Mwanamitindo na mjasiriamali Gloria Ntazola amefunguka kwa uchungu kuhusu masaibu aliyopitia akijitolea kumsaidia ndugu yake aliyekuwa katika uraibu wa dawa za kulevya.
Gloria anasema alitumia zaidi ya shilingi milioni mbili kumpeleka kijana huyo kwenye kituo cha Rehab ili kusaidiwa kuacha matumizi ya dawa hizo. Zaidi ya hapo, amekuwa akimlipia karo ya mtoto wake na kumsaidia kutafuta njia za kujitegemea.
Hata hivyo, licha ya msaada huo wote, anadai kijana huyo alionyesha ukaidi, akakataa kufanya kazi, na tabia zake zikazidi kuwa changamoto. Tukio lililomuumiza zaidi, anasema, ni pale alipopiga mama yao mzazi, jambo lililomlazimu kumfukuza nyumbani kwa ajili ya usalama wa familia.
Kauli ya Gloria imekuja mara baada ya kijana huyo kujitokeza mtandaoni akiomba msaada watu wamsaidie na makazi, madai ambayo Gloria mwenyewe ameyakana akisema kuwa familia yao ina majumba ya kutosha ya kifahari.