John Segawa Amshauri Chameleone Kuachana na Bifu na Alien Skin

John Segawa Amshauri Chameleone Kuachana na Bifu na Alien Skin

Mkurugenzi wa filamu nchini Uganda, John Segawa, ameibua mjadala baada ya kutoa maoni yake kuhusu bifu linaloendelea kati ya nyota wa muziki Jose Chameleone na msanii chipukizi mwenye ushawishi mkubwa, Alien Skin. Akizungumza kuhusu mvutano huo, Segawa amesema wazi kuwa Chameleone, kiongozi wa Leone Island, hana nafasi ya kushindana na Alien Skin kwa sababu ya hali yake kiafya na tofauti ya kizazi. Kwa mujibu wa Segawa, Chameleone ni mgonjwa, hafahamu mienendo ya kisasa ya muziki, na kujaribu kuingia katika mapambano na kundi la Fangone Forest kutamletea madhara makubwa. Amefafanua kuwa Chameleone hana nguvu wala nafasi ya kupigana na Alien Skin kwa kuwa vijana ndio wanaoongoza burudani kwa sasa. Aidha, amesisitiza kuwa msanii huyo mkongwe akijaribu kuendeleza bifu hilo, ataishia kupata mateso zaidi badala ya ushindi. Segawa pia ameeleza kuwa bifu hilo linamnufaisha zaidi Alien Skin, kwa sababu msanii huyo bado ni kijana mwenye nguvu na ana miaka mingi ya kufanya muziki mbele yake. Ameongeza kuwa katika hali yoyote ya mvutano, Fangone Forest ingepata ushindi dhidi ya Chameleone kwa sababu ya nafasi yao kubwa katika mwelekeo wa muziki wa sasa.

Read More
 Baunsa wa Alien Skin Ashushiwa Kichapo Katika Bifu na Kambi ya Chameleone

Baunsa wa Alien Skin Ashushiwa Kichapo Katika Bifu na Kambi ya Chameleone

Bifu kati ya msanii mkongwe Jose Chameleone na msanii mtukutu Alien Skin limechukua mwelekeo mpya baada ya mmoja wa walinzi wa Alien Skin, aitwaye Punisher Pro Max, kudaiwa kushushiwa kichapo cha mbwa na wanachama wa Leone Island usiku wa Alhamisi. Taarifa zinaeleza kuwa tukio hilo lilitokea kufuatia mfululizo wa vitisho na matusi kati ya kambi ya Chameleone na ile ya Fangone Forest inayoongozwa na Alien Skin. Baunsa huyo anadaiwa kuwa katika mstari wa mbele kumtetea bosi wake, hali iliyochochea uhasama na kusababisha mashambulizi hayo. Video zilizozagaa mitandaoni zilimuonyesha Chameleone akionya vikali kambi ya Alien Skin, akisisitiza kuwa atawafundisha nidhamu kwa nguvu ikiwa wataendelea kumvunjia heshima. Kwa upande wake, Alien Skin alijibu vitisho hivyo kwa msimamo mkali, akisisitiza kuwa haogopi mapambano na yupo tayari kukabiliana na Chameleone pamoja na ndugu zake Pallaso na Weasel Manizo. Kichapo cha baunsa huyo kimeibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki, baadhi wakionya kuwa bifu hili linaweza kuathiri taswira ya muziki wa Uganda na hata kupelekea vurugu zaidi endapo pande zote mbili hazitatuliza hasira.

Read More
 Jose Chameleone Akataa Kukabidhi Mali Zake kwa Daniella Kabla ya Kifo

Jose Chameleone Akataa Kukabidhi Mali Zake kwa Daniella Kabla ya Kifo

Mwanamuziki nguli wa Uganda, Jose Chameleone, ameibua mjadala baada ya kuweka wazi kuwa hatakubali kukabidhi mali zake akiwa bado hai, licha ya mkewe Daniella kutaka usimamizi wa baadhi ya mali hizo katika shauri la talaka linaloendelea. Chameleone amesema mali alizojipatia ni kwa ajili ya watoto wake na anataka warithi mali hizo baada ya kifo chake, ili nao wazikabidhi kwa wajukuu wake. Hata hivyo, amesisitiza kuwa hatalazimishwa kuandika wasia mapema kwani anaamini bado ni jukumu lake kulinda urithi huo akiwa hai. Amefafanua kuwa shauri la talaka linaloendelea ni sawa na kumtaka aandike wasia kabla ya kifo chake, jambo analoliona halina mashiko. Pia amekanusha taarifa kwamba anaishi na msongo wa mawazo, akibainisha kuwa anaendelea vizuri na ana mtazamo wa kutambua kuwa mali ni vitu vya kupita ambavyo havipaswi kusababisha wasiwasi. Chameleone ameongeza kuwa, licha ya tofauti zilizopo kati yake na Daniella, wote wawili wanapigania lengo moja, kuhakikisha watoto wao wanapata maisha bora na urithi wa familia unabaki mikononi mwao.

Read More
 Chameleone Ashauriwa Akabidhi Nyumba na Mali kwa Daniella

Chameleone Ashauriwa Akabidhi Nyumba na Mali kwa Daniella

Aliyekuwa mbunge, Mubarak Munyagwa, ameibuka na ushauri kwa msanii nyota wa Uganda, Jose Chameleone, akimtaka akubaliane na masharti yote yaliyowekwa na mkewe, Daniella Atim, katika mchakato wa talaka yao. Munyagwa amesema kuwa Chameleone ni msanii mwenye juhudi na uwezo wa kujenga au kununua nyumba nyingine, hivyo hana sababu ya kushikilia mali hiyo. Aidha, amesisitiza kuwa kukubali hata ombi la Daniella la kupata asilimia 60 ya mali ya Chameleone kutaleta amani na kulinda heshima ya familia. Kwa mujibu wa Munyagwa, Chameleone hafai kuonyesha hasira wala upinzani dhidi ya watoto wake kwani hali hiyo inaweza kuwafanya wamchukie kwa kutowelewa hali ilivyo. Hata hivyo, upande wa Chameleone umekuwa na msimamo tofauti. Ingawa yuko tayari kukubali talaka, amekuwa akipinga baadhi ya masharti ya Daniella, hasa kuhusu nyumba ya familia iliyoko Sseguku na malezi ya watoto. Mwanamuziki huyo anataka nyumba ibaki mali ya familia na malezi yawahusishe wote wawili badala ya Daniella pekee. Daniella, kwa upande wake, ameomba mahakama impe malezi kamili ya watoto wao, umiliki wa nyumba ya Sseguku, pamoja na fedha za matumizi ya kila mwezi kwa ajili yake na watoto. Pia amedai asilimia 60 ya mali za Chameleone ili kufanikisha maisha ya familia yake baada ya talaka hiyo.

Read More
 Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Jose Chameleone na Juliet Zawedde Wazua Gumzo kwa Mabusu Jukwaani

Staa wa muziki kutoka Uganda, Jose Chameleone, amezua mjadala mpya mtandaoni baada ya kuonekana akiwa na ukaribu wa kimahaba na mfanyabiashara maarufu anayeishi Marekani, Juliet Zawedde, katika tamasha la usiku lililofanyika jana. Wawili hao, ambao uhusiano wao wa karibu umekuwa ukileta minong’ono kwa muda mrefu, waliibua shangwe na nderemo kutoka kwa mashabiki waliokuwa ukumbini baada ya kubusiana hadharani jukwaani, hali iliyowafanya mashabiki kuzidi kudai kwa sauti kuwa uhusiano wao upewe hadhi rasmi ya ndoa. Zawedde aliwasili Uganda wiki iliyopita kusherehekea siku yake ya kuzaliwa, huku sherehe kuu ikifanyika Julai 19 katika klabu ya Noni Vie jijini Kampala. Hata hivyo, Chameleone hakuweza kuhudhuria tukio hilo kutokana na kuwa safarini mjini Bujumbura. Lakini jana usiku, wawili hao walipata nafasi ya kukutana tena jukwaani, na tukio hilo lilibadilika kuwa burudani ya kipekee kwa mashabiki waliokuwa wamehudhuria. Video inayosambaa kwa kasi mitandaoni inaonesha Zawedde akipanda jukwaani, kumkumbatia Chameleone kwa nguvu, kisha kumbusu kwa mikono miwili usoni mbele ya umati mkubwa uliokuwa ukishangilia. Kitendo hicho kimewasha moto mpya kwenye mitandao ya kijamii, ambapo mashabiki wengi wamekuwa wakiandika maoni ya kuwataka wawili hao kuhalalisha penzi lao. Hadi sasa, hakuna mmoja kati yao aliyetoa kauli rasmi kuhusu hatua inayofuata katika uhusiano wao, lakini wazi ni kwamba mashabiki wao wana matumaini makubwa kuona penzi hili likibadilika kutoka ‘urafiki wa karibu’ na kuwa rasmi zaidi. Hii si mara ya kwanza wawili hao kuhusishwa kimapenzi, lakini tukio la jana linaonekana kama uthibitisho mpya wa ukaribu wao unaozidi kushika kasi mbele ya macho ya umma.

Read More
 Diamond Aonyesha Heshima kwa Jose Chameleone, Ataka Ushirikiano wa Mwaka

Diamond Aonyesha Heshima kwa Jose Chameleone, Ataka Ushirikiano wa Mwaka

Mwanamuziki nguli kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ametangaza nia yake ya dhati ya kushirikiana na msanii mkongwe wa Uganda, Jose Chameleone, katika wimbo mpya unaotarajiwa kutoka mwaka huu. Akiwa jukwaani katika tamasha la Coffee Marathon huko Ntungamo, Uganda, Diamond aliwajulisha mashabiki kuwa kolabo hiyo ni ndoto aliyokuwa nayo kwa muda mrefu, na sasa anafanya kila juhudi kuhakikisha inatimia. Diamond alisema kuwa licha ya mafanikio yake makubwa katika bara la Afrika, hajawahi kusahau mchango wa Jose Chameleone katika muziki wa Afrika Mashariki. Alimuelezea kama msanii aliyeathiri kizazi kizima na kumvutia hata yeye kuingia kwenye tasnia ya muziki. “Mwaka huu nataka kuhakikisha ninafanya wimbo na Jose Chameleone. Tunamshukuru Mungu kuwa anaendelea vizuri kiafya na tunamshukuru kwa mchango wake mkubwa kwenye muziki,” alisema Diamond mbele ya mashabiki. Kwa upande wake, Jose Chameleone, ambaye ametamba kwa zaidi ya miaka 20 na kubaki kuwa moja ya nguzo za muziki wa Afrika Mashariki, bado anaheshimika kwa nyimbo zake zenye ujumbe mzito na sauti ya kipekee. Kolabo kati ya Chameleone na Diamond inatarajiwa kuwa ya kihistoria, na tayari mashabiki kote kanda ya Afrika Mashariki wanasubiri kwa hamu kusikia kazi yao ya pamoja.

Read More
 Chameleone adokeza mpango wa kubuni bendi ya muziki ya familia

Chameleone adokeza mpango wa kubuni bendi ya muziki ya familia

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amefichua mpango wa kuunda bendi ya familia itakayojumuisha ndugu zake, Pallaso na Weasel. Katika mahojiano hivi karibuni, Chameleone ameeleza kuwa watatu hao bado wapo kwenye mazungumzo kwa ajili ya kufikia makubaliano. Bendi hiyo huenda ikazinduliwa hivi karibuni katika hafla itakayofanyika jijini Kampala, katika uwanja wa Namboole. “Tunapanga kuanzisha bendi ya familia na tutatoa mweelekeo hivi karibuni. Uzinduzi huo unahitaji ukumbi mkubwa ambao hauko tayari kwa sasa. Tunataka eneo ambalo linaweza kuchukua zaidi ya watu 40, 000,” alisema. Jose Chameleone ameweka wazi hayo kwenye mkao na waandishi wa habari wakati akielezea mipango yake juu  tamasha lake “Gwanga Mujje” litakalofanyika huko Lugogo Cricket Oval mwezi Februari mwaka huu.

Read More
 Uongozi wa Jose Chameleone wafunguka kuhusu tuhuma za msanii huyo kumpiga Boda Boda

Uongozi wa Jose Chameleone wafunguka kuhusu tuhuma za msanii huyo kumpiga Boda Boda

Menejimenti ya Mwanamuziki Jose Chameleone kupitia Afisa Uhusiano wake, imetoa maelezo kuhusiana na video ambayo imetoka ikimuonesha mwimbaji huyo maarufu wa nchini Uganda akimpiga mhudumu wa boda boda. Taarifa hiyo imeeleza kwamba tukio hilo lilitokea November 12, mwaka 2022 ambapo mwendesha boda boda huyo aliichuna kwa pembeni gari ya Jose Chameleone aina ya Range Rover. Taarifa hiyo iliendelea kusema, Chameleone angeweza kupuuzia tukio hilo kama sio maneno ya matusi na vitisho kutoka boda boda huyo. Tukio linaloonekana ni Jose Chameleone akijaribu kujilinda mwenyewe dhidi ya mwendesha boda boda huyo ambaye alikuwa akimfuata kwa shari. Aidha taarifa ya menejimenti ya Chameleone inakamilika kwa kulaani kitendo hicho.

Read More
 Rapa Gravitty Omutujju afufua bifu yake na Jose Chameleone

Rapa Gravitty Omutujju afufua bifu yake na Jose Chameleone

Rapa kutoka nchini Uganda Gravity Omutujju amefufua tena bifu yake na msanii mkongwe Jose Chameleone. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Omutujju amesema hana mpango kumuunga mkono Chameleone kwenye shoo yake ijayo, itakayofanyika huko Lugogo, Cricket Oval. Gravity Omutujju amesema shoo ya msanii huyo itabuma vibaya huku akidai kwamba hatokuja kumheshimu Jose Chameleone kwa sababu hajawahi kumfanyia kitu chochote kizuri kwenye maisha yake. “Siwezi kumuunga mkono, hajawahi kunisaidia kwa namna yoyote ile. Mwache apambane na hali yake, asitarajie msaada kutoka kwangu. Sijali hata kuhusu onesho la Chameleone kwa sababu si mtu mzuri,” alisema.

Read More
 King Saha amshukuru Chameleone kwa kusimama naye wakati wa matatizo

King Saha amshukuru Chameleone kwa kusimama naye wakati wa matatizo

Mwanamuziki King Saha ni mwingi wa shukran kwa kitendo cha Jose Chameleone kutumbuiza kwenye shows zake alizokuwa ameratibu kutoa burudani kwa mashabiki zake. King saha ambaye aliruhusiwa kuondoka katika hospitali ya Nakasero wiki iliyopita ambako alikuwa amelazwa, amefarijika na ukarimu waBosi huyo wa Leone Island kumkingia kifua alipokuwa kwenye matatizo ambapo amemtaja kuwa mtu mwema kuwahi kutokea nchini Uganda kwa upande wa wasanii. “Namshukuru Chameleone kwa ukarimu wake. Namheshimu sana kwa kunifanyia shows zangu nilipokuwa nimelazwa hospitalini,” alisema. King Saha kwa sasa amechukua mapumziko kwenye muziki wake kwa ajili ya kuiweka afya yake sawa kabla ya kuanza shughuli zake rasmi.

Read More
 Niko tayari kutumbuiza katika shoo zote za King Saha hadi atakapopata nafuu- Chameleone

Niko tayari kutumbuiza katika shoo zote za King Saha hadi atakapopata nafuu- Chameleone

Msanii mashuhuri kutoka nchini Uganda Jose Chameleone amejitolea kujaza nafasi ya mwanamuziki King Saha katika shoo zake zote alizokuwa ameratibiwa kutumbuiza  hadi atakapopata afueni. Katika mahojiano hivi karibuni, Chameleone amesema yuko tayari kuwapa burudani mashabiki wake bure bila malipo. Bosi huyo wa Leone Island ameeleza kuwa tayari ameanza mazungumzo na meneja wa King Saha aitwaye Mukasa ili kufanikisha hilo. “Sasa hivi mdogo wangu King Saha hayuko vizuri kiafya na tayari nimempigia simu meneja wake, Mukasa kuhusu pendekezo langu. Nitatumbuiza kwenye shoo zake vya alizopewa nafasi bila bila malipo. Huu ni wakati ambao anahitaji wema wetu,” alisema Chameleone. King Saha aliruhusiwa kwenda nyumbani siku ya Jumanne kutoka hospitali ya Nakasero ambapo alishauriwa na madaktari kupumzika kabla ya kuanza tena shughuli zake za muziki.

Read More
 Jose Chameleone atakiwa kuzindua kampuni yake ya simu

Jose Chameleone atakiwa kuzindua kampuni yake ya simu

Msanii mkongwe kutoka nchini Uganda Jose Chameleone ameshauriwa kutekeleza mpango wake wa kuanzisha mradi wake kufungua kampuni ya simu iitwayo Chameleone Phones. Wito huo umetolewa na mwanahabari Douglas Lwaga ambaye amehoji kuwa Chameleone alipoteza fursa kubwa ya kuingiza pesa nyingi kupitia mpango wake wa kuzindua kampuni ya simu. Hata hivyo amesema msanii huyo mkongwe ana nafasi nyingine ya kufaulu kibiashara kupitia wazo lake hilo kwa kuwa ana bado ana ushawishi kwenye tasnia ya muziki Afrika mashariki na barani Afrika kwa ujumla. “Jose Chameleone missed out on a huge opportunity of launching the Chameleone Phone. This could have brought him lots of cash. I think he can still go for it,” Alisema kwenye kipindi cha runinga cha After 5 show. Utakumbuka zaidi mwongo mmoja uliopita Jose Chameleone alikuwa na mpango wa kuzindua kampuni yake ya simu iitwayo Chameleone Phone lakini hakufanikiwa kutekeleza mpango wake huo kwa sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wake.

Read More