Msanii wa Bongofleva, Marioo amesema anajiandaa kuachia albamu yake mpya ambayo imekamilika.
Marioo amesema anachokifanya kwa sasa ni kutayarisha Video za nyimbo zitakazopatikana kwenye albamu hiyo kabla ya kuingia sokoni hivi karibuni.
Hata hivyo marioo hajatuambia jina la album, idadi nyimbo na wasanii aliyowashirikisha kwenye album yake hiyo ila ni jambo la kusubiriwa.
Wasanii wengine tanzania ambao tayari wametangaza kukamilika kwa albamu zao ni pamoja na Diamond Platnumz, Young Lunya, Lava Lava, Tommy Flavour, Maua Sama, Ommy Dimpoz na wengine wengi.