Jose Chameleone Kuzindua Chameleone FM Bujumbura

Jose Chameleone Kuzindua Chameleone FM Bujumbura

Mwanamuziki mkongwe kutoka nchini Uganda, Jose Chameleone, anatarajiwa kuzindua kituo kipya cha redio jijini Bujumbura, Burundi, kitakachoitwa Chameleone FM. Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya karibu na msanii huyo, Chameleone amenunua kituo cha zamani cha Black FM, ambacho sasa kinatarajiwa kuanza upya chini ya jina jipya la Chameleone FM, hatua inayolenga kuimarisha uwepo wake katika sekta ya vyombo vya habari nchini Burundi. Mbali na uwekezaji huo wa redio, ripoti zinaeleza kuwa Chameleone pia yupo katika hatua za mwisho za kufungua hospitali aliyoijenga katika eneo la Cankuzo. Inadaiwa kuwa mradi huo ni sehemu ya juhudi zake za kurudisha fadhila kwa wananchi wa Burundi kupitia huduma za kijamii, hususan katika sekta ya afya. Hatua hizi za uwekezaji zinakuja baada ya ziara ya Chameleone nchini Burundi, ambapo mwishoni mwa mwaka jana alikutana na Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye. Katika kikao hicho, msanii huyo alieleza dhamira yake ya kuwekeza nchini humo na kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Read More
 Jose Chameleone Adhimisha Mwaka Mmoja Tangu Kuugua Kwa Kushukuru Familia, Marafiki na Mashabiki

Jose Chameleone Adhimisha Mwaka Mmoja Tangu Kuugua Kwa Kushukuru Familia, Marafiki na Mashabiki

Msanii nguli wa muziki kutoka Uganda, Jose Chameleone, ameadhimisha mwaka mmoja tangu alipougua na kulazwa kwa muda mrefu, tukio ambalo liliwagusa mashabiki na wadau wengi wa muziki Afrika Mashariki. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Chameleone amesema kuwa siku kama ya leo mwaka mmoja uliopita alikuwa amelazwa kitandani akipambania maisha yake. Ameeleza kuwa kipindi hicho kilikuwa kigumu, lakini kilibadilika kuwa cha matumaini kutokana na msaada mkubwa alioupata kutoka kwa familia, marafiki na mashabiki. Msanii huyo ameeleza kuwa maombi, ujumbe wa faraja, simu pamoja na ziara kutoka kwa watu mbalimbali vilimpa nguvu na matumaini yaliyomsaidia kuvuka kipindi hicho kigumu. Chameleone amesema kuwa bila mchango wa wadau wote, asingefikia hatua alipo sasa kiafya. Amehitimisha ujumbe wake kwa kuwatakia wote Krismasi njema na heri ya Mwaka Mpya, huku akisisitiza kuwa anathamini sana upendo na mshikamano alioupata kutoka kwa mashabiki wake.

Read More
 Chameleone Aonyesha Gari Jipya la Kifahari aina ya Tesla

Chameleone Aonyesha Gari Jipya la Kifahari aina ya Tesla

Nguli wa muziki kutoka Uganda, Jose Chameleone, ameibua gumzo kubwa baada ya kuonesha gari lake jipya aina ya Tesla Cybertruck. Hatua hii inamweka kwenye ramani ya mastaa wakubwa barani Afrika wanaomiliki moja ya magari ya kifahari na ya kisasa zaidi duniani. Kupitia video inayosambaa mtandaoni Chameleone ameonekana akiwa anaendesha Tesla Cybertruck yake mpya ambapo mashabiki wamempongeza kwa mafanikio hayo makubwa. Hata hivyo, kinachomtofautisha Chameleone ni kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kumiliki gari hili, jambo linaloongeza hadhi yake na kuonesha upeo mpya wa mafanikio katika tasnia ya muziki. Chameleone anajiunga na orodha ya majina makubwa katika muziki wa Afrika kama Timaya, Davido, Omah Lay, na Asake, ambao tayari wanamiliki Tesla Cybertruck.

Read More
 Jose Chameleone aeleza sababu za kumuunga mkono Rais Museveni

Jose Chameleone aeleza sababu za kumuunga mkono Rais Museveni

Mwanamuziki nguli kutoka Uganda, Jose Chameleone, ameeleza sababu zinazomfanya aendelee kumuunga mkono Rais Yoweri Museveni na chama tawala cha NRM, licha ya ukosoaji kutoka kwa baadhi ya wananchi. Akizungumza kwenye mahojiano maalum, Chameleone amesema uhusiano wake na Rais Museveni unatokana na heshima, shukrani, na imani kwamba chama hicho ndicho kimekuwa sehemu ya maisha yake tangu utotoni. Ameeleza kuwa anamheshimu Rais Museveni kama kiongozi mwenye uvumilivu, anayefanya maamuzi kwa busara na asiyeongozwa na hisia. Mwanamuziki huyo pia amefichua kuwa Rais Museveni aliwahi kumsaidia kifedha wakati alipokuwa akisumbuliwa na maradhi akiwa nchini Marekani, jambo analolitaja kama ishara ya utu na uongozi bora. Chameleone amesema ataendelea kuwa mwaminifu kwa Rais Museveni na chama cha NRM, akisisitiza kuwa anaamini kiongozi huyo ameendelea kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa la Uganda.

Read More
 Wasanii wa Uganda Wamlilia Raila Odinga, Wamtaja Kama Shujaa wa Afrika

Wasanii wa Uganda Wamlilia Raila Odinga, Wamtaja Kama Shujaa wa Afrika

Kifo cha Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Amolo Odinga, kimegusa hisia za wasanii nchini Uganda, wakiongozwa na Jose Chameleone na Bobi Wine, ambao wametuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu na wananchi wa Kenya. Kupitia Instagram, msanii nyota Jose Chameleone amemtaja Raila kama kiongozi aliyewaunganisha watu wa Afrika Mashariki kupitia siasa, utu, na msimamo wake wa kupigania demokrasia. Chameleone amesema Afrika Mashariki imepoteza kiongozi wa kipekee aliyekuwa mfano wa ujasiri na upendo kwa watu wake. Kiongozi wa chama cha National Unity Platform (NUP), Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, naye kupitia ujumbe wake katika mtandao wa X, amemsifia Raila kama kiongozi ambaye kwa miongo kadhaa alibaki kuwa sauti ya matumaini kwa waliodhulumiwa na aliyetetea haki za watu kwa ujasiri usioyumba. Wasanii wengine kutoka Uganda, akiwemo Eddy Kenzo, Sheebah, Spice Diana, na King Saha, pia wametuma salamu za rambirambi wakisisitiza kuwa Raila alikuwa kiongozi wa watu wote na alichangia kujenga uhusiano wa karibu kati ya Kenya na Uganda. Hata hivyo katika salamu zao za pole, wasanii hao kwa pamoja wametuma rambirambi kwa Mama Ida Odinga, familia ya Raila, na wananchi wote wa Kenya, wakiwatia moyo waendelee kudumisha maono na urithi wa kiongozi huyo. Salamu hizo kutoka Uganda zimepokelewa kwa heshima kubwa na Wakenya, wengi wakisifia umoja wa kikanda ulioonekana katika maombolezo haya, wakisema Raila Odinga ataendelea kukumbukwa kama Baba wa Mapambano na mwanamageuzi wa kweli wa Afrika.

Read More
 Promota Nobart Apewa Onyo Kali na Jose Chameleone

Promota Nobart Apewa Onyo Kali na Jose Chameleone

Msanii mkongwe wa muziki nchini Uganda, Jose Chameleone, ametoa onyo kali kwa promota maarufu Nobart Events kufuatia matamshi yake ya mara kwa mara dhidi ya wasanii wa familia ya Mayanja. Chameleone ameeleza kuwa hajawahi kufanya kazi na Nobart kama promota, na hivyo haoni sababu ya kushambuliwa hadharani. Ameonyesha kutoridhishwa na kile alichokitaja kama chuki na taarifa za uongo inayoenezwa dhidi yake, akisisitiza kuwa hatavumilia tena udhalilishaji huo. Msanii huyo amesisitiza kuwa hana tatizo binafsi na Nobart lakini hatasita kumkabili endapo ataendelea kumhusisha kwa maneno ya kudhalilisha. Onyo hilo limekuja baada ya miezi kadhaa ya mivutano ya maneno kati ya Nobart na wana familia ya Mayanja, wakiwemo wasanii Pallaso na Weasel, ambao wote ni ndugu wa Chameleone.

Read More
 John Segawa Amshauri Chameleone Kuachana na Bifu na Alien Skin

John Segawa Amshauri Chameleone Kuachana na Bifu na Alien Skin

Mkurugenzi wa filamu nchini Uganda, John Segawa, ameibua mjadala baada ya kutoa maoni yake kuhusu bifu linaloendelea kati ya nyota wa muziki Jose Chameleone na msanii chipukizi mwenye ushawishi mkubwa, Alien Skin. Akizungumza kuhusu mvutano huo, Segawa amesema wazi kuwa Chameleone, kiongozi wa Leone Island, hana nafasi ya kushindana na Alien Skin kwa sababu ya hali yake kiafya na tofauti ya kizazi. Kwa mujibu wa Segawa, Chameleone ni mgonjwa, hafahamu mienendo ya kisasa ya muziki, na kujaribu kuingia katika mapambano na kundi la Fangone Forest kutamletea madhara makubwa. Amefafanua kuwa Chameleone hana nguvu wala nafasi ya kupigana na Alien Skin kwa kuwa vijana ndio wanaoongoza burudani kwa sasa. Aidha, amesisitiza kuwa msanii huyo mkongwe akijaribu kuendeleza bifu hilo, ataishia kupata mateso zaidi badala ya ushindi. Segawa pia ameeleza kuwa bifu hilo linamnufaisha zaidi Alien Skin, kwa sababu msanii huyo bado ni kijana mwenye nguvu na ana miaka mingi ya kufanya muziki mbele yake. Ameongeza kuwa katika hali yoyote ya mvutano, Fangone Forest ingepata ushindi dhidi ya Chameleone kwa sababu ya nafasi yao kubwa katika mwelekeo wa muziki wa sasa.

Read More
 Baunsa wa Alien Skin Ashushiwa Kichapo Katika Bifu na Kambi ya Chameleone

Baunsa wa Alien Skin Ashushiwa Kichapo Katika Bifu na Kambi ya Chameleone

Bifu kati ya msanii mkongwe Jose Chameleone na msanii mtukutu Alien Skin limechukua mwelekeo mpya baada ya mmoja wa walinzi wa Alien Skin, aitwaye Punisher Pro Max, kudaiwa kushushiwa kichapo cha mbwa na wanachama wa Leone Island usiku wa Alhamisi. Taarifa zinaeleza kuwa tukio hilo lilitokea kufuatia mfululizo wa vitisho na matusi kati ya kambi ya Chameleone na ile ya Fangone Forest inayoongozwa na Alien Skin. Baunsa huyo anadaiwa kuwa katika mstari wa mbele kumtetea bosi wake, hali iliyochochea uhasama na kusababisha mashambulizi hayo. Video zilizozagaa mitandaoni zilimuonyesha Chameleone akionya vikali kambi ya Alien Skin, akisisitiza kuwa atawafundisha nidhamu kwa nguvu ikiwa wataendelea kumvunjia heshima. Kwa upande wake, Alien Skin alijibu vitisho hivyo kwa msimamo mkali, akisisitiza kuwa haogopi mapambano na yupo tayari kukabiliana na Chameleone pamoja na ndugu zake Pallaso na Weasel Manizo. Kichapo cha baunsa huyo kimeibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki, baadhi wakionya kuwa bifu hili linaweza kuathiri taswira ya muziki wa Uganda na hata kupelekea vurugu zaidi endapo pande zote mbili hazitatuliza hasira.

Read More
 Jose Chameleone Akataa Kukabidhi Mali Zake kwa Daniella Kabla ya Kifo

Jose Chameleone Akataa Kukabidhi Mali Zake kwa Daniella Kabla ya Kifo

Mwanamuziki nguli wa Uganda, Jose Chameleone, ameibua mjadala baada ya kuweka wazi kuwa hatakubali kukabidhi mali zake akiwa bado hai, licha ya mkewe Daniella kutaka usimamizi wa baadhi ya mali hizo katika shauri la talaka linaloendelea. Chameleone amesema mali alizojipatia ni kwa ajili ya watoto wake na anataka warithi mali hizo baada ya kifo chake, ili nao wazikabidhi kwa wajukuu wake. Hata hivyo, amesisitiza kuwa hatalazimishwa kuandika wasia mapema kwani anaamini bado ni jukumu lake kulinda urithi huo akiwa hai. Amefafanua kuwa shauri la talaka linaloendelea ni sawa na kumtaka aandike wasia kabla ya kifo chake, jambo analoliona halina mashiko. Pia amekanusha taarifa kwamba anaishi na msongo wa mawazo, akibainisha kuwa anaendelea vizuri na ana mtazamo wa kutambua kuwa mali ni vitu vya kupita ambavyo havipaswi kusababisha wasiwasi. Chameleone ameongeza kuwa, licha ya tofauti zilizopo kati yake na Daniella, wote wawili wanapigania lengo moja, kuhakikisha watoto wao wanapata maisha bora na urithi wa familia unabaki mikononi mwao.

Read More
 Chameleone Ashauriwa Akabidhi Nyumba na Mali kwa Daniella

Chameleone Ashauriwa Akabidhi Nyumba na Mali kwa Daniella

Aliyekuwa mbunge, Mubarak Munyagwa, ameibuka na ushauri kwa msanii nyota wa Uganda, Jose Chameleone, akimtaka akubaliane na masharti yote yaliyowekwa na mkewe, Daniella Atim, katika mchakato wa talaka yao. Munyagwa amesema kuwa Chameleone ni msanii mwenye juhudi na uwezo wa kujenga au kununua nyumba nyingine, hivyo hana sababu ya kushikilia mali hiyo. Aidha, amesisitiza kuwa kukubali hata ombi la Daniella la kupata asilimia 60 ya mali ya Chameleone kutaleta amani na kulinda heshima ya familia. Kwa mujibu wa Munyagwa, Chameleone hafai kuonyesha hasira wala upinzani dhidi ya watoto wake kwani hali hiyo inaweza kuwafanya wamchukie kwa kutowelewa hali ilivyo. Hata hivyo, upande wa Chameleone umekuwa na msimamo tofauti. Ingawa yuko tayari kukubali talaka, amekuwa akipinga baadhi ya masharti ya Daniella, hasa kuhusu nyumba ya familia iliyoko Sseguku na malezi ya watoto. Mwanamuziki huyo anataka nyumba ibaki mali ya familia na malezi yawahusishe wote wawili badala ya Daniella pekee. Daniella, kwa upande wake, ameomba mahakama impe malezi kamili ya watoto wao, umiliki wa nyumba ya Sseguku, pamoja na fedha za matumizi ya kila mwezi kwa ajili yake na watoto. Pia amedai asilimia 60 ya mali za Chameleone ili kufanikisha maisha ya familia yake baada ya talaka hiyo.

Read More
 Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Staa wa muziki kutoka Uganda, Jose Chameleone, amezua mjadala mpya mtandaoni baada ya kuonekana akiwa na ukaribu wa kimahaba na mfanyabiashara maarufu anayeishi Marekani, Juliet Zawedde, katika tamasha la usiku lililofanyika jana. Wawili hao, ambao uhusiano wao wa karibu umekuwa ukileta minong’ono kwa muda mrefu, waliibua shangwe na nderemo kutoka kwa mashabiki waliokuwa ukumbini baada ya kubusiana hadharani jukwaani, hali iliyowafanya mashabiki kuzidi kudai kwa sauti kuwa uhusiano wao upewe hadhi rasmi ya ndoa. Zawedde aliwasili Uganda wiki iliyopita kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, huku sherehe kuu ikifanyika Julai 19 katika klabu ya Noni Vie jijini Kampala. Hata hivyo, Chameleone hakuweza kuhudhuria tukio hilo kutokana na kuwa safarini mjini Bujumbura. Lakini jana usiku, wawili hao walipata nafasi ya kukutana tena jukwaani, na tukio hilo lilibadilika kuwa burudani ya kipekee kwa mashabiki waliokuwa wamehudhuria. Video inayosambaa kwa kasi mitandaoni inaonesha Zawedde akipanda jukwaani, kumkumbatia Chameleone kwa nguvu, kisha kumbusu kwa mikono miwili usoni mbele ya umati mkubwa uliokuwa ukishangilia. Kitendo hicho kimewasha moto mpya kwenye mitandao ya kijamii, ambapo mashabiki wengi wamekuwa wakiandika maoni ya kuwataka wawili hao kuhalalisha penzi lao. Hadi sasa, hakuna mmoja kati yao aliyetoa kauli rasmi kuhusu hatua inayofuata katika uhusiano wao, lakini wazi ni kwamba mashabiki wao wana matumaini makubwa kuona penzi hili likibadilika kutoka ‘urafiki wa karibu’ na kuwa rasmi zaidi. Hii si mara ya kwanza wawili hao kuhusishwa kimapenzi, lakini tukio la jana linaonekana kama uthibitisho mpya wa ukaribu wao unaozidi kushika kasi mbele ya macho ya umma.

Read More
 Diamond Aonyesha Heshima kwa Jose Chameleone, Ataka Ushirikiano wa Mwaka

Diamond Aonyesha Heshima kwa Jose Chameleone, Ataka Ushirikiano wa Mwaka

Mwanamuziki nguli kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ametangaza nia yake ya dhati ya kushirikiana na msanii mkongwe wa Uganda, Jose Chameleone, katika wimbo mpya unaotarajiwa kutoka mwaka huu. Akiwa jukwaani katika tamasha la Coffee Marathon huko Ntungamo, Uganda, Diamond aliwajulisha mashabiki kuwa kolabo hiyo ni ndoto aliyokuwa nayo kwa muda mrefu, na sasa anafanya kila juhudi kuhakikisha inatimia. Diamond alisema kuwa licha ya mafanikio yake makubwa katika bara la Afrika, hajawahi kusahau mchango wa Jose Chameleone katika muziki wa Afrika Mashariki. Alimuelezea kama msanii aliyeathiri kizazi kizima na kumvutia hata yeye kuingia kwenye tasnia ya muziki. “Mwaka huu nataka kuhakikisha ninafanya wimbo na Jose Chameleone. Tunamshukuru Mungu kuwa anaendelea vizuri kiafya na tunamshukuru kwa mchango wake mkubwa kwenye muziki,” alisema Diamond mbele ya mashabiki. Kwa upande wake, Jose Chameleone, ambaye ametamba kwa zaidi ya miaka 20 na kubaki kuwa moja ya nguzo za muziki wa Afrika Mashariki, bado anaheshimika kwa nyimbo zake zenye ujumbe mzito na sauti ya kipekee. Kolabo kati ya Chameleone na Diamond inatarajiwa kuwa ya kihistoria, na tayari mashabiki kote kanda ya Afrika Mashariki wanasubiri kwa hamu kusikia kazi yao ya pamoja.

Read More