Barnaba Classic: Niliwahi kulala studio na hata kuwa mpishi THT kufuatilia ndoto zangu

Barnaba Classic: Niliwahi kulala studio na hata kuwa mpishi THT kufuatilia ndoto zangu

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Barnaba Classic amefunguka kuhusu changamoto alizopitia mwanzoni mwa safari yake ya muziki, akisema aliwahi kulala studio na kufanya kazi mbalimbali ikiwemo usafi hadi kupika alipokuwa chini ya taasisi ya kukuza vipaji ya Tanzania House of Talent (THT). Barnaba amesema kipindi hicho alikuwa chini ya uongozi wa marehemu Ruge Mutahaba na alilazimika kuvumilia hali hiyo kwa sababu alikuwa na ndoto ya kufanikiwa katika muziki. Kwa mujibu wake, licha ya changamoto na tofauti ndogo ndogo zilizowahi kujitokeza, bado anaona hakuna sababu ya kuwasema vibaya watu waliomsaidia katika safari yake. Aidha, Barnaba amewataka watu wanaosaidia vipaji chipukizi kuhakikisha wanawatendea vijana hao kwa wema wanapowasaidia kufikia ndoto zao, ili hata wakiondoka baadaye waweze kuwakumbuka kwa mema. Kauli ya Barnaba imeibuka wakati sakata linaloendelea mitandaoni likihusisha msanii Mac Voice, ambaye hivi karibuni alidai kuwa aliwahi kulala studio alipokuwa akijaribu kupambana kufikia mafanikio katika muziki. Kauli hiyo imezua mjadala mpana kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya wasanii wakisimulia changamoto walizokumbana nazo mwanzoni mwa safari zao za muziki.

Read More
 Barnaba Classic Awaonya Vijana wa Gen Z Kuhusu Ndoa

Barnaba Classic Awaonya Vijana wa Gen Z Kuhusu Ndoa

Msanii wa muziki wa Bongoflava, Barnaba Classic, amewataka vijana wa kizazi cha Gen Z kuwa waangalifu wanapofanya maamuzi ya kuingia kwenye ndoa, akisisitiza kuwa tamaa za mwili pekee hazitoshi kujenga ndoa imara. Kupitia ujumbe aliotoa hivi karibuni, Barnaba amesema kuwa vijana wengi siku hizi wanaingia kwenye mahusiano ya ndoa wakiongozwa na hisia za muda mfupi na shinikizo la mitandao ya kijamii, jambo ambalo limechangia ongezeko la migogoro na talaka. Aidha, msanii huyo amewataka vijana wa Gen Z kuweka mbele malengo ya maisha, maadili na maono ya baadaye badala ya kukimbilia ndoa kwa sababu ya presha kutoka kwa marafiki au jamii. Kauli ya Barnaba imeibua mjadala mpana mtandaoni, huku baadhi ya vijana wakikubaliana naye na wengine wakisema kizazi cha sasa kina mtazamo tofauti kuhusu mahusiano na ndoa. Hata hivyo, 

Read More
 Barnaba Classic Awataka Wasanii Kusajili Majina Yao ya Kisanii

Barnaba Classic Awataka Wasanii Kusajili Majina Yao ya Kisanii

Msanii wa BongoFleva Barnaba Classic ametoa wito kwa wasanii na wadau wa sanaa nchini Tanzania kuhakikisha wanasajili majina yao ya kisanii pamoja na misemo wanayotumia mara kwa mara, ili kuepuka migogoro ya kisheria inayoweza kujitokeza baadaye. Akizungumza kwenye mahojiano yake hivi karibuni, Barnaba amesema wasanii wengi wamekuwa wakichukulia poa suala la usajili wa majina na misemo yao, jambo linalowafanya kujikuta kwenye sintofahamu pindi haki za matumizi ya majina hayo zinapodaiwa kisheria. Barnaba amesema kumeshuhudiwa matukio ambapo wasanii wamekuwa maarufu kwa majina fulani, lakini baadaye wakazuiwa kuyatumia au kufunguliwa madai kwa sababu hawakuwahi kuyasajili mapema kwa mujibu wa sheria. Msanii huyo amesisitiza kuwa taasisi kama COSOTA zipo kwa ajili ya kulinda haki za wasanii, lakini akabainisha kuwa jukumu la kwanza ni la msanii mwenyewe kuchukua hatua za kujilinda mapema kisheria.

Read More
 Barnaba Classic awapa somo wasanii kuhusu nidhamu kwenye kazi zao

Barnaba Classic awapa somo wasanii kuhusu nidhamu kwenye kazi zao

Mwimbaji nyota wa muziki wa Bongofleva, msanii Barnaba Classic amewakumbusha wasanii wenzake kuwa na heshima pamoja na nidhamu kwa watu wengine. Barnaba ametumia insta story yake kuwatahadharisha wakumbuke kuna kesho.. “Ndugu zangu wasanii tujifunze heshima na kuheshimu mipaka yetu ya kazi kwa kila mmoja. Lakini pia tujifunze kuwa na upendo kweli na kutoleta mashauzi Mbuzi ambayo kuna muda baadhi ya mambo hayahitaji mbwembwe nyingi kuliko busara. Tuwe na hekima wakati mwingine. Sio kama wengine hatujui kuongea ila tumelelewa kwenye busara.” ameandika Barnaba Classic. “Nimekuwa kwenye huu muziki yapata miaka 18 sasa lakini sijawahi kumdharau anayekuja leo na aliyeanza kabla yangu. Lakini nadhani kuna jambo kubwa najivunia sana katika maisha yangu ya muziki kuishi bila kuzoea watu hata kama nawajua na kuwachukulia poa. Kwa hiyo ndugu zangu wasanii wenzangu, tuwe na nidhamu na mnapofanya mambo ya kuvunja heshima na mipaka muwe mnakumbuka kuna kesho”. amemalizia Barnaba Classic kwenye mfululizo wa jumbe zake kupitia insta story yake.

Read More
 Barnaba Classic ampa nyota Diamond Platnumz

Barnaba Classic ampa nyota Diamond Platnumz

Mwanamuziki wa Bongofleva Barnaba Classic ameamua kumpa Diamond Platnumz maua yake akiwa hai kwa kushiriki kwa asilimia kubwa sana kwenye kuufanya mwaka 2022 kuwa wenye mafanikio kwake. Kupitia Instastory yake amemshukuru Bosi huyo wa WCB kwa kuandika ,”Asante sana Mungu akubariki, umetenda pakubwa sana. Mungu akupe njia njema wengi tufaidike na uwepo wako. Unaroho ya kipekee sana”. Mwaka 2022 Diamond Platnumz alishiriki kwa asilimia kubwa sana kwenye Album ya Barnaba, “Love Sounds Different” ambayo imempa mafanikio makubwa sana ya kimuziki.

Read More
 BARNABA CLASSIC ATIMIZA NDOTO YA KUFANYA KAZI NA MALKIA WA MIPASHO BI. KHADIJA KOPA

BARNABA CLASSIC ATIMIZA NDOTO YA KUFANYA KAZI NA MALKIA WA MIPASHO BI. KHADIJA KOPA

Mwanamuziki nyota kutoka nchini Tanzania Barnaba Classic ametimiza ndoto nyingine kubwa katika hatua za kukamilisha Album yake ijayo ambayo amewashirikisha wakali kibao. Barnaba kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza kutimiza ndoto yake ya kufanya kazi na Malkia wa taarab Bi. Khadija Kopa huku akithibitsha kuwa atakuwa miongoni mwa walioshirikishwa kwenye Album yake ijayo. Hata hivyo Barnaba ameongeza kuwa album yake  ijayo itaacha kumbukumbu kwenye muziki wa Tanzania.

Read More
 BARNABA KUMVISHA PETE YA UCHUMBA MPENZI WAKE RAYA

BARNABA KUMVISHA PETE YA UCHUMBA MPENZI WAKE RAYA

Staa wa muziki wa Bongofleva Barnaba Classic yupo mbioni kuufungua ukurasa mwingine wa mapenzi kwa tukio la kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi bibie Raya The Boss ikiwa ni kiashiria cha kuelekea katika ndoa. Barnaba amebainisha ujio wa jambo hilo la kheri kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kushare picha ya pete mbili na kuwapa nafasi mashabiki wake wamchagulie ipi itafaa kumvisha mpenzi wake huyo. “Ipi itafaa, she says Yes ” – ameandika Barnaba. Uhusiano wa wawili hao ulianza mwaka 2018 baada ya Barnaba kuachana na aliyekuwa mpenzi wake.

Read More