Eddy Kenzo Amtaka Bebe Cool Kuachia Nyimbo Badala ya Kugeukia Content Creation

Eddy Kenzo Amtaka Bebe Cool Kuachia Nyimbo Badala ya Kugeukia Content Creation

Msanii nyota wa Uganda Eddy Kenzo amemtaka mkongwe wa muziki nchini humo Bebe Cool kurejea studio na kuachia ngoma kali, badala ya kujikita zaidi katika utengenezaji wa maudhui (content creation) mitandaoni. Akizungumza katika mahojiano ya hivi karibuni, Eddy Kenzo amesema ni jambo la kusikitisha kuona msanii mwenye historia kubwa kama Bebe Cool akigeukia zaidi kazi za kutengeneza content na kuwakosoa wasanii wengine, badala ya kutumia uzoefu na kipaji chake kuendelea kuutumikia muziki kwa kutoa vibao vipya. Kenzo ameongeza kuwa Bebe Cool ana mchango mkubwa katika muziki wa Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla, hivyo mashabiki bado wana matarajio makubwa ya kusikia kazi mpya zenye ubora kutoka kwake. Aidha, Eddy Kenzo amemtaka Bebe Cool kuwaachia vijana wa Gen Z jukumu la kutengeneza content mitandaoni, akisisitiza kuwa kizazi hicho ndicho chenye nguvu na ubunifu mkubwa katika eneo hilo, huku wasanii wakongwe wakipaswa kubaki kwenye msingi wao wa muziki.

Read More
 Eddy Kenzo Amshutumu Bebe Cool Kwa Roho Mbaya na Njama Dhidi ya Wasanii

Eddy Kenzo Amshutumu Bebe Cool Kwa Roho Mbaya na Njama Dhidi ya Wasanii

Msanii nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, amemshutumu Bebe Cool kwa madai ya kuwa na roho mbaya dhidi ya wasanii wengine na kutumia ushawishi wa kisiasa kujinufaisha binafsi huku akiwadhoofisha wenzake. Kwa mujibu wa Kenzo, Bebe Cool amekuwa akijipendekeza kwa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, kwa lengo la kupata nguvu na nafasi ya kuwazima wasanii wengine ndani ya tasnia ya muziki. Kenzo anadai kuwa ushirikiano huo wa karibu na serikali umekuwa ukitumika kama chombo cha kudhibiti na kunyamazisha sauti za wasanii wasiokubaliana na msimamo wa Bebe Cool. Kenzo anadai Bebe Cool alijaribu kukimbia na fedha zilizotolewa na serikali kwa ajili ya kusaidia wasanii, hali iliyoibua mgogoro mkubwa kati yao. Kenzo anasema fedha hizo zilipaswa kuwafikia wasanii wengi, lakini kulikuwa na njama za kuzimiliki kinyume na makubaliano. Ikumbukwe kuwa Eddy Kenzo na Bebe Cool wamekuwa kwenye timu moja ya kampeni ya Rais Yoweri Museveni, wakishiriki katika shughuli mbalimbali za kuhamasisha vijana na wasanii kumuunga mkono kiongozi huyo. Hata hivyo, inadaiwa kuwa uhusiano wao ulianza kuyumba baada ya fedha zilizotolewa na serikali kwa wasanii kuibua mvutano, kila upande ukituhumiana kukosa uwazi na uaminifu.

Read More
 Eddy Kenzo Apendekeza Makaburi Maalum kwa Wasanii ili Kuhifadhi Urithi Wao

Eddy Kenzo Apendekeza Makaburi Maalum kwa Wasanii ili Kuhifadhi Urithi Wao

Msanii nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, amependekeza wazo la kujengwa kwa makaburi maalum kwa wasanii na wabunifu (creatives) kama njia ya kuhifadhi na kuheshimu urithi wao hata baada ya kifo. Akizungumza wakati wa ibada ya kuaga mwili wa mama mzazi wa msanii Fik Fameica, Kenzo amesema wasanii wengi hutoa mchango mkubwa katika jamii kupitia sanaa, muziki na ubunifu wao, lakini mara nyingi historia na kazi zao husahaulika wanapofariki. Hitmaker huyo Sitya Loss, amesema kuwepo kwa makaburi maalum kutasaidia kuhifadhi kumbukumbu zao, kuenzi mchango wao na kuwapa heshima wanayostahili. Kwa mujibu wa Kenzo, wazo hilo halilengi kuwa sehemu ya mazishi pekee, bali pia kuwa kituo cha kihistoria kitakachoonyesha wasifu, mafanikio na safari za kisanaa za wasanii kutoka fani mbalimbali kama muziki, filamu na sanaa za ubunifu.

Read More
 Eddy Kenzo Aemtolea Uvivu Bebe Cool Kufuatia Kauli Zake za Kuwazuia Wasanii

Eddy Kenzo Aemtolea Uvivu Bebe Cool Kufuatia Kauli Zake za Kuwazuia Wasanii

Msanii nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, amemtolea uvivu mkongwe Bebe Cool baada ya madai ya awali kuwa ana uwezo wa kuzuia nyimbo za wasanii fulani kuchezwa kwenye TV na redio. Akihojiwa na chombo kimoja cha habari, Kenzo amesema wazi kuwa hakuna mtu anayeweza kuzizuia baraka zake, akisisitiza kuwa mafanikio yake hayategemei mtu binafsi. Amesema dunia imeumbwa kwa ajili ya kila mtu, na hakuna yeyote aliye na mamlaka ya kuzuia safari yake ya muziki. Kenzo amesema wazi kuwa madai ya Bebe Cool hayana uzito wowote kwake, akiongeza kuwa hatua kama hizo ziliwahi kujaribiwa dhidi yake miaka kadhaa iliyopita lakini hazikuweza kumsimamisha kupaa kimataifa. Kwa sasa, mashabiki na wadau wa muziki wanaendelea kufuatilia kwa makini matamshi ya pande zote mbili, wakisubiri kuona iwapo mvutano huu utazaa maelewano, malumbano mapya, au mwelekeo mpya kwenye tasnia ya burudani nchini Uganda.

Read More
 Eddy Kenzo Aahidi Mabadiliko Makubwa Kwa Wasanii Uganda

Eddy Kenzo Aahidi Mabadiliko Makubwa Kwa Wasanii Uganda

Staa wa muziki kutoka Uganda, Eddy Kenzo, ameibua matumaini mapya kwa wasanii baada ya kutangaza kuwa serikali imeipa kipaumbele marekebisho ya sheria ya hakimiliki ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu. Kenzo ambaye ni rais wa shirikisho la wasanii nchini Uganda, amesema kuwa muswada huo utashughulikiwa mara tu Bunge la mwaka 2026 litakapoketi rasmi kuanza kazi. Kwa mujibu wa Kenzo, mfumo mpya wa usimamizi wa hakimiliki tayari umeidhinishwa, na kilichosalia sasa ni kutoa elimu kwa wadau ili utekelezwe kikamilifu. Amebainisha kuwa serikali, ikiwemo Rais Yoweri Museveni, imeamua kulipa suala hilo uzito wa juu kwa manufaa ya tasnia nzima ya muziki. Hata hivyo amewataka wasanii na wadau wa burudani kuendelea kumuunga mkono Rais Museveni katika uchaguzi ujao, akisisitiza kuwa mabadiliko yanayotarajiwa kwenye sheria mpya za hakimiliki yatawaletea fursa bora za kifedha na kulinda kazi zao dhidi ya wizi wa kimtandao. Hatua hii imeonekana kama mwanga wa matumaini kwa wanamuziki na watayarishaji wa muziki nchini Uganda, ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakipigania mfumo madhubuti wa kulinda haki zao za kiubunifu.

Read More
 Eddy Kenzo Adai Chama cha NUP Kimepoteza Umaarufu Uganda

Eddy Kenzo Adai Chama cha NUP Kimepoteza Umaarufu Uganda

Msanii nyota wa Uganda, Eddy Kenzo, ameibua mjadala mpya baada ya kudai kuwa chama cha National Unity Platform (NUP) kimepoteza umaarufu mkubwa nchini Uganda ikilinganishwa na siku za awali za vuguvugu la People Power. Akizungumza katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini humo, msanii huyo ameweka wazi kuwa wanachama wengi wa NUP wanakata tamaa kwa kile alichokitaja kama kukosekana kwa mwelekeo thabiti ndani ya chama. Amesema kuwa hali hiyo imechochea baadhi ya wanachama kujiondoa na kujiunga na makundi mengine ya kisiasa kutokana na kukerwa na mwenendo wa chama. Kwa mujibu wa Kenzo, vuguvugu lililowahi kushika kasi kubwa nchini Uganda sasa limeporomoka, na anaamini uongozi wa NUP unapaswa kumfikia ili kupata ushauri wa kurejesha tena nguvu na uungwaji mkono wa kitaifa aliohudai aliuchangia kuuanzisha. Ingawa ameendelea kukosoa chama hicho ambacho kinaongozwa na Bobi Wine, NUP bado kinabaki kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Uganda, wakati taifa hilo likijiandaa kuelekea uchaguzi mkuu wa Januari 2026.

Read More
 Eddy Kenzo Afunguka Sababu ya Kukataa Mikataba Kubwa ya Muziki

Eddy Kenzo Afunguka Sababu ya Kukataa Mikataba Kubwa ya Muziki

Mwanamuziki nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, amefunguka kuhusu sababu za kukataa kusaini mikataba na kampuni kubwa za muziki duniani, zikiwemo Sony Music na Universal Music Group. Kenzo, ambaye ni miongoni mwa wasanii waliotukuka zaidi nchini Uganda na mwenye tuzo kama BET Award pamoja na uteuzi kadhaa wa Grammy, amesema amepewa ofa nyingi lakini amezikataa kwa makusudi licha ya mafanikio yake ya kimataifa. Akipiga stori na kituo kimoja cha habari, Kenzo amesema lebo kubwa mara nyingi huwabana wasanii kama gereza, na kuwanyima uhuru wa kufanya maamuzi ya kibunifu. Anadai kuwa kampuni hizo hutanguliza maslahi ya kibiashara kuliko ustawi wa msanii. Kenzo pia ametaja kuwa ameshuhudia mifano ya wasanii waliopitia wakati mgumu chini ya mikataba ya muda mrefu na lebo kubwa, akisema wengine hupoteza mwelekeo au kupungua kwa ubunifu. Hitmaker huyo wa Nsimbudde, anasisitiza kuwa kujitegemea kumempa nafasi ya kujiamulia mambo muhimu bila shinikizo, na kumwezesha kuendelea kujijenga kimataifa kwa njia anayoiona bora kwake.

Read More
 Eddy Kenzo Awakilisha Afrika Mashariki Kwenye Tuzo za Grammy 2026

Eddy Kenzo Awakilisha Afrika Mashariki Kwenye Tuzo za Grammy 2026

Nyota wa muziki kutoka Uganda, Eddy Kenzo, ameweka historia kwa kuwa mwakilishi pekee wa Afrika Mashariki kwenye tuzo za Grammy mwaka 2026. Kenzo amechaguliwa kuwania kipengele cha Best African Music Performance kupitia wimbo wake “Hope & Love” aliomshirikisha mwanamuziki na mtayarishaji maarufu wa vyombo vya muziki, Mehran Martin. Wimbo huo unamenyana na nyimbo kubwa kutoka kwa mastaa wa Afrika wakiwemo Burna Boy kupitia “Love”, Davido na Omah Lay kwa “With You”, Ayra Starr na Wizkid kupitia “Gimme Dat”, pamoja na Tyla kupitia “Push 2 Start”. Tuzo hizo za Grammy 2026 zimeonekana kuwa na ushindani mkubwa zaidi katika kipengele hicho, zikionyesha jinsi muziki wa Afrika unavyozidi kupata kutambulika kimataifa. Sherehe za utoaji wa tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika Los Angeles, California, mwaka 2026, na Eddy Kenzo ameonyesha kuwa muziki wa Afrika Mashariki una nafasi kubwa kwenye jukwaa la kimataifa.

Read More
 Eddy Kenzo Asema Hatatetereka Kwa Propaganda na Chuki

Eddy Kenzo Asema Hatatetereka Kwa Propaganda na Chuki

Staa wa muziki kutoka nchini Uganda, Eddy Kenzo, amewajibu vikali wakosoaji wake baada ya kujipata katika malumbano ya kisiasa na kijamii kufuatia ushiriki wake katika uzinduzi wa albamu ya Rais Yoweri Museveni na kampeni za chama tawala cha NRM. Kwenye mahojiano yake na kituo kimoja cha redio nchini humo, Kenzo amesema hatatishwa na propaganda wala chuki kutoka kwa wale wanaopinga mafanikio yake, akisisitiza kuwa ataendelea kufanya kazi kwa bidii kuendeleza sekta ya muziki wa Uganda. Msanii huyo, ambaye ni mwenyekiti wa Uganda National Musicians Federation (UNMF), amesema ataendelea kusimamia umoja na maendeleo ya wasanii wote bila kubagua, akisisitiza kuwa mafanikio yake hayatatetereka kwa sababu ya chuki au upotoshaji. Hata hivyo, hatua yake ya kushirikiana kwa karibu na serikali imezua chuki kutoka kwa baadhi ya wasanii na mashabiki wanaomuona kama msanii anayependelea chama tawala na kuwapuuza wasanii wakubwa katika tasnia ya muziki. Wengine wameenda mbali zaidi na kumtuhumu kwa kuwapendelea wasanii fulani chini ya UNMF, jambo linalochochea zaidi ukosoaji na propaganda dhidi yake.

Read More
 Eddy Kenzo Aapa Kuchukua Hatua za Kisheria Dhidi ya Promota Nobart

Eddy Kenzo Aapa Kuchukua Hatua za Kisheria Dhidi ya Promota Nobart

Msanii nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, ametangaza mpango wa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya promota wa matukio nchini humo Nobart, kufuatia madai mazito ya mauji yaliyotolewa dhidi yake hivi karibuni. Kenzo, ambaye pia ni mshauri wa rais kuhusu masuala ya muziki, amekanusha vikali madai ya kuhusika na mauji ya msanii chipukizi akiyataja kuwa ya uongo na yenye lengo la kumchafua. Amesema tayari amewasiliana na mawakili wake ili kumshtaki Nobart mahakamani kwa kashfa na uongo wa kuhatarisha heshima yake. Amesisitiza kwamba promota huyo atalazimika kuthibitisha madai yake mbele ya mahakama kwa kuwa ameyasema hadharani, akiongeza kuwa suala hilo ni zito kwa kuwa linahusu maisha ya watu na sifa ya wasanii nchini Uganda. Kwa mujibu wa Kenzo, madai hayo yameathiri jina lake binafsi, heshima yake, na uhusiano wake na wadau wa muziki na siasa. Mwishoni mwa wiki, promota huyo aliibua gumzo kubwa baada ya kudai kwamba rais wa Shirikisho la Wasanii wa Uganda (UNMF), Eddy Kenzo, alihusika katika kifo cha msanii marehemu Danz Kumapeesa, na hata kufikia hatua ya kutaka kumuua yeye binafsi.

Read More
 Eddy Kenzo afafanua dhamira ya albamu ya kumshukuru Rais Museveni

Eddy Kenzo afafanua dhamira ya albamu ya kumshukuru Rais Museveni

Rais wa shirikisho la wanamuziki nchini Uganda, Eddy Kenzo, amefunguka kuhusu ukosoaji unaoendelea baada ya baadhi ya watu kudai kuwa Kenzo na wasanii wenzake walinufaika kifedha kupitia ushiriki wao katika albamu ya muziki ya kusifu uongozi wa Rais Yoweri Museveni, Akizungumza Tiktok Live, Kenzo amesema hakuna msanii aliyelipwa kushiriki kwenye albamu hiyo, akieleza kuwa walifanya kazi hiyo kwa hiari kama zawadi kwa Rais Museveni wakimshukuru kutokana na mchango wake katika sekta ya muziki na taifa kwa jumla. Msanii huyo, amefafanua kuwa yeye na wasanii wenzake walishiriki katika mradi huo kwa nia ya kuonyesha shukrani kwa amani na uhuru ambao Rais amesaidia kuleta katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki. Kwa sasa, albamu hiyo inaendelea kujadiliwa kwenye mitandao ya kijamii, baadhi ya wananchi wakiiona kama ishara ya uzalendo, huku wengine wakiiita propaganda ya kisiasa

Read More
 Eddy Kenzo Awazuia Wasanii wa NUP Kupata Msaada

Eddy Kenzo Awazuia Wasanii wa NUP Kupata Msaada

Rais wa Shirikisho la Wanamuziki nchini Uganda, Eddy Kenzo, amezua gumzo baada ya kutangaza kuwa wasanii wanaoegemea chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) kinachoongozwa na Bobi Wine, hawatakuwa miongoni mwa wanaonufaika na msaada wa kifedha kutoka kwa shirikisho hilo. Kenzo amesema kuwa licha ya baadhi ya viongozi wa juu wa shirikisho, kama vile Pallaso ambaye ni naibu wake, kuwa wafuasi wa NUP, hawataendelea kupata ufadhili wowote kwa kuwa fedha zinazotumika zinatoka kwa serikali inayoongozwa na chama cha NRM. Kwa mujibu wake, shughuli za shirikisho zinafadhiliwa na serikali ya NRM na hivyo haitakuwa sahihi kutoa fedha kwa wasanii wanaopinga sera za serikali. Hata hivyo baadhi ya wasanii wameonyesha kutoridhishwa na kauli ya Kenzo, wakidai kuwa shirikisho hilo la sanaa linapaswa kuwa taasisi huru inayowatumikia wanamuziki wote bila kujali misimamo yao ya kisiasa

Read More