Harmonize Atangaza Kukamilika kwa Albamu Mpya “31”

Harmonize Atangaza Kukamilika kwa Albamu Mpya “31”

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize, ametangaza rasmi kukamilika kwa albamu yake mpya inayojulikana kwa jina la “31”, akieleza kuwa kazi hiyo ni muhtasari wa maisha yake binafsi na safari ya muziki aliyopitia kwa miaka mingi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize ameutaarifu umma kuhusu hatua hiyo muhimu katika taaluma yake, akifichua kuwa albamu hiyo imejaa hisia, uzoefu, mafunzo na mafanikio aliyopitia tangu alipoanza muziki. Katika albamu hiyo, msanii huyo ambaye pia ni mwanzilishi wa lebo ya Konde Music Worldwide, amewashirikisha wasanii wa kimataifa akiwemo nyota wa Nigeria Yemi Alade pamoja na msanii anayechipukia kwa kasi Draco. Mashabiki wake wamepokea taarifa hiyo kwa shangwe, wengi wakieleza kusubiri kwa hamu kusikia ladha mpya ya muziki kutoka kwa Harmonize ambaye amekuwa mstari wa mbele kusukuma muziki wa Afrika Mashariki katika majukwaa ya kimataifa. Ingawa tarehe rasmi ya kuachia albamu hiyo bado haijatangazwa, Harmonize ameahidi kuwa itakuwa kazi ya kipekee yenye ujumbe mzito na burudani ya hali ya juu kwa mashabiki wake kote duniani.

Read More
 Harmonize Atoa Shukrani kwa Mashabiki, Aahidi Makubwa Kutoka Konde Gang

Harmonize Atoa Shukrani kwa Mashabiki, Aahidi Makubwa Kutoka Konde Gang

Staa wa muziki kutoka Tanzania, Harmonize, ameonyesha shukrani zake kwa mashabiki wake duniani kote kufuatia akaunti yake ya Instagram kufikisha wafuasi milioni 3. Kupitia ujumbe maalum aliouweka mtandaoni, Harmonize amewashukuru mashabiki kwa sapoti ya dhati waliyoitoa tangu alipoanza safari yake ya muziki. Mbali na hilo, Harmonize alitumia nafasi hiyo pia kutangaza kuwa kufikia mwisho wa mwaka huu, lebo ya Konde Gang itawatambulisha wasanii wapya wawili, hatua ambayo inalenga kupanua familia ya Konde Gang na kukuza vipaji vipya katika tasnia ya muziki. Aidha, Harmonize aliwaahidi mashabiki wake kuwa kuna ngoma kali zinazokuja hivi karibuni kabla ya mwezi Agosti, akitaja kuwa ataachia kazi mpya zinazofuatia mafanikio ya nyimbo zake zilizopita. Mashabiki wake mitandaoni wameonyesha furaha kubwa kwa hatua hiyo, wakimsifia kwa juhudi zake za kukuza muziki wa Bongo Fleva na kulea vipaji kupitia Konde Gang.

Read More
 Harmonize Atoa Wito kwa Wasanii Watumie Singeli Kuelimisha Jamii

Harmonize Atoa Wito kwa Wasanii Watumie Singeli Kuelimisha Jamii

Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Harmonize, amewataka wasanii kutumia muziki wa Singeli kuibua mijadala ya kijamii na kupeleka ujumbe wenye maana kwa jamii badala ya kuishia kwenye burudani ya kawaida. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Harmonize alisema kuwa Singeli ni mtindo wa muziki wenye nguvu kubwa ya ushawishi na unastahili kutumiwa kuelimisha, kukuza maadili, na kuunganisha vizazi vyote kwa ujumbe wake. Harmonize, anayefahamika pia kwa jina la Konde Boy, alisisitiza kuwa kutumia Singeli kwa maudhui ya kijamii kutaongeza thamani ya muziki huo na kuufanya upokelewe na watu wa rika zote, si kundi moja tu. “Singeli ni mziki mkubwa sana. Wasanii tuutumie kuimba mambo ya msingi yenye maana, si kila siku kufurahisha tu,” aliandika msanii huyo katika ujumbe wake uliopata mapokezi makubwa mtandaoni. Katika hatua nyingine, Harmonize alidokeza kuwa anatarajia kuachia nyimbo mbili kubwa za kimataifa (International Bangers) usiku mmoja ndani ya mwezi Julai. Alisema kuwa ngoma hizo zitakuwa za kipekee na atawashirikisha wasanii wawili wakubwa wa kimataifa, ingawa hakuwataja majina yao. Hii imeongeza hamasa miongoni mwa mashabiki wake waliotamani kuona sura mpya ya kimataifa kutoka kwa bosi huyo wa Konde Gang. Singeli kwa sasa ni miongoni mwa mitindo ya muziki inayoshika kasi sana Tanzania. Julai 3, tulishuhudia msanii mkubwa wa Bongo Flava, Alikiba, akiachia wimbo wake wa kwanza wa Singeli uitwao Ubuyu, ambao mbali na kuburudisha, unatoa ujumbe mkali dhidi ya tabia zisizofaa katika jamii. Harmonize amepongeza mwelekeo huo, akiwahimiza wasanii wengine kuiga mfano huo kwa kutumia muziki kama chombo cha kuelimisha, kuonya, na kujenga.

Read More
 Harmonize Atangaza Harusi Yenye Sherehe Sita

Harmonize Atangaza Harusi Yenye Sherehe Sita

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Harmonize, ameibua mijadala mitandaoni baada ya kuchapisha ujumbe kupitia Insta Story yake akieleza kuwa anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Katika ujumbe huo uliojaa msisimko, msanii huyo alisema harusi yake haitakuwa ya kawaida, bali itahusisha sherehe sita kubwa zitakazofanyika katika maeneo mbalimbali. Kwa mujibu wa maelezo yake, Harmonize amesema harusi hiyo itaanza msikitini, kisha kuendelea kanisani, kufuatiwa na sherehe maalum katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, kabla ya kuhitimishwa na party kubwa uwanjani. Hata hivyo, hakutaja jina la mchumba wake wala tarehe rasmi ya tukio hilo. Licha ya kauli hiyo kuibua hisia tofauti miongoni mwa mashabiki, wengi wamesalia na maswali kuhusu uhalisia wa mpango huo, huku baadhi wakitilia shaka kuwa huenda ni kiki ya kisanaa inayolenga kutangaza wimbo au mradi mpya wa muziki. Harmonize amekuwa maarufu si tu kwa kazi zake za muziki bali pia kwa matukio ya kuvutia umakini mtandaoni, jambo linalowafanya mashabiki wake kuwa waangalifu kila anapotangaza jambo kubwa. Kwa sasa, hakuna tamko rasmi kutoka kwa menejimenti yake kuhusu mipango hiyo ya ndoa.

Read More
 Akaunti ya Instagram ya Konde Gang Yafungwa Ghafla

Akaunti ya Instagram ya Konde Gang Yafungwa Ghafla

Akaunti rasmi ya Instagram ya lebo ya muziki ya Konde Gang, inayomilikiwa na msanii nyota Harmonize, imefungwa ghafla, jambo lililozua maswali mengi miongoni mwa mashabiki na wadau wa muziki. Mpaka sasa, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu sababu ya kufungwa kwa ukurasa huo, ambao ulikuwa na zaidi ya wafuasi milioni 2 na ulikuwa ukitumiwa kwa matangazo ya muziki, matukio ya lebo, pamoja na taarifa za wasanii walioko chini ya Konde Gang. Mashabiki wengi wameeleza mshangao na masikitiko yao kupitia mitandao mingine ya kijamii, wakitaka kufahamu kilichojiri. Wengine wamehisi huenda ni hitilafu ya muda kwenye Instagram, huku baadhi wakihisi huenda akaunti hiyo imefungwa kwa kukiuka masharti ya matumizi ya jukwaa hilo. Harmonize bado hajatoa tamko rasmi kuhusu hatua hiyo, lakini mashabiki wake wanatarajia kupata taarifa kutoka kwake au uongozi wa Konde Gang muda wowote. Kwa sasa, shughuli za lebo hiyo zinaendelea kupitia kurasa binafsi za wasanii na timu ya menejimenti.

Read More
 Harmonize Aendelea Kuumia Kimapenzi, Aandika Machungu Snapchat

Harmonize Aendelea Kuumia Kimapenzi, Aandika Machungu Snapchat

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Harmonize, anaonekana kupitia kipindi kigumu upande wa mahusiano licha ya kuwa na jina kubwa kwenye tasnia ya muziki na utajiri wa kutosha. Kupitia akaunti yake ya Snapchat, Harmonize amemwaga hisia zake kwa uchungu kuhusu mpenzi wake ambaye bado hajawa tayari kumkubali kikamilifu kwenye maisha yake. Katika ujumbe wake, Harmonize alieleza kwa wazi kwamba ana mapenzi ya dhati kwa mwanamke huyo, na kwamba siku atakayokubali kuwa naye rasmi, atamuoa papo hapo bila kuchelewa. Hata hivyo, kwa sasa ameamua kumpa nafasi ya kuendelea na maisha yake huku yeye akiendelea kumsubiri kwa subira. “Mimi ni mtu mzima, niko tayari. Siku akiamua tu, sihitaji hata kupanga… nitamuoa siku hiyohiyo,” aliandika Harmonize kwa hisia kali. Mashabiki wengi wameonesha hisia tofauti, wengine wakimpongeza kwa uvumilivu na upendo wa kweli, huku wengine wakimshauri asijidhalilishe kwa mapenzi yasiyolipwa kwa kiwango sawa. Hii si mara ya kwanza kwa Harmonize kulalamika kuhusu changamoto za kimapenzi, jambo ambalo limezua mijadala mitandaoni kuhusu maisha ya mahusiano ya wasanii mashuhuri.

Read More
 Ibraah Atangaza Kuondoka Rasmi Konde Gang Baada ya Kikao na BASATA

Ibraah Atangaza Kuondoka Rasmi Konde Gang Baada ya Kikao na BASATA

Msanii nyota wa muziki wa Bongo Fleva, Ibrahim Abdallah maarufu kama Ibraah, ametangaza rasmi kuondoka kwenye lebo ya Konde Music Worldwide baada ya kikao cha mwisho kilichowahusisha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na uongozi wa lebo hiyo. Kupitia mahojiano baada ya kikao hicho, Ibraah amethibitisha kuwa wamefikia mwafaka wa kumaliza tofauti zao na uongozi wa Konde Gang. Hata hivyo, ameeleza kuwa bado hajakabidhiwa baadhi ya vitu muhimu vinavyohusiana na kazi yake ya muziki, ikiwemo akaunti zake za digital platforms kama YouTube, Boomplay, na Spotify. Kwa upande wao, uongozi wa Konde Gang kupitia Sandra, ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa lebo hiyo, wamethibitisha kuwa Ibraah atakabidhiwa rasmi akaunti hizo kabla ya mwisho wa leo. Aidha, Sandra amemtakia kila la heri Ibraah katika safari yake mpya ya muziki nje ya Konde Gang, akisisitiza kuwa hakuna uadui kati yao bali ni mabadiliko ya kawaida katika tasnia ya sanaa. Kuondoka kwa Ibraah kunakuja baada ya muda mrefu wa tetesi na hali ya sintofahamu kuhusu mustakabali wake ndani ya Konde Gang. Mashabiki wake sasa wanangoja kwa hamu kuona ni wapi atapeleka kipaji chake na iwapo ataendelea kung’ara kama msanii huru. Hii ni miongoni mwa migogoro ya kimikataba inayozidi kuibuka katika tasnia ya muziki Tanzania, huku mashirika kama BASATA yakihimiza mazungumzo ya kidiplomasia kama njia ya kutatua mizozo kati ya wasanii na lebo zao. Ibraah alikuwa msanii wa kwanza kusainiwa Konde Music mwaka 2020, na ametoa nyimbo kadhaa zilizotikisa chati za muziki Afrika Mashariki, kama vile One Night Stand, Nani, na Dharau akiwa chini ya lebo hiyo.

Read More
 Harmonize Atamani Kuwa Baba, Aonyesha Mradi Mkubwa wa Ujenzi

Harmonize Atamani Kuwa Baba, Aonyesha Mradi Mkubwa wa Ujenzi

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Harmonize, ameonesha hatua nyingine kubwa katika maisha yake ya kifedha na ya binafsi baada ya kuposti kwenye Instagram Story picha ya mjengo mkubwa unaoendelea kujengwa, ishara ya mafanikio na uthibitisho wa ndoto alizowahi kuzielezea huko nyuma. Picha hiyo, iliyopambwa na maneno “My future so bright, I need a son now”, imetoa ujumbe wenye maana pana: si tu kuhusu mafanikio ya sasa, bali pia taswira ya ndoto za baadaye. Harmonize anaonesha kuwa sasa anawaza si tu kuhusu kujenga majumba, bali pia kuanzisha familia na kupata mrithi wa jina lake. Kauli hiyo imeibua mijadala mitandaoni, wengi wakitafsiri kama ishara ya utulivu wa kisaikolojia na kifamilia, huku mashabiki wake wakimpongeza kwa hatua hiyo kubwa ya maisha. Wengine wamekuwa wakitaka kujua iwapo msanii huyo tayari ana mipango ya ndoa au mtoto kwa wakati huu. Harmonize, ambaye amepitia mengi katika maisha yake ya muziki na mahusiano, anaonekana sasa kuelekea kwenye ukurasa mpya unaochochewa na maono ya urithi, utulivu, na mafanikio ya muda mrefu.

Read More
 Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Wakazi Akosoa Mikataba Kandamizi kwa Wasanii Tanzania, Atumia Kisa cha Harmonize Kuonyesha Unyonyaji

Msanii wa Hip Hop nchini Tanzania, Wakazi, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kukosoa vikali aina ya mikataba wanayopewa wasanii wachanga na baadhi ya lebo kubwa za muziki nchini humo. Kupitia chapisho lake kwenye mtandao wa Instagram, Wakazi alisema kuwa mikataba mingi inalenga kuwanufaisha wamiliki wa lebo huku wasanii wakibaki bila mamlaka ya kazi zao hata zile walizozifadhili kwa pesa zao wenyewe. Katika maelezo yake, Wakazi alimtaja msanii Harmonize, akifichua kuwa licha ya yeye kugharamia baadhi ya kazi zake binafsi wakati akiwa chini ya lebo ya Wasafi (WCB), bado alilazimika kulipa kiasi kikubwa cha fedha ili aweze kuchukua catalog ya nyimbo alizotoa akiwa na lebo hiyo.  “Kumbuka Harmonize alikuwa anagharamia baadhi ya kazi zake kutoka mfukoni, lakini Wasafi walitaka alipie hela ili achukue catalog yake (wakati wao hata hawaku-invest on),” aliandika Wakazi. Wakazi aliongeza kuwa hali kama hiyo si ya kipekee, bali ni changamoto ambayo imekuwa ikiwakumba wasanii wengi chipukizi nchini Tanzania. Alisema kuwa kwa kutokuelewa masuala ya kisheria, wengi wao husaini mikataba kwa pupa, hali inayowaacha wakinyonywa kwa muda mrefu bila njia rahisi ya kujinasua. Wakazi ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa wasanii kuhakikisha wanapata ushauri wa kisheria kabla ya kuingia kwenye mikataba, ili kulinda kazi na haki zao. Pia amezitaka lebo za muziki kuwa na uwazi na kuweka mbele maslahi ya wasanii badala ya kutazama faida pekee. “Muziki ni biashara, lakini isiwe biashara ya kumnyonya msanii aliyetoa jasho lake. Tunahitaji mabadiliko ya kweli kwenye mfumo huu,” alisema. Kauli hiyo imeungwa mkono na baadhi ya mashabiki na wadau wa sanaa, huku wengine wakitaka kuanzishwe taasisi huru zitakazosaidia wasanii kusoma na kuelewa mikataba kabla ya kuisaini. Suala la mikataba kandamizi limekuwa likirudiwa mara kwa mara katika mijadala ya burudani nchini Tanzania. Wasanii kama Harmonize, Rayvanny, na wengine waliowahi kujitoa katika lebo kubwa wameelezea wazi namna walivyolazimika kulipa fedha nyingi ili kurejesha uhuru wa kazi zao.

Read More
 Harmonize Ajibu Kwa Hasira Tuhuma za Kumdai Ibraah

Harmonize Ajibu Kwa Hasira Tuhuma za Kumdai Ibraah

Staa wa muziki wa Bongo Fleva na mwanzilishi wa lebo ya Konde Gang, Rajab Abdul Kahali maarufu kama Harmonize, hatimaye ameweka wazi uhusiano wa sasa kati yake na aliyekuwa msanii wake, Ibraah. Hili ni baada ya tetesi nyingi kuzagaa kuhusu kuvunjika kwa ushirikiano wao uliodumu kwa miaka minne. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Harmonize alithibitisha rasmi kuwa Ibraah si sehemu ya Konde Gang tena, na sasa anafanya kazi kama msanii huru. Katika kueleza hali halisi ya kuondoka kwa Ibraah, Harmonize alikanusha vikali madai kwamba alimtoza msanii huyo kiasi cha Shilingi Bilioni 1 kwa ajili ya kuvunja mkataba wao. “Ni kweli mdogo wangu Chinga alinipigia simu na kuniambia anataka kutoka Konde Gang. Nilimtakia kila la kheri, lakini nikamshauri azungumze na viongozi wa lebo iwapo anahitaji kununua catalogue ya nyimbo zake,” alisema Harmonize huku akisisitiza kuwa hakuna madai yoyote ya kifedha baina yao. Harmonize aliongeza kuwa madai yaliyosambaa mitandaoni kuhusu deni hilo hayana ukweli wowote na yamekuwa yakimchafua bila sababu. “Simdai Ibraah pesa hiyo, na siwezi kupenda pesa yangu ije kunichafua mimi mwenyewe,” alisema kwa msisitizo. Katika upande mwingine wa mazungumzo hayo, Harmonize alifunguka kuhusu mustakabali wa Konde Gang, akieleza kuwa lebo hiyo iko tayari kufungua milango kwa vipaji vipya. Alisema kuwa licha ya changamoto, Konde Gang bado inaendelea na jukumu lake la kuibua na kulea wasanii chipukizi wenye ndoto kubwa. Taarifa hiyo imeibua hisia mbalimbali kutoka kwa mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva, wengi wakimpongeza Harmonize kwa ukomavu wake wa kiuongozi na namna alivyosimamia suala hilo kwa hekima na utulivu. Kwa sasa, wadau wa muziki na mashabiki kwa ujumla wanasubiri kuona Ibraah atajielekeza wapi akiwa kama msanii huru, huku nafasi mpya zilizofunguliwa ndani ya Konde Gang zikisubiri kujazwa na vipaji vipya vinavyokuja na njaa ya mafanikio.

Read More
 Harmonize atangaza ujio wa wimbo mpya kuhusu wapenzi wa zamani

Harmonize atangaza ujio wa wimbo mpya kuhusu wapenzi wa zamani

Mwanamuziki wa Bongofleva Harmonize ametangaza kuachia wimbo mpya Ijumaa hii, kueleka siku ya kutoa wimbo huo, Kupitia Insta Story yake kwenye mtandao wa Instagram Harmonize ametoa ufafanuzi kuhusu wimbo wake mpya unaotarajiwa kutoka, akisisitiza kuwa hauhusiani na mpenzi wake wa zamani. “HAIHUSINI NA X WANGU YEYOTE!!! NINA HESHIMA KUBWA SANA KWAO WOTE.”, Amesema Harmonize. Kiongozi huyo wa konde gang ameeleza kuwa hawezi kuimba kuhusu mpenzi wake wa zamani, kwa sababu heshima na upendo wake kwao umebadilika na kuwa wa kifamilia. “KAMA NIKIMUIMBAJI X WANGU YEYOTE HAITOKUWA KAZI KUBWA KAMA MNAVYO DHANI! ILA NDO SIWEZI UPENDO WANGU UNAUPITILIZA NA KUWA KAMA KAKA MDOGO KWENYE FAMILIA. SO HATA TIKTOKA TUMESHINDWA HESHIMA NA ADABU YANGU KWENYE FAMILIA INABAKI PALE PALE, SO HATA AKINIUNIKA TUNAKUTANA KWENYE VIKAO VYA FAMILIA 😂.” Ameeleza. Pia, ameongeza kuwa wimbo huu ni kwa niaba ya watu wote walioachana na wapenzi wao, sio maisha yake binafsi pekee. “HIZI GOMA NI KWA NIABA YA XXX WOTE DUNIANI, MSINIPENDE KUAONA MNAYAWATA WAKWENU TUU KISA NIMEMBA MTE 😂 SEE YOU ON FRIDAY KUMEKUCHA!!!”, Ameongeza Harmonize.

Read More
 Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Bahati adokeza ujio wa kolabo yake na Harmonize

Wakati bado Bahati anaendelea kufanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Nowe Sweety,’ ameonyesha kuwa hataki kulaza damu kuhusu muziki,ameonekana ujio wa kazi yake mpya na msanii wa BongoFleva Harmonize. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Bahati amepost picha akiwa na Harmonize na kuandika ‘2023 are You Ready for Us??? Brother  @Harmonize_tz ‘ na Harmonize akajibu kwa kuandika ‘SEND IT BRO I HAVE ONLY ONE WATSP NUMBER LOVE YOU NO MARA WAA !!! GETO BOYS ‘. Iwapo Bahati atafanikiwa kuachia wimbo wake na Harmonize atakuwa ameongeza orodha ya wasanii wa Bongoflava aliofanya nao kazi ikizingatiwa kuwa ana kazi ya pamoja na  Rayvanny, Mbosso na Aslay.

Read More