifu na wengine wakitaka wasanii kuwa makini wanapogusia mada nyeti zinazoweza kuibua hisia kali katika jamii.

Read More
 Akothee Avunja Ukimya Baada ya Kukosolewa Kuhusu Mavazi

Akothee Avunja Ukimya Baada ya Kukosolewa Kuhusu Mavazi

Mwanamuziki wa Kenya, Esther Akoth maarufu kama Akothee, amejibu vikali ukosoaji unaoendelea mitandaoni kuhusiana na mavazi aliyovaa katika tukio la hivi karibuni huko Homa Bay. Kupitia mitandao ya kijamii, Akothee alisisitiza kuwa hana jukumu la kuwa mfano wa kuigwa kwa mtu yeyote na kwamba anapaswa kuachiwa aishi maisha yake kwa namna anayoona inafaa. Akothee alisema licha ya mashambulizi ya maneno anayopokea, bado ataendelea kushiriki katika matukio anayoalikwa na kufanya maonyesho kwa mtindo wake wa kipekee. Mwanamuziki huyo ameendelea kusisitiza kuwa maamuzi yake ya kisanii na binafsi hayapaswi kupimwa kwa kipimo cha maadili ya mtu mwingine, akiwataka wakosoaji waache kumfuatilia kwa matarajio yasiyoendana na mtindo wake wa maisha. Kauli ya Akothee imeibua mjadala mitandaoni, ambapo wafuasi wake wamegawanyika kati ya wanaomuunga mkono kwa kusimamia haki yake ya kujieleza na wale wanaoamini kuwa umma una haki ya kumkosoa kutokana na hadhi yake kama msanii maarufu. Tukio hili linakuja siku chache tu baada ya picha na video za Akothee akiwa katika vazi lililoibua hisia kali kusambaa mitandaoni, na kusababisha mjadala mkubwa kuhusu mipaka ya uhuru wa msanii na matarajio ya jamii

Read More
 Parroty Afufua Bifu na Toxic Lyrikali Kupitia Picha ya Siri

Parroty Afufua Bifu na Toxic Lyrikali Kupitia Picha ya Siri

Msanii wa muziki wa gengetone, Parroty Vunulu, amezua gumzo mitandaoni baada ya kuwaomba mashabiki wake kumsaidia kutambua picha ya mwanaume asiyejulikana ambaye amekuwa akijitokeza mara kwa mara kwenye sehemu ya maoni ya mitandao yake ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Parroty aliahidi kumpa zawadi ya KSh 1,000 shabiki atakayefanikisha kumtambua mwanaume huyo. Ingawa hakumtaja moja kwa moja, mashabiki wengi wamehusisha picha hiyo na rapa Toxic Lyric Kali, anayejulikana kwa wimbo Backbencher. Inadaiwa kuwa Parroty na Toxic Lyric Likali hawako kwenye uhusiano mzuri baada ya madai kwamba rapa huyo alimuaibisha Parroty mtandaoni alipomwomba kufanya kolabo. Tukio hili limeendeleza mvutano wa chini kwa chini kati ya wasanii hao, huku mashabiki wakisubiri kuona kama Toxic Lyrikali.

Read More
 Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Washindi mara mbili wa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), Morocco, watakuwa na lengo la kurejea kwenye njia ya ushindi leo jioni watakapomenyana na Zambia katika mechi ya Kundi A itakayopigwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi. Atlas Lions walizindua kampeni yao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Angola, lakini wakapoteza mchezo wa pili kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Kenya siku ya Jumapili. Kwa upande mwingine, Zambia bado inawinda ushindi wake wa kwanza, baada ya kupoteza mechi zake zote mbili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Angola. Morocco, ambao wamelenga kufuzu kwa hatua ya robo fainali, wanahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini yao ya kuendelea kushiriki mashindano haya. Nayo Zambia, ambayo inaburuza mkia bila alama yoyote, inahitaji ushindi ili kuhuisha matumaini ya kusalia katika michuano hiyo. Katika mechi nyingine ya kundi hilo hilo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo itachuana na Angola katika uwanja wa Kasarani kuanzia saa mbili usiku. Mchuano huu pia ni wa muhimu katika kuamua hatma ya timu zitakazofuzu kwa hatua inayofuata. Baada ya raundi tatu za michuano ya Kundi A, Kenya inaongoza kwa alama saba, ikifuatiwa na Angola yenye pointi nne. DRC iko nafasi ya tatu kwa pointi tatu, Morocco ya nne, huku Zambia ikiwa mkiani bila pointi yoyote.

Read More
 Google Yazindua Vids, Jukwaa Jipya la Kutengeneza Video

Google Yazindua Vids, Jukwaa Jipya la Kutengeneza Video

Google imezindua jukwaa jipya la kutengeneza video linaloitwa Vids, likiwa sehemu ya hatua zake za kuimarisha huduma kwa watumiaji wake katika uundaji wa maudhui ya kidijitali. Vids ni jukwaa linalotegemea teknolojia ya akili bandia (AI), na limetengenezwa mahsusi kuwasaidia watumiaji kuunda video kwa haraka, kwa urahisi, na kwa ubora wa kitaalamu hata bila kuwa na ujuzi wa kuhariri video. Kupitia Vids, watumiaji wanaweza kuanzisha mradi wa video kwa kuchagua templeti zilizotayari, kisha kupakia picha, sauti, au vipande vya video, na kuacha AI ikisaidie kupanga na kuhariri muundo wa mwisho. Jukwaa hili pia linafanana na huduma nyingine za Google kama Google Docs na Slides, ambapo watumiaji wengi wanaweza kushirikiana kwenye video moja kwa wakati mmoja. Licha ya kuwa bado ipo kwenye hatua ya majaribio, Google Vids tayari imewavutia watumiaji wa Google Workspace waliopata nafasi ya kuijaribu. Kampuni hiyo imesema inalenga kuipanua huduma hiyo ili kuwafikia watu wengi zaidi katika siku zijazo. Uzinduzi wa Vids umeonekana kama hatua ya Google kujiimarisha katika soko la zana za uhariri wa video, na ushindani wake unalenga majukwaa kama Canva, TikTok Video Editor, na CapCut. Watumiaji wengi mitandaoni wameelezea matumaini kuwa Vids itakuwa suluhisho bora kwa wale wanaotaka kuunda maudhui ya video kwa haraka bila kutumia programu ngumu.

Read More
 Guardian Angel: Natumia Milioni 1.5 Kila Mwezi!

Guardian Angel: Natumia Milioni 1.5 Kila Mwezi!

Msanii wa muziki wa injili nchini Kenya, Guardian Angel, amefichua kiwango kikubwa cha fedha anachotumia kila mwezi kugharamia mahitaji yake ya msingi. Akipiga stori na podcast ya Mwakideu live, Guardian Angel amesema kuwa matumizi yake ya kila mwezi ni zaidi ya Shillingi milioni 1.5. Kwa mujibu wa msanii huyo, kiasi hicho kinahusisha gharama za maisha, miradi ya muziki, pamoja na majukumu mengine ya kifamilia na kijamii anayobeba. Amebainisha kuwa licha ya muziki wa injili kutoonekana kama sekta yenye mapato makubwa, yeye ameweza kujipanga kimaisha kuhakikisha anadumisha kiwango chake cha maisha. Kauli yake imezua mjadala mitandaoni, baadhi ya mashabiki wakisifia uaminifu na uthubutu wake wa kuweka wazi hali yake ya kifedha, huku wengine wakishangazwa na ukubwa wa gharama hizo.

Read More
 Miss Omuts Amshutumu Pritty Vishy kwa Kutoa Taarifa za Uongo Kuhusu BBL

Miss Omuts Amshutumu Pritty Vishy kwa Kutoa Taarifa za Uongo Kuhusu BBL

Mjadala mkali umeibuka mtandaoni baada ya Digital Creator, Miss Omuts, kumtuhumu mrembo aliyegeukia maisha ya Usosholaiti Pritty Vishy kwa kutoa taarifa za uongo kuhusu kufanya upasuaji wa kuongeza makalio maarufu Brazilian Butt Lift (BBL). Kupitia mitandao ya kijamii, Miss Omuts amedai kuwa madai ya Vishy hayana ukweli wowote, akieleza kwamba mtu anayefanyiwa BBL hawezi kukaa chini mara moja kutokana na maumivu makali yanayoambatana na upasuaji huo. Kauli hii imezua mjadala miongoni mwa mashabiki na wafuasi wa pande zote mbili, huku baadhi wakimtetea Pritty Vishy na wengine wakiunga mkono hoja za Miss Omuts. Hayo yote yameibuka baada ya Pritty Vishy kuibua gumzo mtandaoni kuhusu maisha yake binafsi, hasa baada ya kudai kuwa alitumia zaidi ya shillingi milioni moja kubadilisha muonekano wa mwili wake kwa upasuaji wa kuongeza makalio kwa mafuta (BBL), kuondoa mafuta ya ziada mwilini (liposuction), na kuondoa ngozi na mafuta tumboni (tummy tuck).

Read More
 Newcastle Yamsajili Malick Thiaw Kutoka AC Milan

Newcastle Yamsajili Malick Thiaw Kutoka AC Milan

Klabu ya Newcastle United imethibitisha kumsajili rasmi beki wa kati wa AC Milan, Malick Thiaw, kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kuwa pauni milioni 30.2, pamoja na marupurupu yanayoweza kufikia pauni milioni 4.3. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, mzaliwa wa Düsseldorf nchini Ujerumani, amejiunga na Newcastle baada ya kipindi cha mafanikio akiwa na miamba wa Italia, AC Milan. Thiaw alijiunga na Milan mwaka 2022 akitokea Schalke 04 ya Bundesliga na ameichezea timu hiyo mechi 85 katika mashindano mbalimbali. Katika msimu uliopita, Thiaw alikuwa sehemu ya kikosi cha Milan kilichoshinda taji la Supercoppa Italiana kwa kuwacharaza mahasimu wao wa jadi, Inter Milan, katika fainali. Ushindi huo uliifanya Milan kutwaa taji lao la nane la Super Italia. Thiaw anatarajiwa kuimarisha safu ya ulinzi ya Newcastle kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL), huku kocha wa timu hiyo Eddie Howe akiweka wazi kuwa ni mchezaji aliyekuwa akimfuatilia kwa muda mrefu kutokana na uwezo wake wa kimataifa na uzoefu katika mashindano makubwa ya Ulaya. .

Read More
 Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Spice Diana Amshambulia Sheebah, Adai Analipa Wanablogu Kumchafua

Msanii nyota wa muziki nchini Uganda, Spice Diana, ameendeleza mashambulizi ya maneno dhidi ya msanii mwenzake Sheebah Karungi, akimtuhumu kuwalipa wanablogu na baadhi ya watu kutoka kwenye timu yake ili kusambaza taarifa za kumchafua mtandaoni. Akizungumza katika mahojiano na kituo cha runinga nchini Uganda, Spice Diana alisema kuwa Sheebah mara nyingi hujikita kumzungumzia kila anapopata nafasi, jambo ambalo kwa upande wake anadai halimsumbui. Spice Diana amesema kuwa hatua ya kum-unfollow Sheebah kwenye Instagram ilitokana na kile alichokiona kama tabia za kimaslahi binafsi na zisizo za ukweli. Alieleza kuwa badala ya kushughulikia masuala yao binafsi kwa njia ya moja kwa moja, Sheebah alichagua kuchapisha ujumbe kwenye mitandao ya kijamii, hali iliyomfanya apoteze imani naye. Kwa upande wake, Sheebah Karungi, kupitia mkutano na wanahabari uliofanyika wiki iliyopita, alikanusha madai ya kumshambulia Spice Diana au kulipa wanablogu waandike habari mbaya kumhusu, akieleza kuwa hana sababu yoyote ya kufanya hivyo. Mvutano kati ya wasanii hawa wawili umeendelea kushika kasi kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakifuatilia kwa karibu maendeleo ya mzozo huo

Read More
 Lava Lava Atangaza Ujio wa EP Mpya ‘Time’

Lava Lava Atangaza Ujio wa EP Mpya ‘Time’

Msanii nyota wa Bongofleva, Lava Lava, ametangaza rasmi ujio wa Extended Playlist (EP) yake mpya inayotarajiwa kuachiwa Ijumaa hii. Kazi hiyo mpya, inayokwenda kwa jina la Time, imebeba jumla ya nyimbo sita za moto, ikiwa na kolabo mbili za kuvutia kutoka kwa wasanii Yammi na Bill Nass. EP hii inakuwa kazi yake ya kwanza tangu ajiondoe kwenye lebo ya WCB, hatua inayoashiria mwanzo mpya katika safari yake ya muziki akiwa msanii huru. Lava Lava amesema anatarajia mashabiki wataipokea kwa hamasa, akieleza kuwa “Time” ni mradi uliojaa ubunifu, hisia na ujumbe wa maisha. Kwa mujibu wa taarifa, EP hiyo itapatikana kwenye majukwaa yote ya muziki mtandaoni kuanzia siku ya uzinduzi. Mashabiki wameshaanza kuonyesha shauku kubwa kupitia mitandao ya kijamii, wakisubiri kusikia ladha mpya kutoka kwa msanii huyo anayefahamika kwa sauti yake ya kipekee.

Read More