Eddy Kenzo: Lugha Sio Kizuizi kwa Mafanikio ya Muziki wa Kimataifa

Eddy Kenzo: Lugha Sio Kizuizi kwa Mafanikio ya Muziki wa Kimataifa

Msanii nyota kutoka Uganda, Eddy Kenzo, amesema kuwa lugha haipaswi kuwa kikwazo kwa wasanii wanaotamani kupata mafanikio ya kimataifa katika tasnia ya muziki. Akizungumza katika mahojiano yake hivi karibuni, Kenzo alisisitiza kuwa muziki ni lugha ya kipekee inayovuka mipaka ya maneno na kueleweka na watu wa mataifa tofauti duniani. Eddy Kenzo, ambaye alitambulika kimataifa kupitia kibao chake Sitya Loss, alisema kuwa watu wengi hawakuelewa maneno ya wimbo huo, lakini waliweza kuupenda na kucheza kwa hisia, jambo linalothibitisha kuwa hisia na midundo vinaweza kuunganishwa na hadhira ya aina yoyote. Kenzo, anawahimiza wasanii wa Kiafrika kujiamini na kuendeleza utamaduni wao kupitia sanaa, bila kujaribu kubadilisha lugha yao kwa ajili ya soko la kimataifa. Anasema kuwa dunia sasa iko tayari kukumbatia utofauti wa kitamaduni na kisanaa kutoka barani Afrika. Kauli yake inakuja wakati muziki wa Afrika unazidi kuvuma duniani kupitia majina makubwa kama Burna Boy, Diamond Platnumz, Tyla, na Ayra Starr, ambao baadhi yao pia wanatumia lugha za asili katika nyimbo zao.

Read More
 Eddy Kenzo Akerwa na Malipo ya Diamond Platnumz Katika Mbio za Coffee Marathon

Eddy Kenzo Akerwa na Malipo ya Diamond Platnumz Katika Mbio za Coffee Marathon

Mwanamuziki nyota wa Uganda, Eddy Kenzo, ameeleza masikitiko makubwa dhidi ya waandaaji wa Coffee Marathon kwa kumpa kipaumbele msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz, badala ya kuwatambua na kuwaunga mkono wasanii wa ndani ya nchi. Katika mahojiano aliyofanya na kituo cha televisheni cha ndani mapema wiki hii, Kenzo alieleza kusikitishwa kwake na taarifa kuwa Diamond alilipwa shilingi milioni 750 za Uganda kwa kushiriki katika tamasha hilo, kiasi anachokiona kuwa ni kikubwa mno, hasa ikizingatiwa kuwa wasanii wa Uganda wamekuwa wakipuuzwa kwenye matukio ya kitaifa. Katika hatua nyingine, alikosoa maisha ya kifahari aliyotengewa msanii huyo kutoka Tanzania huku wasanii wa Uganda wakiachwa bila msaada au kutambuliwa.  Kenzo amesisitiza kuwa hawezi kuiga chochote kutoka kwa Diamond Platnumz licha ya shinikizo zinazotolewa na Waganda kuwa wasanii wao wanapaswa kuboresha chapa zao na muonekano wao wa kisanii ili kuendana na nyakati zilizopo. “Mimi siwezi kuiga chochote kutoka kwa Diamond Platnumz. Hayo mambo wanayosema kuhusu chapa na kila kitu, siwezi kuwa hivyo. Siwezi kuanza kuvaa minyororo ya dhahabu ishirini, malezi yangu hayakuniandaa kwa hilo. Siwezi kuishi maisha ya kifahari wakati watoto wa Ghetto wanateseka. Bora nitumie pesa hizo kuboresha maisha yao,” alisema Kenzo katika mahojiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Uganda. Diamond Platnumz na Eddy Kenzo wanachukuliwa kuwa miongoni mwa wasanii wakubwa zaidi wa Afrika Mashariki kimataifa. Hata hivyo, Kenzo anaonekana kuwa mbele katika upande wa tuzo za kimataifa alizoshinda, ikiwemo uteuzi wake wa kihistoria katika Tuzo za Grammy.

Read More
 Eddy Kenzo Apuzilia Mbali Madai ya Bebe Cool ya Kudhibiti Muziki

Eddy Kenzo Apuzilia Mbali Madai ya Bebe Cool ya Kudhibiti Muziki

Msanii nyota wa Uganda, Eddy Kenzo, ameibuka na kauli kali dhidi ya madai ya Bebe Cool kwamba yeye hudhibiti namna nyimbo zinavyopigwa kwenye redio na runinga nchini humo. Kenzo, ambaye ni miongoni mwa wasanii waliofanikiwa kimataifa kutoka Afrika Mashariki, amesema Bebe Cool hana ushawishi mkubwa kama anavyodai. “Bebe Cool hana uwezo wa kudhibiti airplay kama anavyodhani. Sisi tulipata mafanikio makubwa wakati yeye bado yupo kwenye tasnia, kwa hiyo kauli zake hazina uzito wowote,” alisema Kenzo katika mahojiano na msanii Vampino. Kauli hii ni majibu ya moja kwa moja kwa matamshi ya Bebe Cool aliyotoa mwezi Aprili, ambapo alijisifu kuwa ana ushawishi mkubwa kwenye vituo vya habari na anaweza kuzuia wimbo wowote usipigwe Uganda. “Mimi si rafiki tu wa DJs, bali pia wa wamiliki wa vituo vya redio na TV. Naweza kuamua wimbo gani usipigwe popote nchini,” alisema Bebe Cool awali, akidai wasanii wachanga wanafaa kumheshimu kama mlezi wa tasnia. Lakini kwa Eddy Kenzo, mafanikio hayatokani na upendeleo au vitisho vya watu maarufu bali kutokana na bidii, kipaji na kujituma kwa msanii binafsi. “Wasanii wapya wasihangaike na matamshi kama haya. Wajikite kwenye kazi yao. Mafanikio hayaletiwi na maneno ya mtu bali kazi nzuri,” alisisitiza Kenzo. Bifu hili la kauli kati ya mastaa hawa wawili linaashiria mvutano mkubwa wa ushawishi ndani ya tasnia ya muziki nchini Uganda, huku mashabiki wakigawanyika kati ya kuunga mkono upande wa Kenzo au Bebe Cool. Lakini kwa sasa, Kenzo ameweka wazi msimamo wake kwamba hana muda wa kuendekeza maneno yasiyo na msingi.

Read More
 Eddy Kenzo Ataka Mazungumzo ya Amani na Azawi Kuondoa Mvutano wa Kisiasa

Eddy Kenzo Ataka Mazungumzo ya Amani na Azawi Kuondoa Mvutano wa Kisiasa

Msanii maarufu wa Uganda na Rais wa Umoja wa Wasanii (Uganda National Musicians Federation), Eddy Kenzo, ametangaza nia ya kuanzisha mazungumzo ya wazi na msanii mwenzake Azawi, ili kutatua tofauti zao za kisiasa ambazo zimeibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wanamuziki nchini humo. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Kenzo amesema kuwa tofauti hizo hazipaswi kuendelezwa kwa njia ya mivutano ya mitandaoni bali kupitia mazungumzo ya moja kwa moja na ya wazi, akibainisha kuwa anathamini mchango wa Azawi katika tasnia na anataka suluhisho la kudumu. “Kama viongozi wa sanaa, ni jukumu letu kuonyesha mfano. Ningependa tuketi na kuzungumza hadharani ili tuweze kuelewana na kusaidia kuunganisha tasnia yetu,” alisema Kenzo. Wito huo wa Kenzo umepokelewa kwa hisia mseto mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakipongeza hatua hiyo kama ishara ya utu uzima na uongozi wa kweli, huku wengine wakimtaka aonyeshe vitendo zaidi badala ya maneno. Kwa sasa, bado haijajulikana iwapo Azawi atakubali mwaliko huo wa mazungumzo ya hadharani, lakini mashabiki wengi wana matumaini kwamba tofauti hizo zitatatuliwa kwa njia ya amani na kwa manufaa ya sekta ya muziki nchini Uganda. Taarifa hii inakuja baada ya Azawi kumkosoa hadharani mara kadhaa, akimtuhumu Kenzo kwa kushindwa kutumia nafasi yake ya uongozi kutetea masilahi ya wasanii na raia wa Uganda kwa ujumla. Azawi amekuwa akieleza kuwa Kenzo amekuwa kimya katika masuala muhimu yanayohitaji sauti ya msanii mwenye ushawishi kama yeye.

Read More
 Eddy Kenzo Kutatua Mgogoro wa Ofisi za UMA Zilizofungwa kwa Madeni

Eddy Kenzo Kutatua Mgogoro wa Ofisi za UMA Zilizofungwa kwa Madeni

Rais wa Shirikisho la Wanamuziki Uganda (UNMF) na mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Uganda katika masuala ya ubunifu, Eddy Kenzo, ameahidi kuingilia kati na kusaidia Chama cha Wanamuziki Uganda (UMA) kurejeshewa ofisi zake zilizofungwa kutokana na deni la kodi. Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga nchini humo, Kenzo amesema hatua hiyo inalenga kutunza heshima ya taasisi ya UMA ambayo, kwa mujibu wake, imekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya muziki nchini Uganda kabla ya kuanzishwa kwa UNMF. “Hatuwezi kuwaacha katika hali hii. UMA walifanya kazi kubwa kabla sisi hatujaja. Tutaingilia kati na kuona namna ya kuhakikisha ofisi zao zinafunguliwa tena,” alisema Kenzo katika mahojiano na kituo cha televisheni cha ndani. Kauli yake imekuja kufuatia hatua ya Kituo cha Kitaifa cha Utamaduni cha Uganda (UNCC), kinachomiliki jengo la National Theatre, kufunga rasmi ofisi za UMA kwa kile kilichoelezwa kuwa malimbikizo ya kodi ya karibu mwaka mmoja. Hatua hiyo imeathiri moja kwa moja uendeshaji wa shughuli za chama, huku ofisi za viongozi wakuu kama Cindy Sanyu (Rais wa UMA) na Phina Masanyalaze (Katibu Mkuu) zikiwa zimefungwa na kuwekewa zuio la kuingia. UMA, chini ya Cindy, imekuwa ikikosoa waziwazi uongozi wa UNMF na haswa Kenzo, huku mvutano kati yao ukijidhihirisha mara kadhaa katika majukwaa ya umma. Hata hivyo, Kenzo amechukua hatua ya kukutana na viongozi husika ili kushughulikia suala hilo kwa njia ya amani, akisema huu si wakati wa kutazama tofauti bali kushikamana kwa maslahi ya wanamuziki wote nchini Uganda. Sakata hili linaendelea kuwavutia wadau wengi wa sekta ya burudani nchini Uganda, huku wengi wakisubiri kuona ikiwa hatua ya Kenzo itazaa matunda na kumaliza mgogoro unaoathiri ustawi wa chama kongwe cha wanamuziki nchini.

Read More
 Nina Roz Afichua Sababu za Kujiondoa UNMF, Amsuta Vikali Eddy Kenzo kwa Kuwa Mbinafsi

Nina Roz Afichua Sababu za Kujiondoa UNMF, Amsuta Vikali Eddy Kenzo kwa Kuwa Mbinafsi

Mwanamuziki maarufu na mwanasiasa chipukizi, Nina Roz, ameibua mjadala mpya katika tasnia ya muziki nchini Uganda baada ya kufichua sababu zilizomfanya kujiondoa kwenye Shirikisho la Kitaifa la Wanamuziki nchini humo (UNMF) Katika mahojiano aliyofanya hivi karibuni na vyombo vya habari, Nina Roz alieleza kuwa walibuni shirikisho hilo pamoja na  Eddy Kenzo kwa madhumuni ya kuwatetea wasanii, kusimamia haki zao, na kuendeleza ustawi wa sekta ya muziki nchini Uganda. Hata hivyo, alidai kuwa hali hiyo ilianza kubadilika muda mfupi baada ya kuanzishwa kwa shirikisho hilo mwaka 2023.  “Nilidhani tunaunda jukwaa la kweli la kuwaunganisha wasanii na kuwatetea, lakini baadaye nikabaini kuwa viongozi, hususan Eddy Kenzo, walikuwa na maslahi binafsi pamoja na ajenda za kisiasa ambazo hazikuwiana na malengo ya awali,” alisema Nina Roz. Nina, ambaye aliwahi kushika wadhifa wa kusimamia masuala ya maadili ndani ya UNMF, alieleza kuwa shirikisho hilo lilianza kupoteza dira na kuonyesha ukaribu usiofaa na serikali. Kwa maoni yake, hali hiyo ilikuwa kinyume na misingi ya uhuru wa kujieleza na uhuru wa kisanii. Tangu kujiondoa kwake, Nina Roz amekuwa mkosoaji wa wazi wa shirikisho hilo, akilituhumu kwa kile alichokitaja kuwa ni siasa za upendeleo katika tasnia ya muziki. Anadai kuwa wasanii wanaoonekana kukosoa serikali wamekuwa wakibaguliwa katika upatikanaji wa fursa, mikataba, na msaada kutoka kwa taasisi hiyo. “UNMF haikuwakilisha tena maslahi ya wasanii wote. Iligeuka kuwa jukwaa la upande mmoja, ambapo wale waliokuwa karibu na serikali ndio walipewa kipaumbele,” aliongeza. Kwa sasa, Nina Roz anajiunga na orodha ya wasanii wakubwa kama King Saha, Ziza Bafana, na Spice Diana, ambao wote wamejitenga na UNMF, wakieleza kutoridhishwa  na namna taasisi hiyo inaendeshwa.

Read More
 Eddy Kenzo ajibu madai ya Bebe Cool kuwa amebebwa na bahati kwenye muziki

Eddy Kenzo ajibu madai ya Bebe Cool kuwa amebebwa na bahati kwenye muziki

Nyota wa muziki nchini Uganda Eddy Kenzo amejibu madai ya Bebe Cool kuwa bahati ndio imembeba kwenye muziki. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Kenzo amesema Bebe Cool anatumia madai hayo kujifariji huku akidai kuwa bidii ndio imempa mafanikio makubwa kwenye muziki wake kwa miaka 10 na sio bahati kama namna ambavyo Bosi huyo wa Gagamel anavyodai. Hitmaker huyo wa “Nsimbudde” amesema Bebe Cool anapaswa kukubali kuwa ameacha alama kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda badala ya kuwahada mashabiki na taarifa za uongo. “Bebe Cool alisema nina bahati kwa sababu alitaka kujifariji. Huwezi kuwa na bahati milele, najua ninachofanya na nimestahili kile nilichonacho. Anapaswa kukubali na kuwaambia watu wake kwamba Kenzo amefanya muziki kwa zaidi ya miaka 10 na anafahamu hilo,” alisema Eddy Kenzo. Kauli ya Eddy Kenzo inakuja mara baada ya Bebe Cool kuachia orodha ya wasanii waliofanya vizuri mwaka 2022 ambapo alimtaja Kenzo kama msanii aliyebebwa na bahati kwenye muziki.

Read More
 Bebe Cool Alinisaidia Kupata Mawakili katika kesi dhidi ya Luba Events – Eddy Kenzo

Bebe Cool Alinisaidia Kupata Mawakili katika kesi dhidi ya Luba Events – Eddy Kenzo

Msanii Eddy Kenzo amekiri kwamba Bebe Cool alimsaidia kuondokana na kesi iliyokuwa ikimuandama kutoka kwa Luba Events. Katika mahojiano yake hivi karibuni, Kenzo amesema Bebe Cool alimuunganisha na mawakili walioshughulikia kesi yake dhidi ya promota huyo. “Alinipigia simu na kuniuliza anawezaje kusaidia. Hakutaka kuniona nikiwa kwenye matatizo. Ni rafiki wa kweli,” alisema. Utakumbuka Luba Events alimburuza mwimbaji huyo wa ‘Tweyagale’ mahakamani Novemba mwaka 2022 baada ya tamasha la ‘Eddy Kenzo’ kufanya vizuri, akimtuhumu kuvunja mkataba wa kuandaa Tamasha hilo. Luba alieleza kuwa alipata hasara ya takriban shillingi millioni 9 ambayo aliwekeza katika tamasha hilo mwaka 2020. Kenzo alipigwa marufuku kwa muda kutumbuiza jijini Kampala kabla ya marufuku hiyo kuondolewa na mahakama. Utakumbuka Eddy Kenzo na Bebe Cool walianza kuwa marafiki baada ya Kenzo kuwa karibu na chama cha NRM, mrengo wa kisiasa ambao Bebe Cool anaunga mkono.

Read More
 Eddy Kenzo sio gwiji wa muziki – Bebe Cool

Eddy Kenzo sio gwiji wa muziki – Bebe Cool

Msanii Bebe Cool amedai kwamba Eddy Kenzo hana vigezo vya kuitwa lejendari kwenye tasnia ya muziki nchini Uganda. Kwenye mahojiano hivi karibuni amesema hitmaker huyo wa “Nsimbudde” ana mengi ya kufanya kwenye muziki kama kweli anataka kufikia hadhi ya kuitwa nguli. Bosi huyo wa Gagamel anasema Eddy Kenzo ni msanii mwenye bahati tu na anaweza kushinda tuzo ya Grammy mwaka 2023. “Eddy Kenzo ni mwanamuziki mzuri lakini hajavuka mstari wa kuitwa nguli, hata kwa tuzo alizoshinda. Inabidi atie bidii zaidi ili kufikia viwango vya Chameleone, Bobi Wine, na mimi mwenyewe. Sio tu kwa nyimbo na tuzo,” alisema. Utakumbuka juzi kati, Bebe Cool alitoa orodha yake ya kila mwaka ya wasanii waliofanya vizuri mwaka 2022. Bebe Cool aliwataja wanamuziki anaoamini wamepata hadhi ya kuitwa malejendari kwenye kiwanda cha muziki nchini Uganda. Kwenye orodha hiyo aliwataja; Jose Chameleone, Bobi Wine, Afrigo Band, na Maddox Sematimba huku akisisitiza kuwa wanaweza kukaa bila kutoa wimbo mkali kwa miaka mingi ijayo kutokana nyimbo zisizochuja walizoziachia miaka ya hapo nyuma.

Read More
 Mahakama yatupilia mbali kesi iliyowasilishwa na Luba Events dhidi ya msanii Eddy Kenzo

Mahakama yatupilia mbali kesi iliyowasilishwa na Luba Events dhidi ya msanii Eddy Kenzo

Mwimbaji kutoka nchini Uganda Eddy Kenzo ana kila sababu ya kutabasamu baada ya mahakama kutupilia mbali kesi iliyowasilishwa na  Luba Events kumzuia kutumbuiza jijini Kampala. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Kenzo amewataarifu mashabiki zake kuwa ameruhusiwa tena kutumbuiza jijini Kampala kufuatia kesi ya Luba Events kukosa ushahidi wa kutosha mahakamani. Kenzo ambaye kwa sasa yupo nchini Marekani kwa ajili ya tuzo za Grammy aliwakilishwa mahakamani na mawakili wake Kabega Musa, pamoja na Faisal Balikurungi. Mnamo Novemba, Eddy Kenzo alipigwa marufuku kutumbuiza jijini Kampala baada ya promota Moses Lubuulwa wa Luba Events kumburuza mahakamani kwa kukiuka mkataba wa kuandaa tamasha la “Eddy Kenzo Festival” lililomalizika hivi karibuni. Luba alieleza kuwa Eddy Kenzo alimsaliti aliposhindwa kumhuisha kwenye mandalizi ya tamasha hilo licha ya kumlipa fedha za kufanya ziara za “Eddy Kenzo Festival” katika maeneo mbalimbali nchini Uganda ikiwemo Masaka, Bundibujo na maeneo mengine. Hata hivyo alifichua kwamba alipata hasara ya kiasi cha Kshs, million 27 alipoandaa Tamasha la Eddy Kenzo mwaka 2020 ambalo halikufanyika kwa sababu ya Covid 19.

Read More
 Eddy Kenzo agoma kuingia makubaliano na promota wa Uganda Luba Events

Eddy Kenzo agoma kuingia makubaliano na promota wa Uganda Luba Events

Bosi wa Big Talent, Msanii Eddy Kenzo anaonekana kutofurahishwa na kesi dhidi yake kwamba alivunja mkataba alioingia na Luba Events ya kufanya show ya pamoja. Siku ya Jumatatu, Kenzo aliitwa na polisi wa CPS Kampala kujadiliana na Luba Events juu ya jinsi wanavyoweza kutatua tofauti zao lakini hakujitokeza. Luba anataka Kenzo amfidie pesa alizowekeza katika kuandaa tamasha la Eddy Kenzo mnamo 2020 kabla ya kufutiliwa mbali kwa sababu ya Covid-19. Kulingana na mwakilishi kutoka Luba Events, Polisi watatekeleza kwa ufanisi agizo la mahakama linalomzuia Kenzo kutumbuiza jijini Kampala. Ikumbukwe kwamba Kenzo hivi karibuni alifanya tamasha lake katika Uwanja wa Ndege wa Kololo bila kumhusisha Luba Events.

Read More
 Nitawaunganisha wasanii wa Uganda na waandaaji wa Grammy -Eddy Kenzo

Nitawaunganisha wasanii wa Uganda na waandaaji wa Grammy -Eddy Kenzo

Mwanamuziki Eddy Kenzo ameahidi kuwaunganisha wanamuziki wengine wa Uganda na waandaaji wa tuzo za Grammy pindi atakapohudhuria hafla ya utoaji wa tuzo hizo mwakani nchini marekani. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni, Kenzo amebainisha kuwa kuteuliwa kwenye tuzo za Grammy 2023 itawafungulia milango wasanii wengi nchini humo kuupeleka muziki wao kimataifa na kushiriki tuzo kubwa duniani . “Nataka kwenda Marekani na kukutana na watu hawa. Nataka kuwajua ili niweze kuwaunganisha na wanamuziki wa Uganda. Nataka kufungua mlango kwa kila mtu,” alisema Eddy Kenzo. Eddy Kenzo ametajwa kuwania Tuzo za Grammy mwaka 2023 kupitia kipengele cha Best Global Music Performance na wimbo wake ‘Gimme Love’ aliomshirikisha Matt B.

Read More