Zuchu Azindua Brand Mpya ya Mavazi “Goo People Clothing Line”

Zuchu Azindua Brand Mpya ya Mavazi “Goo People Clothing Line”

Mwanamuziki nyota kutoka lebo ya WCB, Zuchu, ameweka wazi hatua yake mpya nje ya muziki baada ya kudokeza ujio wa brand yake ya mavazi aliyoipa jina la Goo People Clothing Line. Kupitia mitandao ya kijamii, Zuchu amefungua ukurasa rasmi wa Instagram wa brand hiyo ambapo amechapisha picha zake za kwanza akiwa amevalia T-shirt zenye maandishi “Amanda”. Hatua hii imeashiria kuwa msanii huyo anapanua upeo wake wa ubunifu na kuingia kwenye tasnia ya mitindo. Mashabiki wake wamepokea habari hizi kwa shangwe, wengi wakimpongeza kwa kuonyesha mfano wa kuwekeza katika biashara sambamba na kazi yake ya muziki. Brand mpya ya Zuchu inatarajiwa kuvutia vijana na mashabiki wa muziki wake, huku ikimuweka kwenye ramani ya wasanii wa Afrika Mashariki wanaojitanua zaidi ya muziki. Kwa sasa, bado haijafahamika lini mavazi kutoka Goo People Clothing Line yataanza kuuzwa rasmi, lakini mashabiki wanasubiri kwa hamu kutinga nguo hizo mpya zenye jina la msanii wao

Read More
 Zuchu Apokea Malipo Yake ya Show ya Fainali za CHAN Kenya

Zuchu Apokea Malipo Yake ya Show ya Fainali za CHAN Kenya

Staa wa muziki kutoka WCB, Zuchu, hatimaye amethibitisha kupokea malipo yake ya onyesho alilolifanya katika fainali za Mashindano ya CHAN yaliyofanyika nchini Kenya. Kupitia ukurasa wake wa Instastory, Zuchu aliandika kuwa anashukuru mashabiki na watu wote waliowezesha ujumbe wake kufika kwa mashirika husika. Alisema kuwa tayari amepokea malipo yake yote na sasa anaendelea mbele na kazi zake. Hii inakuja siku chache baada ya msanii huyo kuibua malalamiko mitandaoni akidai kuwa tangu atumbuize kwenye fainali hizo hakulipwa stahiki zake. Kauli yake ya sasa imeondoa sintofahamu na kuthibitisha kuwa suala hilo limepatiwa suluhisho. Mashabiki wake wamefurahia kuona tatizo hilo limekwisha huku wengine wakimpongeza kwa uthubutu wa kulizungumza waziwazi.

Read More
 Mashabiki Tanzania Wakosoa Muziki wa Zuchu kwa Kudai Ni wa Kitoto

Mashabiki Tanzania Wakosoa Muziki wa Zuchu kwa Kudai Ni wa Kitoto

Baadhi ya mashabiki wa muziki nchini Tanzania wameeleza kutoridhishwa kwao na muziki wa staa wa Bongo Fleva, Zuchu, wakidai nyimbo zake zinaonekana kuwa za kitoto na hazina mvuto wa kipekee kwa watu wazima. Kwenye maoni yaliyosambaa mitandaoni, mashabiki hao wamesema wanapata ugumu kusikiliza nyimbo zake kwa muda mrefu kwani sauti na mitindo yake inawafanya kuhisi kwamba muziki huo unalenga zaidi watoto kuliko hadhira pana ya muziki wa kizazi kipya. Hata hivyo, upande mwingine wa mashabiki wake umejitokeza kumtetea, wakisisitiza kuwa Zuchu ni msanii mwenye kipaji cha kipekee na nyimbo zake zimekuwa zikifanya vizuri si tu Tanzania, bali pia kwenye majukwaa ya kimataifa. Wanasema sauti yake ya kipekee ndiyo inamtofautisha na wasanii wengine, na ndicho kilichompa nafasi ya kufanikisha mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi. Zuchu, ambaye ni msanii wa lebo ya WCB Wasafi, amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na nyimbo kama “Sukari”, “Cheche” na “Kwikwi”. Pamoja na ukosoaji huu, nyimbo zake bado zinaendelea kupata mamilioni ya watazamaji na wasikilizaji kwenye majukwaa ya kidijitali, jambo linaloonyesha kuwa bado ana hadhira kubwa na yenye ushawishi.

Read More
 Mashabiki Wataka Zuchu Atumbuize Kombe la Dunia 2026

Mashabiki Wataka Zuchu Atumbuize Kombe la Dunia 2026

Mashabiki wa muziki Afrika Mashariki wameonyesha shauku kubwa ya kutaka msanii wa WCB Zuchu kutumbuiza kwenye ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026, baada ya kuandika historia usiku wa kuamkia leo katika Siku ya Yanga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Katika onyesho hilo lililohudhuriwa na zaidi ya mashabiki elfu 60, Zuchu alidhihirisha ubunifu wa kimataifa kwa mtindo wa kipekee wa kuingia jukwaani. Msanii huyo alifika uwanjani ndani ya chombo kilichofanana na ua kubwa, ambacho baadaye kilifunguka taratibu kama ua linalochanua, na Zuchu akaibuka kutoka ndani yake huku akiibua shamrashamra za burudani. Mbali na hilo, aliwashangaza mashabiki kwa kuingia na kundi kubwa la madansa zaidi ya 200, hali iliyoongeza hamasa na kuifanya show yake kuzungumziwa kote mitandaoni. Zuchu alisema kuwa kiwango cha ubunifu kilichoonyeshwa hakijawahi kutokea kwenye historia ya shoo kubwa za uwanjani Tanzania. Hali hiyo imezua mjadala mitandaoni, wengi wakimpongeza kwa hatua kubwa ya kuvuka mipaka ya burudani ya ndani na kuonyesha kwamba wasanii wa Afrika Mashariki wanaweza kushindana kimataifa. Baadhi ya mashabiki wameenda mbali zaidi wakimtaka Zuchu aorodheshwe miongoni mwa wasanii watakaopamba ufunguzi wa FIFA World Cup 2026, wakisema ubunifu na hadhi yake sasa inatosha kushindana na wakali wa dunia.

Read More
 Zuchu Akanusha Madai ya Kupuuzwa Kasarani Wakati wa Fainali za CHAN

Zuchu Akanusha Madai ya Kupuuzwa Kasarani Wakati wa Fainali za CHAN

Msanii kutoka Tanzania, Zuchu, amejitokeza na kukanusha vikali madai kwamba alipuuziwa na mashabiki wakati wa onyesho lake katika Uwanja wa Kasarani, wakati wa fainali za mashindano ya CHAN kati ya Morocco na Madagascar. Ripoti zilizosambaa mitandaoni zilisema kuwa baadhi ya mashabiki waliokuwepo uwanjani walionekana kuimba wimbo wa taifa la Kenya wakati Zuchu alipokuwa akiendelea na maonesho jukwaani, hali iliyotafsiriwa na baadhi ya watumiaji wa mitandao kama ishara ya kutompa usikivu au heshima anayostahili. Kupitia mitandao ya kijamii, hususan Instagram, Zuchu alikanusha madai hayo akisisitiza kuwa video zilizozagaa mtandaoni zimehaririwa kwa nia ovu ya kueneza taarifa potofu. Alieleza kuwa onyesho hilo lilirushwa moja kwa moja (live) na linapatikana kwa ukamilifu kwenye YouTube, hivyo kama tukio hilo lingetokea kweli, lingeonekana bayana kwenye rekodi ya moja kwa moja. Hitmaker huyo wa Amanda ameendelea kusisitiza kuwa mafanikio ya kazi yake hayawezi kutikiswa na kauli za watu wachache mitandaoni, kwani chapa yake inasimamiwa na juhudi, maombi, na mashabiki wake wa kweli walioko ndani na nje ya Tanzania. Tukio hilo, ambalo lilidaiwa kutokea wakati wa mechi kubwa ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), limezua mjadala mitandaoni huku baadhi ya mashabiki wakimtetea vikali Zuchu, wakisema alitoa burudani ya hali ya juu licha ya kelele za mtandaoni.

Read More
 Zuchu: Ashurey Ndiye Dansa Namba Moja Afrika Mashariki

Zuchu: Ashurey Ndiye Dansa Namba Moja Afrika Mashariki

Staa wa Bongo Fleva, Zuchu, amempa nyota tano dansa wake maarufu Ashurey akimtaja kuwa ndiye Dansa bora namba moja Afrika Mashariki kwa sasa. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zuchu alipakia video ya Ashurey akifanya challenge ya wimbo wake mpya “Inama”, kisha akaandika ujumbe wa kumpa heshima kubwa kwa umahiri wake wa kucheza. Wakati mashabiki wake wakiendelea kufurahia wimbo wake maarufu “Amanda”, Zuchu ametangaza kuwa yupo mbioni kuachia rasmi wimbo mpya uitwao “Inama”, akidai kuwa utafunika hata mafanikio ya hitsong yake, “Sukari”, ambayo imepata streams na views nyingi kwenye majukwaa ya kidigitali. Tangazo hili limeongeza hamasa kwa mashabiki wake kote Afrika Mashariki, ambao sasa wanasubiri kwa shauku kuona iwapo “Inama” itavunja rekodi na kufikia viwango vikubwa zaidi ya nyimbo zake zilizopita.

Read More
 Zuchu Akutana na Dada Anayemwigiza Kenya

Zuchu Akutana na Dada Anayemwigiza Kenya

Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Zuchu, ameonyesha furaha na upendo wake baada ya kukutana ana kwa ana na pacha wake kutoka Kenya anayemwigiza. Binti huyo, ambaye mashabiki wanamuita “Zuchu wa Mchongo”, amejizolea umaarufu mitandaoni kutokana na kumwigiza Zuchu katika mitindo ya uchezaji na mavazi, sambamba na kufanya challenges za nyimbo zake. Kutokana na kufanana kwao kimuonekano, mara nyingi mashabiki huchanganyikiwa kumtambua nani ni nani. Katika video iliyosambaa, Zuchu alionekana akimkumbatia dada huyo kwa upendo na kumshukuru kwa namna anavyounga mkono kazi zake za muziki. Msanii huyo wa WCB alikiri wazi kwamba anamthamini na anafarijika kuona kazi zake zikileta nafasi ya kuibua vipaji vipya hata nje ya Tanzania. Mashabiki mitandaoni wamefurahishwa na ukaribu huo, wakibainisha kuwa ni jambo la kipekee kwa Zuchu kumtambua na kumpongeza mtu anayemwigiza badala ya kuona kama ni ushindani.

Read More
 Zuchu Afunguka Kuhusu Madai ya Kubeza Wasanii wa Kenya Kablaya Fainali za CHAN

Zuchu Afunguka Kuhusu Madai ya Kubeza Wasanii wa Kenya Kablaya Fainali za CHAN

Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Zuchu, amekanusha taarifa zilizokuwa zikisambaa mitandaoni zikidai kwamba hatoshirikiana na wasanii wa Kenya kwa sababu ya madai ya Wakenya kumtusi Rais Samia Suluhu Hassan. Katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Kiss 100, Zuchu ameeleza kuwa hajawahi kutoa kauli hiyo na kusisitiza kuwa habari hizo hazina ukweli wowote. Amesema kuwa taarifa hizo zilitungwa kwa lengo la kumharibia jina na kumkosanisha na mashabiki wake wa Kenya. Zuchu ameweka wazi kuwa hana nia yoyote mbaya kwa wasanii wa Kenya, bali anawaheshimu kwa vipaji vyao. Ameeleza pia kuwa tayari ameshirikiana nao kwenye miradi yake ya muziki, wakiwemo wasanii wa kundi la Hart the Band, waliopata nafasi kwenye albamu yake. Taarifa hizo ziliibuka muda mfupi baada ya Zuchu kuwasili Kenya kwa ajili ya kutumbuiza leo kwenye fainali za CHAN 2024 katika uwanja wa Kasarani, ambapo atashiriki jukwaa moja na wasanii wengine wakubwa akiwemo Savara na Eddy Kenzo. Kauli yake sasa imeweka wazi msimamo wake na kumaliza tetesi zilizokuwa zikisababisha mjadala mkali mitandaoni kuhusu mahusiano ya muziki kati ya Tanzania na Kenya, akisisitiza mshikamano na ushirikiano wa kisanaa badala ya mgawanyiko. Baadhi ya wadau wa michezo na mashabiki wamehoji iwapo pesa hizo zitatolewa, huku wengine wakisisitiza kuwa wasanii wanapaswa kuwa makini na ahadi wanazotoa kwa umma ili kuepusha migongano na kuharibu taswira ya michezo nchini.

Read More
 Zuchu Apewa Heshima Kutumbuiza Kwenye Fainali za CHAN 2025 Kenya

Zuchu Apewa Heshima Kutumbuiza Kwenye Fainali za CHAN 2025 Kenya

Msanii maarufu wa Tanzania, Zuchu, ameteuliwa kuwa msanii kinara atakayetumbuiza kwenye sherehe za kufunga mashindano ya CHAN 2025 yatakayofanyika wikiendi hii katika Uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani jijini Nairobi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zuchu alieleza furaha yake akitangaza kuwa atakuwa msanii mkuu wa burudani kwenye fainali hizo, hatua ambayo imepokelewa kwa shangwe na mashabiki wake barani Afrika na kwingineko. Tangazo hilo pia liliibua pongezi kutoka kwa mastaa wa muziki, akiwemo Diamond Platnumz, ambaye alionyesha kufurahishwa na mafanikio ya mpenzi wake na kueleza kuwa hatua hiyo ni kubwa na inamfanya ajivunie zaidi. Sherehe za kufunga mashindano zinatarajiwa kuwa na burudani ya kipekee kabla ya mchezo wa fainali utakaozikutanisha timu za Morocco na Madagascar Jumamosi, tarehe 30 Agosti 2025, ambapo mshindi atavikwa taji la ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wa ndani.

Read More
 Zuchu Awagusa Mashabiki kwa Ujumbe wa Kuandika Nyimbo Bila Msaada

Zuchu Awagusa Mashabiki kwa Ujumbe wa Kuandika Nyimbo Bila Msaada

Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Zuchu, amefunguka kuhusu namna ambavyo kuandika nyimbo kumekuwa sehemu muhimu ya maisha yake, akifananisha mchakato huo na tiba ya kihisia licha ya kuwa kazi ngumu isiyo na msaada mkubwa. Kupitia Instastory yake, Zuchu aliandika ujumbe ulioambatana na video yake akiwa ndani ya studio, akionyesha jinsi anavyojitoa kwa moyo wote katika uandishi wa nyimbo zake. Ameeleza kuwa mara nyingi anapokuwa katika harakati za kuandika, huwa hana msaada wowote kutoka kwa waandishi wengine bali huwa pekee yake pamoja na producer. Ujumbe wake huo umetafsiriwa na mashabiki wake kama uthibitisho wa kujituma kwake katika sanaa ya muziki, hali inayomuweka juu miongoni mwa wasanii wa kike wanaoheshimika kwenye tasnia ya muziki Afrika Mashariki. Wengi wamepongeza uaminifu wake na juhudi anazoweka nyuma ya pazia kuleta kazi bora kwa mashabiki wake. Wengine wameelezea kuwa maelezo yake hayo yamewapa msukumo wa kufuata ndoto zao bila kutegemea msaada mkubwa kutoka kwa wengine.

Read More
 Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Diamond Platnumz na Zuchu Wafunga Ndoa ya Kiislamu kwa Faragha

Msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz, hatimaye amethibitisha kumuoa mpenzi wake wa muda mrefu, Zuchu, katika sherehe ya ndoa iliyofanyika kwa faragha mwishoni mwa wiki. Taarifa za ndoa hiyo zilithibitishwa kupitia picha na video zilizoshirikiwa kwenye mitandao ya kijamii, ambapo Diamond na Zuchu walionekana wakiwa kwenye vazi la Kiislamu, pamoja na familia na marafiki wa karibu. Video hizo zilionyesha Zuchu akimwita Diamond “mume wangu” huku wakiwa kwenye gari baada ya sherehe, jambo lililozua msisimko mkubwa miongoni mwa mashabiki. Mama wa Diamond, Bi Sandra Dangote, alituma ujumbe wa pongezi kupitia ukurasa wake wa Instagram, akiwatakia heri wanandoa hao wapya na kusisitiza kuwa ni hatua muhimu kwa mwanaye. Ndoa hii imekuja baada ya uvumi wa muda mrefu kuhusu uhusiano wao, huku Diamond akiwahi kutangaza hadharani kuwa ana mpango wa kumuoa Zuchu kabla ya mwezi mtukufu wa Ramadan mwaka huu. Hata hivyo, mipango hiyo ilicheleweshwa, na hatimaye wawili hao wamefanikisha lengo hilo kwa shangwe na furaha. Mashabiki na wadau wa muziki wameendelea kuwatumia salamu za heri na baraka kwa maisha yao mapya ya ndoa. Wengi wameeleza matumaini kuwa ndoa hiyo italeta utulivu na kuimarisha zaidi kazi zao za muziki. Kwa sasa, wawili hao hawajatoa taarifa ya kina kwa vyombo vya habari, lakini mashabiki wanatarajia tamko rasmi kutoka kwao hivi karibuni.

Read More
 Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Zuchu Asema Hatima ya Ndoa Yake na Diamond Ipo Mikononi mwa Mungu

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Zuchu, amezua gumzo mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu mustakabali wa uhusiano wake na staa wa muziki,Diamond Platnumz Akihojiwa katika kipindi cha Refresh Show kinachorushwa na Wasafi TV, wakati wa hafla ya JP Night 2025, Zuchu alionesha wazi kuwa ndoa haipo kwenye mipango yake na Diamond, licha ya uhusiano wao wa muda mrefu ambao umeendelea kuibua gumzo mitandaoni. Mkali huyo wa ngoma ya “Sukari” ameweka wazi kuwa hatima ya ndoa kati yake na mpenzi wake, Diamond Platnumz, haiko mikononi mwake bali yaachwe kwa Mwenyezi Mungu kuamua. “Tumuachie Mungu, Atajua Wakati Sahihi na Mtu Sahihi.”, alisema Zuchu kwa utulivu, Huku akionekana mwenye utulivu na kujiamini, Zuchu hakufafanua zaidi kuhusu hali halisi ya uhusiano wao, lakini maneno yake yameeleweka kama ishara ya kuwepo kwa mashaka au uwezekano wa mabadiliko katika safari yao ya kimapenzi. Kauli hiyo imeibua hisia mseto miongoni mwa mashabiki na wafuasi wa wawili hao ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakifuatilia kwa karibu uhusiano wao wa kimapenzi. Wengi walitarajia kuwa mwaka huu huenda ungekuwa wa hatua kubwa kama uchumba au ndoa, lakini kauli ya Zuchu imeonyesha bado kuna sintofahamu. Diamond Platnumz na Zuchu wamekuwa wakihusishwa kimapenzi kwa muda mrefu, ingawa mara kadhaa wamekana au kutoa majibu ya kujihami kuhusu uhusiano huo. Licha ya kuonekana pamoja mara kwa mara kwenye matamasha na hafla za kifamilia, bado hakuna uthibitisho rasmi wa ndoa au uchumba kutoka kwa wawili hao.

Read More