Baba Levo Amzawadia Mke Wake Range Rover

Baba Levo Amzawadia Mke Wake Range Rover

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini ambaye pia ni msanii wa muziki, Baba Levo, amegusa hisia za wengi baada ya kumzawadia mke wake gari jipya aina ya Range Rover kama ishara ya shukrani kwa mchango wake mkubwa katika safari yake ya kisiasa. Akizungumza kuhusu zawadi hiyo, Baba Levo amesema mke wake alikuwa nguzo muhimu wakati wa kampeni zake za kuwania ubunge wa Kigoma Mjini, akimhudumia, kumpa moyo na kusimama naye bega kwa bega katika kipindi kigumu cha kampeni. Mkali huyo wa Shusha, amesema zawadi hiyo siyo tu gari, bali ni ishara ya kuthamini juhudi, uvumilivu na msaada wa dhati alioupata kutoka kwa mke wake tangu mwanzo wa harakati zake za kisiasa hadi kufanikisha ushindi.

Read More
 Baba Levo Akanusha Taarifa za Kumkimbia Diamond Baada ya Kuteuliwa Mbunge

Baba Levo Akanusha Taarifa za Kumkimbia Diamond Baada ya Kuteuliwa Mbunge

Mbunge wa Kigoma Mjini, Baba Levo, amejitokeza kufafanua madai yaliyosambaa mtandaoni yakidai kuwa angekimbia msanii Diamond Platnumz mara tu baada ya kuteuliwa kuwa mbunge. Akizungumza baada ya kukula kiapo nje ya majengo ya Bunge, Baba Levo amesema hajawahi na hatarajii kumkimbia Diamond, kwani ndiye mtu aliyemsaidia kupanda ngazi kutoka kudharauliwa na jamii hadi kuwa mtu mwenye heshima. Msanii huyo aliyegeukia siasa, ameeleza kuwa uhusiano wake na Diamond bado upo imara na kwamba nafasi yake ya kisiasa haitabadilisha ukaribu wao. Kauli yake imekuja kufuatia tetesi zilizodai kuwa kuteuliwa kwake kungekuwa chanzo cha yeye kujitenga na kundi la Wasafi.

Read More
 Baba Levo Akerwa na Tukio la Mfanyakazi wa Ndani Kumfanyia Ukatili Mtoto Wake

Baba Levo Akerwa na Tukio la Mfanyakazi wa Ndani Kumfanyia Ukatili Mtoto Wake

Msanii wa Bongo Fleva Baba Levo ameonyesha maumivu makubwa na kukerwa sana baada ya kanda ya CCTV kufichua tukio la ukatili lililofanywa na mfanyakazi wa ndani dhidi ya mtoto wake, Platnum, wakati yeye na mke wake hawakuwepo nyumbani. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Baba Levo ameeleza jinsi tukio hilo lilivyomuathiri yeye na mke wake Mama Ruby, akisema kuwa video ya tukio hilo imeumiza sana familia yake. Msanii huyo aliyegeukia siasa, amefunguka kwamba mara nyingi huwa anamwomba mke wake abaki nyumbani na watoto ili yeye aweze kushughulika na kazi zake, lakini mara nyingi ombi hilo huonekana kama jaribio la kumfanya mke wake kuwa tegemezi. Hata hivyo, amesema video hiyo imempa mke wake maumivu makubwa na kuthibitisha umuhimu wa wazazi kuwa karibu na watoto wao. Kauli ya Baba Levo inakuja mara baada ya kanda ya CCTV kumuonyesha mfanyakazi wake wa ndani akimfunga miguu mtoto wake, kitendo ambacho kimezua hasira na masikitiko makubwa kwa familia ya msanii huyo.

Read More
 Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mbosso Amtaka Diamond Kuvunja Ukimya Kuhusu Kauli za Baba Levo

Mwanamuziki Mbosso ameibuka na kuweka wazi msimamo wake kufuatia mvutano unaoendelea mitandaoni kati yake, Diamond Platnumz, na Baba Levo, kuhusu tuhuma za kushirikiana kumchafua kwa jina au kazi zake. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Mbosso amesema kwa uwazi kuwa hana ukaribu wowote na Baba Levo, na hivyo hawezi kushirikiana naye kwa jambo lolote, tofauti na madai yanayoenezwa. Amefafanua kuwa yeye si mtu wa migogoro, na kwamba anamuheshimu Diamond kama kiongozi na kama msanii mkubwa aliyechangia ukuaji wa muziki wake. Hata hivyo, Mbosso amesisitiza kuwa ni wajibu wa Diamond kuzungumza hadharani kumkemea Baba Levo, kwani ukimya wake unaweza kutafsiriwa kama kukubaliana au kuunga mkono vitendo vya matusi na kejeli vinavyotolewa hadharani na Baba Levo. Kauli ya Mbosso imekuja muda mfupi baada ya Baba Levo kumuomba msamaha na Diamond Platinumz akidai kuwa hana ajenda yoyote na Mbosso ya kumchafulia brand yake. “Mzee Lukuga, sina Agenda yoyote na Mbosso na wala siwezi kupanga njama yoyote na Mbosso, nisamehe mzee wangu” Aliandika Instagram. Ikumbukwe jana kulizuka sintofahamu kati ya Mbosso na Baba Levo baada ya Baba Levo kudai kuwa ngoma ya Pawa imetungwa na Diamond Platnumz, ambapo Mbosso alikasirika na kudai huenda WCB inamfanyia figisu wakati aliondoka salama na anaheshimu sana mchango wao kwenye muziki na mara zote amekuwa akiwashukuru.

Read More
 Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Baba Levo ahaidi kumsaidia Anjella baada ya Harmonize kumkimbia

Sakata la Harmonize na msanii wake Anjella limemgusa mwanamuziki wa Bongofleva Baba Levo ambaye ameweka wazi atamsaidia msanii huyo matibabu ya mguu wake kwa kumpeleka India na Qatar. Kupitia ukurasa wake instagram Baba Levo amesema “Dada Anjella Naitwa Baba Levo NAKUHAKIKISHIA UTAENDA QATAR NA UTAENDA INDIA PIA KWA AJILI YA MATIBABU …!! KIRANDAGE PAMOJA NA BANGE ZAKE ILA AMEKUTOA MBALI SEMA TU AMEISHIWA HELA KWA SASA NA HII NI KWASABABU YA KUTAKA KUSHINDANA NA DIAMOND PLATINUMZ AMEJIKUTA AMEFILISIKA KABISA…!” Ikumbukwe, jana Harmonize kupitia insta story yake aliweka ujumbe akitaka mtu yeyote anaeweza kuendeleza kipaji cha Anjella asisite kujitokeza kwa ajili ya kumsaidia msanii huyo. Hata hivyo, kwenye ujumbe huo boss huyo wa Konde Gang hakuweka wazi kama lebo yake ndio imeachana rasmi na Anjella.

Read More
 LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

LINEX AMCHANA BABA LEVO KWA MADAI YA KUMZUNGUMZIA VIBAYA

Mwanamuziki wa Bongofleva Linex mjeda ameamua kumtolea uvivu baba levo baada ya msanii huyo kuendelea kuongelea maisha yake mara kwa mara kwenye vyombo vya habari Kupitia ukurasa wake wa Instagram Linex amemchana Baba Levo kuwa aache kuongelea maisha yake kwenye redio kwani jambo hilo linamkosesha amani huku akimuomba baba levo msamaha kama amewahi kumkosoa. Linex na Baba Levo ni marafiki wa miaka mingi na Baba Levo ameshawahi kukiri mara nyingi kuwa Linex ni kati ya watu ambao walimsaidia miaka ya hapo nyuma akiwa Dareesalaam akijaribu kuupambania kipaji chake cha muziki. Hata hivyo Baba Levo amekuwa akifunguka matukio na tabia za Linex ambazo walikuwa wanazipitia miaka ya nyuma. Lakini pia amekuwa akilitaja jina la Linex kwenye mifano mbalimbali afanyapo mahojiano na vyombo vya habari jambo ambalo limemfanya Linex kukwazika

Read More