Zuchu Awagusa Mashabiki kwa Ujumbe wa Kuandika Nyimbo Bila Msaada

Zuchu Awagusa Mashabiki kwa Ujumbe wa Kuandika Nyimbo Bila Msaada

Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Zuchu, amefunguka kuhusu namna ambavyo kuandika nyimbo kumekuwa sehemu muhimu ya maisha yake, akifananisha mchakato huo na tiba ya kihisia licha ya kuwa kazi ngumu isiyo na msaada mkubwa. Kupitia Instastory yake, Zuchu aliandika ujumbe ulioambatana na video yake akiwa ndani ya studio, akionyesha jinsi anavyojitoa kwa moyo wote katika uandishi wa nyimbo zake. Ameeleza kuwa mara nyingi anapokuwa katika harakati za kuandika, huwa hana msaada wowote kutoka kwa waandishi wengine bali huwa pekee yake pamoja na producer. Ujumbe wake huo umetafsiriwa na mashabiki wake kama uthibitisho wa kujituma kwake katika sanaa ya muziki, hali inayomuweka juu miongoni mwa wasanii wa kike wanaoheshimika kwenye tasnia ya muziki Afrika Mashariki. Wengi wamepongeza uaminifu wake na juhudi anazoweka nyuma ya pazia kuleta kazi bora kwa mashabiki wake. Wengine wameelezea kuwa maelezo yake hayo yamewapa msukumo wa kufuata ndoto zao bila kutegemea msaada mkubwa kutoka kwa wengine.

Read More
 Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, hatimaye amethibitisha kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Zuchu, katika sherehe ya ndoa iliyofanyika kwa faragha mwishoni mwa wiki. Taarifa za ndoa hiyo zilithibitishwa kupitia picha na video zilizoshirikiwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo Diamond na Zuchu walionekana wakiwa kwenye vazi la Kiislamu, pamoja na familia na marafiki wa karibu. Video hizo zilionyesha Zuchu akimwita Diamond “mume wangu” huku wakiwa kwenye gari baada ya sherehe, jambo lililozua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki. Mama wa Diamond, Bi Sandra Dangote, alituma ujumbe wa pongezi kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiwatakia heri wanandoa hao wapya na kusisitiza kuwa ni hatua muhimu kwa mwanaye. Ndoa hii imekuja baada ya uvumi wa muda mrefu kuhusu uhusiano wao, huku Diamond akiwahi kutangaza hadharani kuwa ana mpango wa kumuoa Zuchu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadan mwaka huu. Hata hivyo, mipango hiyo ilicheleweshwa, na hatimaye wawili hao wamefanikisha lengo hilo kwa shangwe na furaha. Mashabiki na wadau wa muziki wameendelea kuwatumia salamu za heri na baraka kwa maisha yao mapya ya ndoa. Wengi wameeleza matumaini kuwa ndoa hiyo italeta utulivu na kuimarisha zaidi kazi zao za muziki. Kwa sasa, wawili hao hawajatoa taarifa ya kina kwa vyombo vya habari, lakini mashabiki wanatarajia tamko rasmi kutoka kwao hivi karibuni.

Read More
 Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Zuchu, amezua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu mustakabali wa uhusiano wake na staa wa muziki,Diamond Platnumz Akihojiwa katika kipindi cha Refresh Show kinachorushwa na Wasafi TV, wakati wa hafla ya JP Night 2025, Zuchu alionesha wazi kuwa ndoa haipo kwenye mipango yake na Diamond, licha ya uhusiano wao wa muda mrefu ambao umeendelea kuibua gumzo mitandaoni. Mkali huyo wa ngoma ya “Sukari” ameweka wazi kuwa hatima ya ndoa kati yake na mpenzi wake, Diamond Platnumz, haiko mikononi mwake bali yaachwe kwa Mwenyezi Mungu kuamua. “Tumuachie Mungu, Atajua Wakati Sahihi na Mtu Sahihi.”, alisema Zuchu kwa utulivu, Huku akionekana mwenye utulivu na kujiamini, Zuchu hakufafanua zaidi kuhusu hali halisi ya uhusiano wao, lakini maneno yake yameeleweka kama ishara ya kuwepo kwa mashaka au uwezekano wa mabadiliko katika safari yao ya kimapenzi. Kauli hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki na wafuasi wa wawili hao ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakifuatilia kwa karibu uhusiano wao wa kimapenzi. Wengi walitarajia kuwa mwaka huu huenda ungekuwa wa hatua kubwa kama uchumba au ndoa, lakini kauli ya Zuchu imeonyesha bado kuna sintofahamu. Diamond Platnumz na Zuchu wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu, ingawa mara kadhaa wamekana au kutoa majibu ya kujihami kuhusu uhusiano huo. Licha ya kuonekana pamoja mara kwa mara kwenye matamasha na hafla za kifamilia, bado hakuna uthibitisho rasmi wa ndoa au uchumba kutoka kwa wawili hao.

Read More
 Zuchu hana mpenzi wala mchumba -Khadija Kopa

Zuchu hana mpenzi wala mchumba -Khadija Kopa

Mama mzazi wa msanii Zuchu kutoka WCB Wasafi, Khadija Kopa amerejelea na kusisitiza kuwa mwanawe bado yuko singo na hana mwanaume yeyote awe mchumba au mpenzi. Kopa amesema kutokana na umaarufu wa Zuchu, siku akipata mchumba dunia nzima itajua na itakuwa ni habari ya mijini na vijijini, ila kwa watu wawe na subira na kutopotoshwa na kile ambacho wamekuwa wakikisikia mitandoani na kwenye mablogu ya udaku. “Zuchu bado yupo single, hana mpenzi wala Mchumba na wala hajanitambulisha kwa Mwanaume yoyote kwamba Mama huyu ndiye Mwanaume wangu, Zuchu ni maarufu hata mimi Mama yake ni maarufu siku atakapopata Mchumba akanitambulisha matajua tu muwe na subira,” alisema Khadija Kopa. Ikumbukwe Zuchu anatajwa kuwa na mahusiano na Diamond Platnumz lakini wenyewe wamekuwa wakikanusha hilo, ila mitandaoni wanaonekana kama wapenzi.

Read More
 Zari anyosha maelezo ishu ya kushindana na Zuchu kumteka kimapenzi Diamond Platnumz. 

Zari anyosha maelezo ishu ya kushindana na Zuchu kumteka kimapenzi Diamond Platnumz. 

Mrembo maarufu wa Uganda, Zari The Bosslady ameonyesha kuchukizwa na habari za uongo kuhusu kile kinachodaiwa yupo katika mashindano na Zuchu ili kuunasa moyo wa Diamond Platnumz. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Zari amesema “Halafu wajinga wote hapa wanaamini maoni hayo yaliyoambatanishwa na picha yangu? Nimekuwa nikiwaonya kuwa siku moja nitawashtaki kiwango cha nyinyi kuuza figo zenu ili mueze kunilipa. Wacheni uongo na upuzi. Shenzi type,” Kauli yake imekuja mara baada ya ukurasa mmoja wa Instagram kuweka picha iliyoonyesha Insta story za Zari akimsihi Zuchu kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, Diamond Platnumz. Kwenye picha hiyo ‘Zari’ alisema kuwa Diamond ataishi kuwa mpenzi wake na mapenzi yake na Zuchu hayatadumu. Kwa sasa Zari The Bosslady ambaye amekuwa anaishi Afrika Kusini na familia yake, alijaliwa watoto wawili na Diamond Platnumz, Tiffah na Nillan.

Read More
 Matamasha ya Zuchu Jijini Nairobi na Eldoret yaahirishwa

Matamasha ya Zuchu Jijini Nairobi na Eldoret yaahirishwa

Mwanamuziki kutoka Tanzania Zuchu amefutilia mbali matamasha yake ambayo yalikuwa yamepangwa kufanyika jijini Nairobi na Eldoret mwezi huu. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kampuni ya Trueblaq Limited na Jabali entertainment, matamasha hayo yamepangwa kufanyika mwaka ujao wikendi ya Pasaka. “Kutokana na mazingira yaliyo nje ya uwezo wetu, tunasikitika kukujulisha kwamba vybez connect events iliyopanga kufanyika jijini Nairobi na Eldoret tukishirikiana na Zuchu pamoja na wasanii wengine wa Kenya haitaendelea kama ilivyopangwa.”, Ilisomeka taarifa hiyo Matamasha ambayo yalikuwa yafanyike tarehe 10 na 11 Desemba 2022, sasa yatafanyika tarehe 8 na 9 Aprili 2023. Waandaaji matamasha hayo wameomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza kwa mashabiki huku wakiwahakikishia wale ambao tayari walikuwa wamenunua tiketi wataweza kuzitumia tiketi hizo kwa ajili ya tamasha la Pasaka lililopangwa upya. Hata hivyo wamesema pesa zitarejeshwa kwa wale ambao hawatafanikiwa kuhudhuria tamasha la Vybez Connect Events mwaka ujao.

Read More
 Zuchu ashindwa kujizuia jukwaani baada ya show yake Houston Marekani kukosa watu

Zuchu ashindwa kujizuia jukwaani baada ya show yake Houston Marekani kukosa watu

Staa wa muziki wa Bongofleva Zuchu amewashukuru mashabiki zake wote waliojitokeza kwenye show yake huko Houston, Texas nchini Marekani licha ya idadi ndogo ya mashabiki kuhudhuria show hiyo. Kupitia insta-story kwenye mtandao wa Instagram amesema kwamba kilichotokea kimempa hasira ya kufanya zaidi na anakubali kushindwa kama sehemu ya mafanikio yake. “Nimejiuliza sana kwanini nilichagua kazi hii ya muziki lakini kwa matukio kama haya yananipa majibu kwamba wachache hutolewa kama mfano ili ije kuwa rahisi kwa wengine” aliandika Zuchu Zuchu kwa sasa yupo kwenye ziara yake kimuziki (tour) nchini Marekani ambayo ilianza Novemba 18 hadi Desemba 3 mwaka huu. Ziara hiyo ya Zuchu ni pamoja na kutumbuiza kwenye hafla ya utoaji wa tuzo za African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA) zitakazotolewa Novemba 19 huko Dallas, Texas nchini Marekani ambapo Zuchu anawania kipengele cha Msanii Bora Afrika.

Read More
 Zuchu afikisha jumla ya streams Millioni 130 BoomPlay

Zuchu afikisha jumla ya streams Millioni 130 BoomPlay

Mwimbaji nyota wa kike kutoka WCB, Zuchu anazidi kufanya vizuri kupitia digital platforms pamoja na kuongeza rekodi katika upande wa wasanii wa kike Afrika. Kwa sasa Zuchu ni miongoni mwa wanamuziki wakike wenye idadi kubwa ya STREAMS katika mtandao wa Boomplay, hii ni baada ya kufikisha jumla ya streams Millioni 130 katika mtandao huo, hivyo anakuwa msanii wa pili Afrika baada ya Simi (Nigeria) mwenye streams 131.7 utakumbuka, Ijumaa ya wiki hii (Nov 18) Zuchu anatarajia kuanza tour yake ya muziki huko Marekani ambapo anatarajia kutumbuiza katika sherehe za utoaji wa tuzo za Afrimma 2022, pamoja na miji zaidi ya mitano.

Read More
 Zuchu atangaza kufanya ziara ya muziki nchini Marekani

Zuchu atangaza kufanya ziara ya muziki nchini Marekani

Msanii wa Bongofleva, Zuchu anatarajia kufanya ziara yake kimuziki (tour) nchini Marekani kuanzia Novemba 18 hadi Desemba 3 mwaka huu. Ziara hiyo ya Zuchu ni pamoja na kutumbuiza kwenye hafla ya utoaji wa tuzo za African Muzik Magazine Awards (AFRIMMA) zitakazotolewa Novemba 19 huko Dallas, Texas nchini Marekani ambapo Zuchu anawania kipengele cha Msanii Bora Afrika. Hii itakuwa ni ziara ya kwanza ya Zuchu nchini Marekani tangu ajiunge na WCB Wasafi Aprili mwaka 2020, hivyo anajiunga na Staa mwingine wa Bongofleva, Ali kiba ambaye tayari yupo nchini humo kwa ajili ya tour yake.

Read More
 Zuchu kulipa millioni 9.6 kwa tuhuma za kuiba mashairi wimbo

Zuchu kulipa millioni 9.6 kwa tuhuma za kuiba mashairi wimbo

Mwimbaji wa Bongofleva kutoka WCB Wasafi, Zuchu huenda akakamuliwa millioni 9.6 kwa kudaiwa kuiba wimbo wa msanii wa Injili, Enock Jonas huku lebo yake ikionesha kutokuwa tayari kuzilipa fedha hizo. Katika malalamiko hayo Jonas, amedai Zuchu amechukua sehemu ya kibwagizo na staili ya kucheza katika wimbo wake wa ‘Wema wa Mungu’ ambao ulitoka mwaka 2012 lakini ulijulikana zaidi kwa jina la ‘Zunguka’, akiutumia katika wimbo wake mpya ‘Kwikwi’. Taarifa za madai hayo zilianza kusambaa mitandaoni kupitia barua iliyoandikwa na kampuni ya wanasheria ya Gerpat Solution, ambapo mmoja wake Gerlad Magubuka, ameiambia Mwananchi leo Jumamosi Oktoba 22 kuwa mteja wao alikwenda kuwalalamikia Zuchu kutumia kionjo cha wimbo wake huo. Magabuka amesema tayari wameshawapelekea wahusika barua ya madai hayo na nakala nyingine wamepeleka Taasisi ya Hakimiliki Nchini (Cosota) na Shirikisho la Wanamuzi Tanzania (Shimuta). Akizungumza na Mwananchi, Enock amesema amelazimika kuchukua hatua hiyo baada ya mazungumzo na upande wa Zuchu kushindikana kwa kumwambia kuwa katika madai hayo hata laki mbili hawawezi kumlipa. Kwa upande wao Cosota kupitia Katibu Mtendaji wake, Doreen Sinare, amekiri suala hilo kutua mezani kwake na kueleza kilichofanyika ni wasanii wenyewe kuandikiana barua na wao wamepelekewa kama taarifa hivyo hawawezi kusema lolote kwa sasa wameacha wasanii wenyewe ndio wawasiliane kwanza na baadaye wao watakuja kuichambua na kuitolea tamko. Kwa upande wake Babu Tale alipotafutwa kuhusiana na tuhuma hizo, alikiri kuwasiliana na msanii huyo na kumpa majibu hayo ya kutompa hela aliyoitaka.

Read More
 Zuchu kutumbuiza kwenye tuzo za AFRIMMA 2022

Zuchu kutumbuiza kwenye tuzo za AFRIMMA 2022

Mwimbani wa Bongofleva toka WCB Wasafi, Zuchu amechaguliwa kutumbuiza kwenye tuzo za AFRIMMA zitakazotolewa Novemba 19 huko Dallas, Texas nchini Marekani. Kupitia ukurasa wao rasmi wa Instagram, AFRIMMA walipakia video ya kudensi ya Zuchu akicheza wimbo wake mpya wa Kwikwi na kusema kwamba ni rasmi msanii huyo atakuwa miongoni mwa watumbuizaji watakaopamba sherehe hizo. Wameandika; “Zuchu atatumbuiza moja kwa moja kwenye onyesho la TUZO ZA AFRIMMA mwaka huu. Zuchu ni mwimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka Tanzania mzaliwa wa Zanzibar lakini mwenye makazi yake jijini Dar es Salaam” Hatua hiyo inakuja siku chache baada ya Zuchu kutajwa kuwania tuzo za MTV EMA katika kipengele cha Best African Act. Utakumbuka pia Zuchu anawania AFRIMMA katika kipengele cha Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki, anachuana na Nandy, Maua Sama na wengineo.

Read More
 Diamond Platnumz asema hawezi kumuoa Zuchu

Diamond Platnumz asema hawezi kumuoa Zuchu

Msanii nyota wa Bongofleva Diamond Platnumz ameamua kutoa ya moyoni baada ya meneja wake Babu Tale kumshinikiza amuoe Zuchu kutokana na video aliyoichapisha kwenye ukurasa wake Instagram akibusiana na hitmaker huyo wa “Sukari”. Kulingana na comment yake akimjibu Babu Tale, hawezi kumuoa msanii wake Zuchu kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakiamini. “Sasa nitamuoaje wakati ni Msanii wangu Bosi, hilo busu hapo lisiwatishe viongozi, ni salamu tu za Kijerumani” amesema Diamond. Utakumbuka wawili hao wamekuwa na ukaribu sana kiasi cha kuzawadiana zawadi jambo lililofanya baadhi ya watukuamini kuwa Diamond na Zuchu wapo katika mahusiano ya kimapenzi.

Read More