VJ Patelo Akerwa na Mashabiki Waliomtusi Mke Wake Kupitia TikTok Live

VJ Patelo Akerwa na Mashabiki Waliomtusi Mke Wake Kupitia TikTok Live

Msanii wa muziki wa Arbantone kutoka Kenya, VJ Patelo, ameonesha maumivu na hasira baada ya baadhi ya mashabiki kumtusi mke wake wakidai ana sura kombo wakati wa mazungumzo kupitia TikTok Live. Akijibu kwa ukali, VJ Patelo amewakemea waliotoa maneno hayo, akisema hawana haki ya kudharau mke wake wala kuingilia maisha yake binafsi. Ameeleza kuwa anampenda mke wake jinsi alivyo na hataruhusu mtu yeyote kumkashifu. VJ Patelo amesema iwapo kuna mtu anaona sura ya mke wake siyo nzuri, hilo halimhusu, akiwataka watu wajishughulishe na maisha yao badala ya kumdharau mtu ambaye yeye amechagua kumpenda. Katika mazungumzo hayo, VJ Patelo pia amejibu kwa hasira shinikizo kutoka kwa mashabiki waliomtaka arudi studio kuendelea na muziki. Amesema hana mpango wowote wa kurejea studio kwa sasa na akawaomba watu waache kufuatilia na kuingilia maisha yake binafsi.

Read More
 VJ Patelo Apuzilia Mbali Sakata la Mama Anayedai Ni Mama Halisi ya Bahati

VJ Patelo Apuzilia Mbali Sakata la Mama Anayedai Ni Mama Halisi ya Bahati

Msanii wa Arbantone VJ Patelo ameibuka na mtazamo mkali kuhusu sakata linalomkabili mwanamuziki Bahati, baada ya mwanamke mmoja kujitokeza mtandaoni akidai ndiye mama halisi wa msanii huyo. Kwa mujibu wa VJ Patelo, huenda Bahati alimlipa mama huyo kwa lengo la kuvuta umakini wa mashabiki kabla hajaachia kazi mpya. Ameonekana kukosoa vikali hatua hiyo, akisema kuwa kitendo cha kuibua madai ya kifamilia kupitia mitandao ya kijamii kinaacha maswali mengi kuhusu ukweli wake. Kauli ya VJ Patelo imezua mijadala zaidi mtandaoni, mashabiki wakigawanyika kati ya wanaomuunga mkono na wanaoamini Bahati anapaswa kutoa ufafanuzi wa kina kuhusu madai hayo ya mama halisi.

Read More
 VJ Patelo Ataka Vijana Kuchukua Tahadhari Baada ya Kuongezeka kwa HIV

VJ Patelo Ataka Vijana Kuchukua Tahadhari Baada ya Kuongezeka kwa HIV

Msanii wa arbantone, VJ Patelo, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kutoa kauli tata kuhusiana na taarifa za kuongezeka kwa maambukizi mapya ya virusi vya HIV nchini Kenya. Kupitia video aliyochapisha kwenye mtandao wa TikTok, Patelo amesema kuwa takwimu hizo zinamfanya ajisikie vizuri kwa sababu zinatoa onyo kali kwa watu wanaofanya ngono kiholela. Patelo amesisitiza kuwa wale wanaopenda kujihusisha na ngono kupita kiasi wanapaswa kutambua madhara ya tabia hizo. Kwa mujibu wake, ongezeko la maambukizi ni ujumbe mzito unaopaswa kuchukuliwa kwa umakini na jamii nzima ili kuongeza tahadhari na kuimarisha nidhamu. Kauli hiyo imeibuka muda mfupi baada ya Ripoti ya Makadirio ya HIV 2025 iliyotolewa na Baraza la Kitaifa la Kudhibiti Magonjwa ya Mlipuko (NSDCC) kuonyesha kuwa Kenya imerekodi maambukizi mapya 19,991, ikilinganishwa na 16,752 mwaka uliopita. Ripoti hiyo imebainisha kuwa maambukizi mapya yanajitokeza zaidi miongoni mwa vijana wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 34, huku kaunti kumi zikichangia jumla ya asilimia 60 ya visa vipya. Kaunti hizo ni pamoja na Nairobi, Migori, Kisumu, Homa Bay, Busia, Siaya, Kakamega, Nakuru, Mombasa, na Bungoma.

Read More
 VJ Patelo Awakosoa Arrow Bwoy na Masauti Kwa Wimbo Wao Mpya ‘Kilimani’

VJ Patelo Awakosoa Arrow Bwoy na Masauti Kwa Wimbo Wao Mpya ‘Kilimani’

Mwanamitandao maarufu nchini Kenya, VJ Patelo, ameibua gumzo baada ya kutoa kauli kali dhidi ya wimbo mpya wa Arrow Bwoy na Masauti unaoitwa Kilimani. Kupitia mitandao ya kijamii, Patelo amekosoa vikali kazi hiyo akidai haina ubora na kwamba haitapata mashiko kwenye tasnia ya muziki. Amesema kuwa wimbo huo utabaki kusikilizwa na wasanii hao wenyewe pekee, akiwashutumu kwa kile alichokitaja kama kuleta mzaha katika muziki wa Kenya. Katika malalamiko yake, Patelo amewashutumu wasanii hao akisema kuwa tasnia haihitaji wasanii wanaotoa kazi ambazo hazina ubunifu au ubora wa kuvutia. Aidha, amemkebehi Arrow Bwoy kwa kumlinganisha na jina la mitaani “Arrow Roots,” akionyesha kutoridhishwa kabisa na kazi waliyoitoa.

Read More
 Mke wa VJ Patelo Athibitisha kuwa Mjamzito

Mke wa VJ Patelo Athibitisha kuwa Mjamzito

Mke wa msanii wa Arbantone VJ Patelo, anayejulikana kwa jina Dee, amethibitisha kuwa ni mjamzito kufuatia maswali ya mashabiki waliotaka kujua sababu ya kutokuonekana hadharani katika siku za hivi karibuni. Kupitia ujumbe alioutoa kwenye mitandao ya kijamii, Dee amewaomba radhi mashabiki wake, hasa wale wa Lodwar, kwa kutojumuika nao katika matukio ya hivi karibuni na kueleza kuwa hali yake ya ujauzito imemlazimu kupumzika kwa muda. Mwanamama huyo, amesema kuwa mashabiki wanapaswa kuelewa hali yake kwa sasa na akaahidi kwamba atashiriki kwenye matukio ya burudani mara atakapokuwa na nguvu za kutosha. Kauli yake inakuja baada ya VJ Patelo kufanya club appearance wiki hii bila mke wake, hali iliyozua maswali kutoka kwa mashabiki waliotaka kufahamu sababu ya kutokuwepo kwake.

Read More
 VJ Patelo Amshambulia Toxic Lyrikali kwa Kuishi Maisha ya Feki

VJ Patelo Amshambulia Toxic Lyrikali kwa Kuishi Maisha ya Feki

Msanii wa Arbantone VJ Patelo ameibua upya mzozo na msanii wa hip-hop Toxic Lyrikali, akimtuhumu kuishi maisha bandia na kukosa ubunifu katika muziki wake. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, Patelo amedai kuwa Lyrikali hudanganya katika mashairi ya muziki kuhusu utajiri na mali anazomiliki, ikiwemo madai ya kuwa na gari la kifahari aina ya Mercedes-Benz S-Class. Amesema kuwa msanii huyo anaishi maisha ya kuigiza na kwamba madai yake kuhusu magari na pesa ni ya kutafuta umaarufu tu. Patelo pia ameongeza kuwa nyimbo nyingi za Lyrikali si za asili, akidai kwamba amekuwa akiiga nyimbo za wasanii wa Jamaica na kuzitafsiri kwa Sheng ili kuwavutia mashabiki wa muziki nchini Kenya. Amesema hakuna ubunifu wa kweli katika kazi zake, bali ni nakala za nyimbo za nje zilizotiwa ladha ya mitaani. Kauli za Patelo zimezua gumzo mitandaoni, huku mashabiki wakigawanyika kati ya wanaomuunga mkono na wale wanaomtetea Toxic Lyrikali. Hadi sasa, msanii huyo hajatoa majibu rasmi kuhusu tuhuma hizo, ingawa hii si mara ya kwanza anakosolewa kuhusu uhalisia wa nyimbo zake.

Read More
 VJ Patelo Apuuzilia Uvumi wa Kuibiwa Dandora

VJ Patelo Apuuzilia Uvumi wa Kuibiwa Dandora

Msanii kutoka Kenya VJ Patelo amekanusha vikali tetesi zilizokuwa zikisambazwa mitandaoni kwamba alivamiwa na kuibiwa Chains zake za dhahabu katika eneo la Dandora, Nairobi. Akijibu madai hayo, Patelo amesema anashangazwa na watu wanaobuni stori za uongo ili kutafuta umaarufu na kufuata vichwa vya habari. Ametoa msimamo wake kwamba hajawahi kuibiwa wala kushambuliwa Dandora, na kwamba ukimya wake mtandaoni ni wa kawaida kutokana na ratiba zake binafsi. Aidha, amewataka wafuasi wake kupuuza taarifa zisizo na msingi na kuendelea kumuunga mkono katika kazi zake za sanaa. Uvumi huo ulianza baada ya jamaa mmoja kudai kuwa Patelo alinyang’anywa mali zake, jambo ambalo limepelekea mashabiki wengi kuhoji ni kwa nini hakuwa akiposti kwenye mitandao ya kijamii kwa siku mbili zilizopita.

Read More
 VJ Patello Amchana Diana B Baada ya Madai ya Chain Feki

VJ Patello Amchana Diana B Baada ya Madai ya Chain Feki

Mzozo kati ya VJ Patello na Influencer aligeukia muziki Diana B umeendelea kuchukua sura mpya baada ya Patello kujibu vikali madai ya kwamba mikufu yake ya dhahabu ni bandia. Kupitia Instagram, Patello alimshutumu Diana na mumewe Bahati kwa kushindwa kulipa shilingi milioni moja kwa Harambee Stars, akiongeza kuwa wawili hao hawana uhalali wa kuzungumzia vitu vya thamani. Ugomvi huo ulianza baada ya Patello kukosoa wimbo mpya wa Diana B uitwao Bibi ya Tajiri, ambapo Diana alisikika akijinadi kuwa ndiye rapa bora nchini Kenya huku akionekana kwenye video akirarua picha za marapa maarufu kama Khaligraph Jones na Nyashinski. Kitendo hicho kilimkera Patello ambaye alimtolea uvivu kwa kudai kuwa hana heshima kwa wasanii halisi wa hiphop, akamtaka aendelee na masuala ya content creation kwa sababu hajui kurap. Diana B hakusita kujibu mashambulizi hayo kwa kumdharau Patello, akisema kwa kejeli kwamba ni ajabu mtu mwenye mikufu bandia anathubutu kukosoa kazi ya “Bibi ya Tajiri”

Read More
 DJ Shiti Asababisha Vicheko kwa Video ya Maombi ya Sheng kwa Patelo

DJ Shiti Asababisha Vicheko kwa Video ya Maombi ya Sheng kwa Patelo

Mchekeshaji maarufu DJ Shiti ameibua kicheko mitandaoni baada ya kujitokeza kwa njia ya ucheshi kumuombea VJ Patelo, kufuatia tetesi kwamba ndoa yake na mkewe Dee imeingiwa na ukungu. Kupitia video ambayo kwa sasa inasambaa, DJ Shiti amesikika akitumia lugha tata ya Sheng kuomba mikosi imuondokee Patelo. Lugha hiyo, iliyojaa maneno ya ucheshi na misemo isiyoeleweka kirahisi, imewafanya mashabiki wengi kucheka huku wengine wakisema maombi hayo ndiyo dawa ya jini mkata kamba linalodaiwa kuingia kwenye ndoa ya Patelo. “Baba nakabidhi Patelo mikono mwako, chude ngenje, chude ngenje siku zombotote ngezo zikuje nyingi. Ngezo zikuje kama zombotote apate shagla kama zombotote. Nakataa maroho ya chang’ili nakataa roho ya black devil. Nambariki na roho ya Captain Morgan siku zombotote. Gota hatujawahi bugunda!!”, Alisikika akisema kwenye video inayosambaa mtandaoni. Video ya DJ Shiti imekuja siku chache baada ya ile iliyosambaa ikimuonyesha Dee akimzaba kofi Patelo walipokuwa katika nightclub moja jijini Nairobi, tukio lililoibua tetesi kwamba ndoa yao inakumbwa na changamoto. Hata hivyo, VJ Patelo mwenyewe amekanusha vikali madai hayo, akisisitiza kuwa ndoa yake iko imara na haina misukosuko. Akiwa amekasirishwa na tetesi hizo, Patelo aliwaambia wakosoaji wake wajishughulishe na maisha yao badala ya kufuatilia mambo ya kifamilia yake. Kauli ya Patelo imeonekana kama onyo kali kwa wanaoendeleza uvumi mitandaoni, huku DJ Shiti akigeuza sakata hilo kuwa kichekesho kwa maombi yake ya Sheng ambayo yamewachekesha wengi.

Read More