Harmonize Ajigamba Wimbo Wake wa Leo Ndiyo Bora wa 2026
Msanii wa Bongo Fleva Harmonize amewatolea uvivu wasanii wanaotumia teknolojia ya Artificial Intelligence (AI) kutengeneza video za nyimbo zao. Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Harmonize amesema kuwa video ya wimbo wake uitwao leo, aliomshirikisha Mboso, ni bora zaidi kuliko video nyingi zinazotolewa na wasanii wanaotumia AI kwa sasa. Kwa mujibu wa Konde Boy, kazi hiyo imezingatia ubora wa hali ya juu na uhalisia unaogusa hisia za mashabiki. Mbali na hilo, Harmonize amejiamini zaidi kwa kudai kuwa wimbo wake wa Leo ndio wimbo bora wa mwaka 2026, akiwataka mashabiki na wadau wa muziki kuupokea na kuupa tathmini kwa haki. Kauli ya Harmonize inakuja wakati ambapo wimbo wake umeendelea kufanya vizuri kwa kasi kubwa, ukifikisha zaidi ya views milioni 5 kwenye YouTube na kushika nafasi ya kwanza nchini Tanzania, jambo linaloonyesha nguvu na ushawishi mkubwa wa msanii huyo katika tasnia ya muziki.
Read More