Zuchu Awagusa Mashabiki kwa Ujumbe wa Kuandika Nyimbo Bila Msaada
Mwanamuziki nyota kutoka Tanzania, Zuchu, amefunguka kuhusu namna ambavyo kuandika nyimbo kumekuwa sehemu muhimu ya maisha yake, akifananisha mchakato huo na tiba ya kihisia licha ya kuwa kazi ngumu isiyo na msaada mkubwa. Kupitia Instastory yake, Zuchu aliandika ujumbe ulioambatana na video yake akiwa ndani ya studio, akionyesha jinsi anavyojitoa kwa moyo wote katika uandishi wa nyimbo zake. Ameeleza kuwa mara nyingi anapokuwa katika harakati za kuandika, huwa hana msaada wowote kutoka kwa waandishi wengine bali huwa pekee yake pamoja na producer. Ujumbe wake huo umetafsiriwa na mashabiki wake kama uthibitisho wa kujituma kwake katika sanaa ya muziki, hali inayomuweka juu miongoni mwa wasanii wa kike wanaoheshimika kwenye tasnia ya muziki Afrika Mashariki. Wengi wamepongeza uaminifu wake na juhudi anazoweka nyuma ya pazia kuleta kazi bora kwa mashabiki wake. Wengine wameelezea kuwa maelezo yake hayo yamewapa msukumo wa kufuata ndoto zao bila kutegemea msaada mkubwa kutoka kwa wengine.
Read More