Harmonize Atoa Ahadi Nzito kwa Kajala Kabla ya Birthday Yake
Msanii nyota wa Bongo Flava Harmonize ametoa ahadi kubwa kwa mpenzi wake, Frida Kajala, kuelekea siku yake ya kuzaliwa inayotarajiwa kusherehekewa Machi 15. Kupitia InstaStory yake, Harmonize amechapisha ujumbe wenye hisia akielezea namna anavyotamani kuwa pamoja na Kajala wakati wa kusherehekea kutimiza miaka 32. Katika ujumbe huo, msanii huyo amesema kuwa anatamani siku moja kumfanya Kajala kuwa mwanamke tajiri na mwenye furaha kubwa, akisisitiza kuwa anaamini anastahili mambo mazuri maishani. Kauli hiyo ya kumfanya tajiri imeibua tafsiri mbalimbali kutoka wajuzi wa mambo huku baadhi wakiamini huenda Harmonize ana mpango wa kumshirikisha Kajala katika miradi mikubwa ya kibiashara, uwekezaji au hata kumpa mali zitakazomsaidia kusimama imara kifedha.
Read More