Harmonize Afurahia Mapokezi Makubwa ya Video ya “LALA”
Msanii nyota wa Bongo Fleva, Harmonize, amejipatia sifa kemkem baada ya mashabiki wake kuipokea kwa kishindo video ya wimbo wake mpya “LALA” aliyomshirikisha Abby Chams. Video hiyo, ambayo imekuwa gumzo mitandaoni, imepewa nyota tano na mashabiki wengi, huku ikitajwa kuwa Video Bora ya Mwaka 2025 katika ukanda wa Afrika Mashariki. Harmonize kupitia ukurasa wake wa Instagram ameonesha furaha yake, akisema kuwa hathamini sana namba au nyota alizopewa, bali anafarijika kuona kazi yake ikipokelewa kwa upendo. Msanii huyo amesifu jitihada za director Joma, akisema amefanya kazi safi na kuibua ubora uliowavutia wengi. Wengi wa mashabiki kupitia mitandao ya kijamii wameeleza kuwa “LALA” ndiyo video bora zaidi mwaka huu, wakisisitiza ubunifu, ubora wa picha na utayarishaji uliosukwa kwa umakini mkubwa. Kauli kama “LALA Looks Like East African Video of the Year 2025” zimekuwa zikijirudia mara kwa mara kwenye maoni ya mashabiki.
Read More