Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Akothee Ataka Jamii Iache Kuingilia na Kukosoa Mtindo Wake wa Mavazi

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amewataka wakosoaji wake kuacha kuingilia mtindo wake wa mavazi na maisha binafsi, akisema lawama nyingi zinazomkabili zinatoka kwa watu wasioishi kulingana na maadili wanayoyahubiri mitandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee ameweka wazi kuwa hataki kuelekezwa jinsi ya kuvaa na watu anaodai wanaficha maovu yao binafsi nyuma ya pazia la maadili ya kijamii. Ameeleza kuwa kuna watu wanaojifanya walinzi wa maadili ilhali familia zao zinakumbwa na matatizo makubwa kama ulevi, usaliti katika ndoa na kuvunjika kwa familia. Msanii huyo amesisitiza kuwa sanaa ni njia ya kujieleza na kwamba jamii inapaswa kujifunza kuheshimu uhuru wa wasanii badala ya kuwahukumu kwa misingi ya mitazamo binafsi. Aidha, amewataka wanaomkosoa waangalie kwanza mienendo yao kabla ya kumshambulia hadharani. Kauli hiyo ya Akothee imekuja baada ya kukosolewa vikali na baadhi ya wanajamii kufuatia kusambaa kwa vipande vya video ya wimbo wake mpya uitwao Society. Video hiyo inaonyesha mavazi yanayobana na kufichua sehemu nyeti za mwili wake.

Read More
 Akothee Awaonya Mabinti zake Dhidi ya Kuingia Kwenye Mahusiano na Wanasiasa

Akothee Awaonya Mabinti zake Dhidi ya Kuingia Kwenye Mahusiano na Wanasiasa

Mwanamuziki, Akothee, ameibua mjadala mitandaoni baada ya kutoa onyo kali kwa mabinti zake kuhusu kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanasiasa. Akizungumza kupitia mitandao yake ya kijamii, Akothee amesema kuwa ameshuhudia visa vingi vya vijana wa kike kuumizwa kihisia na hata kifedha wanapodanganywa na viongozi wanaotumia nafasi zao kwa anasa na starehe. Akothee amesisitiza kuwa wanasiasa wengi huwa na maisha yenye mkanganyiko na ratiba isiyoeleweka, jambo linalofanya mahusiano yao kuwa na changamoto nyingi. Amehitimisha ujumbe wake kwa kusema anataka mabinti wake wakue wakiwa na uthabiti wa kimaamuzi na wasikubali kushawishiwa na hadhi au pesa. Kauli ya Akothee imezua mjadala mtandaoni, baadhi wakikubaliana naye kuwa vijana wengi wanahitaji ushauri wa namna hii, huku wengine wakiona kila mtu anapaswa kupewa nafasi ya kufanya maamuzi yake ya kimahusiano.

Read More
 Akothee Akerwa na Swali la Shabiki Kuhusu Nelly Oaks

Akothee Akerwa na Swali la Shabiki Kuhusu Nelly Oaks

Mwanamuziki na mfanyabiashara Akothee ameonekana kukerwa na shabiki aliyemuuliza kuhusu aliyekuwa mpenzi wake, Nelly Oaks, wakati akiwa nchini Afrika Kusini. Akothee alikataa kabisa kujadili kuhusu uhusiano wake wa zamani, akionyesha kwamba amesonga mbele na hataki kurudi kwenye mada hizo. Ameeleza kuwa yeyote anayevutiwa na habari za Nelly Oaks anapaswa kufuatilia taarifa zake mtandaoni, badala ya kumrudisha kwenye uhusiano uliokwisha. Akiwa katika mazingira mapya na shughuli mbalimbali Afrika Kusini, Akothee ameonyesha kutoridhishwa na mashabiki wanaoendelea kumhusisha na maisha yake ya zamani, akisisitiza kuwa yupo katika hatua tofauti ya maisha na kwamba kuna wanaume wengi kwenye dunia, hivyo hajafungamana na yaliyopita. Kauli yake imewafanya mashabiki kutofautiana mtandaoni, baadhi wakimwelewa Akothee kwa kutaka kuheshimu maisha yake mapya, huku wengine wakionyesha udadisi zaidi kuhusu historia yake ya kimapenzi.

Read More
 Akothee Awakosoa Mastaa Wanaoishi Maisha ya Kuigiza Mtandaoni

Akothee Awakosoa Mastaa Wanaoishi Maisha ya Kuigiza Mtandaoni

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amewakosoa vikali baadhi ya mastaa nchini humo kwa kile alichokiita kuishi maisha ya uongo kwenye mitandao ya kijamii. Akothee anadai kuwa mastaa wengi wanajionyesha kama watu wenye utajiri mkubwa mtandaoni, lakini ukweli ni kwamba wengi wao hawana uwezo huo katika maisha ya kawaida. Mwanamama huyo, amewataka mashabiki kutopoteza muda kujilinganisha na maisha ya watu wanaowaona mtandaoni, akisema maisha ya mtandaoni mara nyingi hayalingani na uhalisia. Sanjari na hilo, Akothee amewakosoa baadhi ya content creators wanaotafuta umaarufu kwa kutumia matusi na kuwashambulia mastaa, akisema aina hiyo ya maudhui inachochea chuki na inakosa ubunifu. Amewahimiza kutengeneza maudhui yanayozingatia kazi yenye thamani badala ya kutegemea kiki za muda mfupi.

Read More
 Akothee Amkingia Kifua Winnie Odinga Dhidi ya Ubaguzi wa Kisiasa

Akothee Amkingia Kifua Winnie Odinga Dhidi ya Ubaguzi wa Kisiasa

Mwanamuziki na mfanyabiashara maarufu nchini Kenya, Akothee, amejitokeza kutoa msimamo mkali, akimkinga kifua Mbunge wa EALA, Winnie Odinga dhidi ya kile anachokiita ubaguzi wa kisiasa. Akothee amekemea vikali wale wanaomdhalilisha Winnie Odinga, binti ya hayati Raila Odinga, kwa kigezo cha kuwa hajaingia kwenye ndoa. Kupitia ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, Akothee, amesisitiza kuwa sifa za mtu katika siasa hazipaswi kuhukumiwa na hali yake ya ndoa. Akizungumzia suala la ndoa, amesema kwa shauku kwamba ndoa haifai kuchukuliwa kama mafanikio, akidai kuwa taasisi hiyo ya ndoa ni kwa ajili ya wanawake ambao hawana mwelekeo wa maisha na ambao wanahitaji kuongozwa. Akothee amewaonya vikali wanasiasa na wafuasi wao wanaotumia lugha chafu na unyanyasaji dhidi ya wanawake katika ulingo wa siasa, akisisitiza umuhimu wa kuzingatia akili, bidii, na mafanikio ya wanawake badala ya kuzingatia hali yao ya kibinafsi ya ndoa. Mwanamama huyo amemalizia ujumbe wake kwa kusema kwamba hata kama watu hawakubaliani na mawazo ya kisiasa ya Winnie, wanapaswa kukosoa kwa staha na kuheshimu utu wake kama binadamu.

Read More
 Akothee Aachia Rasmi EP Yake Mpya

Akothee Aachia Rasmi EP Yake Mpya

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, ameachia rasmi EP yake mpya inayokwenda kwa jina “Tatu Bora”, kazi ambayo imeimbwa kwa lugha ya Dholuo. Tatu Bora EP ina jumla ya ngoma tatu kali, ambazo zote amezifanya bila kolabo na msanii yeyote, ikiwa ni hatua inayoonyesha ubunifu na ubora wake binafsi. Nyimbo zilizopo ndani ya EP hiyo ni Bi Mos, Tururu, na Koyo, na zinapatikana exclusive katika majukwaa yote ya kusikiliza na kupakua muziki mtandaoni. Kupitia ujumbe wake kwa mashabiki, Akothee ameeleza kuwa ameachia kazi hii kama zawadi kwa wafuasi wake na kama msukumo kwa wanawake, akisisitiza kuwa katika ulimwengu wa ndoa na changamoto zake, muziki unaweza kuwa tiba na faraja. “Tatu Za Bora EP” ni kazi ya kwanza kutoka kwa Akothee tangu atoke hospitalini ambako alikuwa amelazwa kutokana na matatizo ya tumbo.

Read More
 Akothee Atoka Hospitalini Baada ya Matatizo ya Tumbo

Akothee Atoka Hospitalini Baada ya Matatizo ya Tumbo

Msanii asiyeishiwa na matukio kila leo, Akothee, ameibuka na taarifa njema kwa mashabiki wake baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini kufuatia kulazwa kwa muda kutokana na matatizo ya tumbo. Akizungumza mara baada ya kutoka hospitalini, Akothee ametoa shukrani za dhati kwa wote waliomuombea apone haraka na waliomtumia salamu za faraja wakati wa kipindi hicho kigumu. Ameeleza kuwa maombi na upendo wa mashabiki wake yamempa nguvu na matumaini makubwa ya kupona. Hata hivyo, amewashangaza wengi baada ya kufichua kuwa kulikuwa na baadhi ya watu waliotumia mitandao ya kijamii kumtakia mabaya, akiwemo wanaodaiwa kumtakia kifo. Amesema tukio hilo halikumvunja moyo, bali limempa sababu zaidi ya kuthamini wale wanaomuunga mkono kwa dhati. Akothee alikuwa amelazwa hospitalini baada ya kukumbwa na matatizo ya tumbo yaliyomfanya kupata maumivu makali. Kwa sasa, anasema afya yake imeimarika na ameanza kuendelea vyema chini ya uangalizi wa madaktari.

Read More
 Akothee Akimbizwa Hospitalini Baada ya Maumivu Makali ya Tumbo

Akothee Akimbizwa Hospitalini Baada ya Maumivu Makali ya Tumbo

Mwanamuziki kutoka Kenya, Akothee, amefichua tukio la kutisha alilopitia alfajiri ya jana baada ya kuanguka chooni kutokana na maumivu makali ya tumbo. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee amesema kuwa hali hiyo ilianza usiku wa manane baada ya kushuhudia video ya kutisha ya msichana aliyekuwa nyumbani kwake. Amesema tukio hilo lilimshtua kiasi cha kumsababishia maumivu makali, kutapika, kuharisha, na hisia za woga ambazo zilimfanya kushindwa hata kulala. Akothee ameeleza kuwa maumivu yalimfanya kulala ndani ya choo kwa kujaribu kupunguza hali hiyo. Amesema kufikia saa tisa asubuhi, nguvu zake zilimwishia na akaanguka sakafuni huku akijaribu kufika chumbani kwa watoto wake akiwa analia kwa maumivu makali. Mwanamama huyo amesema watoto wake walimpata akiwa amelala chooni na mara moja walimkimbiza hospitalini kupitia kitengo cha dharura. Amedai familia yake ilikabiliana na changamoto ya kupokea matibabu haraka baada ya muuguzi kuonyesha ukatili na kutokuwa na huruma. Hata hivyo Akothee amesema baada ya jitihada hizo, hatimaye alipatiwa matibabu na sasa anaendelea kupona, ingawa tukio hilo limemuacha akiwa na hofu kubwa.

Read More
 Msanii Akothee Afunguka Kuhusu Mipango Yake ya Mazishi

Msanii Akothee Afunguka Kuhusu Mipango Yake ya Mazishi

Mwanamuziki kutoka Kenya, Akothee, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kutoa tamko jipya kuhusu mipango yake ya mazishi. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, ameeleza kuwa hataki chakula chochote kipikwe siku ya mazishi yake, akisisitiza kuwa watu wanaohudhuria wanapaswa kubeba chakula chao kutoka nyumbani badala ya kutegemea familia yake. Akothee amehoji ni vipi watu wanaweza kumudu kula kwenye mazishi, akiongeza kuwa yeyote anayetaka kula siku hiyo anapaswa kuchangia gharama mapema na kula nyumbani kwao. Mwanamama huyo, amesema wazi kuwa hafurahishwi na utamaduni wa baadhi ya watu kutumia mazishi kama fursa ya kula na kunywa badala ya kutoa heshima kwa marehemu. Kauli yake inakuja siku chache baada ya kueleza kuwa atakapoaga dunia angependa kuzikwa ndani ya saa 48, bila kujali mahali atakapofia, akisisitiza kuwa hataki mchakato wa mazishi wake ucheleweshwe.

Read More
 Akothee Aeleza Namna Magonjwa Yalivyobadilisha Maisha Yake

Akothee Aeleza Namna Magonjwa Yalivyobadilisha Maisha Yake

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya, Akothee, amefunguka kuhusu mabadiliko makubwa kwenye maisha yake baada ya kugunduliwa na matatizo ya kiafya yakiwemo mashambulizi makali ya kichwa (migraine), damu kuganda, na fibroids. Kupitia ujumbe mrefu kwenye ukurasa wake wa Instagram, Anasema hali hizo zimemlazimisha kupunguza kasi na kubadili mtazamo wake kuhusu maana ya nguvu na maisha. Akothee amesema changamoto hizo zimemfundisha kuwa nguvu ya kweli si kupambana kila wakati, bali ni kujipa nafasi ya kupumzika na kupona. Ameeleza kuwa sasa anaheshimu mwili wake zaidi, anaepuka presha zisizo za lazima, na kutilia mkazo amani na utulivu kama tiba yake kuu. Aidha, amewatia moyo wanawake wengine wanaopitia changamoto za kiafya kimyakimya, akisema hawapaswi kuona hali hizo kama udhaifu, bali kama safari ya mabadiliko na ukuaji.. Ameongeza kuwa sasa anaheshimu zaidi mwili wake na kuepuka presha zisizo za lazima. Kwa ucheshi wake wa kawaida, Akothee ametaniana na wafuasi wake akisema wanaweza kumuita “Fibroids, Migraines, Bloodclot Akoth Kokeyo,” huku akisisitiza kwamba upendo wa kweli ni ule unaoonyeshwa mtu akiwa hai, na kwamba huu ni wakati wake wa kuthamini utulivu.

Read More
 Akothee Akosoa Vikali Wanaodhihaki Maumbile ya Raila Odinga Junior

Akothee Akosoa Vikali Wanaodhihaki Maumbile ya Raila Odinga Junior

Msanii kutoka Kenya, Akothee, ameonyesha masikitiko makubwa kufuatia dhihaka zinazomlenga Raila Odinga Junior, mwana wa hayati Raila Amolo Odinga, baada ya picha na video kusambaa mitandaoni zikionyesha baadhi ya watu wakicheka maumbile yake. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Akothee amelaani vikali tabia ya baadhi ya watu kutumia mitandao vibaya kwa kumkejeli Junior kutokana na maumbile yake. Amesema kizazi cha sasa kimepoteza utu, heshima na huruma, na kwamba baadhi ya vijana wanatumia mitandao ya kijamii vibaya kutokana na malezi duni. Msanii huyo amesema kuwa matendo kama hayo yakiachwa bila kudhibitiwa yanaweza kuchochea unyanyasaji hata kwa watu wenye ulemavu mitaani. Amesisitiza kuwa vijana wanaohusika lazima wachukuliwe hatua za kisheria ili wajifunze kuishi kwa heshima na utu katika jamii. Aidha, Akothee amemtumia ujumbe wa faraja Raila Junior, akimtaja kama shujaa anayestahili upendo na heshima kutoka kwa Wakenya. Pia amempongeza Mama Ida Odinga kwa uvumilivu wake na kuahidi kupigania heshima ya familia hiyo, akisema yuko tayari kushughulikia suala hilo kwa ukaribu. Kauli ya Akothee imezua mjadala mkubwa mitandaoni, wengi wakimpongeza kwa kusimama kidete dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni.

Read More
 Akothee Asema Hawezi Kuolewa na Mwanaume wa SDA

Akothee Asema Hawezi Kuolewa na Mwanaume wa SDA

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Akothee, amezua mjadala mitandaoni baada ya kutoa matamshi yenye utata kuhusu wanaume wa Kanisa la Waadventista (SDA). Kupitia video aliyoiposti kwenye mitandao yake kijamii, amesema kuwa hawezi kamwe kuolewa na mwanaume kutoka kanisa hilo kwa kuwa wanaume wengi wa SDA ni wakali na wenye masharti mengi kuhusu maisha ya kila siku, jambo analoliona haliendani na mtindo wake wa maisha. Mwanamama huyo ameongeza kuwa hawezi kuishi kwenye ndoa inayomnyima uhuru wa kufurahia maisha, akitaja mambo kama kunywa mvinyo na kula nyama kuwa sehemu ya starehe anazopenda. Hata hivyo amesema kuwa licha ya yeye mwenyewe kuwa Mwaadventista, bado hawezi kumpendekeza mtu kuolewa na wanaume kutoka dhehebu hilo.

Read More