Akothee Amkingia Kifua Azziad Dhidi ya Wakosoaji wa Mitandaoni

Akothee Amkingia Kifua Azziad Dhidi ya Wakosoaji wa Mitandaoni

Mwanamuziki, Akothee, amejitokeza kumtetea TikTok queen na mtangazaji Azziad Nasenya baada ya kuvamiwa mitandaoni kwa madai ya kuishi maisha ya kuigiza. Kupitia waraka wake Instagram, Akothee ameeleza kuwa anampenda na kumheshimu Azziad kwa kuwa na ndoto kubwa na kuonesha ujasiri wa kukimbizana na maisha. Amesisitiza kuwa hatua ya mrembo huyo kupata mkopo wa millioni 25 za Kenya na kununua nyumba akiwa na umri wa miaka 25 ni jambo la kupongezwa na si kulaumiwa, kwani ni nadra vijana kufanikisha mambo makubwa wakiwa na umri mdogo. Amesema kuwa wakati vijana wa rika la Azziad leo wanajitahidi kujenga maisha yao, wengi wa kizazi kilichomtangulia walihangaika na changamoto kubwa kama ndoa zilizoshindikana, kulea watoto peke yao na hata kutokuwa na akaunti ya benki wala ajira. Kwa maoni yake, hatua ya Azziad kuwekeza katika nyumba ni mfano bora wa kuchukua jukumu la maisha yake mapema. Akothee pia amekosoa wanaume wanaoendelea kumsema vibaya Azziad mitandaoni ilhali wao bado wanashindwa hata kumudu mikopo midogo. Kwa mtazamo wake, badala ya kumkosoa, Wakenya kwa jumla wana nafasi ya kujifunza kutoka kwake. Hata hivyo amehitimisha ujumbe wake kwa kusema kuwa Azziad ni msichana mwenye ndoto kubwa, anayeendelea kujijenga na kuwa chanzo cha msukumo kwa vijana wengi, na kwamba jamii inapaswa kusherehekea ujasiri wake badala ya kumshusha

Read More
 Akothee Alazwa Hospitalini Baada ya Kuteseka kwa Miezi Miwili

Akothee Alazwa Hospitalini Baada ya Kuteseka kwa Miezi Miwili

Mwanamuziki na mfanyibiashara maarufu nchini, Esther Akoth maarufu kama Akothee, amefichua kuwa amekuwa akisumbuliwa na maumivu makali kwa zaidi ya miezi miwili na hatimaye amelazwa hospitalini tangu Jumatatu wiki hii. Kupitia waraka mrefu kwenye Instagram, Akothee alieleza kuwa maisha yake yamekuwa ya faragha kiasi kwamba mashabiki wake hawakujua hali yake ya kiafya hadi alipoamua kufunguka. Alisema alijisukuma kupita kiasi licha ya kubeba maumivu kwa zaidi ya miezi miwili. Shida hiyo ilijitokeza zaidi wakati wa mtihani wa pili ambapo ghafla akili yake iliganda, karatasi ya mtihani ikaonekana kumlemea na akaanza kuhisi kichefuchefu. Akiwa Homa Bay, alikiri kuwa alitegemea dawa za kupunguza maumivu na za kulegeza misuli ili kuendelea na majukumu yake, akiwemo kumalizia ratiba aliyokuwa ameahidi mashabiki wake. Hata hivyo, alipata shambulio jingine kali wakati alipotarajia kuruhusiwa kuondoka hospitalini, hali iliyomlazimu kuendelea kupata uangalizi wa karibu. Ujumbe wake umeonyesha ni kwa namna gani alijitolea kukamilisha majukumu yake licha ya hali ngumu ya kiafya, jambo lililoibua mjadala mkubwa kuhusu shinikizo la kazi na athari zake kwa wasanii na viongozi wa kijamii. Mashabiki wake wamejitokeza kwa wingi kumtakia nafuu ya haraka, huku wakimsifu kwa ujasiri wa kuendelea kusimama imara licha ya changamoto alizopitia.

Read More
 Akothee Avunja Ukimya Baada ya Kukosolewa Kuhusu Mavazi

Akothee Avunja Ukimya Baada ya Kukosolewa Kuhusu Mavazi

Mwanamuziki wa Kenya, Esther Akoth maarufu kama Akothee, amejibu vikali ukosoaji unaoendelea mitandaoni kuhusiana na mavazi aliyovaa katika tukio la hivi karibuni huko Homa Bay. Kupitia mitandao ya kijamii, Akothee alisisitiza kuwa hana jukumu la kuwa mfano wa kuigwa kwa mtu yeyote na kwamba anapaswa kuachiwa aishi maisha yake kwa namna anayoona inafaa. Akothee alisema licha ya mashambulizi ya maneno anayopokea, bado ataendelea kushiriki katika matukio anayoalikwa na kufanya maonyesho kwa mtindo wake wa kipekee. Mwanamuziki huyo ameendelea kusisitiza kuwa maamuzi yake ya kisanii na binafsi hayapaswi kupimwa kwa kipimo cha maadili ya mtu mwingine, akiwataka wakosoaji waache kumfuatilia kwa matarajio yasiyoendana na mtindo wake wa maisha. Kauli ya Akothee imeibua mjadala mitandaoni, ambapo wafuasi wake wamegawanyika kati ya wanaomuunga mkono kwa kusimamia haki yake ya kujieleza na wale wanaoamini kuwa umma una haki ya kumkosoa kutokana na hadhi yake kama msanii maarufu. Tukio hili linakuja siku chache tu baada ya picha na video za Akothee akiwa katika vazi lililoibua hisia kali kusambaa mitandaoni, na kusababisha mjadala mkubwa kuhusu mipaka ya uhuru wa msanii na matarajio ya jamii

Read More
 Mashabiki Wamkemea Akothee kwa Kudharau Kazi ya Fundi

Mashabiki Wamkemea Akothee kwa Kudharau Kazi ya Fundi

Msanii nyota wa Kenya, Akothee, amezua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii baada ya kutoa kauli kali iliyotafsiriwa kama dharau kwa fundi aliyemtengenezea meza. Kauli yake kwamba meza hiyo “inafanana na jeneza”, imechukuliwa na mashabiki kama ya kudhalilisha na kukosa heshima kwa mafundi wanaojituma kujitafutia riziki. Mashabiki waliitaja kauli hiyo kuwa ya kuumiza na kukosa utu, wakimtaka msanii huyo kuheshimu bidii ya mafundi wanaojituma licha ya changamoto. “Hata kama hukupenda kazi, si lazima kumdhalilisha mtu. Huo ni ukatili,” aliandika shabiki mmoja. Wengine walimtaka Akothee kutumia umaarufu wake kuhamasisha heshima kwa watoa huduma wa kawaida badala ya kuwavunjia hadhi hadharani. Pia, walihimiza mawasiliano ya moja kwa moja na ya staha kama njia bora ya kushughulikia changamoto za kibiashara. “Umaarufu haumpi mtu ruhusa ya kumshusha mwingine hadharani. Wafanyakazi wa mikono wanastahili heshima pia,” aliongeza mwingine Hadi sasa, Akothee hajatoa tamko lingine zaidi ya kauli yake ya TikTok, huku mjadala ukiendelea kushika kasi mitandaoni na wengi wakimtaka azingatie lugha na heshima anapotoa mrejesho kwa umma. Mzozo huo ulianza baada ya fundi seremala kumuanika Akothee kwenye mitandao ya kijamii akidai kuwa hajalipwa salio la kazi yake, licha ya kumkabidhi meza aliyokuwa ameagiza. Katika kujibu kupitia TikTok Live, Akothee alidai tayari alimlipa fundi huyo asilimia 80 ya malipo lakini kazi aliyopokea haikukidhi matarajio yake. “Nilimlipa 80%, lakini kazi si ya kiwango nilichotaka. Aichukue tu, hiyo meza inafanana na jeneza,” alisema Akothee mbele ya mashabiki wake mtandaoni.

Read More
 Akothee Afunguka Kuhusu Mzozo na Fundi, Adai Hakutimiza Makubaliano

Akothee Afunguka Kuhusu Mzozo na Fundi, Adai Hakutimiza Makubaliano

Mwanamuziki kutoka Kenya, Akothee, ameibuka na kutoa kauli yake kuhusiana na mgogoro unaoendelea kati yake na fundi seremala aliyemtengezea samani. Kupitia mitandao ya kijamii, Akothee ameeleza kwa kina kwamba fundi huyo hakutimiza masharti ya kazi kama walivyokubaliana. Akothee amesema licha ya kutoridhishwa na kazi iliyofanyika, tayari alikuwa amemlipa fundi huyo asilimia 80 ya malipo yaliyokubaliwa. Alidai kuwa meza aliyoletwa haikukidhi viwango vya ubora aliokuwa ameelekeza, hivyo hakusita kuonyesha kutoridhishwa kwake. “Sio kila mtu anayeitwa fundi anaelewa kazi. Nilimlipa 80% lakini alileta meza isiyokidhi viwango tulivyokubaliana,” aliandika Akothee. Mwanamuziki huyo ambaye pia ni mfanyabiashara ameonya mafundi dhidi ya kutumia majina ya watu maarufu kujinufaisha kibiashara ilhali hawatimizi kazi kwa kiwango kinachotarajiwa. Aliongeza kuwa ana ushahidi wote wa mawasiliano na malipo aliyofanya. “Naomba arudishe hela zangu na achukue meza yake. Sina haja nayo,” alisema kwa msisitizo. Sakata hilo limevutia hisia mbalimbali mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimuunga mkono Akothee kwa kusimamia haki yake, huku wengine wakitaka pande zote mbili kusuluhisha suala hilo kwa njia ya amani.

Read More
 Mwanamume Amuanika Akothee Mtandaoni kwa Kosa la Kutolipa Deni la Miezi Mitano

Mwanamume Amuanika Akothee Mtandaoni kwa Kosa la Kutolipa Deni la Miezi Mitano

Msanii maarufu wa Kenya, Akothee, amejikuta katika hali ya lawama baada ya mwanamume mmoja kujitokeza hadharani akimshutumu kwa kutolipa deni linalodaiwa kudumu kwa zaidi ya miezi mitano. Katika video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, mwanamume huyo anadai kuwa alifanya kazi ya design na kurekebisha reception ya ofisi ya Akothee, akajitahidi kufanya kila aliloagizwa, hata kurekebisha makosa yaliyotokea wakati wa utekelezaji wa majukumu yake.  “Akothee nilikufanyia kazi. Saa hii ni miezi mitano. Kazi nilifanya, reception nilifanya, ukatoa makosa nikarekebisha,” alisema kwa masikitiko. Anadai kuwa baada ya kumaliza kazi hizo, Akothee alizima simu yake, akamzuia kwenye WhatsApp, na hata hakuwahi kujibu ujumbe wowote wala kupokea simu zake. Pia alifichua kuwa licha ya matatizo ya kifedha anayopitia, bado analazimika kulipa baadhi ya gharama alizotumia wakati wa kazi, ikiwemo gari aliloleta hadi kwenye ofisi ya msanii huyo.  “Bado kuna vitu nafaa kulipa. Ile gari ilinileta mpaka kwa ofisi yako, hiyo gari nafaa kulipa. Tafadhali tu, naomba nilipe,” aliongeza kwa sauti ya unyonge. Mwanamume huyo alisisitiza kuwa hana nia mbaya na Akothee, wala hajitafutii umaarufu kupitia mgogoro huo, bali analilia haki yake kama mfanyakazi. Mpaka sasa, Akothee hajatoa kauli rasmi kuhusu tuhuma hizo, lakini mashabiki na wafuasi wake kwenye mitandao wamegawanyika, baadhi wakimtetea na wengine wakitaka atoe maelezo au kumlipa mwanaume huyo ikiwa madai ni ya kweli. Hata hivyo, tukio hilo limezua mjadala mitandaoni kuhusu haki za wafanyakazi na uwajibikaji wa watu maarufu katika kulipa huduma wanazopewa.

Read More
 Akothee Amwandikia Rais Ruto: “Tufungue Mlango wa Mazungumzo”

Akothee Amwandikia Rais Ruto: “Tufungue Mlango wa Mazungumzo”

Mwanamuziki, mfanyabiashara, na mwanaharakati wa kijamii Akothee maarufu kama Rais wa Akina Mama Wasio na Wenzi, ameandika barua ya wazi kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, akitoa kilio cha kina kwa niaba ya akina mama, vijana, wazazi, na wajasiriamali nchini. Katika barua hiyo yenye hisia nzito, Esther anasema haandiki kama mtu maarufu tu, bali kama mzazi anayeishi na vijana wa kizazi cha Gen Z, ambao wamekuwa mstari wa mbele katika maandamano ya hivi karibuni kote nchini. “Nakuandikia si tu kama raia, bali kama mama, mama asiye na mwenzi wa vijana wa Gen Z – na kama Mkenya ambaye bado anaamini katika roho ya taifa hili,” alianza kwa maneno yenye kugusa moyo. Esther anaelezea hali ya taifa kwa sasa kuwa ya kusikitisha, mitaa imejaa hofu, anga limefungwa na huzuni, na familia pamoja na biashara ziko katika hali ya taharuki. Anasema vijana na wananchi kwa ujumla hawatafuti tu mabadiliko ya sera, bali wanalilia usalama, uthabiti, na uongozi unaosikiliza. “Wakenya sasa hawapigi kelele kwa mabadiliko tu. Wanapaza sauti kwa ajili ya usalama, uthabiti na uelewa. Wanataka uongozi unaosikiliza; nchi ambayo watoto wao wanaweza kwenda shule bila vurugu, biashara kufunguliwa bila hofu ya uporaji, na familia zisizopoteza wapendwa kwa risasi au kipigo,” alieleza kwa uchungu. Esther pia anahoji uhalali wa taifa kuhubiri amani ulimwenguni huku picha halisi ya ndani ikionyesha vurugu, mauzoo ya matumaini, na uharibifu wa kiuchumi unaowatesa wananchi wa kawaida. Akitilia mkazo kuwa barua hiyo si ya lawama, bali ya uwajibikaji wa pamoja, anamtaka Rais kuchukua hatua ya kidiplomasia ya kuanzisha mazungumzo ya kweli. “Hili si suala la lawama. Ni kuhusu uwajibikaji wa pamoja. Tukivutana, tunapoteza sote. Na anayepoteza zaidi ni Kenya.” Kama mama, anasema anaelewa kiu ya vijana kusikilizwa, ndiyo maana baadhi yao walijaribu kuingia bungeni. Sio kwa fujo, bali kama njia ya kuonyesha kutotambuliwa kwao katika maamuzi ya taifa. Alihitimisha barua hiyo kwa ombi la moja kwa moja kwa Rais, kuwakutanisha na wazazi, akina mama, na vijana Ikulu kwa mazungumzo ya wazi. “Nakuomba kwa unyenyekevu unikubalie nafasi ya kusikilizwa, si kwa ajili yangu tu, bali kwa ajili ya mama wote, wazazi, na vijana wetu. Tufungulie mlango. Tuweke tofauti kando. Tufikirie pamoja. Natumaini mazungumzo yanaweza kuokoa roho ya taifa hili.” Barua hiyo imeendelea kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, ambapo wengi wameisifu kama sauti ya ujasiri, huruma, na matumaini, sauti inayozungumza kutoka moyoni mwa mzazi wa kawaida hadi juu ya meza ya mamlaka.

Read More
 Akothee Atangaza Kumsamehe Dada Yake Licha ya Maumivu ya Zamani

Akothee Atangaza Kumsamehe Dada Yake Licha ya Maumivu ya Zamani

Mwanamuziki na mfanyabiashara maarufu wa Kenya, Akothee, amegusa mioyo ya wengi baada ya kushiriki ujumbe wa kihisia kwa dada yake, Elseba Awuor, akifichua kuwa amemsamehe na kuamua kuendelea na maisha bila chuki. Kupitia mitandao ya kijamii, Akothee aliandika ujumbe uliojaa hisia, akieleza kuwa msamaha wake haukutokana na ombi la dada yake, bali ni kwa ajili ya kutafuta amani ya moyo na kuondoa mzigo wa hasira alioubeba kwa muda mrefu. “Nimekusamehe, si kwa sababu uliomba msamaha, si kwa sababu ulirekebisha madhara hadharani, bali kwa sababu nastahili amani. Moyo wangu ni mzito mno kubeba hasira tena,” aliandika Akothee kwa hisia. Ujumbe huo mzito wa kihisia umeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki wake na wafuasi wa familia hiyo, wengi wakimsifu Akothee kwa kuchagua msamaha na kuponya nafsi yake badala ya kubeba chuki. Ingawa hakufafanua kwa kina yaliyotokea kati yake na dada yake Elseba, maneno yake yanaashiria majeraha ya kihisia yaliyomgusa kwa kiwango kikubwa. Hata hivyo, msanii huyo mwenye ujasiri amesema hatua hiyo ya kusamehe ni sehemu ya safari yake ya uponyaji na kutafuta utulivu wa ndani. Mashabiki na watu maarufu wamejitokeza kumpongeza kwa uamuzi huo, wakisema ni mfano mzuri wa ukuaji wa kiroho na kiakili. Wengine walimtia moyo kuendelea na safari ya upendo na mshikamano wa kifamilia, licha ya changamoto zilizopo. Akothee, anayejulikana kwa ujasiri wake wa kusema mambo bila kuficha, ameendelea kuwahamasisha watu wengi kuhusu umuhimu wa kuachilia chuki na kuchagua amani kama njia ya maisha

Read More
 Akothee amuombea msamaha kwa Mungu shabiki aliyemuombea mabaya

Akothee amuombea msamaha kwa Mungu shabiki aliyemuombea mabaya

Msanii na mfanyibiashara tajika Akothee amezua gumzo mtandaoni baada ya kumjibu Shabiki kwenye post yake. Akothee kwenye mtandao wake wa kijamii alipost picha akiwa mjamzito lakini Shabiki Kwa jina Mercy Joe aliandika kwenye komenti akiombea ujauzito huo upotee. Jambo ambalo limeleta hisia chungu nzima huku Akothee akimjibu na kukwambia maombi yake yalijibiwa na alipoteza ujauzito huo. Hata hivyo amemalizia kwa kumuombea msamaha kwa Mungu shabiki huyo aliyeuombea ujauzito wake mabaya. Baadhi ya wakenya wameonekana kumhurumia Akothee huku wengine wakimshambulia shabiki huyo kwa kumtakia maneno mabaya mwimbaji huyo.

Read More
 Akothee kuwachukulia hatua kali za kisheria wanablogu wanaotumia maudhui yake bila ruksa

Akothee kuwachukulia hatua kali za kisheria wanablogu wanaotumia maudhui yake bila ruksa

Staa wa muziki nchini Akothee ametishia kuwachukulia hatua kali za kisheria wanablogu wanaotumia maudhui anayochapisha kwenye mitandao yake ya kijamii. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema anapania kuzifungulia kesi blogu hizo kwa kutumia maudhui yake bila ridhaa yake huku akisisitiza kuwa huenda akawatoza faini ya shillingi millioni 300 ili iwe funzo kwao wanapoandika habari zisizo na uhakika. Mama huyo wa watoto 5 amesema wanablogu mara nyingi wamekuwa wakipendelea kuchapisha taarifa hasi dhidi yake badala ya kumsaidia kukuza biashara yake. Akothee amewatolea uvivu wanablogu wa kenya akiwataja kama watu wasiokuwa na kipato ambao wamekuwa na mazoea ya kujificha nyuma kompyuta kumharibia brand au chapa yake ya muziki.

Read More
 Akothee akanusha kununulia gari na mpenzi wake mwenye asili ya kizungu

Akothee akanusha kununulia gari na mpenzi wake mwenye asili ya kizungu

Staa wa muziki nchini Akothee amekanusha kununuliwa gari na mpenzi wake mwenye asili ya kizungu siku chache baada ya kudai kuwa amepewa kama zawadi. Kupitia instagram yake mama huyo wa watoto watatu amedai kuwa gari hilo lilikuwa la serikali ya kaunti. “Gari ni ya county usikonde sweetie. Sasa 6.8 m nikitu ya kupigia kelele ,hata sijaongelea haki ,hiyo ni pesa kidogo sana kwangu” Ameandika Instagram akimjibu shabiki aliyetilia shabiki gari aliyezawadi. Hata hivyo kauli hiyo ya Akothee imetafsiriwa kama kejeli kwa baadhi ya watu waliokuwa wanamkosoa baada ya kuweka wazi kuzawadi gari aina na mpenzi wake. Utakumbuka katika siku za hivi karibuni Akothee amekuwa akitamba sana mtandaoni na mpenzi wake mpya tangu atangaze tena kurejea kwenye ulimwengu wa mapenzi akiwa na matarajio ya kuingia katika maisha ya ndoa amtambulishe mpenzi wake.

Read More
 Akothee awajia juu wanaomhusisha na Wakenya wanaodhulumiwa Saudia Arabia

Akothee awajia juu wanaomhusisha na Wakenya wanaodhulumiwa Saudia Arabia

Msanii na mfanyabiashara maarufu nchini Akothee amechukizwa na kitendo cha mashabiki zake kumhusisha na taarifa za wakenya wanaodhulumiwa na waajiri wao katika nchi za miliki ya kiarabu. Kupitia Instagram yake mwanamama huyo ameandika ujumbe wenye makasiriko akiwataka walimwengu waache tabia hiyo ambayo kwa mujibu wake inamuumiza kila mara akiona habari za wakenya wenzake wakinyanyaswa ughaibuni. Akothee hata hivyo ametoa changamoto kwa wanaomshinikiza kutatua tatizo la wakenya kudhulumiwa Saudia Arabia kumteua kwenye wadhfa wa kisiasa kwani kwa sasa hana uwezo wa kufanikisha hilo. Kauli yake imekuja wiki mbili baada ya kudaiwa kuwa anamiliki taasisi inayowasajili wakenya kwa ajili ya kuwatafutia kazi katika miliki za kiarabu. Madai ambayo aliyapinga vikali akisema kwamba hayana msingi wowote ambapo alienda mbali zaidi na kutoa changamoto kwa walioibua tuhuma hizo kumshtaki kwenye vyombo vya usalama ili achukuliwe hatua kali za kisheria.

Read More