Zuchu Aiwakilisha Tanzania Katika Filamu ya Iyabo Ojo

Zuchu Aiwakilisha Tanzania Katika Filamu ya Iyabo Ojo

Msanii nyota wa muziki kutoka Tanzania, Zuchu, ametajwa kuwa miongoni mwa mastaa watakaoonekana katika filamu mpya ya kimataifa ya muigizaji maarufu wa Nigeria, Iyabo Ojo, inayofahamika kwa jina la “The Return of Arinzo.” Ushiriki wa Zuchu katika filamu hiyo umeibua gumzo kubwa miongoni mwa mashabiki wake, wengi wakisubiri kwa hamu kuona namna atakavyojitokeza katika ulimwengu wa filamu za kimataifa. Hii ni hatua nyingine muhimu kwa Zuchu katika kupanua wigo wake nje ya muziki na kuiwakilisha Tanzania kwenye jukwaa la kimataifa. Mbali na Zuchu, filamu hiyo pia inawakutanisha mastaa wengine kutoka Tanzania akiwemo Juma Jux pamoja na Prisca Lyimo, huku wakijiunga na waigizaji wakubwa kutoka Nigeria. Mradi huu unalenga kuunganisha tasnia ya filamu na muziki barani Afrika na kuimarisha ushirikiano kati ya wasanii wa mataifa tofauti. “The Return of Arinzo” inaandaliwa chini ya Iyabo Ojo kwa kushirikiana na Soso Sobrekon pamoja na Abazee Productions, na inatarajiwa kuwa miongoni mwa filamu kubwa zitakazofanya vizuri zaidi katika soko la kimataifa. Ushiriki wa Zuchu na mastaa wengine umeongeza matarajio makubwa, huku Afrika ikishuhudia hatua mpya ya ukuaji wa filamu zake katika soko la dunia.

Read More
 Inama ya Zuchu Yashusha Woza ya Nadia Mukami Kwenye Trending YouTube Kenya

Inama ya Zuchu Yashusha Woza ya Nadia Mukami Kwenye Trending YouTube Kenya

Wimbo “Inama” wa msanii wa WCB Wasafi, Zuchu, umeendelea kutikisa chati za muziki Afrika Mashariki baada ya kushika namba moja na kuishusha ngoma “Woza” ya Nadia Mukami kwenye orodha ya trending ya YouTube Kenya. Kupitia ukurasa wake rasmi wa mitandao ya kijamii, lebo ya WCB Wasafi imewashukuru mashabiki wa Kenya kwa kuonyesha upendo mkubwa kwa Zuchu na kazi zake, ikisema kuwa sapoti hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya wimbo huo kwenye soko la Kenya. Kwa mujibu wa takwimu za YouTube, Inama imeshika namba moja ikiwa na views milioni 2.1 ndani ya siku 6 tu, kasi iliyoifanya kuongoza trending nchini Kenya. Kwa upande mwingine, Woza ya Nadia Mukami inashikilia nafasi ya pili na views milioni 1.3 ndani ya kipindi cha wiki tatu, jambo linaloonesha ushindani mkubwa wa wasanii wa kike kutoka Tanzania na Kenya.

Read More
 Zuchu Amzuia Shabiki Kumkumbatia Diamond Kisa Wivu wa Mapenzi

Zuchu Amzuia Shabiki Kumkumbatia Diamond Kisa Wivu wa Mapenzi

Msanii nyota wa Bongo Fleva Zuchu amezua mjadala mitandaoni baada ya kuonekana akimzuia shabiki wa kike aliyekuwa akitaka kumkumbatia mume wake, Diamond Platnumz, wakati akiwa location kwenye video shoot ya wimbo wao uitwao Inama. Kwa mujibu wa video inayosambaa mitandaoni, Zuchu alionekana awali akizungumza na shabiki huyo kwa utulivu. Hata hivyo, hali ilibadilika pale shabiki huyo alipojaribu kuelekea eneo alilokuwepo Diamond. Zuchu alichukua hatua ya haraka na kumzuia, akionesha wazi kutoridhishwa kwake na jaribio hilo. Katika video hiyo, Hitmaker huyo wa Amanda amesikika akiwaagiza mashabiki kumsalimia Diamond kwa mikono, kitendo ambacho wengi wametafsiri kama dalili ya wivu wa kimapenzi, wakieleza kuwa huenda Zuchu alikuwa akilinda mipaka ya ndoa yake.

Read More
 Zuchu: Sipo Kwenye Mashindano ya Muziki

Zuchu: Sipo Kwenye Mashindano ya Muziki

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Zuchu, ameonyesha wazi kukerwa na kitendo cha mashabiki na wadau wa tasnia ya muziki wanaoendelea kumshindanisha na wasanii wengine mtandaoni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Story, Zuchu amechapisha ujumbe wa kimafumbo uliodhihirisha msimamo wake kuhusu mashindano ya kisanii. Katika ujumbe huo, amesisitiza kuwa yupo kwenye safari yake binafsi ya muziki na hana mpango wa kushindana na mtu yeyote, jambo lililoonyesha wazi kuchoshwa kwake na mijadala hiyo. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Walimwengu kuanza kulinganisha wimbo wake mpya “Reason” na kazi za wasanii wengine wa Bongo Fleva, wakidai kuwa wimbo huo haujapata mapokezi makubwa kama ilivyokuwa kwa nyimbo zake za awali zilizovunja rekodi kwenye majukwaa ya kidijitali. Ujumbe wa Zuchu umetafsiriwa na wengi kama msisitizo wa kauli yake ya mwaka wa 2022 ambapo alinukuliwa akisema kwamba hataki kabisa kushindanishwa na wasanii wa kike maana ngoma zake zipo kwenye ligi ya wasanii wa kiume.

Read More
 Zuchu Afunguka Kuhusu Mipango ya Muziki na Biashara Kabla na Baada ya Ramadhan

Zuchu Afunguka Kuhusu Mipango ya Muziki na Biashara Kabla na Baada ya Ramadhan

Msanii nyota wa Bongo Fleva, Zuchu,ameweka wazi mipango yake mikubwa ya muziki na biashara kwa kipindi kijacho cha mwaka wa 2026 hasa kabla na baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhan. Kupitia Instastory yake, Zuchu amesema kuwa bado ana matoleo mawili ya nyimbo (releases) kabla ya Ramadhan kuanza. Ameeleza kuwa nyimbo hizo ni sehemu ya maandalizi yake ya kuendelea kuwapa mashabiki burudani huku akiimarisha safari yake ya muziki. Mbali na muziki, Zuchu pia ametangaza kuwa yuko katika hatua za mwisho za kuandaa clothing line yake, ambayo inatarajiwa kuwa tayari kabla au wakati wa Ramadhan. Hatua hiyo inaonesha upanuzi wa chapa (Brand) yake binafsi nje ya muziki na kuingia zaidi katika ulimwengu wa biashara na mitindo. Baada ya Ramadhan, Zuchu amethibitisha kuwa ataachia albamu yake mpya ya Bongo Fleva, ambayo amesema itakuwa na ladha tofauti na yenye ubora wa kimataifa. Ameongeza kuwa albamu hiyo ni sehemu ya mkakati wake wa kuifikisha muziki wa Tanzania katika majukwaa ya kimataifa.

Read More
 Zuchu Awasihi Mashabiki Waamini Kazi Zao

Zuchu Awasihi Mashabiki Waamini Kazi Zao

Mwanamuziki nyota kutoka WCB Wasafi, Zuchu, ametoa ujumbe mzito kwa mashabiki na vijana wanaojitafuta kwenye sanaa na kazi zao, akiwahimiza waache kujihukumu kupita kiasi na badala yake waamini uwezo wao bila woga. Kupitia ujumbe aliouchapisha mtandaoni, Zuchu amesema hakuna muda sahihi wa kufanya jambo, bali mtu anapaswa kuchukua hatua, kufanya kazi na kuondoa mawazo hasi yanayokatisha tamaa. Amesisitiza kuwa ubora wa kazi mara nyingi hutazamwa tofauti na mashabiki, hivyo kujikosoa kupita kiasi kunaweza kuua ndoto kabla hata ya kuanza. Msanii huyo amefichua kuwa alipatwa na hofu kubwa kabla ya kuachia wimbo wake “Reason”, ambao aliimba kwa Kiingereza tofauti na mtindo wake wa kawaida. Zuchu amekiri kuwa aliwazia kuufuta kabisa wimbo huo kwa kuhofia ukosoaji na kuhisi kuwa ni kazi duni ambayo isingeweza kukubalika. Hata hivyo, baada ya kumsikilizisha prodyuza wimbo huo, alipokea mrejesho mzuri, jambo lililomtia moyo zaidi na kuamua kuwashauri wengine wasikubali kushindwa na hofu au kujikosoa kupita kiasi. Zuchu ametoa somo hilo akisema anaamini wengi hukwamishwa na mashaka yanayotokana na mawazo hasi, huku akisisitiza umuhimu wa kuamini safari na ubunifu wa mtu bila kuyumbishwa na hofu za ndani

Read More
 Zuchu Amkingia Kifua Diamond Kufuatia Madai ya Kuvuliwa Ubalozi wa Pepsi

Zuchu Amkingia Kifua Diamond Kufuatia Madai ya Kuvuliwa Ubalozi wa Pepsi

Mwanamuziki wa Bongofleva Zuchu ameibuka na kukanusha vikali madai yaliyoenea mtandaoni kwamba mume wake Diamond Platnumz amevuliwa wadhifa wake wa ubalozi wa Pepsi kutokana na kuhusishwa na siasa za CCM. Katika ufafanuzi wake, Zuchu ameeleza kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote, akisema zimetengenezwa na watu wanaotaka kupotosha umma lakini pia kutafuta kiki mtandaoni. Hitmaker huyo wa Amanda, ameeleza kuwa Diamond anaendelea kutekeleza majukumu yake kama balozi wa Pepsi bila changamoto yoyote, na mahusiano kati ya WCB na kampuni hiyo bado ni thabiti. Kauli yake imekuja wakati tetesi hizo zikisambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, huku baadhi ya mashabiki wakionesha wasiwasi kuhusu mustakabali wa ushirikiano huo. Ufafanuzi huo umeondoa sintofahamu na kuthibitisha kuwa mahusiano kati ya Diamond na Pepsi yanaendelea kuwa thabiti kama ilivyokuwa awali.

Read More
 Zuchu Aomba Amani Baada ya Ghasia Tanzania

Zuchu Aomba Amani Baada ya Ghasia Tanzania

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Zuchu, amevunja ukimya wake kufuatia taarifa za ghasia zilizoibuka nchini Tanzania baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, ambazo zimeripotiwa kusababisha vifo vya baadhi ya wananchi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zuchu ameomba Mungu aihifadhi Tanzania na kuijaalie amani, umoja na upendo, akionekana kuguswa na machafuko yanayoripotiwa katika baadhi ya maeneo nchini humo wakati wa uchaguzi. Kauli ya Zuchu inakuja wakati ambapo mashabiki na wananchi kadhaa wamekuwa wakiwakosoa mastaa wa Tanzania kwa kile kinachoonekana kama ukimya wao kuhusu matukio ya ukatili na ghasia zilizoripotiwa kufuatia uchaguzi huo. Hadi sasa, mamlaka husika bado hazijatoa takwimu rasmi za watu walioumia au kupoteza maisha katika vurugu hizo, huku viongozi wa dini na wasanii wengine wakihimiza mazungumzo na utulivu nchini.

Read More
 Zuchu Amimina Ujumbe wa Mahaba kwa Diamond Platnumz Siku ya Kuzaliwa

Zuchu Amimina Ujumbe wa Mahaba kwa Diamond Platnumz Siku ya Kuzaliwa

Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Zuchu, ameshindwa kuficha mapenzi yake kwa msanii nyota Diamond Platnumz kupitia ujumbe wa mahaba aliouandika kwenye ukurasa wake wa Instagram wakati wa kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Diamond. Katika ujumbe wake, Zuchu amemtakia Diamond kheri ya siku ya kuzaliwa huku akimpa heshima kama msanii, kiongozi na mpenzi. Ameweka wazi hisia zake akimtaja Diamond kwa majina ya mahaba ikiwemo Shmugum wangu, Kiboko yangu, Boss wangu, Hero wangu, Mentor wangu, Msimamizi wangu, Danga langu, Last Say wangu, Muchuchu wangu, Boyfriend na Mume wangu. Zuchu pia ameeleza kuwa ataendelea kusimama naye kwa hali na mali, akimtaka ajiandae kisaikolojia kwa changamoto na mapenzi yao ya milele. Aidha, amemtakia maisha marefu yenye furaha huku akimtaja kama msanii bora zaidi wa kizazi chake (GOAT) Kupitia utani wa kimahaba, Zuchu amemkumbusha Diamond kuwa zawadi aliyo nayo kubwa zaidi ni yeye mwenyewe, na hivyo hana haja ya zawadi nyingine zaidi ya kumrudishia zile alizowahi kuchukua.

Read More
 Zuchu Azindua Brand Mpya ya Mavazi “Goo People Clothing Line”

Zuchu Azindua Brand Mpya ya Mavazi “Goo People Clothing Line”

Mwanamuziki nyota kutoka lebo ya WCB, Zuchu, ameweka wazi hatua yake mpya nje ya muziki baada ya kudokeza ujio wa brand yake ya mavazi aliyoipa jina la Goo People Clothing Line. Kupitia mitandao ya kijamii, Zuchu amefungua ukurasa rasmi wa Instagram wa brand hiyo ambapo amechapisha picha zake za kwanza akiwa amevalia T-shirt zenye maandishi “Amanda”. Hatua hii imeashiria kuwa msanii huyo anapanua upeo wake wa ubunifu na kuingia kwenye tasnia ya mitindo. Mashabiki wake wamepokea habari hizi kwa shangwe, wengi wakimpongeza kwa kuonyesha mfano wa kuwekeza katika biashara sambamba na kazi yake ya muziki. Brand mpya ya Zuchu inatarajiwa kuvutia vijana na mashabiki wa muziki wake, huku ikimuweka kwenye ramani ya wasanii wa Afrika Mashariki wanaojitanua zaidi ya muziki. Kwa sasa, bado haijafahamika lini mavazi kutoka Goo People Clothing Line yataanza kuuzwa rasmi, lakini mashabiki wanasubiri kwa hamu kutinga nguo hizo mpya zenye jina la msanii wao

Read More
 Zuchu Apokea Malipo Yake ya Show ya Fainali za CHAN Kenya

Zuchu Apokea Malipo Yake ya Show ya Fainali za CHAN Kenya

Staa wa muziki kutoka WCB, Zuchu, hatimaye amethibitisha kupokea malipo yake ya onyesho alilolifanya katika fainali za Mashindano ya CHAN yaliyofanyika nchini Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Zuchu aliandika kuwa anashukuru mashabiki na watu wote waliowezesha ujumbe wake kufika kwa mashirika husika. Alisema kuwa tayari amepokea malipo yake yote na sasa anaendelea mbele na kazi zake. Hii inakuja siku chache baada ya msanii huyo kuibua malalamiko mitandaoni akidai kuwa tangu atumbuize kwenye fainali hizo hakulipwa stahiki zake. Kauli yake ya sasa imeondoa sintofahamu na kuthibitisha kuwa suala hilo limepatiwa suluhisho. Mashabiki wake wamefurahia kuona tatizo hilo limekwisha huku wengine wakimpongeza kwa uthubutu wa kulizungumza waziwazi.

Read More
 Mashabiki Tanzania Wakosoa Muziki wa Zuchu kwa Kudai Ni wa Kitoto

Mashabiki Tanzania Wakosoa Muziki wa Zuchu kwa Kudai Ni wa Kitoto

Baadhi ya mashabiki wa muziki nchini Tanzania wameeleza kutoridhishwa kwao na muziki wa staa wa Bongo Fleva, Zuchu, wakidai nyimbo zake zinaonekana kuwa za kitoto na hazina mvuto wa kipekee kwa watu wazima. Kwenye maoni yaliyosambaa mitandaoni, mashabiki hao wamesema wanapata ugumu kusikiliza nyimbo zake kwa muda mrefu kwani sauti na mitindo yake inawafanya kuhisi kwamba muziki huo unalenga zaidi watoto kuliko hadhira pana ya muziki wa kizazi kipya. Hata hivyo, upande mwingine wa mashabiki wake umejitokeza kumtetea, wakisisitiza kuwa Zuchu ni msanii mwenye kipaji cha kipekee na nyimbo zake zimekuwa zikifanya vizuri si tu Tanzania, bali pia kwenye majukwaa ya kimataifa. Wanasema sauti yake ya kipekee ndiyo inamtofautisha na wasanii wengine, na ndicho kilichompa nafasi ya kufanikisha mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi. Zuchu, ambaye ni msanii wa lebo ya WCB Wasafi, amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na nyimbo kama “Sukari”, “Cheche” na “Kwikwi”. Pamoja na ukosoaji huu, nyimbo zake bado zinaendelea kupata mamilioni ya watazamaji na wasikilizaji kwenye majukwaa ya kidijitali, jambo linaloonyesha kuwa bado ana hadhira kubwa na yenye ushawishi.

Read More